KWELI Hii picha imepigwa Posta, Dar es Salaam

KWELI Hii picha imepigwa Posta, Dar es Salaam

Taarifa hii imethibitika kuwa ya kweli baada ya kufanya tathmini ya kina
Image.jpg
 
Tunachokijua
Uhakiki wa Picha kwa kutumia Reverse Image Search ni njia muhimu ya kubaini asili au maelezo zaidi kuhusu picha fulani.

JamiiCheck imekuandalia utaratibu wa hatua kwa hatua wa jinsi ya kutumia Nyenzo hii kufanya uhakiki wa picha. Rejea kiungo hiki kufuata hatua zote.


Mfano picha hii inayoonesha eneo la mji lililopo pembezoni mwa fukwe za chanzo cha maji. Je, ilipigwa wapi na lini?

Uhalisia

Jamiicheck imejiridhisha kuwa picha hiyo ni halisi ambapo kupitia Google Reverse Image Search imebainika picha hiyo ilichapishwa katika tovuti ya Pinterest Juni 09, 2015 na ueleza kuwa ni muonekano wa Dar es salaam miaka ya 1970.

Kadhalika picha hiyo imewahi kutumiwa na tovuti ya The Citizen katika moja ya makala yake iliyoitwa "Tanzania in the 1970s: A difficult decade" na kueleza pia kuwa muonekano wa Dar es Salaam miaka ya 1970.

Aidha pichani linaonekana kanisa lenye mnara mrefu ambalo linafanana kabisa na kanisa kuu la Mtakatifu Joeseph Posta Dar es Salaam. Rejea hapa kwenye ramani kuona lilipo kanisa hilo.​
1780480770692-png.3600470
Hii ni stone town Zanzibar
 
This historical photo depicts a view of the harbor and coastline in Dar es Salaam, Tanzania, during the 1970s.

The prominent church tower visible on the right is the Roman Catholic Cathedral.

The image captures the waterfront area, including Sokoine Drive, as it appeared in that era..
 
Hii picha ni Tanga, Tanzania mkuu 📍

Hii ni picha ya zamani sana - postcard ya miaka ya 1960s/70s hivi. Unaona:

1. Kanisa la juu lenye mnara mkali
Hilo ni Kanisa Kuu la Mtakatifu Antoni - St. Anthony's Cathedral. Ndio alama kubwa ya Tanga hadi leo. Mnara wake unaonekana kutoka mbali.

2. Barabara ya pwani
Hiyo ni barabara ya Mkwepu/Indian Ocean Drive. Upande wa kushoto ni Bahari ya Hindi. Miti iliyopangwa kando ya barabara ndio utamu wa Tanga.

3. Bandari ndogo
Sehemu ya bandari ya Tanga inaonekana upande wa kushoto. Tanga ilikuwa bandari muhimu sana zamani kabla ya Dar kuongezeka.

Tanga ni mkoa wa pwani kaskazini mwa TZ, mpaka na Kenya. Inajulikana kwa hewa safi, miamba, na majengo ya zamani ya kikoloni ya Kijerumani na Kiingereza.

Umeipata wapi picha hii? Ni ya baba/bibi yako? Tanga kuna kitu maalum kwako mkuu?
 
Back
Top Bottom