Zitto: Ndio ninautaka urais

Zitto: Ndio ninautaka urais

Status
Not open for further replies.
mmmmh, kuna vitu vingine hata havifai jadili, ni karatasi ya kupigia kura tu.
 
Kuna wakati Zitto alituhumiwa na mdau hapa mtandaoni kuwa anamiliki Ghorofa Dodoma maeneo ya Kisasa. Alijitokeza mwenyewe humu jamvini akakanusha kwa nguvu zote hadi wengi tukajiridhisha kuwa anasingiziwa.
Sasa kwa ishu km hii ya Wassira kufika nyumbani kwa Zitto inaleta utata kidogo maana kama ni urafiki-HAPANA. ni urafiki gani uliopo kati ya Nuru na Giza, Uhai na Kifo...ni wazi hakuna!
Zitto, tolea majibu kwa haya mambo yanayoleta kiwingu katika safari yako ya Kisiasa.
 
Wanajf wenzangu assalaam aleikum! imekuwa ikijadiliwa kila mara humu jamvini kuwa ZITTO anautaka urais, swali langu ni kwamba anataka urais wa awamu ya ngapi?. Lakini pia nimekuwa nikiwasikiliza watu wenye mahaba binafsi na zitto wakisema eti watu hawajamwelewa zitto,kwanini haeleweki,na je ni kweli kuwa hawajamwelewa au yeye ndo hajaelewa watu.Na kama anautaka urais ni kwa kupitia chama gani? Na kama ni kupitia cdm,je njia anazotumia zitamfanya atimize ndoto zake? Na amejuaje kama katiba ijayo ita-regulate umri wa kugombea urais? Na kama yote hayo nimeyasema kwa sababu sijamwelewa,je haoni sasa ni wakati wa kunifanya mpiga kura wake nimwelewe? Nilimpenda sana zitto jamani na hata nilikuwa nikimwona anazungumza nasisimkwa, lakini kwa mwenendo huu wa sasa ambao kwake yeye kuutaka urais ni kwenda kinyume na wenzake kwa mambo ya msingi,basi itanichukuwa mda kumwelewa.
1)Kutoonekana sana kwenye M4C
2)kutounga mkono uamuzi wa cdm kutomtambua jk
3)kuunga mkono malipo ya tanesco kwa dowans kinyume na msimamo wa chama
4)Kuungana na jk ktk mazishi ya dictator zenawi
Haya yote na mengine mengi tunalalamika tu kwa sababu hatujamelewa? Tutamuelewa lini wakati bado miaka 2 tu ya uchaguzi mkuu. ZITTO kama upo humu nifanye nikuelewe katika haya.
 
Mkuu just give zitto a break kwani hata yeye ana haki ya kugombea nafasi ya urais kama alivyo Mbowe au Slaa and any other CDM member.
Pia hizi pia hizi dialogue hebu tuzuache na tujenge chama chetu.

Most tuwaheshimu viongozi wote wa chama ikiwemo na Zitto.
 
Wanajf wenzangu assalaam aleikum! imekuwa ikijadiliwa kila mara humu jamvini kuwa ZITTO anautaka urais, swali langu ni kwamba anataka urais wa awamu ya ngapi?. Lakini pia nimekuwa nikiwasikiliza watu wenye mahaba binafsi na zitto wakisema eti watu hawajamwelewa zitto,kwanini haeleweki,na je ni kweli kuwa hawajamwelewa au yeye ndo hajaelewa watu.Na kama anautaka urais ni kwa kupitia chama gani? Na kama ni kupitia cdm,je njia anazotumia zitamfanya atimize ndoto zake? Na amejuaje kama katiba ijayo ita-regulate umri wa kugombea urais? Na kama yote hayo nimeyasema kwa sababu sijamwelewa,je haoni sasa ni wakati wa kunifanya mpiga kura wake nimwelewe? Nilimpenda sana zitto jamani na hata nilikuwa nikimwona anazungumza nasisimkwa, lakini kwa mwenendo huu wa sasa ambao kwake yeye kuutaka urais ni kwenda kinyume na wenzake kwa mambo ya msingi,basi itanichukuwa mda kumwelewa.
1)Kutoonekana sana kwenye M4C
2)kutounga mkono uamuzi wa cdm kutomtambua jk
3)kuunga mkono malipo ya tanesco kwa dowans kinyume na msimamo wa chama
4)Kuungana na jk ktk mazishi ya dictator zenawi
Haya yote na mengine mengi tunalalamika tu kwa sababu hatujamelewa? Tutamuelewa lini wakati bado miaka 2 tu ya uchaguzi mkuu. ZITTO kama upo humu nifanye nikuelewe katika haya.


Nilikuwa ninampinga... Tumewasiliana humu kwenye JAMII FORUMS nimemuona Ana Lengo lake; Kanielezea kidogo tu kuhusu

Wizara ya MADINI na Uongozi wake, na imenipa FIKRA mpya za kuona Maamuzi anayoyafanya kama yana nia ya Kuendelea na

anaweza kuwa RAIS
 
Mkuu just give zitto a break kwani hata yeye ana haki ya kugombea nafasi ya urais kama alivyo Mbowe au Slaa and any other CDM member.
Pia hizi pia hizi dialogue hebu tuzuache na tujenge chama chetu.

Most tuwaheshimu viongozi wote wa chama ikiwemo na Zitto.

hivi unajua kuwa majority ya watu wanaomponda Zitto si wana-Chadema?

wengi wao ni wana-CCM, motive yao ni moja - ku-create mazingira ya kuhasimiana na kutokuaminiana miongoni mwa viongozi wakuu wa Chadema.

mwanzisha thread hii nahisi ni mmoja wa hao wasiotakia mema Chadema!

kama Chadema (hususani viongozi wakuu) mnataka kuwa salama na kubakia kwenye mshikamano come 2015, you must ignore all these sentiments against Zitto. Kama ilivyo tofauti ya tabia kati ya Lema na Mnyika, ama Sugu na Nassari, ndivyo hivyo hivyo ilivyo tofauti kati ya Mbowe na Slaa, Zitto na Slaa, etc, etc, etc.

JK alipounda tume ya Warioba (katiba mpya), Edwin Mtei alitoa outburst against composition ya wajumbe wa tume - outbusrt ambayo wengi walii-adjudge kama imesheheni udini. kauli rasmi ya Chadema iliipinga outburst ya mwasisi wa chama chao wenyewe in the strongest terms possible. thereafter hakukuwa na kelele za kum-single out Mtei kama muasi au mkorofi or anything. Why, kwa sababu Mtei kwa nafasi yake isiyo executive ndani ya chama chake si mtaji strong ambao CCM wanaweza kuutumia kuibomoa Chadema!!

rai yangu kwa wana-Chadema.....mkifanikiwa kukaa pamoja kama timu hadi 2015, ni wazi mtaweza kunyakuwa uongozi wa nchi....just like Real Madrid inavyochukua mataji huku ndani yake kukiwa na wanung'unikaji (whinners) kama Ronaldo au Man City kuchukua ubingwa ikiwa na wakorofi kama Balloteli kwenye line-up yake!!
 
Mkuu just give zitto a break kwani hata yeye ana haki ya kugombea nafasi ya urais kama alivyo Mbowe au Slaa and any other CDM member.
Pia hizi pia hizi dialogue hebu tuzuache na tujenge chama chetu.

Most tuwaheshimu viongozi wote wa chama ikiwemo na Zitto.
Kaka chama hakijengwi kwa tofali na mchanga,kinajengwa kwa hoja.Tutampa break kama na yeye ataamua kutupatia break, maneno hujenga,napenda nimwele zitto anataka nini? kama unafahamu vema niambie tu na hutoniona tena nazungumza habari za zitto.Hakuna aliyemnyima haki ya kugombea,lakini naomba nikuulize,unaridhika na juhudi za zitto katika kujenga cdm ambayo mimi na wewe ni wanachama waaminifu?
 
Kinachokusumbua wewe ni udini tu. Jaribu kuangalia habari imetoka wapi sio kukurupuka. Labda anaongelea urais 2025 Dr Slaa akishamaliza vipindi vyake, which kila mwana CDM atamuunga mkono. Lakini kwa sasa Zitto HAJAKWIVA kuwa rais na hata katiba haimruhusu
Wewe ndio udini unakusumbua, hakuna cha Slaa hapa.
 
Mti wenye matunda ndio hupigwa mawe...zitto ni mshindani wa kweli wa urais kama akitangaza nia, go !go.! zitto go go.! cdm
 
Na kwa cdm huyu ndio mtu anae faa kuwa Rais. Wengine wote wakina M & S Company wana tamaa tu za madaraka. Nawaomba wana cdm muungeni mkono Zitto na apitishwe na chama
mchukue ukanywe nae chai huko chama cha mabwe pande
 
Kuna wakati Zitto alituhumiwa na mdau hapa mtandaoni kuwa anamiliki Ghorofa Dodoma maeneo ya Kisasa. Alijitokeza mwenyewe humu jamvini akakanusha kwa nguvu zote hadi wengi tukajiridhisha kuwa anasingiziwa.
Sasa kwa ishu km hii ya Wassira kufika nyumbani kwa Zitto inaleta utata kidogo maana kama ni urafiki-HAPANA. ni urafiki gani uliopo kati ya Nuru na Giza, Uhai na Kifo...ni wazi hakuna!
Zitto, tolea majibu kwa haya mambo yanayoleta kiwingu katika safari yako ya Kisiasa.

huyo anajulikana kuwa anatumiwa na ccm na nia yao ni kuiangamiza chadema.hafai,hafai.
 
mi nadhani uraisi wa tanzania ni haki ya kila mtanzania nani atakuwa raisi ni jukumu la watanzania ni vema tukajadili hoja bila kujali imetolewa na nani.Tusipinge au kukubali hoja kwa sababu katoa fulani.Tufungue ufahamu wetu bila kujali tofauti zetukwani ardhi ya Tanzania ilikuwepo kabla ya vyote.Tukumbuke kwamba Tanzania is a permenent interest.Hivyo ni vema kupima mazuri na mabaya ya hoja yenyewe.
 
Makala imejitosheleza lakini inawafikiaje Watanzania wa kawaida kabisa ambao hata gazeti hawana uwezo wa kununua.Busara na hekima kubwa inatakiwa ili kutafakari kwa kina makala hii.Watanzania ndio waamuzi wa hoja za Zito.
 
Zitto anafaa na ana
uwezo mkubwa sana, ila swala kubwa ni alama za nyakati ndizo huamua.
Yeye azisome tu na wakati muafaka ukifika ataupata tu huo Uraisi.
Singependa sana kumkatisha tamaa. Ana nafasi kubwa ya kuupata, ila
asikurupuke.

Zitto anafaa na ana
uwezo mkubwa sana, ila swala kubwa ni alama za nyakati ndizo huamua.
Yeye azisome tu na wakati muafaka ukifika ataupata tu huo Uraisi.
Singependa sana kumkatisha tamaa. Ana nafasi kubwa ya kuupata, ila
asikurupuke.

Hii ni point.Zito kama unasoma thread hii ni kweli una nafasi kubwa ya kuwa kiongozi mkubwa ktk nchi hii,lakini ni vizuri kuwa na uvumilivu.Umri wako unakuruhusu hata kama hutagombea 2015.Kwa sasa shirikiana na viongozi wenzako kujenga chama achana na masuala ya urais kwa sasa.Kwani badala ya kujenga chama utajikuta muda mwingi unafanyia kazi nia yako ya urais ambayo si wakati muafaka kwa sasa.
 
Wanaomtetea Zitto kila siku wanasema Zitto hapendwi kwa sababu ya dini yake. Kwangu mimi naona hii ni hoja Dhaifu kuliko, ukweli ni kwamba Zitto hapendwi kwa sababu ya matendo yake. Yakiwemo kushirikiana na Mafisadi wa Ccm na watu wenye mawazo mgando kama mzee wa Bunda. Huu utetezi wa dini hauna nguvu. Mimi binafsi Zitto na Shibuda ndani ya Chadema siwaelewi, one day nikisikia wameenda chama cha Kijani itakuwa safi.
 
Zitto ni kansa inayoitafuna chadema!!muda unafika!!na haupo mbali ambapo cdm italazimika kupunguza kiungo chake kimoja kama si kusubiria kufa kwa cancer hii!! Tufikiri na kuchukua hatua kabla cancer hii haijasambaa mwili mzima.
 
conventional wisdom aliyoikosa Zitto inaonyesha kuwa Zitto ana abuse vitu vya msingi.Well, hayo ndio matokeo ya india,wamesham-format long time.
 
hebu mpeni haki yake mh Zitto naye ajaribu....mh Mbowe alijaribu akashindwa.......dr Slaa naye vilevile.....tunahitaji sura mpya.....tena itaondoa dhana ya udini ndani ya cdm.....siyo kila siku walewale....tuko watanzania zaidi ya milioni 40...hakuna chuo kinachotoa elimu ya urais
 
hebu mpeni haki yake mh Zitto naye ajaribu....mh Mbowe alijaribu akashindwa.......dr Slaa naye vilevile.....tunahitaji sura mpya.....tena itaondoa dhana ya udini ndani ya cdm.....siyo kila siku walewale....tuko watanzania zaidi ya milioni 40...hakuna chuo kinachotoa elimu ya urais

Weee.... who told u Zitto anachukiwa kisa dini..?? Zitto ana uchu wa madaraka, pili ANACHUNGUZWA KUHUSU KASHFA YA WIZARA YA NISHATI NA MADINI, kuhusu IPTL, each month Tanesco walikuwa wanalipa IPTL FEDHA ZA MAFUTA KUENDESHEA GENS, HUKU MAJI YAPO KUMBE NI MCHEZO WA KUKATA MAJI PURPOSELY, the wana amuru tanesco iwalipe fedha ili kununua mafuta kuwasha generators za IPTL, Zitto alikuwa anapata GAWIO LAKE TENA KUBWA TU, KAMATI YA NISHATI NA MADINI YA BUNGE HADI IMEVUNJWA, ila ZITTO yupo CHC of which anajua inside out ya scandal nzima long time na alikuwa anachukua chake, Zitto mla rushwa mkubwa, HUONI KATULIA AIBU IMEMFIKA ANADECLARE HATAKI ALLOWANCES ZA BUNGE KUMBE ANAKULA RUSHWA KUBWA thru IPTL dili la mafuta, Prof. Muhongo kasema wengi wataaibika.... So stop defending a guy u don't know.....

Refer ---- BUNGE LILILOPITA -----
 
Hongera Zitto. Hakika yeye ni asset kwa Tanzania lakini from the bottom of my heart asubiri mpaka 2025 atakuwa amekomaa vya kutosha.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom