The Palm Beach
JF-Expert Member
- Dec 30, 2015
- 821
- 1,697
Kwa maoni yangu;Zitto Kabwe amesema mwaka 2012 alipata changamoto chama chake cha wakati huo cha CHADEMA akidai ilikuwa juhudi ya kumzuia kuwa mwenyekiti wa chama hicho, Zitto amesema kulikuwa na makubaliano baada ya kugombea uchaguzi wa nyuma yake kwamba amuachie kijiti Freeman Mbowe na atampokea miaka mitano ijayo na badala yake miaka miwili kabla aliondolewa nyazifa zote za uongozi Chadema na wapo katika kundi lao walisema waende CCM.
Zitto Kabwe amesema Jakaya Kikwete alimuita na kumwambia ana machaguo mawili kwa kuwa alikuwa anachipukia kwenye siasa, kwanza kujiunga na chama tawala cha CCM na endapo angefanya hivyo angempa uwaziri wa fedha siku inayofata.
Rais mstaafu Kikwete alimpa angalizo Zitto Kabwe kwamba kwa maono yake CCM haitakuwepo madarakani muda mrefu ilhali Zitto bado kijana mdogo na kumshauri kutafuta jukwaa lingine lakini sio la chama tawala.
Zitto amesema kwenye hicho kikao mmoja wa waliokuwepo ni rafiki yake Deo Fulikunjombe naye akamshauri asiende CCM.
1. Hata kama Zito Kabwe ingetokea akasimama na Freeman Mbowe na kushindanishwa katika sanduku la kura la Uenyekiti taifa, asingeweza kutoboa kwa mwamba.!
2. Na kwa upande mwingine, tu - assume basi kuwa angetoboa. Uhakika na ukweli ni kuwa, CHADEMA isingekuwepo leo na CCM wangekuwa wanatamba watakavyo.!
3. Hata hivyo tatizo la Zito Kabwe na wenzake kwa sababu ya kuyataka madaraka kwa njia yoyote (ukiwa ni mpango wa CCM yaJakaya Kikwete kwa kuitumia TISS kuivuruga na pengine kuisambaratisha CHADEMA by then), Hawa kina Zito Kabwe na wenzake hao kwa kujua au kutojua waliingia kwenye mkakati wa CCM through TISS wakajikuta wanatumia taratibu zilizo nje ya chama ili kuupindua uongozi halali uliokuwepo chini ya Uenyekiti wa Freeman Mbowe.
4. Thank to God kwa kuwa CHADEMA waliuona uasi huo mapema na kuchukua hatua kuudhibiti.
5. Zito Kabwe mwenyewe anathibitisha leo kuwa walitumwa na CCM kuivuruga CHADEMA wakati huo. Anasem kuwa baada ya kushindwa kwa mkakati wao immediately, walikutana na mwenyekiti wa CCM na Rais wa nchi wakati huo Jakaya Kikwete na kumwambia hiki anachokisema leo kuwa; "...sasa bwana mdogo naona mkakati wetu umefeli, tunafanyeje Sasa..?"
Mtazameni usoni na kile kinachotoka mdomoni kwake. Mara Moja mtu anaweza kugundua kuwa anadanganya na kutengeneza story tu ya kumwezesha kusonga mbele ..