Mwenyekiti na Rais wangu Magufuli lazima 'asemwe binafsi' kwakuwa 'aliongoza binafsi'. Lissu na wengineo wako sahihi katika kumtajataja

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Nov 25, 2010
6,135
17,802
Kuanzia kwenye Kampeni zake mwaka 2015, Dr. Magufuli alijipambanua kuwa ataongoza Serikali ya Magufuli na si Serikali ya CCM. Na akayasimamia maneno yake ya kwenye kampeni, baada ya ushindi wake, kwa maneno na vitendo. Aliita Serikali ni ya Magufuli na si vingine. Mbunge Mstaafu wa Kilwa Kusini na mtani wangu Suleiman Bungara alias Bwege alizungumzia suala hili Bungeni mapema sana. Msikilize hapa alipozungumza suala hilo Bungeni na hata 'kuisambaratisha' taarifa ya Waziri Jenista Mhagama.

cheka kidogo na huyu Mbunge anayejiita Bwege na hivi vituko vyake - Bing video

Dr. Magufuli, Rais na Mwenyekiti wangu wa CCM alisema na kutenda kadiri alivyoahidi kwenye kampeni na 'akawaambukiza' makada, viongozi wa chama na Serikali na hata wananchi wa kawaida kuwa hii iliyopo madarakani ni Serikali ya Magufuli. Kuna wakati Hayati Mkapa alikikosoa kitendo hiki cha 'kuhodhi' jina la Serikali. Ikasemwa na kutendwa kuwa Rais ametoa; Rais amechukua; Rais ameanzisha; Rais amejenga; Rais ametugawia na kadhalika. Akatamba Dr. Magufuli.

Sasa tumefika kwenye uchaguzi mkuu mwingine. Wapinzani wamekuja kivingine. Wanamtajataja binafsi Dr. Magufuli kwenye kauli zao. Wanakosea hadi wapigwe vijembe na Waziri Mkuu, Viongozi wa kidini na wengineo? La hasha! hawakosei. Wapinzani wanaendana na yaliyosemwa na kufanywa na hata makada wa CCM kwa miaka yote ya uongozi wa Rais Magufuli. Kama kila jema lililofanywa na Serikali sifa zinamiminwa kwa Rais Magufuli binafsi, kwanini kukosolewa ikosolewe CCM au Serikali kwa ujumla? Mkosolewaji abaki yuleyule msifiwaji.

Natarajia wakati wa kampeni jina la Dr. Magufuli litatawala vinywani mwa wapinzani kama lilivyotawala vinywani mwa makada katika kipindi hiki cha awamu ya kwanza ya uongozi wake. Mwenyekiti, Rais na Mtani wangu Magufuli akubali matokeo yaliyotokana na matukio. Ajibu mapigo kwa hoja za haja na kuonesha mazuri yake ambayo yamefanyika chini yake. Lakini, kuwakataza wapinzani-akina Lissu na wengine wasimtajetaje si dawa wala sahihi.

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa jijini Dodoma)
 
Msemeniii, mwisho wa siku mtamwita Mh Raisi wa Tanzania Ndg John Pombe Magufuli

Kwa sababu, yeye ndiye mshindi tena Kwa kipindi hiki kingine,

Kazi kwenu sasa, kumsema au kuacha, Kwa maana, umseme au usimseme, yeye ndiye Raisi atakayewekwa madarakani na Wananchi wengi na Kwa kishindo cha Hali ya juuuu!
 
1597834080599.jpeg
 
Kweli wazee wanaona mbali tuwaheshimu mfano maneno haya ya Mkapa, VUTA-NKUVUTE umefafanua vyema kabisa hawa makada wa chama Dodoma na Lumumba pamoja na wengine kama mawaziri, RC, DC , DED, RAS , wabunge wa CCM walivyomkabidhi kila kitu mheshimiwa Rais wametoa, itakavyompendeza, kutofuata katiba, ukweli anao yeye pekee yake tumuamini wakiongozwa na Polepole na Palamagamba..
.

5 Julai 2018
CCM ndio imekuweka madarakani, hii ni serikali ya CCM, sio yako "MZEE MKAPA"
 
Magu amekwisha shinda uchaguzi mapema.....
"Kwa mara ya kwanza Tanzania tunafanya uchaguzi kwa fedha za ndani" jaji Kaijage
Sijui amejuaje kama ni fedha za ndani au zinakuaga na alama??

Sasa kama pesa sa kusomeshea wanafunzi wetu tunasubiri hadi tupate msaada kutoka WB wa $300 milion halafu tunajisifu kugaramia uchaguzi kwa TZS 300 billion hivi hiyo ni akili au ni matope. Mambo mengine unasikiliza halafu unajiuliza hivi hizi promo mwisho wake lini. Hata chembe ya aibu hatuna. Yaani tunajisifia kugaramia uchaguzi unaofanyika mara moja kwa miaka mitano halafu jukumu la kusomesha watoto wetu tumewaachia WB wawe wanatupatia kila mwaka $300 milion halafu tunajisifu.
 
Magu amekwisha shinda uchaguzi mapema.....
"Kwa mara ya kwanza Tanzania tunafanya uchaguzi kwa fedha za ndani" jaji Kaijage
Sijui amejuaje kama ni fedha za ndani au zinakuaga na alama??

Jaji Kaijage, Nani kakuambia tunafanya uchaguzi kwa FEDHA za ndani?

Una uhakika ni FEDHA za ndani hadi utoke hadharani kutangaza kuwa tunafanya uchaguzi kwa FEDHA za ndani?

HIYO NI KAMPENI INAYOFANYWA NA TUME HURU YA UCHAGUZI.
 
Msemeniii, mwisho wa siku mtamwita Mh Raisi wa Tanzania Ndg John Pombe Magufuli

Kwa sababu, yeye ndiye mshindi tena Kwa kipindi hiki kingine,

Kazi kwenu sasa, kumsema au kuacha, Kwa maana, umseme au usimseme, yeye ndiye Raisi atakayewekwa madarakani na Wananchi wengi na Kwa kishindo cha Hali ya juuuu!
Ulishindwa nn kutuliza akili kwwnza,kisha ungemjibu mtoa mada huku akili ikiwa imetulia
 
Muheshimiwa Rais ametoa bilioni 2 kujenga uwanja wa ndege
Muheshimiwa Rais ametoa milioni 600 kujenga hospital ya rufaa ya mkoa
Muheshimiwa Rais ametoa bilioni 1 kujenga uwanja wa mpira
Muheshimiwa Rais ametoa bilioni 2 kujenga fire brigade
Na wala sio serikali imetoa.
 
Jina lenyewe bayaa kisha hataki litajwe !!! Magufuli!!
Bora likitajwatajwa limapungua kidoogo kutisha!
 
Msemeniii, mwisho wa siku mtamwita Mh Raisi wa Tanzania Ndg John Pombe Magufuli

Kwa sababu, yeye ndiye mshindi tena Kwa kipindi hiki kingine,

Kazi kwenu sasa, kumsema au kuacha, Kwa maana, umseme au usimseme, yeye ndiye Raisi atakayewekwa madarakani na Wananchi wengi na Kwa kishindo cha Hali ya juuuu!

Ila akili itamkaa vizuri, na kwa hiyo tabia yake ataiacha ccm ikizidi kuwa dhaifu. Hata bondia Mohamed Ali alikuwa anashinda mapambano, ila hata yeye ngumi alipigwa za kutosha, na madhara ya ngumi zile japo alishinda mapambano, yako wazi kwenye afya yake hivi sasa.
 
Ila akili itamkaa vizuri, na kwa hiyo tabia yake ataiacha ccm ikizidi kuwa dhaifu. Hata bondia Mohamed Ali alikuwa anashinda mapambano, ila hata yeye ngumi alipigwa za kutosha, na madhara ya ngumi zile japo alishinda mapambano, yako wazi kwenye afya yake hivi sasa.
Sawa Kaka, nakuelewa haswa!
 
Back
Top Bottom