Invisible
Robot
- Feb 11, 2006
- 9,075
- 7,878
Kuna taarifa (toka TBC1) kuwa leo Zitto katoa tamko rasmi kuwa ana mpango wa kugombea urais wa Tanzania mwaka 2015 na akawaomba wananchi wampe kura nyingi ili apate hadhi ya kuweza kugombea urais wa nchi hii.
Kila la heri mkuu Zitto, walau una nia! Je, katiba itabadilishwa?
LAKINI
Kila la heri mkuu Zitto, walau una nia! Je, katiba itabadilishwa?
LAKINI
Zitto hawezi kuwa mgombea Urais wa CHADEMA kwenye uchaguzi wa 2015 kwa sababu hizi zifuatazo:
1. Zitto amezaliwa September 24, 1976. Hivyo, mwaka 2015 atakuwa ametimiza miaka 39 Inshallah. Katiba inasema mgombea Urais Tanzania awe na si chini ya miaka 40.
2. Zitto amechafuka ndani ya CHADEMA kama Lowassa alivyochafuka ndani ya CCM. Wakati CCM wanaweza kumchagua Lowassa kuwa mgombea wao wa Urais 2015 kutokana na upumbavu wao, CHADEMA si wapumbavu.
3. Bado Watanzania wanamhitaji na kumwamini DK. WILLIBROD SLAA. Pamoja na kuwa DK. SLAA mwenyewe hana mpango wa kugombea 2015, wito wa Watanzania utakuwa ni mkubwa sana na nadhani ataitikia wito huo.
4. Hata yeye Zitto anajua kuwa hana nafasi ya kuwa mgombea Urais wa CHADEMA, hata kama DK. SLAA akiamua hagombei. Amejiharibia mwenyewe kwa uhusiano wake wa kifisadi na Rostam Aziz na watawala wa serikalini.
5. Zitto akiwa mgombea Urais wa CHADEMA, Watanzania wengi wataamua kutopiga kura au kumpigia kura mgombea Urais wa CCM.