Zitto kugombea urais 2015?

Zitto kugombea urais 2015?

Status
Not open for further replies.
Musembi,

Usiwe mpumbavu kwa kushabikia upuuzi, werevu walio wengi wanajua ushujaa wa huyu kijana wa kigoma, na si kweli kuwa CDM imemvumilia kwa ajili ya ukomavu wa kisiasa usitudanganye we know mchezo mchafu wa viongozi wenu wanapoona mtu anae jiweza anatishiia umaarufu.

Unapotaja watu waliofulia ktk chadema na bado wamekumbatiwa na chama huwezi Mzito Kabwela ndugu, ukamuucha mwenyekiti Freeman Mbowe................. mbowe alipata umaarufu ktk bunge from 2000-2005 akautumia kugombea urais na watu mlimsifia, lakini leo dogo janja katangaza nia mnamponda kwa sababu mmelishwa sumu.

Chadema wamemkaba Zitto muda mrefu..... Tazama Mnyika alivyotengenezewa njia akiwa mgongoni kwa Zitto, kutoka kaimu naibu katibu mkuu mpaka kapora tonge la Zitto la kambi ya upinzani bungeni.............

Huyu jamaa yuko juuu hata kama CDM imeona alivyo na mlengo wa kulia coz wao ni Conservatives
 
Zitto is a quality young leader ila nadhani he is rushing na hiyo ndoto yake ya urais ya 2015
Urais hautafutwi by hook and crook kama utashi wa mtu binafsi kwa sababu tu yeye kama yeye anataka kuwa rais. Rais ni kiongozi wa jamii na jamii ndio inayoona ni nani anayefaa kuwa rais na siyo personality.

Urais anaoutaka Zitto ni kwa ajili tu ya kujiridhisha na kuandika historia lakini siyo kwa sababu anapenda sana kuwatoa watanzania point A kwenda point B hivyo tuache kumshabikia.
 
Hizo ni hisia zako lkn kamwe sitoziamini, ninavyoona mimi Zitto Kabwe ni mpigani shupavu. Na kuwa mbunge wa chama cha upinzani hakumaanishi usiwe na uhusiano wa karibu na wabunge au viongozi wa chama tawala.

Jamani vyama vingi visiwe sababu ya kuwaacha marafiki zetu au kutokukaribisha marafiki wapya. Imekuwa muda mrefu akishutumiwa mhe Zitto kuwa ni kibaraka wa chama tawala especially alipotaka kugombania nafasi ya uwenyekiti wa CHADEMA na hii ilikuwa ni haki yake kikatiba. Kwa hiyo kwangu mimi hizi zote ni njama za kumuondoa Zitto katika duru ya kisiasa. Na ndugu zangu siasa sio ugomvi siasa ni hoja.

Kwa hiyo Zitto kuwa na ukaribu na viongozi wa chama tawala sio kosa sisi hatupigani vita na CCM tunapambana nao kisiasa so hakuna sababu ya mwanachadema au kiongozi wa chadema kutokuwa na mawasiliano na viongozi wa CCM.

Jamani hapa kuna kitu nyuma yake na ikiwa huu ndio itakuwa mwenendo wetu hatutofika popote na tutake tusitake Zitto kama mzito ametoa msaada mkubwa sio tu ktk chama bali kwa taifa kwa ujumla na asiyejua ni mchango Zitto kautoa ktk chama na taifa kwa ujumla basi ni mbumbumbu.

mimi sioni kama unatakiwa kutukana ndo ueleweke,kumbuka humu ndani watu wamesoma na ni watafiti wazuri sana,so be polite and wise,usikurupuke,sasa naomba ukae ulete facts ili tukujibu kwa facts,usilete taarabu

kwanza naomba nikuulize na ujibu critically,hivi wakati Zitto akihutubia na kusema 2015 yeye ndo ataipeperusha bendera ulimsikia mwenyewe ama uliipata kama SHOP TALKS? kama ulimsikia naomba utwambie alifata taratibu ZIPI na za CHAMA kipi

Pili,unasema siasa si ugomvi ndo maana Zitto anawasiliana na CCM kwa hyo tusimlaumu,mbona juzi kati Mbowe alikutana na JK wakatokea kwenye gazeti wamekumbatiana,kwanini hapa wanaCDM hawamsemi Mbowe?

Tatu,kukifanyia chama kazi haialalishi mtu atende kinyume na chama,kuna taratibu kwa viongozi na kwa wanachama,kwanini ukiuke taratibu za chama alafu ukisemwa unajitetea eti umekifanyia kazi nyingi chama kwahiyo wasikuseme?unaona sawa?
 
mimi sioni kama unatakiwa kutukana ndo ueleweke,kumbuka humu ndani watu wamesoma na ni watafiti wazuri sana,so be polite and wise,usikurupuke,sasa naomba ukae ulete facts ili tukujibu kwa facts,usilete taarabu

kwanza naomba nikuulize na ujibu critically,hivi wakati Zitto akihutubia na kusema 2015 yeye ndo ataipeperusha bendera ulimsikia mwenyewe ama uliipata kama SHOP TALKS? kama ulimsikia naomba utwambie alifata taratibu ZIPI na za CHAMA kipi

Pili,unasema siasa si ugomvi ndo maana Zitto anawasiliana na CCM kwa hyo tusimlaumu,mbona juzi kati Mbowe alikutana na JK wakatokea kwenye gazeti wamekumbatiana,kwanini hapa wanaCDM hawamsemi Mbowe?

Tatu,kukifanyia chama kazi haialalishi mtu atende kinyume na chama,kuna taratibu kwa viongozi na kwa wanachama,kwanini ukiuke taratibu za chama alafu ukisemwa unajitetea eti umekifanyia kazi nyingi chama kwahiyo wasikuseme?unaona sawa?

ndugu yangu naona umekurupuka kunijibu lakini sijaluelewa kabisa mimi naomba
1; umesema nimetukana ni wapi nimetukana?
2😛ili sijaandika sehemu yyte kuwa zitto anataka kugombea urais 20159 nilichosema alipotaka kugombea uwenyekiti wa chadema)
3:na mwisho kuhusu mbowe kukumbatiana na jk kwanini hakusemwa na zitto asemwe ni wewe wa kujiuliza kwani mimi ndiyo niliyesema kuwa na mahusiano na viongozi wengine sio dhambi. kwahiyo wewe na wengine wenye kumshutumu zitto ndio mnaotakiwa kujiuliza kwanini hamukumshutumu mbowe na mnamshutumu zitto.

MWISHO NAKUOMBA KABLA YA KUANZA KUMJIBU MTU HUMU NDANI USHIRIKISHE UBONGO WAKO VIZURI.
 
Kati ya vitu ambavyo CHADEMA wame-prove kuwa wapo makini ni namna ambavyo wameweza kum-handle Zitto, chama ndiyo kilimfikisha hapo alipo, umaarufu wake ulianza pale alipotolewa bungeni lakini CDM ikaamua kumbeba na kuunganisha watu ili ichukulie kitendo cha kufukuzwa bungeni na matokeoa ya ushujaa wake, na msimamo dhidi ya maslahi ya taifa, kweli watu wakjitokeza kwa wingi baada ili kuitikia wito wa chama.

Alipoona makutano ya watu kiasi kile akajua hii ni shauri ya yeye kama yeye kama Zitto na si chama, imani ikajengeka ndani yake kuwa yeye ni zaidi ya chama, akaanza kufuata utashi na hisia zake, kama treni iliyoacha reli...waandishi waliokuwa wanamsifia wakaona mwelekeo wake hatari, Kibanda akaandika kuonya, Ngurumo akaandika, Happiness Katabazi akaandika, wengi wakaandika, sikio la kufa halisikii dawa, magazeti makini yakaachana naye, akaenda kuibukia kwenye magazeti ya udaku, akayashambulia magazetu yetu kuwa, magazeti ya udaku ndiyo yenye nguvu na yasomwayo na watu wengi duniani, hakufafanua watu wa aina gani. Muda si mrefu urafiki na magazet hayo ukaisha baada ya kuandika skendo zake za ngono na wasichana kadhaa wanaodhani kuwa majina yao ni makubwa hapa nchini, kumbe yanafahamika tu na wala hayana ukubwa wowote.

Turudi kwenye mada...akazua hali ambayo ilitafsiriwa kama kizaazaa ndani ya CDM, nadhani alifanya makusudi ili afukuzwe aondoke "kishujaa"(kama alivyopokewa jangwani) kwasababu kuna watu ndani ya CCM walimdanganya kuwa akifukuzwa na hata akiipoteza nafasi ya ubunge, atapewa wa kuteuliwa na rais, pia kupewa unaibu waziri, na ili kumhakikishia hilo akajengewa ukaribu na idara za usalama na watu mashuhuri walio pretend kwenda kwake kupata ushauri na msaada wa mambo kadhaa, akazidi kuwa jeuri, lakini maskini kijana huyu hakujua kuwa watanzania walishamuona kimeo muda mrefu uliopita kiasi cha viongozi wa CDM kuwekwa katika msukosuko na wananachama wao kuwa kwa nini wanamlea, lakini uongozi ulionyesha ukomavu kwa kuendelea kuwa naye na kumkumbusha maadili ya chama na siasa kwa ujumla.

Kabla ya kampeni mwaka za mwaka jana, alitishia kutogombea, lakinibaadaye akapima akapima akaona namna maisha yatakavyokuwa magumu nje ya siasa, kwani hakuna kazi itakayomlipa kama siasa, ukichukulia kwa muda huo alishaamua kushiriki siasa kwa maslahi binafsi, hivyo akabatilisha msimamo wake na kuamua kutetea kiti chake, kampeni zilipowadia, akijua kuwa chama chake kimesimamisha mgombea wa nafasi ya urais, lakini akaonyesha kuibeza hatua hiyo kwa kusema kuwa, tunakwenda kuchagua wabunge na madiwani kwani rais tayari tunae tumuache amalize muda wake, lakini uongozi wa CDM uliendelea kumvumilia, Kitendo hicho cha uongozi wa CDM kuendelea kumvumilia kimebomoa sana Image ya Zitto kwa jamii,na kuifanya CDM ionekana kama chama imara kinachoweza kuishi pamoja hata inapotokea wakatofautiana mawazo kati yao.....kwa hili CDM nawapa sifa sana. Zitto amechuja lakini hilo halitambui tena kwasababu sasa hivi anaishi kwa kutegemea taarifa za wapambe. Ameaminishwa kuwa kila ampingae ni walewale wanaotumiwa dhidi yake.

Sasa hivi ni naibu Kiongozi wa kambi ya Upinzani bungeni anaongoza watu wasio mkubali watu ambao walipiga kura ya kumkataa, maamuzi ambayo hayakuwahi batilishwa popote pale, lakini kwasababu ya upenzi wake kwa madaraka bila kujari anaongoza kwa mazingira gani as long as anapata chake, katika hili Zitto hataki kutumia akili yake kama mwanasiasa kijana na msomi kama anavyotaka kutambulika, ameamua kung'ang'ania madaraka hayo bila suluhu ya aina yoyote, hataki kupisha nafasi hiyo kwa mtu mwingine anekubalika.

Zitto ambaye nahisi kila aonapo wakina Mnyika, Lema Lissu na wengineo wakitoa hoja zinazotikisa bunge huwa hajisikii vizuri kwa kuumia moyo, akitamani hali hiyo ya bunge kutetemeshwa kwa hoja ingesababishwa na yeye. alijaribu kutengeneza 'msukule/Zombi' wake pale bunge (Kafulila), lakini sijui ulipoishia, japo kuna yule bint, simkumbuki jina lake ila nadhani ni wa viti maalum CDM, lakini wote wapo off-color.

Huyo ndiye Zitto kabwe, ambaye sasa anataka atambulike kama rais mtarajiwa, kwani ameshatangaza dhamira yake ya kugombea urais mwaka 20015, Zitto ambaye watu wakimkubusha wajibu yeye anadhani ni watu wanaomuonea husda kwa 'mafanikio' yake kisiasa, Zitto anayeamini moyoni na kichwani mwake kuwa yeye ni zaidi ya chama, lakini mdomoni anahubiri kuwa hakuna aliye zaidi ya chama.

Nimeandika si kwa mtiririko rasmi wa uandishi na utoaji habari, bali kwa mtindo wa kugusia gusia tu ili kukumbusha, kwa lengo la kuendelea kufikiri na kutafakari kwa pamoja.


Ongea mambo ya msingi acha majungu,ndo maana hatuendelei.
 
Kati ya vitu ambavyo CHADEMA wame-prove kuwa wapo makini ni namna ambavyo wameweza kum-handle Zitto, chama ndiyo .......

Alipoona makutano ya watu kiasi kile akajua hii ni shauri ya yeye kama yeye kama Zitto na si chama, imani ikajengeka ndani yake kuwa yeye ni zaidi ya chama, akaanza kufuata utashi na hisia zake, ..........................


tatizo la hili jukwaa wote sisi tunajidai ni watu wa kukosoa. Ukiuliza ebu great thinker chagua wizara , shiraka au jimbo moja unaloweza kuwa kiongozi. Taja mikakati mipango na maamuzi gani utafanya. Only few can answer this question

Most of us are just reactive waiting Ziitto to do this or kikwete to do this or Slaa to that.

Please let stop this trend.

Musembi Ungekuwa wewe ndo zitto ungefanya nini?
 
Hivi mbona Zitto anaonekana kuto kuelewana na chama chake kwa watu ambao wapo nje ya chama tu? Na nasema nje kwa sababu najua watu wengi humu ni mashabiki wa Chadema lakini hawana influence yoyote ndani ya chama kwa maana maamuzi yaki fanyika wao hawapo. Kama kweli Zitto ange kua msaliti wa chama basi angesha fukuzwa uanachama. Kama yote unayo sema ni kweli na bado Chadema hawa muondoi hiyo ina semaje kuhusu uongozi wa chama? Tusi take kujidai wote humu tupo katika inner circle wakati wengi wetu tuna leta story za vijiweni kama facts.
 
tatizo la hili jukwaa wote sisi tunajidai ni watu wa kukosoa. Ukiuliza ebu great thinker chagua wizara , shiraka au jimbo moja unaloweza kuwa kiongozi. Taja mikakati mipango na maamuzi gani utafanya. Only few can answer this question

Most of us are just reactive waiting Ziitto to do this or kikwete to do this or Slaa to that.

Please let stop this trend.

Musembi Ungekuwa wewe ndo zitto ungefanya nini?

Umepatia ndugu yangu. Zito ni mwanasiasa, na siasa haziko kati ya Chama tawala na vyama tawaliwa bali hata ndani kwa ndani, yaani inaruhusiwa pia kuwa na siasa kati ya wenyewe kwa wenyewe. Zito hana kosa kufanya hivyo ni sehemu ya maisha ya siasa. Asiyekomaa kiasi hicho basi akae pembeni aepushe msongamano.
 
Agenda yenu ya kumuuwa Zitto kisiasa kamwe haitafanikiwa, kila ukifungua JF ni Zitto tu, kwani Zitto atakuwa na umri gani 2015, kama sio njama tu za kumuuwa kisiasa. Naona siasa za kupakana matope zinainyemelea CDM. Jengeni hoja mmeandaa mpango gani wa kutatua kero za wananchi mkichukua madaraka, watu wanajua ipi pumba na upi mchele, watachagua tu wanachokitaka
 
Kwanza nimezitaja hizo sifa ili aelewe aliyetowa "analysis" za hao "viongozi" watatu ni mtu mwenye upeo wa kuchambuwa.

Kuhusu hizo sifa (ni baadhi tu), hunijuwi sikujuwi, ukipenda zikubali ukipenda usizikubali.

Kuhusu kuziongelea kiingereza, napenda uelewe kuwa mimi nimeanza masomo yangu ya awali wakati bado tu Tanganyika na wakati huo, kiswahili kilikuwa ni somo moja tu la "swahili", masomo yote yalikuwa ya kiingereza, utaniwia, mtaniwia radhi ikiwa nnatumia maneno ya kiingereza kujielezea. Msamiati wa kiswahili cha kisasa hunipiga chenga na kuna kauafadhali fulani nitumiapo kiingereza kwa baadhi ya maneno. Hujitahid sana kuandika kiswahili kila niwezapo.

MHHH! Wengi wamesema ficha upumbavu wako usifiche hekima yako. Sina hakika kama wingi wa maneno ndo kwenye hekima ama mpangilio wa hoja ndo kwenye hekima! Weledi na ujuvi katika mambo ni vema kuendana na kauli tunazotoa kwa jamii, na wakati mwingine si vema kuwalazimisha watu kuona kijani wakati rangi iliyowazi ni zambarau. Nawakilisha
 
namkubali zitto kama mwanasiasa msomi na makini zaidi katika chadema, ila pia naukubali ukweli kwamba zitto hana msimamo na hii inatokana na kujiamini kwake kupita kiasi.
 
Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni. Mimi maono yangu ni kwamba katika CDM ni ZITTO peke yake ambaye anaweza kutusogeza toka point A to B nchini Tanzania. Wengine wote wanafaa kuwa wasaidizi wake. Sisemi kwamba hawafai, lakini katika Presidential level, Zitto is the right choice. Slaa ni mtendaji, let him be PM na Mbowe labda VP. Huu ni ukweli ambao hata Stevie Wonder anaweza kuuona.
Napita.

Ehee ebu nieleweshe

  • Right choice ya zito kuwa presdent na sio Mkuu wa mkoa au Waziri wa fedha? kwa nini ?ana siffa gani au atafanya nini?
  • Slaa ni mtedaji ina maana Zitto sio mtendaji ?
  • Kwani kazi ya president ni nini hasa na kazi ya PM ni nini hasa.
Ebu fafanua
 
MIMI NI CDM 100% YULE MNAFIKI NA MPENDA MASIFA ZITO KABWE IKIWA HIVYO MIMI NA CHADEMA BASI,NDO MAANA LINAENDESHA HUMMER NA KWAO HAMNA BARABARA YA KUENDESHEA:smile-big:
 
tatizo la hili jukwaa wote sisi tunajidai ni watu wa kukosoa. Ukiuliza ebu great thinker chagua wizara , shiraka au jimbo moja unaloweza kuwa kiongozi. Taja mikakati mipango na maamuzi gani utafanya. Only few can answer this question

Most of us are just reactive waiting Ziitto to do this or kikwete to do this or Slaa to that.

Please let stop this trend.

Musembi Ungekuwa wewe ndo zitto ungefanya nini?

Zing.....nadhani unaona namna ambavyo mitazamo inapotofautiana tu, watu hupata hisia tofauti juu ya upande wa pili. Nimerejea matukio ambayo yalitokea na ambayo kila mmoja amekuwa ni shahidi, sidhani kama hapo kunakujifanya great thinker kweli? Sidhani kama nastahili hata kuigiza nafasi ya great thinker katika maigizo, kwani naamini sina nikijuacho, lakini nina uwezo wa kutunza kumbukumbu na kuoanisha na matukio yajayo, nafasi ya great thinker hiyo ni ya kwenu, huo ukuu mimi siuwezi.
Pia ikumbukwe kuwa kwa wadhifa alionao Zitto katika jamii, na mambo yanayohusishwa na yeye, anajadilika bila wasiwasi, hakuna sababu ya watu kusema ni unafiki au ni mkakati wa kumuuwa kisiasa au majungu, ikumbukwe kuwa kwa mtu mwenye akili timamu ikatokea akaongelewa kwa mazuri au mabaya, huo ndiyo wakati wake wa kujipima na kujirekebisha. Kwa wafuasi wake wanatakiwa kuwa wavumilivu na kukabili kwa umakini na utulivu hisia na hoja zote zitolewazo dhidi role model wao.
Mimi au wengine wenye mtazamo kama wangu ni kioo tu hamna haja ya kutuchukia, kwani kinachoonekana katika kioo hiki ndiyo image ya mhusika, hivyo ni wajibu wake kuji-shape upya.
Mimi binafsi huwa napenda kufanya jitihadi kufanya mambo yaliyo sahihi, lakini huwa ninasisitiza kusikia habari zilizo mbaya mbaya mapema ili nizifanyie kazi mapema, sina muda wa kusikiliza sifa au mafanikio yanayonihusu.
Kuhusu ningefanya nini? hilo lipo dhahiri, kuwa ningefanya tofauti na yale yanayoonekana kuwa ni kasoro katika mlolongo mzima niliouainisha.
Ila kwa kufupisha tu na kuwa a little obvious, kipindi hiki ningejitahidi kuwa makini na ku-walk under radar, ili ku-avoid much attention,
 
Tusimshambulie msembi hayo ni mawazo yake,pia naomba nimuunge mkono msembi,hebu niulize wapenda mageuzi ktk tanzania hii inayomilikiwa na watu wachache,yuko wapi zitto kama yule wakati ni kiongozi UDSM?yukowapi zitto kama yule kabla hajafukuzwa bungeni?yuko wapi zitto kabla hajateuliwa kuwa mwenyekiti kamati ya hesabu za mashirika ya umma?jibu siyo zitto yule tuliyemzoea kabadilika hata ufunguzi wa matawi ya chama chake UDOM,ST JOHNS,MIPANGO,na kwingineko hatujamwona akijihusisha kitu ambacho kwa miaka ya nyuma ni lazima yeye ndo angekuwa mstari wa mbele,ni ukweli usiofichika mh zitto anahitaji kurudi kundini kabla ya huo uamzi wake huo na sisi kama vijana tuko tayari kumpokea kwa gharama yoyote maana hiki ndo chama pekee chenye kutufikisha safari tuliyoianzisha.TOGETHER WE CAN.dalali
 
Musembi,

Usiwe mpumbavu kwa kushabikia upuuzi, werevu walio wengi wanajua ushujaa wa huyu kijana wa kigoma, na si kweli kuwa CDM imemvumilia kwa ajili ya ukomavu wa kisiasa usitudanganye we know mchezo mchafu wa viongozi wenu wanapoona mtu anae jiweza anatishiia umaarufu.

Unapotaja watu waliofulia ktk chadema na bado wamekumbatiwa na chama huwezi Mzito Kabwela ndugu, ukamuucha mwenyekiti Freeman Mbowe................. mbowe alipata umaarufu ktk bunge from 2000-2005 akautumia kugombea urais na watu mlimsifia, lakini leo dogo janja katangaza nia mnamponda kwa sababu mmelishwa sumu.

Chadema wamemkaba Zitto muda mrefu..... Tazama Mnyika alivyotengenezewa njia akiwa mgongoni kwa Zitto, kutoka kaimu naibu katibu mkuu mpaka kapora tonge la Zitto la kambi ya upinzani bungeni.............

Huyu jamaa yuko juuu hata kama CDM imeona alivyo na mlengo wa kulia coz wao ni Conservatives

Wewe ndio mpuzi kwa sababu huoni madudu ya zitto, wala mnyika hajatengenezewa njia na Mwasi Zitto huyu ni mhujumu mwenye kuona zaiidi kuliko wengine. Dr ndio amewatengenezea njia wengi ndani CDM lakini kwa uelewa wako finyu hutakubali lakini habari ndiio hiyo
 
mimi sioni kama unatakiwa kutukana ndo ueleweke,kumbuka humu ndani watu wamesoma na ni watafiti wazuri sana,so be polite and wise,usikurupuke,sasa naomba ukae ulete facts ili tukujibu kwa facts,usilete taarabu

kwanza naomba nikuulize na ujibu critically,hivi wakati Zitto akihutubia na kusema 2015 yeye ndo ataipeperusha bendera ulimsikia mwenyewe ama uliipata kama SHOP TALKS? kama ulimsikia naomba utwambie alifata taratibu ZIPI na za CHAMA kipi

Pili,unasema siasa si ugomvi ndo maana Zitto anawasiliana na CCM kwa hyo tusimlaumu,mbona juzi kati Mbowe alikutana na JK wakatokea kwenye gazeti wamekumbatiana,kwanini hapa wanaCDM hawamsemi Mbowe?

Tatu,kukifanyia chama kazi haialalishi mtu atende kinyume na chama,kuna taratibu kwa viongozi na kwa wanachama,kwanini ukiuke taratibu za chama alafu ukisemwa unajitetea eti umekifanyia kazi nyingi chama kwahiyo wasikuseme?unaona sawa?

hata mimi nilimsikia kupitia runinga,issue siyo uongozi lakini anapitia njia gani?
 
Tusimshambulie msembi hayo ni mawazo yake,pia naomba nimuunge mkono msembi,hebu niulize wapenda mageuzi ktk tanzania hii inayomilikiwa na watu wachache,yuko wapi zitto kama yule wakati ni kiongozi UDSM?yukowapi zitto kama yule kabla hajafukuzwa bungeni?yuko wapi zitto kabla hajateuliwa kuwa mwenyekiti kamati ya hesabu za mashirika ya umma?jibu siyo zitto yule tuliyemzoea kabadilika hata ufunguzi wa matawi ya chama chake UDOM,ST JOHNS,MIPANGO,na kwingineko hatujamwona akijihusisha kitu ambacho kwa miaka ya nyuma ni lazima yeye ndo angekuwa mstari wa mbele,ni ukweli usiofichika mh zitto anahitaji kurudi kundini kabla ya huo uamzi wake huo na sisi kama vijana tuko tayari kumpokea kwa gharama yoyote maana hiki ndo chama pekee chenye kutufikisha safari tuliyoianzisha.TOGETHER WE CAN.dalali

zitto anautaka uwenyekiti,zitto anautaka uraisi!Mbona hautaki ukatibu Mkuu maana hata unaibu hautendei kazi?Hii inaonyesha zitto si mtendaji bali anapena atambulike.mawazo yangu
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom