Zitto kugombea urais 2015?

Zitto kugombea urais 2015?

Status
Not open for further replies.
tatizo la hili jukwaa wote sisi tunajidai ni watu wa kukosoa. Ukiuliza ebu great thinker chagua wizara , shiraka au jimbo moja unaloweza kuwa kiongozi. Taja mikakati mipango na maamuzi gani utafanya. Only few can answer this question

Most of us are just reactive waiting Ziitto to do this or kikwete to do this or Slaa to that.

Please let stop this trend.

Musembi Ungekuwa wewe ndo zitto ungefanya nini?

kweli mkuu hii ni kweli watz wengi kazi kulalamika tuuuuuuuuuuu lakini ukimwambia toa option hana kabisa ..pale cdm kuna watu kibao wanamuona zitto ni tisho kwao wanakaa wanazusha tuu inakera sana
 
umeongea kweli ndugu huu ni mkakati ambao una mgongo wa vizito wa chadema nia yao kumuundosha zitto katika duru ya siasa lkn kamwe wakimuuondosha kwa hila yyte ile na wao wajichimbie kaburi lao

umeandika uzushi
 
Nahic mwisho wa Zitto hautakuwa tofauti sana na Warid Kaburu kisiasa lets wait...
 
Kuna wastani wa thread moja au zaidi mpya kila siku inayomhusu Zitto Kabwe, tunavitu vingi kujadiliana tofauti hizi habari zinazojurudia tena za mtu mmoja kila mara. Je? ni kweli hatuna kitu kizuri tunachoweza sema kuhusu Zitto ? Zaidi ya hizi personal attacks..??

Kati ya vitu ambavyo CHADEMA wame-prove kuwa wapo makini ni namna ambavyo wameweza kum-handle Zitto, chama ndiyo kilimfikisha hapo alipo, umaarufu wake ulianza pale alipotolewa bungeni lakini CDM ikaamua kumbeba na kuunganisha watu ili ichukulie kitendo cha kufukuzwa bungeni na matokeoa ya ushujaa wake, na msimamo dhidi ya maslahi ya taifa, kweli watu wakjitokeza kwa wingi baada ili kuitikia wito wa chama.

Alipoona makutano ya watu kiasi kile akajua hii ni shauri ya yeye kama yeye kama Zitto na si chama, imani ikajengeka ndani yake kuwa yeye ni zaidi ya chama, akaanza kufuata utashi na hisia zake, kama treni iliyoacha reli...waandishi waliokuwa wanamsifia wakaona mwelekeo wake hatari, Kibanda akaandika kuonya, Ngurumo akaandika, Happiness Katabazi akaandika, wengi wakaandika, sikio la kufa halisikii dawa, magazeti makini yakaachana naye, akaenda kuibukia kwenye magazeti ya udaku, akayashambulia magazetu yetu kuwa, magazeti ya udaku ndiyo yenye nguvu na yasomwayo na watu wengi duniani, hakufafanua watu wa aina gani. Muda si mrefu urafiki na magazet hayo ukaisha baada ya kuandika skendo zake za ngono na wasichana kadhaa wanaodhani kuwa majina yao ni makubwa hapa nchini, kumbe yanafahamika tu na wala hayana ukubwa wowote.

Turudi kwenye mada...akazua hali ambayo ilitafsiriwa kama kizaazaa ndani ya CDM, nadhani alifanya makusudi ili afukuzwe aondoke "kishujaa"(kama alivyopokewa jangwani) kwasababu kuna watu ndani ya CCM walimdanganya kuwa akifukuzwa na hata akiipoteza nafasi ya ubunge, atapewa wa kuteuliwa na rais, pia kupewa unaibu waziri, na ili kumhakikishia hilo akajengewa ukaribu na idara za usalama na watu mashuhuri walio pretend kwenda kwake kupata ushauri na msaada wa mambo kadhaa, akazidi kuwa jeuri, lakini maskini kijana huyu hakujua kuwa watanzania walishamuona kimeo muda mrefu uliopita kiasi cha viongozi wa CDM kuwekwa katika msukosuko na wananachama wao kuwa kwa nini wanamlea, lakini uongozi ulionyesha ukomavu kwa kuendelea kuwa naye na kumkumbusha maadili ya chama na siasa kwa ujumla.

Kabla ya kampeni mwaka za mwaka jana, alitishia kutogombea, lakinibaadaye akapima akapima akaona namna maisha yatakavyokuwa magumu nje ya siasa, kwani hakuna kazi itakayomlipa kama siasa, ukichukulia kwa muda huo alishaamua kushiriki siasa kwa maslahi binafsi, hivyo akabatilisha msimamo wake na kuamua kutetea kiti chake, kampeni zilipowadia, akijua kuwa chama chake kimesimamisha mgombea wa nafasi ya urais, lakini akaonyesha kuibeza hatua hiyo kwa kusema kuwa, tunakwenda kuchagua wabunge na madiwani kwani rais tayari tunae tumuache amalize muda wake, lakini uongozi wa CDM uliendelea kumvumilia, Kitendo hicho cha uongozi wa CDM kuendelea kumvumilia kimebomoa sana Image ya Zitto kwa jamii,na kuifanya CDM ionekana kama chama imara kinachoweza kuishi pamoja hata inapotokea wakatofautiana mawazo kati yao.....kwa hili CDM nawapa sifa sana. Zitto amechuja lakini hilo halitambui tena kwasababu sasa hivi anaishi kwa kutegemea taarifa za wapambe. Ameaminishwa kuwa kila ampingae ni walewale wanaotumiwa dhidi yake.

Sasa hivi ni naibu Kiongozi wa kambi ya Upinzani bungeni anaongoza watu wasio mkubali watu ambao walipiga kura ya kumkataa, maamuzi ambayo hayakuwahi batilishwa popote pale, lakini kwasababu ya upenzi wake kwa madaraka bila kujari anaongoza kwa mazingira gani as long as anapata chake, katika hili Zitto hataki kutumia akili yake kama mwanasiasa kijana na msomi kama anavyotaka kutambulika, ameamua kung'ang'ania madaraka hayo bila suluhu ya aina yoyote, hataki kupisha nafasi hiyo kwa mtu mwingine anekubalika.

Zitto ambaye nahisi kila aonapo wakina Mnyika, Lema Lissu na wengineo wakitoa hoja zinazotikisa bunge huwa hajisikii vizuri kwa kuumia moyo, akitamani hali hiyo ya bunge kutetemeshwa kwa hoja ingesababishwa na yeye. alijaribu kutengeneza 'msukule/Zombi' wake pale bunge (Kafulila), lakini sijui ulipoishia, japo kuna yule bint, simkumbuki jina lake ila nadhani ni wa viti maalum CDM, lakini wote wapo off-color.

Huyo ndiye Zitto kabwe, ambaye sasa anataka atambulike kama rais mtarajiwa, kwani ameshatangaza dhamira yake ya kugombea urais mwaka 20015, Zitto ambaye watu wakimkubusha wajibu yeye anadhani ni watu wanaomuonea husda kwa 'mafanikio' yake kisiasa, Zitto anayeamini moyoni na kichwani mwake kuwa yeye ni zaidi ya chama, lakini mdomoni anahubiri kuwa hakuna aliye zaidi ya chama.

Nimeandika si kwa mtiririko rasmi wa uandishi na utoaji habari, bali kwa mtindo wa kugusia gusia tu ili kukumbusha, kwa lengo la kuendelea kufikiri na kutafakari kwa pamoja.
 
Nimefanya utafiti humu JF members, wengi wanaumwa hili gonjwa.
ZITTOPHOBIASIS, kupona kazi sana
 
Agenda yenu ya kumuuwa Zitto kisiasa kamwe haitafanikiwa, kila ukifungua JF ni Zitto tu, kwani Zitto atakuwa na umri gani 2015, kama sio njama tu za kumuuwa kisiasa. Naona siasa za kupakana matope zinainyemelea CDM. Jengeni hoja mmeandaa mpango gani wa kutatua kero za wananchi mkichukua madaraka, watu wanajua ipi pumba na upi mchele, watachagua tu wanachokitaka

Lakini lisemalo lipo.Zitto kabadirika sana kuna kitu kipo mbele yake.
 
Tatizo la Zitto ni kulewa kushabikiwa, halafu fedha za kuwafadhili akina Kafulila alizitoa wapi? au naye na kati ya mafisadi watakaojivua gamba Chadema?
 
Tunapungukiwa watu makini(Great thinkers) hapa JF, sidhani kama mtu makini ukishapitia thread kama hii na reply zake utaona haja ya kuweka mchango wowote, coz kinachoendelea hapa ni mipasho na majungu yasiyo na tija. Ningeomba ingawa tuna uhuru wa kuanzisha na kuchangia mijadala mbalimbali, mods mngekuwa mnaangalia thread zisizo na tija mziondoe!
 
Tunapungukiwa na watu makini(Great thinkers) hapa JF, sidhani kama mtu makini ukishapitia thread kama hii na reply zake utaona haja ya kuweka mchango wowote, coz kinachoendelea hapa ni mipasho na majungu yasiyo na tija. Ningeomba ingawa tuna uhuru wa kuanzisha na kuchangia mijadala mbalimbali, mods mngekuwa mnaangalia thread zisizo na tija kuziondoa.
 
Duh! Hivi ma-great thinkers ni wepesi kutolewa na kuhamishwa kwenye hoja namna hii?
Tuanze kujadili matatizo yetu ya msingi na halisi, nini kifanyike ili kusambaza huduma za maji safi na salama katika mikoa ya kati kusini na magharibi mwa Tanzania? Mkishindwe jipatieni wenyewe mji.
 
Jamani mbona MAgufuli katangaza nia kwenye facebook hasemwi? Zitto Kama katangaza mwache CDM iache wananchi watakachosema na kuamua..
 
Zitto ni ndumila kuwili kwa sababu ya tamaa zake ya madaraka na fedha wakati uongozi hawezi bali mpenda sifa tu.Chadema wala msimfukuze mwacheni ajikaange kwa mafuta yake mwenyewe ili mumdhibiti asiiletee chama kashfa kwa tamaa zake.
 
Zitto is done politically and there is no coming back. It's good to see he got his sense back and be Chadema one more time. The issue is "Trust and Credibility" Zitto had lost all and I will never forget all the spy and dirty works he did for ccm. Something still itch me that Zitto still work for Kikwete, just a thought. I think Zitto should be happy where he is and continue to represent his constituents thats it, but if he want to pursue something large i.e. presidential bid, the man is done for good. No one destroyed Zitto he did to himself thats end of the story. Guys lets move away from Zitto discussions.
 
kweli mkuu hii ni kweli watz wengi kazi kulalamika tuuuuuuuuuuu lakini ukimwambia toa option hana kabisa ..pale cdm kuna watu kibao wanamuona zitto ni tisho kwao wanakaa wanazusha tuu inakera sana
Anazushiwa yapi mkuu.watu hapa wanajadili maneno na vitendo vyake na si mambo ya nyuma ya pazia,utaje huo uzushi basi.mbona akitoa hoja za msingi bungeni kila mtu humu anamsifia?bado naamini Zitto ana move aliyopania kuifanikisha and time will tell kwasababu hawezi kuikimbia cdm kwa mazingira ya sasa ya kisiasa.Nyerere alikuwa Kichwa lakini daima mnyenyekevu na hiyo hata ukimwangalia unaona inatoka moyoni na penye mgongano wa mawazo alitumia nguvu ya hoja na watu wote kumuunga mkono na hatujawahi sikia kuwa aliwahi kushawishi watu kwa hila ili aungwe mkono.
 
Moto wawaka Chadema, NI VITA YA KAMBI ZA MBOWE, ZITTO


Sunday, 01 May 2011 22:56
Mbunge wa Kigoma Kaskazini na Naibu kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni Zitto Kabwe
Ramadhan Semtawa
VITA vya makundi vimezidi kuviandama vyama vikubwa vya siasa nchini, ambapo sasa hali si shwari ndani Chadema, ambako kunadaiwa kuwepo mkakati wa kumng'oa Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho, Zitto Kabwe.
Kabwe ambaye pia ni Mbunge wa Kigoma Kaskazini na Naibu Kiongozi wa Upinzani Bungeni, anadaiwa kuponzwa na msimamo wake kupinga ununuzi wa magari mitumba yenye thamani ya Sh480 milioni ya Chadema.
Hali hiyo ilijitokeza katika kikao cha Kamati Kuu ya Chadema kilichoketi juzi Jumamosi chini ya Mwenyekiti wa Chadema Taifa, Freeman Mbowe, kikao ambacho pia kilimg'oa John Shibuda katika nafasi ya kukaimu uenyekiti mkoa wa Shinyanga.Shibuda ambaye ni mbunge wa Maswa Magharibi ameondolewa baada ya kukalia nafasi hiyo takriban kwa siku nne tu tangu ateuliwe, kufuatia kifo cha aliyekuwa mwenyekiti wa Chadema mkoani Shinyanga Philip Shelembi ambaye alizikwa April 27, 2011.

Chanzo cha mvutano


Habari kutoka ndani ya kikao hicho cha Kamati Kuu na kuthibitishwa na baadhi ya wajumbe wa kikao hicho zinasema kuwa mbunge wa Arusha mjini, Godbless Lema, ndiye alianzisha mvutano wa kutaka Zitto ang'olewe kutokana na kupinga wazo la kununua magari chakavu kutoka India.

Chanzo chetu cha uhakika kilidokeza kuwa mashambulizi dhidi ya Zitto yalianza pale alipounga mkono hoja ya Profesa Mwesiga Baregu na Dk Kitila Mkumbo ambao walinukuliwa wakisema kwamba, isingekuwa sahihi kwa chama hicho kinachopinga ufisadi kufanya ufisadi kwa kununua magari chakavu wakati wamekuwa wakiibana serikali isifanye hivyo.

Baada ya Zitto kuunga mkono hoja hiyo, vyanzo hivyo nifafanua kuwa ndipo vurugu zilipoanza kwani Lema alianza kumrushia vijembe akisema kwamba Zitto ni tatizo na kwamba amekuwa akimtetea Shibuda.

Habari zinasema baadhi ya wajumbe walisema hoja ya Lema haikuwa na nguvu ya kumshutumu Zitto kwani Shibuda ni mbunge halali wa Chadema.

Duru zaidi za kisiasa kutoka ndani ya kikao hicho zinasema wakati mvutano huo ukiendelea, Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa alikuwa kimya huku kwa mara ya kwanza Mbunge wa Ubungo, John Mnyika akiwa mmoja wa wajumbe waliomtetea Zitto.

"Wakati Lema akisema hivyo, Dk Slaa wakati wote alikuwa kimya na hakusema chochote. Mnyika alisimama na kumtetea Zitto kwa mara ya kwanza, na katika utetezi pia alikuwepo Grace Kiwelu," kiliweka bayana chanzo hicho.

Katika majibizano hayo inadaiwa ulifika wakati Zitto alisimama na kumwambia mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe, kwamba mpango mkakati wake huo wa kujenga mtandao utakuja kumgharimu katika siku za usoni."Zitto alimwambia Mbowe mpango wake huo wa kujenga mtandao ungekuja kumletea matatizo hapo baadaye, "kilisema chanzo hicho kikimnukuu Zitto ndani ya kikao.

Kung'olewa kwa Shibuda


Mbali ya Zitto, Kamati Kuu hiyo pia iliazimia kutengua nafasi ya Shibuda, kukaimu nafasi ya uenyekiti ya Chadema mkoa wa Shinyanga.Vyanzo hivyo viliongeza kwamba, kabla ya mpango huo genge linalompinga Zitto lilimshutumu kwamba alikwenda Shinyanga na kushirikiana na baadhi ya wanachama kumweka Shibuda ili kutimiza ajenda zao.

Mvutano huo unaondelea ndani ya Chadema unazidi kukiweka chama hicho kinachokua na kuwa na malengo ya kukamata dola katika wakati mgumu kutokana na makundi mawili, huku moja likimuunga mkono Zitto na jingine Mbowe.

Zitto na Shibuda ni viongozi ambao wamekuwa wakikumbwa na misukosuko ndani ya Chadema na mara kadhaa Zitto amenusurika kung'olewa katika nafasi zake za uongozi kutokana na kile kinachodaiwa ni hulka yake ya kutofautina na wenzake hata katika mambo yenye maslahi kwa chama hicho kikuu cha upinzani nchini.

Kauli za Zitto, Shibuda


Zitto alipoulizwa na Mwananchi jana jioni kuhusu tafrani hiyo alisema "….tafadhali sana, naomba nisiongee chochote kwa sasa, hiki ni kipindi cha kukijenga chama, si kipindi cha kuonyesha umma kwamba Chadema kuna mgogoro".

Pale mwandishi alipomhoji zaidi alisema "…tafadhali naomba nikupigie baadaye" kisha kukata simuKwa upande wake Shibuda alikiri kusikia taarifa hizo na kuongeza kwamba, anasubiri apate taarifa rasmi kwani yeye alipewa heshima hiyo na wanachama wa Shinyanga kupitia vyombo vyao vya maamuzi.
 
Zitto practices modern politics,siasa zinazo endana na dunia ya leo.tatizo wana CDM wengi wapo biased na wmekaa ki chama chama zaidi kuliko ku focus issues...hii kasumba ipo ccm pia,so its the same trend,mzimu huu unawakumba wana CDM bila ya wao kujua..

Mfano: Zitto alipogombea uenyekiti wa CHADEMA ...hapa ndo matatizo yalipo anza na Zitto kuonekana mtovu wa nidhamu,mroho wa madaraka,puppet,ametumwa na mafisadi.kila neno baya alipewa.

Ukweli ni kwamba alikua anatimiza wajibu wake kama mwana chama na kwa kua muda ulikua umefika wa uchaguzi, katiba na kanuni zina mruhusu kugombea alifanya hivyo...

Mbowe na wapambe wake wakati wa uchaguzi wakaleta hoja ya uchanga wa chama,mara chama kitagawanyika na kumshauri zitto ajitoe, yes alikubali. Kama matatizo ya kugawanyika chama na chama kua bado kichanga kuhimili vishido vya uchaguzi, kwanini MBOWE aliye liona tatizo hili mapema asinge jitoa yeye kumpisha Zitto?

Jamani kila siku Zitto, Zitto, Zitto mbona majungu mengi kwa huyu mtoto kuna nini? Hao malaika wenu mbona hamjawahi kuwaandika vibaya au hawana mapungufu kabisa?
Wewe mama mtu mzima unasubuliwa na upenzi au maslahi kwa Zito. Huyu si wakumwani kabisa. Mtoa mada ameleza vizuri kabisa kama hujaelewa, basi toa hayo maslahi yako binafsi usome tena. Mimi sina imani na huyu mtu mpaka mwisho wa dunia.
 
U knw wt?mimi cioni umuhimu wa malumbano ya wana cdm kwa upande wangu zito yuko sahihi kabisa chama hakiwezi kununua magari chakavu kutoka india kwa sh 486 milions wakati cdm wenyewe wanaipiga ccm kufanya hivyo mbowe anamfwata lema aliyemchanga kwenye siasa mpashkuna huyu mi nashauri zito aendendelee na msimamo wake kabisa
 
Kati ya vitu ambavyo CHADEMA wame-prove kuwa wapo makini ni namna ambavyo wameweza kum-handle Zitto, chama ndiyo kilimfikisha hapo alipo, umaarufu wake ulianza pale alipotolewa bungeni lakini CDM ikaamua kumbeba na kuunganisha watu ili ichukulie kitendo cha kufukuzwa bungeni na matokeoa ya ushujaa wake, na msimamo dhidi ya maslahi ya taifa, kweli watu wakjitokeza kwa wingi baada ili kuitikia wito wa chama.

Alipoona makutano ya watu kiasi kile akajua hii ni shauri ya yeye kama yeye kama Zitto na si chama, imani ikajengeka ndani yake kuwa yeye ni zaidi ya chama, akaanza kufuata utashi na hisia zake, kama treni iliyoacha reli...waandishi waliokuwa wanamsifia wakaona mwelekeo wake hatari, Kibanda akaandika kuonya, Ngurumo akaandika, Happiness Katabazi akaandika, wengi wakaandika, sikio la kufa halisikii dawa, magazeti makini yakaachana naye, akaenda kuibukia kwenye magazeti ya udaku, akayashambulia magazetu yetu kuwa, magazeti ya udaku ndiyo yenye nguvu na yasomwayo na watu wengi duniani, hakufafanua watu wa aina gani. Muda si mrefu urafiki na magazet hayo ukaisha baada ya kuandika skendo zake za ngono na wasichana kadhaa wanaodhani kuwa majina yao ni makubwa hapa nchini, kumbe yanafahamika tu na wala hayana ukubwa wowote.

Turudi kwenye mada...akazua hali ambayo ilitafsiriwa kama kizaazaa ndani ya CDM, nadhani alifanya makusudi ili afukuzwe aondoke "kishujaa"(kama alivyopokewa jangwani) kwasababu kuna watu ndani ya CCM walimdanganya kuwa akifukuzwa na hata akiipoteza nafasi ya ubunge, atapewa wa kuteuliwa na rais, pia kupewa unaibu waziri, na ili kumhakikishia hilo akajengewa ukaribu na idara za usalama na watu mashuhuri walio pretend kwenda kwake kupata ushauri na msaada wa mambo kadhaa, akazidi kuwa jeuri, lakini maskini kijana huyu hakujua kuwa watanzania walishamuona kimeo muda mrefu uliopita kiasi cha viongozi wa CDM kuwekwa katika msukosuko na wananachama wao kuwa kwa nini wanamlea, lakini uongozi ulionyesha ukomavu kwa kuendelea kuwa naye na kumkumbusha maadili ya chama na siasa kwa ujumla.

Kabla ya kampeni mwaka za mwaka jana, alitishia kutogombea, lakinibaadaye akapima akapima akaona namna maisha yatakavyokuwa magumu nje ya siasa, kwani hakuna kazi itakayomlipa kama siasa, ukichukulia kwa muda huo alishaamua kushiriki siasa kwa maslahi binafsi, hivyo akabatilisha msimamo wake na kuamua kutetea kiti chake, kampeni zilipowadia, akijua kuwa chama chake kimesimamisha mgombea wa nafasi ya urais, lakini akaonyesha kuibeza hatua hiyo kwa kusema kuwa, tunakwenda kuchagua wabunge na madiwani kwani rais tayari tunae tumuache amalize muda wake, lakini uongozi wa CDM uliendelea kumvumilia, Kitendo hicho cha uongozi wa CDM kuendelea kumvumilia kimebomoa sana Image ya Zitto kwa jamii,na kuifanya CDM ionekana kama chama imara kinachoweza kuishi pamoja hata inapotokea wakatofautiana mawazo kati yao.....kwa hili CDM nawapa sifa sana. Zitto amechuja lakini hilo halitambui tena kwasababu sasa hivi anaishi kwa kutegemea taarifa za wapambe. Ameaminishwa kuwa kila ampingae ni walewale wanaotumiwa dhidi yake.

Sasa hivi ni naibu Kiongozi wa kambi ya Upinzani bungeni anaongoza watu wasio mkubali watu ambao walipiga kura ya kumkataa, maamuzi ambayo hayakuwahi batilishwa popote pale, lakini kwasababu ya upenzi wake kwa madaraka bila kujari anaongoza kwa mazingira gani as long as anapata chake, katika hili Zitto hataki kutumia akili yake kama mwanasiasa kijana na msomi kama anavyotaka kutambulika, ameamua kung'ang'ania madaraka hayo bila suluhu ya aina yoyote, hataki kupisha nafasi hiyo kwa mtu mwingine anekubalika.

Zitto ambaye nahisi kila aonapo wakina Mnyika, Lema Lissu na wengineo wakitoa hoja zinazotikisa bunge huwa hajisikii vizuri kwa kuumia moyo, akitamani hali hiyo ya bunge kutetemeshwa kwa hoja ingesababishwa na yeye. alijaribu kutengeneza 'msukule/Zombi' wake pale bunge (Kafulila), lakini sijui ulipoishia, japo kuna yule bint, simkumbuki jina lake ila nadhani ni wa viti maalum CDM, lakini wote wapo off-color.

Huyo ndiye Zitto kabwe, ambaye sasa anataka atambulike kama rais mtarajiwa, kwani ameshatangaza dhamira yake ya kugombea urais mwaka 20015, Zitto ambaye watu wakimkubusha wajibu yeye anadhani ni watu wanaomuonea husda kwa 'mafanikio' yake kisiasa, Zitto anayeamini moyoni na kichwani mwake kuwa yeye ni zaidi ya chama, lakini mdomoni anahubiri kuwa hakuna aliye zaidi ya chama.

Nimeandika si kwa mtiririko rasmi wa uandishi na utoaji habari, bali kwa mtindo wa kugusia gusia tu ili kukumbusha, kwa lengo la kuendelea kufikiri na kutafakari kwa pamoja.

Kwa mtazamo wangu Mh ZItto arudi kundini ashirikiane na wenzake kwa ajili ya kukiimarisha chama. Mh Zitto kumbuka wanaokushabikia wengi ni watu wa CCM na unajua wanalengo gani na CHADEMA. CHADEMA ikishavurugika hutamwona hata mtu mmoja watawakimbia wanawaacha mkiwa njia panda. CHADEMA hapa mlipofikia ni mahali pazuri ila panahitaji uvumilivu na kuvumiliana. Tunamdharau kamanda LEMA lakini anajitahidi sana kuwa kwenye ukweli.
 
Kwa maoni yangu kamanda Lema anatisha kisiasa kuliko Zitto, siku akikatiwa uzi anaweza kusema yasiyotarajiwa. Kifupi sidhani kama ni mwanasiasa mzuri kwani anaropoka sana.
 
Tusimshambulie msembi hayo ni mawazo yake,pia naomba nimuunge mkono msembi,hebu niulize wapenda mageuzi ktk tanzania hii inayomilikiwa na watu wachache,yuko wapi zitto kama yule wakati ni kiongozi UDSM?yukowapi zitto kama yule kabla hajafukuzwa bungeni?yuko wapi zitto kabla hajateuliwa kuwa mwenyekiti kamati ya hesabu za mashirika ya umma?jibu siyo zitto yule tuliyemzoea kabadilika hata ufunguzi wa matawi ya chama chake UDOM,ST JOHNS,MIPANGO,na kwingineko hatujamwona akijihusisha kitu ambacho kwa miaka ya nyuma ni lazima yeye ndo angekuwa mstari wa mbele,ni ukweli usiofichika mh zitto anahitaji kurudi kundini kabla ya huo uamzi wake huo na sisi kama vijana tuko tayari kumpokea kwa gharama yoyote maana hiki ndo chama pekee chenye kutufikisha safari tuliyoianzisha.TOGETHER WE CAN.dalali

Jiweke katika nafasi yake na uone utakuwa wapi!
Kila mwanasiasa ana ndoto ya kuwa step moja au zaidi ya alipo sasa, Zitto alitaka kugombea umwenyekiti wa chama chake anachokipenda. Na kwa kujua kwamba atashinda, wazee wa chama kina Mtei (Baba Mkwe wa Mbowe) walikaa naye chini kwa lazima na kumlazimisha aondoe jina, hii ni baada ya dikteta Mbowe kukataa kumsemesha Zitto, hatimaye Zitto akatii na tokea hapo hakuna siku Zitto kasemwa vizuri. Magazeti hasa gazeti la Mwana Halisi liliandika vitu vingi vibaya kuhusu Zitto mpaka ikafikia Zitto kuwataja wamililki wa gazeti hilo (Kubenea na Kiongozi Mkubwa Chadema-Finance and Administration Manager) akiwalalamikia. Toka hapo Mwanahalisi wakajivua gamba na hawakumwandika tena Zitto.

Ninachokiona Chadema; Zitto ni tishio na ana mipango ya kugombea nafasi kubwa kwenye chama sasa wenye chama (Wakaskazini) wanahaha na wameleta ngumi mkononi (Lema) kwenye chama ili amnyamazishe Zitto kwa sababu wanajua kwa hoja hawamwezi na atawashinda. Chezeni demokrasia ya kweli, CHADEMA (Chama cha Demokrasia na Maendeleo) tunautegemea mfano kutoka kwenu sio manguvu bali hoja.

Na tukiendelea hivi hiki kizazi kitakufa kabla hatujaitoa CCM madarakani, tunazungumzia mabanzi ndani ya macho ya maadui bila kuangalia mabolt machoni kwetu. Tuache demokrasia ichukue mkondo wake.

Nawasilisha.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom