Salaam Wakuu,
Je, MwanaJF gani yupo Lupaso? Rais wetu Mpendwa yupo hapo? Naomba Aje PM nimuuize maswali Mawili.
Mimi nafuatilia Mazishi ya Marehemu Mkapa kupitia Online Youtube Channel ya JamiiForums.
Lakini Kilichonitia Wasiwasi na Mambo yanayoendelea pale Kanisani Lupaso. Kiti alichotakiwa...
Jana wakati Rais Magufuli anasoma hotuba ya Tanzia juu ya kifo cha Rais Mstaafu Benjamin William Mkapa, alizungumza mambo mengi mazito ambayo rais huyo aliyetutoka alilifanyia Taifa.
Kwa kweli Mkapa ameacha alama katika nchi hii, yeye ndiye aliyesuka engine ya Tanzania ya leo tunayoiona. Yeye...
IGP AWAONYA WALIOPANGA KUVURUGA SHUGHULI YA MAZISHI YA MZEE MKAPA
“Kama kuna watu wanataka kuiharibu hii shughuli yetu tutawashughulikia,” – Kauli ya IGP Simon Sirro akiwaonya wanaopanga kuvuruga shughuli ya mazishi ya Mzee Mkapa.
Ikiumbukwe mapema ya leo Vikosi vya Ulinzi na Usalama Vilizuia...
RAIS wa Tanzania, John Pombe Magufuli, amejikuta akitokwa machozi hadharani baada ya shindwa kujizuia wakati akielezea mazungumzo yake ya mwisho na Rais mstaafu awamu ya tatu, Benjamin William Mkapa. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam
Hilo limejitokeza leo Jumanne tarehe 28 Julai 2020...
Msafara wa Viongozi Wakuu wa CHADEMA, wakiongozwa na Mwenyekiti wa Chama Taifa, Mhe. Freeman Mbowe, wamezuiliwa kuingia Uwanja wa Uhuru walikokuwa wameenda kuhudhuria shughuli ya kutoa heshima za mwisho na kumuaga Rais Mstaafu wa Awamu Tatu, Hayati Benjamin William Mkapa.
Mwenyekiti wa Chama...
Nimesikiliza mambo ambayo Rais Magufuli anayasema kuhusu Mkapa binafsi naona Mkapa ni shujaa mkubwa mno wa Taifa hili maana alianzisha mambo muhimu mno mpaka sasa na sisi ambao wengi hatujui tulijua hayo yalianzishwa na Mwl. Nyerere au Mzee Mwinyi kumbe ni Mkapa, pia naona yale maubabe aliyokuwa...
Rais Magufuli amesema "Mzee Mkapa aliujenga uwanja mkubwa wa michezo. Wengi wanataka uitwe Mkapa Stadium. Alikuwa hapendi vitu viitwe kwa jina lake, lakini hawezi kuniadhibu amelala. Natamka rasmi uitwe Mkapa Stadium'
Serikali ya Burundi imetangaza siku 3 za maombolezo kufuatia kifo cha Rais mstaafu wa Tanzania Benjamin Mkapa. Kwa siku zote tatu Bendera zitapepea nusu mlingoti ikiwa ni kuanzia leo, jumatatu.
Anaandika Mo Dewji:-Leo nimeamua kuanzisha petition (maombi) kwa Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt John Pombe Magufuli kubadili jina la Uwanja wa Taifa kuwa: Uwanja wa Benjamin William Mkapa.
Amesema Itakuwa ni heshima kubwa kama uwanja wetu pendwa utaitwa jina la Uwanja wa...
Aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Tanzania, Bernard Membe amesema kuwa Rais wa Awamu ya Tatu, Benjamini Mkapa, alikuwa Kiongozi wa dunia, mshauri wa masuala ya Uchaguzi na kinara katika kulisaidia bara la Afrika kutatua migogoro bila kuchoka
Amesema siku zote Mkapa alikuwa anathamini akili...
Tukiwa katika Majonzi kuna watu wanataka kuvuruga msiba kwa lengo la Kutafuta umaarufu wa Kiasiasa msibani si mahali pake naomba Wakuu wa Vituo vya Staki Shari, Buguruni na Tazara msimamie hili hatuko tayari kuona mambo ya Kihuni yakijitokeza katika Taifa letu lenye tunu ya amani.
Kwa Vijana...
Nimefikiri na kujiuliza sana kwanini baadhi ya marafiki wa kizungu wanaonekana waziwazi kumtetea sana Lissu. Je, huyu Lissu amewaahidi kitu gani atakachowapa kutoka nchini kwetu ikiwa atachaguliwa na Watanzania katika uchaguzi wa mwaka huu kuwa Rais wa Tanzania, japo kiuhalisia Lissu kamwe...
Hii haivumiliki na GENTAMYCINE nasema tena kuwa hii haivumiliki na namuomba Waziri wa Michezo aamuru Jeshi la Polisi nchini Tanzania chini yake IGP upesi sana wamsake (wamtafute) popote pale alipo Kocha wa Yanga SC Raia Ubelgiji Luc Eymael kwa ‘ Matamshi ‘ ya Kuidhalilisha Tanzania na hadi Sisi...
Haya, leo mzizi wa uzushi umekatwa. Sababu ya kifo cha Rais mstaafu Mkapa imetajwa: ni mshituko wa moyo.
Licha ya hivyo, hicho sicho kilichompeleka hospitali.
Kilichompeleka hospitali ilikuwa ni kutojisikia kwake vizuri, ambapo baadaye ilikuja kugundulika kuwa ni malaria, kwa mujibu wa taarifa...
UTANGULIZI:
Kwa neema ya Mungu nimefanikiwa kuishi kwenye uongozi wa marais wote 5 wa nchi yetu hadi sasa nikiwa tayari na uwezo wa kuelewa kinachoendelea duniani (kwa sehemu). Kwa kuwa nina shahuku (enthusiasm) kubwa na uongozi na dhana nzima ya kutumikia watu (ambayo siasa ni sehemu yake)...
Mtia nia ya Urais kwa tiketi ya CHADEMA mh Lazaro Nyalandu amesema wakati wa utawala wa Rais Mkapa yeye alikuwa msaidizi wa Mama Anna Mkapa hivyo amesafiri sana huko Duniani na mzee Mkapa.
Nyalandu amesema hayo wakati akiweka saini kitabu cha maombolezo msiba wa mzee Mkapa.
Chanzo: ITV habari...
Ndugu Watanzania wenzangu
Kwa hakika Taifa letu limepoteza kichwa, kichwa makini sana kilichoacha alama katika nyumba hii ya maendeleo tunayoendelea kuijenga.
Rais Benjamin William Mkapa amefanya mambo mazito sana kwa nchi hii. Kwa kweli nchi hii ina afadhali leo hii kwa sababu alikuwepo mtu...
Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan amesema kifo cha Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa ni msiba mzito kwa Taifa na umekuja kwa mshtuko mkubwa kwasababu umetokea hakuna aliyetarajia au kutegemea
Amesema, "Hakuna aliyetarajia kwasababu kama tungesikia Mzee amelazwa anaumwa kwa wiki na tumekwenda...
Mwakilishi wa kudumu wa Tanzania kwenye Umoja wa Mataifa Balozi Kennedy Gastorn amesema kifo cha Rais mstaafu wa Tanzania Benjamin William Mkapa kilichotokea usiku wa kuamkia leo jijini Dar es salaam sio pigo kwa Tanzania tu bali kwa jumuiya nzima ya kimataifa.
Balozi Gastorn amesema kuwa...
Habari wakuu!
Huyu Makonda aliyesifiwa kukamata wauza madawa ya kulevya na kutikisa jiji na nchi aliongezewa ulinzi ghafla na Rais(serikali) mpaka pale hali ilipotulia.
Baadaye aliendelea kuwa na ulinzi kiasi kutoka Vyombo mbalimbali vya Ulinzi vya mkoa wa Dar es Salaam mpaka alipoachia...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.