Zitto Kabwe: Nakushukuru Rais Samia kwa kudumisha utulivu wa kisiasa kwenye taifa letu

The Phylosopher

JF-Expert Member
Mar 11, 2015
1,503
2,046
Alipozungumza kwenye mkutano wa rais amesema Rais ameleta utulivu wa kisiasa kwa nchi yetu hasa baada ya kuunda kikosi kazi.

Amesema Rais Samia ana dhamira ya dhati ya kufanya mambo makubwa kwa taifa letu, akiwaomba wananchi wampokee na kumuunga mkono.
---




"Rais wetu ana dhamira njema sana, ana maono na matamanio makubwa sana sio kwa nchi bali pia kwa Kigoma, niongee kama mwami, mama huyu hapa mpokeeni, tufanye naye kazi, tushirikiane naye tulete mabadiliko katika nchi" - Zitto Kabwe
 
Naam, Equilibrium imeanza kurejea polepole.
troll.png
 
Zitto katisha sana hapo tena pembeni ana buyu lake la asali ni mwendo wa kufyonza tu.
Ndio inavyotakiwa. Ili amani iwepo kila mtu anatakiwa apate. Ukitaka upate wewe na familia yako tu wengine wakose, amani itatoka wapi?
 
Mlamba asali

Zitto Kabwe asema "Rais wetu ana dhamira njema sana, ana maono na matamanio makubwa sana sio kwa nchi bali pia kwa Kigoma, niongee kama mwami, mama huyu hapa mpokeeni, tufanye naye kazi, tushirikiane naye tulete mabadiliko katika nchi"

Screenshot_20221018-153910_1.jpg

i
 
Alipozungumza kwenye mkutano wa rais amesema Rais ameleta utulivu wa kisiasa kwa nchi yetu hasa baada ya kuunda kikosi kazi.

Amesema Rais Samia ana dhamira ya dhati ya kufanya mambo makubwa kwa taifa letu, akiwaomba wananchi wampokee na kumuunga mkono.
Zito ni mnafiki mkubwa, utulivu gani ameleta huku akiwa amewafunga wapinzani wake mikono na midomo?
 
Zitto ni zezeta, juzi kule Songea mkoani Ruvuma, ACT Wazalendo wamekataliwa kufanya mkutano kwa kisingizio kwamba mikutano na mikusanyiko yote hairuhusiwi sababu ya tishio la ugaidi, lakini jioni hiyohiyo Mwamposa akafanya mkutano mkubwa sana nanukaendelea kwa siku tatu

Ungekua wewe umepewa V8 lako la kikosi kazi, mshahara milioni 12 kila mwezi na 2025 unapewa kiinua mgongo sawa na mbunge ungeacha kusifia tuache utani basi
 
Utulivu gani wa kisiasa?. Juzi chadema wamezuiliwa morogoro Tena kwenye msafara wa Katibu Mkuu. Aache unafiki.

Viongozi wa CHADEMA zindukeni mapema, kabla usiku haujaingia mkashtuka mmegeukwa.
 
Ndio inavyotakiwa. Ili amani iwepo kila mtu anatakiwa apate. Ukitaka upate wewe na familia yako tu wengine wakose, amani itatoka wapi?
"........KILA MTU APATE........",hapa sijakuelewa na wewe humo ktk kundi la hao watu..........
 
Back
Top Bottom