Zitto: Ndio ninautaka urais

Zitto: Ndio ninautaka urais

Status
Not open for further replies.
Ukiangalia kwa undani sana,ukithink BIGF as a great5 thinker,utagundua kuwa CCM wanamuogopa sana Dr Slaa, wanajua kuwa kama akigombea 2015, wataface upinzani mkali sana,zaid ya hata ule wa 2010,wanajua kabisa CDM wanaweza kuchukua dola (Naliombea hilo kila siku),wanajua kabisa kuwa Mtu atakayegombea urais na kuwalaza usingizi kimsingi si mwingine zaid ya Dr Slaa, now wanamtumia Zitto, ama kwa kujua au kutokujua kumpinga Dr Slaa ndani ya chama, hii technique ya CCM watu wanaweza wasii note, lakini woga wa CCM kwa Dr Slaa unakuwa revealed na Matamshi kama ya kina Zitto, hope CDM are smart enough to notice this...
Najua Zitto ana Fans wengi hapa JF ambao ama kwa kujua ama kutokujua watajikuta wanaingia katika mtego huu wa CCM kupitia Zitto.
THIS IS THE PAINFULL TRUTH TO ACCEPT

Acha unafiki usiokuwa na ukweli kama unaushahidi Mh Zitto anatumika na CCM tumwagie kuliko kuweka majungu isitoshe nae ni mtanzania anayo haki ya kugombea endapo atakuwa anavyo vigezo,wewe hutaki agombee kwa kuwa wewe ni mfuasi wa Mbowe umakundi ndani ya chama unasumbua kweli kweli kama hipo hipo tu hakuna wa kubana ndoto za Mh Zitto mungu kama kapanga hakuna wa kuzuia!
 
Achana na wanafki, hivi inawezekana vipi jitu linashinda jukwaa la siasa siku zote halafu akwambiye hana chama anachokiunga mkono!!.....huu ni utoto, na kuna mwingine anaitwa Mohamed Shossi tangu CUF ife eti naye anajifanya hana chama wanafki wakubwa hawa!!


Alaaa kumbe nilikuwa CUF sina habari hiyo ndio naipata kutoka kwako enh kadi yangu ya uanachama ninamba ngapi?
 
Alaaa kumbe nilikuwa CUF sina habari hiyo ndio naipata kutoka kwako enh kadi yangu ya uanachama ninamba ngapi?
Kweli itakuweka huru mkuu.... hapa sana sana unaidanganya nafsi yako tu, kila member anayekuja hapa jukwaani ana mapenzi au anakisapoti chama fulani, ni unafki wa hali ya juu kusema huna upande, na wewe ni mwislamu nenda kasome vizuri kitabu unachokiamini Koran uone kinasema nini kuhusu wanafki halafu ndio urudi hapa kukanusha kama wewe hauna mahaba na CUF.
 
2005 ulikuja upepo wa vijana na mara wakasema wamepata kijana tena mtanashati na mchangamfu. amekaa ikulu sasa mnalia na hali ngumu ya maisha hata u handsome wake mmeusahau. sasa mnaleta issue ya ujana tena eti umri upungue na Zitto apewe nchi. Mh......

Kama vigezo vya uraisi ndo hivi vya Mh. Zitto basi JK aendelee kuongoza miaka 20 zaidi.
Angalau tunajua JK ni mzembe wa kuwahukumu washkaj zake japo nia anayo. ni mapungufu yake kibinadam ila Mh. Zitto ana asili ya unafiki na kama hamauamini mpeni nchi tu japo kwa mwaka mmoja kama hatujakimbilia Burundi.
 
Jamani kwani kuongea ndo kua!, hebu tuache jazba na tujadili mambo ya msingi,Kama kwa nini sasa kilo ya mchele ni sh.2500/-,lita moja ya mafuta ya petrol ni 2144,Mbona bei ya bia imepanda mnaanza kujadili mada za vichaa wanaotaka urais mwaka 2015?!
 
Alliance ndani ya the same part, same slogan,the same vision, the same mwenyekiti,why all that for?Sijapata kusikia Alliance ndani ya chama kimoja,nimeshuhudia alliance kiaina ndani ya CCM ikabatizwa jina MTANDAO [NETWORK] madhara yake tiba yake mpaka leo ndio ugonjwa unaotka kuitia CCM matatizoni.
Ni maajabu sana kuwasoma watu waki question alliance ndani ya vyama wakati hawa hawa hawamkubali Zitto mwanachama mwenzao na hivyo kuunda kundi dhidi yake. Ningependa sana watu wanaopinga mgawanyiko ndani ya chama waonyesha wenyewe mfano kwanza na sio kupinga mtazamo wa mtu mwingine kwa sababu tu hakubaliani na mtazamo wao na wakifanya yale yale wanayo yalaani.
 
Tatizo ni katiba yetu,haya mazee yalijitengenezea kinga mapema, ukianagalia walikuwa mawaziri wakiwa na miaka 20 yaka weka ngao,mpaka leo mawaziri pambafu zao tunatakiwa kuondoa hiyo kitu,
 
Kweli itakuweka huru mkuu.... hapa sana sana unaidanganya nafsi yako tu, kila member anayekuja hapa jukwaani ana mapenzi au anakisapoti chama fulani, ni unafki wa hali ya juu kusema huna upande, na wewe ni mwislamu nenda kasome vizuri kitabu unachokiamini Koran uone kinasema nini kuhusu wanafki halafu ndio urudi hapa kukanusha kama wewe hauna mahaba na CUF.

Mi nasapot chama gani? Ni fikra lemavu kudhani kila mtu hapa anachama among the current parties, wengine Tuko Njee ya hizi petty parties. Fikiri
 
Jamani hebu tujadilini ugumu wa maisha,mwaka 2015 hakuna mgombea wa Urais mambo yakiendelea hivi lazima mapinduzi yatokee period. Ngoja nikapate kiroba kwanza.
 
Zitto siyo kuwa hajakoma, ana haki na kakomaa, hebu fikilieni wanajamvi hivi mnakumbuka marais wa nchi hii, mbona wengine Zitto keshawashinda vigezo? Labda umri lakini mambo mengine yuko juu yao, Kwa hekima hebu pima kati ya Zitto na Mkapa!!
Kila siku huwa nasema Zitto hafikirii mbali na anapenda masifa ya kipumbavu lakini skeleweki. Huyu Zitto ni pandikizi la CCM ambalo limejificha. Muulizeni nyumba na gari alizohongwa na Nimrod Mkono zilikuwa zawadi za nini? Ama yeye Zitto kapata nafasi katika moyo wa Nimrod?

Tunahangaika na kampeni Arumeru, huku Tundu Lissu kabanwa makusudi, Mnyika yaleyale, sasa tumepapasa na kuishia kukosea kumleta Mdee maana na yeye katekwa na siasa za chooni 'toilet politics', Zitto kama kiongozi wa juu kabisa CDM hakupaswa kuwa ngumbalu kiasu hicho, ni
afadhali angejikita ktk harakati za kampeni Arumeru kuliko kuhojiana ujinga na akina Kibonde wa "Clouds CCM 2" ambao wanasikilizwa siku hizi na wavuta bange maana wenye akili zao hawawezi kupoteza muda kusikiliza upuuzi wa Jahazi.

Zitto wakati Kikwete akienda kutalii south sudan siku zile inajitenga na kutambuliwa rasmi alikuwa bega kwa bega na Kikwete, na nakumbuka Kikwete alisema 'anatamani kama rais ajaye atakuwa kijana'. Sasa hivi ni mjinga gani atakayempa kura Zitto anayezungukwa na mashutuma lukuki yakiwemo ya umalaya uliokubuhu! Mods nivumilieni nimpe ukweli wake.

Hivi toka lini mroho wa madaraka kama Zitto akawa mzalendo!? Ndio maana nawaaminisha wana jf kwamba zitto ataiua CDM kabla ya 2015, nasema haya kwa kuwa moja kama huyu ndumilakuwili na mnafki atafukuziwa mbali atoke chadema basi chama kitapoteza wanachama wajinga wengi wengi na itakuwa too late kujijenga kama ilivyo sasa, pili kama Zitto akiachwa basi hili ni timing bomb siku zikikaribia 2015 atajilipua mwenyewe ili kuimaliza CDM na hapo CDM itabakia at the footnotes of political history, na mwisho kama mnafki huyu akinyamaziwa muda huu atajijenga na atazidi kuropoka maujinga na CDM itakuwa vulnerable kuliko kuda wowote.

Mwenye hekima na asome mawazo haya na ayatambue, haya ni ya kisiasa na hekima tu, na tafsiri yake ni ya kihistoria, someni nyakati.

Ni mimi Pangu Pakavu,
Nimerudi kivingine,
Nawasalimia.
 
Kila siku huwa nasema Zitto hafikirii mbali na anapenda masifa ya kipumbavu lakini skeleweki. Huyu Zitto ni pandikizi la CCM ambalo limejificha. Muulizeni nyumba na gari alizohongwa na Nimrod Mkono zilikuwa zawadi za nini? Ama yeye Zitto kapata nafasi katika moyo wa Nimrod?

Tunahangaika na kampeni Arumeru, huku Tundu Lissu kabanwa makusudi, Mnyika yaleyale, sasa tumepapasa na kuishia kukosea kumleta Mdee maana na yeye katekwa na siasa za chooni 'toilet politics', Zitto kama kiongozi wa juu kabisa CDM hakupaswa kuwa ngumbalu kiasu hicho, ni
afadhali angejikita ktk harakati za kampeni Arumeru kuliko kuhojiana ujinga na akina Kibonde wa "Clouds CCM 2" ambao wanasikilizwa siku hizi na wavuta bange maana wenye akili zao hawawezi kupoteza muda kusikiliza upuuzi wa Jahazi.

Zitto wakati Kikwete akienda kutalii south sudan siku zile inajitenga na kutambuliwa rasmi alikuwa bega kwa bega na Kikwete, na nakumbuka Kikwete alisema 'anatamani kama rais ajaye atakuwa kijana'. Sasa hivi ni mjinga gani atakayempa kura Zitto anayezungukwa na mashutuma lukuki yakiwemo ya umalaya uliokubuhu! Mods nivumilieni nimpe ukweli wake.

Hivi toka lini mroho wa madaraka kama Zitto akawa mzalendo!? Ndio maana nawaaminisha wana jf kwamba zitto ataiua CDM kabla ya 2015, nasema haya kwa kuwa moja kama huyu ndumilakuwili na mnafki atafukuziwa mbali atoke chadema basi chama kitapoteza wanachama wajinga wengi wengi na itakuwa too late kujijenga kama ilivyo sasa, pili kama Zitto akiachwa basi hili ni timing bomb siku zikikaribia 2015 atajilipua mwenyewe ili kuimaliza CDM na hapo CDM itabakia at the footnotes of political history, na mwisho kama mnafki huyu akinyamaziwa muda huu atajijenga na atazidi kuropoka maujinga na CDM itakuwa vulnerable kuliko kuda wowote.

Mwenye hekima na asome mawazo haya na ayatambue, haya ni ya kisiasa na hekima tu, na tafsiri yake ni ya kihistoria, someni nyakati.

Ni mimi Pangu Pakavu,
Nimerudi kivingine,
Nawasalimia.
Hivi ni nani asiye Mroho wa madaraka Chadema?
 
Hehehee haya bwana!
Mwambie kuna watu wanaitwa Pelle Tanzania kwani wanausiano na Pelle wa Brazili,mwambie yaweza kuwa mzazi wako alilipenda jina la Nyerere akakuita,kama nyerere alivyolipenda jina la madaraka day akamuita mwanae madaraka.Au anashanga ilo akashangae jina Gauncho Usiwamini Waongo ilo jinandani Kisanga Msangule Kisalawe Pwani,wakati mwenye jina Gaunch yuko Brzailia.

Majina anataka kujua kwani anataka kutambika.
 
Zitto kwa Sasa Ana weweseka...ka change sana.. kitu kinachomfanya watu wengi wakose imani nae! Uyu dogo amesha sahau alipotoka anaropoka tuu, bila ata ridhaa ya chama chake..hatafika mbali Uyu mtu..
 
Aisee kwa kweli sijajuwa ni kwa nini unatumia nguvu nyingi sana kwa jambo ambalo liko wazi, hapa hoja sio umri wa mgombea Urais bali hoja ni nani mwenye sifa za kuwa Rais bila kujali umri wake, ndio maana tunasema ikulu hakuna mashindano ya urijali kusema wanaitajika vijana tu.

Ni hivi hatuwezi kutengeneza katiba ya kumfurahisha Zitto Kabwe wala January Makamba, tunatengeneza katiba ya kutupeleka miaka 50 ijayo kwahiyo hata ikionekana umri wa Urais uwe ni miaka 20 is fine lakini hatumtengenezei mtu katiba ili apate fursa ya kugombea, why don't u think out of this box?......

Mbona umri wa vijana kugombea ubunge hauwazuii lakini kuna vijana kiasi gani wanaoleta angalau positive results katika ubunge wao? sijasahau ni juzi juzi tu hapa Lawrence Masha aliaminiwa na Rais kupewa wizara nyeti na nzito kwenye nchi na matokeo yake kila mtu anajuwa, halafu leo hii uje kwa mtu makini na gia za ujana sidhani kama atakuelewa labda Adam Malima ndio mtaelewana katika hoja hizi mufilisi.

Tatizo lako unaangalia majina ya watu.Huangalii logic,tukienda hivi hata katiba mpya ibadilishwe tutakuwa tunatwanga maji kwenye kinu tu

Unatoa mfano wa vijana walioshindwa? Unaweza kuongelea ufanisi katika bunge la Tisa na bunge la kumi kwa kuzingatia Ratio ya wazee na vijana na kuweka share katika ufanisi huo?

Mkuu,unashindwa kuelewa hata katiba ya chama chetu inatambua vijana ni taifa la leo?Tuache kuwa na mawazo ya ki-CCM.mbona wenzetu kenya kwa muda mrefu umri wa kugombea ni mika 35 na hajapatikana kijana wa umri huo so far?Hofu yetu ni nini hasa? Natumia nguvu nyingi?Mimi ama ninyi?
 
"Ndio Uraisi ninautaka" Zitto Zuberi Kabwe.
Kauli hii imepokelewa ama kwa furaha au kwa mshangao inategemea wewe unafikiri vipi. nimesoma mara kadhaa habari ya Zitto ili kujaribu kuelewa nini alimaanisha. Aliandika habari yake vyema na alijenga hoja zake kwa umakini mkubwa, hakuonyesha ni lazima ila alionyesha nia yake.

Maendeleo yanapatikana kwa kutaka kufika juu kama ni biashara lazima utamani kumfikia mwenye fedha nyingi, kama ni vyeo utatamani kuwa CEO na kama ni siasa utatamani kuwa Raisi hayao ndiyo mafanikio na ni matamanio ya kila mwenye utashi wa kuishi na kufanikiwa ndivyo wanaoshinda huwa hufikiria juu na mbali sana.

Furaha ya kundi moja ni kwamba kijana anaonyesha nia na wako nyuma yake, wanatamani siasa zitawaliwe na vijana shupavu, mahiri na wenye upeo elimu na ujuzi wa hali ya juu. kundi hili linakwenda na siasa za wakati huu ambapo dunia imekuwa kama kijiji.

kundi la pili linaona huu ni mshtuko na sio wakati muafaka. kundi hili linaendeshwa na busara hekima na uzoefu, linaaminbi timing ndio kila kitu. Kundi hili linaamini kujenga base kuwa na wanachama kukuza chama na kuonyesha uchapakazi kukubalika kwa wananchi na kujishughulisha kukuza demokrasia na kuongeza wanachama ili kuweza kupata kura za mtaa, udiwani, ubunge halafu uraisi.

Kundi jingine ni lile lisilopenda mabadiliko wala mawazo mapya. Kundi hili linaogopa kila kitu linaona ni hatari kujaribu kusema au hata kutamani. Kundi hili linahodhi likiwa na mashaka.

Kundi la nne ni wale wasio mtakia mema yeyote, watakushauri vibaya, watakudanganya watakushangilia ukianguka na watakuacha kwa kukuona hamnazo.

kundi la mwisho ni lile linalotumia watu ama kujenga au kuharibu.

Matamko ya Bwana Zitto yanaweza kuwa yana mashiko au la. Siasa za Tanzania za vyama vingi bado ni changa. Chadema ni chama kinachokuwa kwa kasi sana, kipindi hiki kinakumbana na changamoto nyingi. Chama chenye wabunge 48 wa kwanza kwa wingi kinahitaji msikamano mkubwa sana kwa viongozi wake na utendaji. Ukijaribu kusoma akili za wale wanaoogopa matamko ya kuwania ubunge, Uraisi kabla ya wakati mapema sio kwamba hawataki watu kupenda kugombea la hasha, demokrasia ya kweli inahitaji ushindani wa ndani ili kuweza kujenga watu mahiri.

Tatizo la matamko linaogopesha wengi ndani ya vyama vya siasa kwani kutokana na mfumo wa siasa zetu unaweza ama kujenga chama au kukibomoa kwani ili kuwania uongozi ni lazima upitie ndani ya chama, kutangaza nia mapema kunajenga makundi kwani inawezekana wapo wengi wenye nia hiyo. Kazi ya kujenga chama inakufa inabakia kazi ya kila kundi kujijenga na kusahau kura ni wanachama.

Sina tatizo lolote na kutangaza nia au kutamani ili timing is everything. Je unahitaji kura za watu, je unahitaji mtando mzuri wa chama ili kushinda? kama haya ni kweli kwa nini tusijikite kujenga chama na kujenga kukubalika ndani ya chama ili wakati ukifika iwe rahisi kupata kura za ndani au kuwa na mvuto kwa wapiga kura?

Ikumbukwe elimu ya uraia, na elimu ya siasa na uchumi nchini bado changa sana, siasa zetu bado zinaendeshwa kwa mipasho wananchi bado hawajapata elimu ya kutosha kuweza kuchambua sera, mfumo wa chama, misimamo ya chama na weledi wa mgombea. Ni siasa za sahani na skafu, kitenge na kanga mwenye fedha anashinda. Siasa amabzo bado wananchi wanaelewa taratibu sana kuwa kura zao ndio maendeleo yao kama maji, barabara, umeme, hudma bora za afya na ulinzi wa rasilimali zao. Siasa ambazo bado mwananchi anamshangilia fisadi, mhujumu, mwizi, mvivu ilimradi tu kaweza kuiba na kumnunulia sahani ya ubwabwa.

Kizazi kipya kinakazi kubwa sana ya kubadili siasa hizi. Badala ya kupambana na wazee kuwaona wamechoka lazima tujue muda na mazingira ndio yanawatesa. wapo wazee wenye busara na wapo walioweka busara zao matumboni kama kwa vijana wapo wote. Ni vyema kabla ya kufanya maamuzi yeyote kutumia busara debate your ideas make sure to explore every possibilities and outcome.

Zitto amejitahidi sana kuwafanya vijana wengi kuvutiwa ndani ya siasa za sasa, anawajibu wa kulinda mtaji wake. Siasa ni muda, huwezi kufananisha siasa za USA na Tanzania au UK na TZ. Ndio unaweza kutumia baadhi ya mambo ila huwezi copy.

Nafikiri tungejikita kujenga Chama kwanza, hakuna anaweza kushinda uchaguzi bila kujenga chama na mtando mzuri. Kama kauli hizi zinamanufaa kwa watoa kauli waendelee kuzitoa, kama zinawasaidia kufikia lengo sawa. Ila kama kauli zinaleta tafrani na kudhoofisha chama watoa kauli wajipime na waamue. Ninaamini kuwa ni haki ya kila mtanzania kugombea cheo chochote cha kisiasa na ni haki yaki kutangaza muda wowote ule anaotaka. Ila ninaamini ni watu makini tu wanapima na kujua wakati madhara na kijinsi ya kufika watakako.

Ni mimi
kinepi wa kinepi.
 
Huyu kijana ana ujasiri wa aina yake! "NDIO, NATAKA KUWA RAIS"
Uzuri wa kujiwekea malengo makubwa ni kwamba hata usipoyafikia hautakuwa mbali sana. Naamini Taifa hili litaendelea kunufaika sana na michango ya Zitto kupitia nafasi mbalimbali anazopata, iwe direct or indirect.
Go Zitto
 
Hivi ni kata ngapi ambapo CDM imesimamisha wagombea wake na maendeleo ya kampeni kwenye kata hizo yakoje kuelekea uchaguzi mdogo Jumapili? Viongozi wa CDM wanafanya nini kuwavutia wanaCCM ambao hawajafurahia chaguo la Siyoi kuwa mgombea ili wabadilishe kura zao na kumpigia Nassari?
 
Hivi ni kata ngapi ambapo CDM imesimamisha wagombea wake na maendeleo ya kampeni kwenye kata hizo yakoje kuelekea uchaguzi mdogo Jumapili? Viongozi wa CDM wanafanya nini kuwavutia wanaCCM ambao hawajafurahia chaguo la Siyoi kuwa mgombea ili wabadilishe kura zao na kumpigia Nassari?

Arumeru ndilo jimbo pekee kwenye uchaguzi wa ubunge, ila nasikitishwa na campaign za uko, zimeelekeza concetration kwenye kupigana vijembe zaidi ya kuzungumzia matatizo ya wananchi na ufumbuzi wake.
Udiwani naelewa CHADEMA wana wagombea vijibweni-Kigamboni DSM, Kiwira-Mbeya, Lizaboni-Songea, Tanga and Kirumba-Mwanza. Nafikiri kuna maeneo mengine pia lakini haya ndiyo ninayoyafahamu.
 
Arumeru ndilo jimbo pekee kwenye uchaguzi wa ubunge, ila nasikitishwa na campaign za uko, zimeelekeza concetration kwenye kupigana vijembe zaidi ya kuzungumzia matatizo ya wananchi na ufumbuzi wake.
Udiwani naelewa CHADEMA wana wagombea vijibweni-Kigamboni DSM, Kiwira-Mbeya, Lizaboni-Songea, Tanga and Kirumba-Mwanza. Nafikiri kuna maeneo mengine pia lakini haya ndiyo ninayoyafahamu.
Umejiingiza mwenyewe kwenye mkenge wa Mwanakijiji bila kujielewa, hapo mwakijiji maana yake ni kwamba Zitto ni mpuuzi tu kama wapuuzi wengine watu wanachohitaji kukisikia na kudiscuss kwa sasa ni hizi chaguzi na sio ulafi wake Zitto wa Madaraka. Got it!!??....
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom