chadema

CHADEMA (Chama cha Demokrasia na Maendeleo)
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ni chama cha kiasiasa nchini Tanzania ambacho kilianzishwa tarehe 28 Mei 1992 na mwanasiasa mkongwe Edwin Mtei, aliyewahi kuwa Waziri wa Fedha katika miaka 1997 hadi 1979.

Mwaka 2000 CHADEMA hakikuwa na mgombea wa Urais. Mwaka 2005 mgombea wa CHADEMA Freeman Mbowe alikuwa namba tatu kati ya wagombea kumi akapata asilimia 5.88 za kura.

Mwaka 2010 CHADEMA ilipata asilimia 27.1% na mgombea Urais wa chama Wilbroad Peter Slaa na kura 4,627,923 kwa 31.75%.

Hata hivyo CHADEMA imekataa matokeo mengi kutokana na mchakato mzima kuwa mikononi mwa Tume ya Uchaguzi isiyo huru.
  1. YEHODAYA

    GE2020 Felix Mkosamali Mgombea Ubunge wa CHADEMA atangaza biashara ya uwakili kinyume cha Maadili ya Uwakili

    Sera ya CHADEMA ni maendeleo ya watu sio vitu Wakili Felix Mkosamali Mgombea Ubunge CHADEMA Muhambwe ampinga Lissu na CHADEMA anadi sera ya maendeleo ya vitu kuwa hizo ndizo sera kinyume na Lissu anayepinga maendeleo ya vitu Wakili Mkosamali pia ametangaza biashara yake ya Uwakili kwenye...
  2. funaku

    GE2020 Membe akanusha kuiunga mkono CHADEMA, yeye ndiye Mgombea Urais wa ACT-Wazalendo

    Kupitia ukurasa wa twitter Ndg. Benard Membe amekanusha kujiondoa mbio za Urais na kumuunga mkono mgombea wa Chadema.
  3. A

    CHADEMA imekomaa na kuvuma mikoa mingi Tanzania

    Mwanzo CHADEMA ilikuwa inavuma Arusha na Moshi,baadae Mbeya na Morogoro kidogo,kwa kampeni za mwaka huu naona maeneo mengi ambayo sikuyatarajia naona hamasa kubwa za watu kuhudhuria mikutano ya CHADEMA,sasa hivi kila anapotembelea Lissu anavunja rekodi ya mkutuno uliopita. Leo Kagera naweza...
  4. Subira the princess

    GE2020 Sera ya majimbo sio ya CHADEMA, ilipendekezwa kwenye rasimu ya Katiba ya Jaji Warioba

    Wasalaam, Huwa inashangaza kwa mtu msomi mwenye akili timamu anapoamua kwa makusudi kupotosha jambo lenye maslahi kwa umma, ambalo linatambulika vema kwa jamii husika. CCM wameparamia kujibu hoja Lissu kuhusu sera ya majimbo eti tutarudi enzi za ukoloni, ukiisoma rasimu ya katiba ya Warioba...
  5. Erythrocyte

    GE2020 Yaliyojiri kwenye kampeni za Mgombea Urais wa CHADEMA, Tundu Lissu Mikoa ya Kagera na Geita

    Wakuu natanguliza salamu na baada ya salamu naingia moja kwa moja kwenye mada, kama mnavyojua Kampeni zinaendelea na leo tena Mh Lissu ambaye anapewa asilimia kubwa kutwaa urais wa nchi atakuwa kwenye mikoa ya Kagera na Geita, katika kanda hii kunatarajiwa kupigwa mkutano maalum wa kipekee...
  6. funaku

    Kukosekana kwa Sura mpya za Wagombea ubunge CHADEMA kunaashiria kutokubalika

    Mwaka 2010 na 2015 Chadema ilifanikiwa kupata wagombea ubunge wengi ambao ni ingizo jipya. Mwaka huu sijasikia kamanda mpya anayetajwatajwa kujiunga na Chadema na kugombea ubunge. Kwa upande wa CCM wapo wagombea wengi wenye influence na ni damu mpya itakayoleta chachu ya majadiliano bungeni.
  7. J

    GE2020 Mzee Lukanga anaisambaratisha CCM Mwanza. Amekuwa kivutio cha kampeni, na msafisha njia kwa wagombea wa CHADEMA

    Mzee Lukanga anazungumza mambo magumu kwa njia na mifano rahisi kueleweka. Anafafanua masuala mazito kwa namna ambayo msikilizaji hawezi kusahau. Wakati mwingine kampeni za siasa hazihitaji watu maarufu wenye visomo vikubwa, bali watu wakaida kama Mzee Lukanga.
  8. Sadock Kabuko

    Sera za CCM dhidi ya Sera za CHADEMA

    Nimekuwa nikifuatilia kampeni za CCM na CHADEMA, kuna utofauti mkubwa sana wa sera kati ya CHADEMA na CCM, Sera za CCM imejikita kueleza yafuatayo kwa wananchi 1. Kujenga miundo mbinu wezeshi kumrahisishia mwananchi kufanya shughuli zake kwa urahisi mfano. barabara, ujenzi na upanuzi wa...
  9. M

    GE2020 Yaliyojiri kwenye Kampeni za Mgombea Urais wa CHADEMA, Tundu Lissu mikoa ya Kigoma na Kagera

    Mgombea Urais wa Tanzania kupitia CHADEMA, Tundu Lissu Jana ameingia Kigoma kwa kishindo kikuu. Alilakiwa na Maelfu Elfu ya watu waliojipanga majiani huku wakitandika mikeka chini shujaa huyo wa karne hii apite juu yake. Akihutubia umati mkubwa unaokadiriwa kuwa na watu zaidi ya Elfu 30 katika...
  10. YEHODAYA

    GE2020 Kitengo cha habari cha CHADEMA wanyoosha mikono juu, waeleza tu mafuriko ya wanampokea Lissu si alichosema sababu hakipo

    Vyombo vingi vya habari viliacha kabisa kuandika au kutangaza habari za mikutano ya kampeni ya Tundu Lissu baada ya kuona hawaoni waandike nini kwani hanadi sera Sasa Kitengo cha habari cha CHADEMA pia wamenyoosha mikono juu wanaeleza tu sana mafuriko ya wanampokea Lissu sio alichosema sababu...
  11. funaku

    ‘Lobbying’ ni kazi muhimu ya kibunge ambayo Wabunge wa CHADEMA waliishindwa

    Moja ya kazi muhimu sana ya Mbunge ndani ya bunge ni kufanya lobbying yaani kushawishi ili mradi au maendeleo flani yafike jimboni mwake na sio ulalamishi. Katika hili wabunge wengi wa upinzani walifeli sana tofauti na ilivyokuwa kipindi cha nyuma. Wabunge wote wa Chadema waliopita walionesha...
  12. Dam55

    Hongereni vijana wa chadema kwa aina hii ya kampeni

    Watu kama hawa ni haki yao kutafuna Ruzuku ya chama hapo badae wamefanya kazi kubwa sana wapewe heshima yao. Note: ni burudani na vituko tu vya kampeni.
  13. MIMI BABA YENU

    GE2020 Viongozi wetu wa CHADEMA Kanda ya Magharibi, mkoa wa Katavi na Wilaya ya Mlele hujuma mlizomfanyia Tundu Lissu kwa sababu tu ya pesa hazikubaliki

    Jana Tarehe 18/09/2020 Mgombea wetu wa Urais Tundu Lissu alikuwa na ratiba ya kufanya Kampeni katika Mkoa wetu wa Katavi maeneo ya Majimoto katika jimbo la Kavuu Wilaya ya Mlele na Mpanda MJINI katika jimbo la Mpanda. Hakika viongozi wetu (Musa Masanja Mwenyekiti wa CHADEMA Kanda ya Magharibi...
  14. J

    Tundu Lissu anastahili kuwa Mwenyekiti wa CHADEMA lakini siyo Rais wa Tanzania

    Nimefuatilia kwa karibu harakati za wakili msomi Tundu Lisu tokea aingie nchini kutoka Ubelgiji hadi sasa anapogombea urais wa JMT. Kiukweli ingependeza sana kama Tundu Lisu angekuwa ndiye mwenyekiti wa CHADEMA kwa sababu anamzidi sana Freeman Mbowe kimaarifa na kwa kukubalika. Lakini kwa...
  15. GENTAMYCINE

    Kama wana CHADEMA 'wanaozunguka' kuomba 'Kura' za Halima Mdee 'Kawe' wana 'Udhaifu' huu, basi 'namtabiria' Askofu Gwajima Ushindi asubuhi tu!

    Jana nilibahatika Kukutana na wana CHADEMA baadhi ambao nadhani ( nahisi ) walipewa 'Jukumu' la Kupitapita Kawe hasa katika 'Nyumba' za Watu na Kumuombea 'Kura' Mgombea Ubunge CHADEMA Halima Mdee. Sina tatizo na 'Mbinu' yao hii ila GENTAMYCINE nina tatizo Kubwa sana na 'Competence' ya hawa wana...
  16. Q

    Bernard Membe: ACT - Wazalendo na CHADEMA tunaongea ili tusimamishe mgombea mmoja

    Ndugu zangu najua mtakuwa mnanishanga . kila kukicha ukweli ni kwamba bado ACTwazalendo wanaongea na CHADEMA tuweze kuwa kitu kimoja, lakini hadi sasa mambo ni mazuri na kama mnavyo ona hi graph ndivyo mdogo wangu @TunduALissu atakavyo shinda kama wa Tanzania, tukiamua. - Bernard Membe
  17. S

    GE2020 CHADEMA imeshanyakuwa miji mikuu yote katika kila mkoa, hauhitaji darubini kuuona ukweli

    Kila alipopita Mgombea wa Urais wa CCM akipita wa CHADEMA mahudhurio wananchi waliofikia umri wa kupiga kura inakuwa ni mara mbili,Ni ukweli usio pingika ambao utadhihirishwa kwa usahihi zaidi siku na baada ya upigaji kura na kura kuhesabiwa. Unajua Mheshimiwa Magufuli chama chake kinawavutia...
  18. V

    CHADEMA, Corona imekwisha?

    Na Victor Yohana (uvccmichenjezya@gmail.com) Mapema mwaka huu tulitangaziwa kuwa Dunia imeingiwa na ugonjwa wa CORONA. Tanzania ilikuwa nchi moja wapo ambayo ilishukiwa kuwa kuna watu wana dalili za virusi vya CORONA alimaarufu COVID -19. Wakati Dunia ikiendelea kutafuta tiba, Tanzania ilikuwa...
  19. Erythrocyte

    GE2020 Yaliyojiri kwenye kampeni za Mgombea Urais wa CHADEMA, Tundu Lissu Mkoani Katavi na Kigoma, azungumzia Katiba Mpya

    Wakuu nawasalimu kwa salamu ya Ukombozi , leo tena Mh Lissu anaendelea kuwatembelea Watanzania wenzake kwa lengo la kuwaomba ridhaa ya kupewa kura ili awe Rais wa Tanzania , mikutano ya leo itapigwa Mkoani Katavi na Kigoma . Endelea kubaki hapa hapa JF kwa habari za uhakika. ---- Napenda...
  20. Analogia Malenga

    Afisa maudhui CHADEMA kizimbani

    Afisa Maudhui wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Dominic Mgaya amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, kwa kosa la kuchapisha maudhui mtandaoni bila kuwa na leseni ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA). Akisoma hati ya mashitaka mbele ya Hakimu Mkazi...
Back
Top Bottom