domokaya
JF-Expert Member
- Apr 22, 2010
- 3,545
- 1,719
Hatua ya Zitto Kabwe kufanikiwa kuwapokea wanachama wa CUF karibu wote walioshusha tanga, ilikuwa turufu kubwa ya kisiasa kwa upande wake!
Hatua ya pili ilikuwa ya kumuweka Othman Masoud Othman katika nafasi ya Makamu wa Kwanza wa Rais baada ya kifo cha Maalim Seif Shariff Hamad. Hapa Zitto alitengeneza bargaining power kwa watawala. Yaani nipe I majimbo ya Pemba niwawekee mtu dhaifu kupoza siasa za Zanzibar. Ni wazi Zitto asingemtaka tena Babu Juma Duni Haji katika siasa za chama chake!
Kufanikiwa kwa Zitto kumshawishi Rais Hassan kumfutia makosa Mwenyekiti wa Chadema na kumshawishi Mbowe kuwa baridi atapoachiwa gerezani ni wazi kunamuhakikishia wabunge wengi Pemba ambapo ni ngome imara ya ACT kuliko Unguja. Zitto kwake wapemba wana faida kubwa kuliko waunguja, hivyo kukumbatia waunguja ni hasara, isipokuwa wale tu atakaoweza kushirikiana nao angalau kubakisha taswira ya Zitto Unguja.
Zitto anaaminika sana na Rais na Zitto ana ndoto ya kugombea urais. Vipi baada ya timu ya kina Makamba na Nape kukatwa mkia, Zitto anaona uwezekano wa kugombea urais 2030 kupitia CCM? Rais rafiki yake aliyepo madarakani atakuwa na nguvu ya kumlinda Zitto ili kumlipa fadhila za Zitto kuudhoofisha upinzani kufikia hatua ya kukidhoofisha chama chake mwenyewe?
Zanzibar imekuwa kitovu cha siasa zenye msisimko. Je, kama Zitto akifanikiwa kumpandikiza mtu wake asiye mwanasiasa, aliyepooza, asiyekuwa na historia na siasa za upinzani, Zanzibar itakuwaje? Wazanzibar watakata tamaa na kususia siasa ili rafiki zake Zitto waendelee kutawala?
Zitto Zuberi Kabwe ni bingwa wa siasa za kimkakati kufanikisha alichotumwa. Hakika katika hili Zitto atakuwa amefanikiwa kupoozesha upinzani nchi nzima, kuipa ACT hadhi ya chama msindikizaji CCM inapihitaji support na kubwa kuliko yote amefanikiwa kuwagonganisha Wazanzibar ndani ya ACT na kukijengea nyufa huku tayari akiwa amakilaza kitandani wodini, chama cha wananchi CUF!
Siasa lengo lake ni kupata mamlaka, hakika Zitto Zuberi Kabwe amefanikiwa!
Hatua ya pili ilikuwa ya kumuweka Othman Masoud Othman katika nafasi ya Makamu wa Kwanza wa Rais baada ya kifo cha Maalim Seif Shariff Hamad. Hapa Zitto alitengeneza bargaining power kwa watawala. Yaani nipe I majimbo ya Pemba niwawekee mtu dhaifu kupoza siasa za Zanzibar. Ni wazi Zitto asingemtaka tena Babu Juma Duni Haji katika siasa za chama chake!
Kufanikiwa kwa Zitto kumshawishi Rais Hassan kumfutia makosa Mwenyekiti wa Chadema na kumshawishi Mbowe kuwa baridi atapoachiwa gerezani ni wazi kunamuhakikishia wabunge wengi Pemba ambapo ni ngome imara ya ACT kuliko Unguja. Zitto kwake wapemba wana faida kubwa kuliko waunguja, hivyo kukumbatia waunguja ni hasara, isipokuwa wale tu atakaoweza kushirikiana nao angalau kubakisha taswira ya Zitto Unguja.
Zitto anaaminika sana na Rais na Zitto ana ndoto ya kugombea urais. Vipi baada ya timu ya kina Makamba na Nape kukatwa mkia, Zitto anaona uwezekano wa kugombea urais 2030 kupitia CCM? Rais rafiki yake aliyepo madarakani atakuwa na nguvu ya kumlinda Zitto ili kumlipa fadhila za Zitto kuudhoofisha upinzani kufikia hatua ya kukidhoofisha chama chake mwenyewe?
Zanzibar imekuwa kitovu cha siasa zenye msisimko. Je, kama Zitto akifanikiwa kumpandikiza mtu wake asiye mwanasiasa, aliyepooza, asiyekuwa na historia na siasa za upinzani, Zanzibar itakuwaje? Wazanzibar watakata tamaa na kususia siasa ili rafiki zake Zitto waendelee kutawala?
Zitto Zuberi Kabwe ni bingwa wa siasa za kimkakati kufanikisha alichotumwa. Hakika katika hili Zitto atakuwa amefanikiwa kupoozesha upinzani nchi nzima, kuipa ACT hadhi ya chama msindikizaji CCM inapihitaji support na kubwa kuliko yote amefanikiwa kuwagonganisha Wazanzibar ndani ya ACT na kukijengea nyufa huku tayari akiwa amakilaza kitandani wodini, chama cha wananchi CUF!
Siasa lengo lake ni kupata mamlaka, hakika Zitto Zuberi Kabwe amefanikiwa!