LEMA, SUGU WAMPONGEZA DKT. SAMIA KUUNDA TUME YA KUCHUNGUZA UVUNJIFU WA AMANI
Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA, Godbless Lema na Mwenyekiti wa CHADEMA kanda ya Nyasa, Joseph Mbilinyi maarufu Sugu wamempongeza Rais wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuunda Tume Huru ya Uchunguzi wa Matukio ya Uvunjifu wa Amani yaliyotokea wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu uliofanyika tarehe 29 Oktoba 2025.
Viongozi hao wamesema hatua hiyo inaleta mustakabali mzuri wa Taifa kurudi katika umoja na Rais Samia amejibu kilio cha Wana-CHADEMA na kuwakemea wachache wanaotaka kuvuruga amani.
“Alichofanya Rais Samia ni hatua kubwa sana, Jumuiya za Kimataifa zinapaswa kumpongeza. Sisi Chadema tunaona kile tulichokipigania anakifanya kwasababu tunataka...