Hismastersvoice
JF-Expert Member
- Jan 26, 2013
- 18,678
- 22,266
Azam Tv imekua na tabia ya kutuibia wateja wa vifurushi vya Azam Tv, mteja ananunua kifurushi cha bei kadhaa na chaneli kadhaa kwenye kifurushi husika lakini kabla haujamaliza muda wa kifurushi husika Azam Tv wananyofoa baadhi ya chaneli ulizolipia, huu ni wizi na ni sawa na mwenye basi anayekatisha safari kwenye njia aliyopewa.
Nimelipia kifurushi cha shs.23,000/= kikiwa na chaneli nilizozihitaji 146 na 147 cha ajabu ghafla wahuni hawa wamezinyofoa! Tatizo hili lipo na tunapolalamika TCRA wanaziba masikio yao wasitusikie, kama kawaida mbele ya viongozi wetu mwarabu siku zote yuko sawa mbele ya mwafrika.
Licha ya wizi huu tumelalamika sana kuhusu uduni wa ving'amuzi na madishi yao lakini TCRA na Tume ya Ushindani hawachukui hatua yoyote kwani wanaona tunamsumbua mwarabu, sijui hali hii ya wizi itakwenda mpaka lini.
Nimelipia kifurushi cha shs.23,000/= kikiwa na chaneli nilizozihitaji 146 na 147 cha ajabu ghafla wahuni hawa wamezinyofoa! Tatizo hili lipo na tunapolalamika TCRA wanaziba masikio yao wasitusikie, kama kawaida mbele ya viongozi wetu mwarabu siku zote yuko sawa mbele ya mwafrika.
Licha ya wizi huu tumelalamika sana kuhusu uduni wa ving'amuzi na madishi yao lakini TCRA na Tume ya Ushindani hawachukui hatua yoyote kwani wanaona tunamsumbua mwarabu, sijui hali hii ya wizi itakwenda mpaka lini.