Kuna huu uzi nimukutana nao umenikumbusha nilikua mdogo nilikua naambiwa sana stori za uwezo wa Kondoo kupambana na Radi,
Hapa stephot kwenye uzi wake alisema "kuna kipindi nilipokuwa likizo nilitembelea mikoa ya Dodoma, Singida, Manyara na Arusha, nilichokigundua ni kuwa wafugaji karibu wote wa Ng'ombe wanakuwa na kundi la Kondoo, nilipouliza niliambiwa kuwa Kondoo wanasaidia kuzuia Radi. Mwenye ufahamu wa kina naomba anifafanulie utaalamu uliopo nyuma ya hii kitu"
Sasa JamiiCheck mtusaidie kuna ukweli hapa?