Makosa ya Zitto tunayafahamu wote, hivi wana Chadema wote wangeyapuuza makala hiyo, wote wakamuunga mkono Zitto dhidi ya mwandishi wa makala ilomtafuna Zitto wangepoteza kitu gani?..Majuzi kuna makala ilitolewa ktk gazeti la Mtanzania yakidai kwamba Rostam ameipa support Chadema huko Arumeru, lakini sikuwasikia CCM wakirushiana marungu hata mara moja, badala yake waliyadharau makala hiyo na kuendelekeza nguvu zao ktk uchaguzi, CDM tumeshindwa kitu gani?
- Vijana vijana ukomavu wa kisiasa hamna...
Mkandara,
Uliyosema ni kweli ndiyo maana kuna mahali jana niliwaambia watu wote wanaotumia visingizio vya timing kwamba ati sijui kuna kampeni Arumeru wapuuze basi hii makala.Wote wanajadili kama vile watu wenye hofu fulani,hii mihemko si healthy katika kutoia mtazamojuu ya jambo kubwa linaloathiri mustakabali wa Taifa.Mtu kajibu makala ya mwandishi watu tena wengine ni wasomi kabisa wanalalama.Je,walitaka mwandishi wamakala ile aendelee kupotosha au watu waendelee kuamini kitu ambacho si cha kweli?kwa wale waandishi nguli(simaanishi makanjanja) au yeyote mwenye busara ya pekee anaelewa juu ya falsafa ya reliability na Longevity of an information/story.sasa sijui ni kwa nini busara hiyo isitumike katika mtazamo chanya wa makala ya Zitto?
Umeongelea kuhusu suala la CCM kupuuza ile story ya Mtanzania,sikubaliani na wewe unaposema kuwa ni vijana.Kwenye makala hii ya Zitto umeshuhudia hadi wazee ambao tulitegemea wawe kinara cha kunusuru kampeni zinazoendelea (kama kweli makala ya zitto inaathiri) kwa kuipuuza makala yake,badala yake wamekuwa wakipigana vikumbo kwenye vyombo vya habari kutoa mawazo/matamanio yao juu ya hili jambo.Wapo vijana,wazee,wasomi na waandishi wote wameunga tela.sijawasikia wanaharakati makini kama akina Deus Kibamba,Annanilea Nkya na wengineo wakioongea,kwa muktadha huu i salute them!
Tatizo kubwa hapa ni hofu ya mabadiliko,watanzania tumecharazwa kweli kweli na CCm hadi tunakosa imani/kujiamini kila wakati.Nashangaa ni watanzania wa aina gani waliokubaliana na wimbi la mageuzi ya kisiasa,kiuchumi na kijamii kuingia kwenye mfumo wa vyama vingi9oh kumbe matakwa yao yalipinduliwa -coup civillien kwa kukataa mfumo wa vyama vingi kwa asilimia 80).Nashanga ni watanzania gani waliokubali masharti ya SAPs ,nashangaa ni watanzania wa aina gani waliokubaliana na masharti ya uwekezaji kiholela.
Nadhani tunaweza kufanya uitafiti kutafiti resistance ya watanzania dhidi ya doctrine ya ujamaa na kujitegemea ambayo baadae walikuja kuishabikia na kuijutia lilipokuja azimio la Zanzibar na kufeli sambamba na matumizi ya fedha na kushamiri kwa ufisadi wa kutisha serikalini na uzembe wa daraja la kwanza
. Mkuu wangu Mkandara,Tatizo ni kubwa kuliko tunalofikiria.siyo Zitto,siyo timing na wala siyo hekima na busara za vijana
Natoka kidogo online niko safarini charge inaniishia,niombee safari njema!