TCRA lindeni walaji wa habari

kavulata

JF-Expert Member
Aug 2, 2012
12,317
12,617
Vyombo vya habari redio na tv havipaswi kuwa na ratiba za vipindi vyao zinazoonyesha muda na siku? Kama zipo ratiba ni nani anapaswa kuhakikisha kuwa ratiba hizi zinafuatwa na vyombo vya habari ili kuwalinda wasikilizaji na watazamaji wa vipindi vyao?

Mfano, Redio inasema watakuwa na taarifa ya habari saa 1 asubuhi au michezo saa 2 usiku au magazeti saa 3 asubuhi, mlaji anasubiri taarifa ya habari isomwe saa 1 asubuhi lakini redio au tv inasoma taarifa hiyo nusu saa baada ya muda wa kipindi kupita, hii inaleta usumbufu mkubwa kwa wasikilizaji na watazamaji ambao wanataka kusikiliza kipindi husika ambacho kimecheleweshwa kuanza bila taarifa kwa walaji kuwa kipindi kitachelewa kutokana na sababu fulani.

Na mara nyingi kipindi kinachelewa kwa mambo ya kipuuzi kabisa. Nchi inaonekana kuwa haijali muda wa wananchi unaopotezwa na vyombo hivi vya habari.

Je, TCRA hamlioni hili hili? Je, kila chombo cha habari kinajiamulia tu ratiba yake? Je, mnasema nini kuhusu usumbufu huu kwa wananchi?
 
Mfano hai ni clouds fm katika kipindi chao cha michezo kiitwacho sports extra kinachoanza saa tatu usiki huwa kinachelewa dakika zisizopungua tano au zaidi. Rfa nao wana kipindi cha uchambuzi wa magazeti saa kumi na mbili na nusu asubuhi nacho huchelewa kuanza
 
Mfano hai ni clouds fm katika kipindi chao cha michezo kiitwacho sports extra kinachoanza saa tatu usiki huwa kinachelewa dakika zisizopungua tano au zaidi. Rfa nao wana kipindi cha uchambuzi wa magazeti saa kumi na mbili na nusu asubuhi nacho huchelewa kuanza
Tanzania kila kitu ni vuluvulu TU, wako makini kwenye tozo TU lakini sio vile vinavyowaudhi wananchi. Serikali inajenga barabara ya mkopo kabla mkopo haujaisha inaibomoa ili kujenga barabara ya mwendokasi ya mkopo,
 
Back
Top Bottom