Zitto anataka kusaliti CHADEMA?

Zitto anataka kusaliti CHADEMA?

Status
Not open for further replies.
Hii makala imetoka katika gazeti la Mwanahalisi la wiki iliyopita. Imeandikwa na Ansbert Ngurumo, Mhariri wa Tanzania Daima na Press Secretary wa Mwenyekiti wa Taifa wa CHADEMA. MwanaHalisi linamilikiwa na Mkurugenzi wa Fedha na Utawala wa CHADEMA ndugu Antony Komu. MwanaHalisi limekuwa mstari wa mbele kunipaka matope na kutoa propaganda chafu dhidi yangu na sijui ni kwa faida ya nani.
Why all these, kama ni mchawi ni wewe mwenyewe kulikuwa na ulazima gani kuwataja viongozi wakuu wa Chadema, hivi ungesema hii makala ni ya MwanaHalisi isingetosha. Hata kama unasema watu wanakuzushia lakini mzushi mkubwa ni wewe, umekuwa ukianzisha controversial na chama baadaye unakuja kusema wanakuzushia, mfano uliposema siri za kura kwenye public nani alikuzushia kama si wewe kuanzisha matatizo. Zitto kama hutajirekebisha mdogo wangu hutafika mbali nakushauri kama una muda jaribu kuangalia uwezekano wa kuchukua short course ya Public Relations.
 
Zito huko bungeni unawez kuhoji kama kama Idara ya usalama wa taifa ina kitengo cha Economic na technology Intelligency. Na kama vipo nikitaka kupata ajira kwenye mojawapo ya vitengo hivyo nifanyeje.

Teh Teh teh

Zitto nacheka lakini sio mzaha
 
Mwaka 2010 - 2011 nimeamua kujikita kwenye Rural Growth, Gas and Petroleum sub-sectors and Leadership Ethics. Rural growth kwa ajili ya kusukuma nguvu katika cutting poverty levels vijijini. Bado ukuaji wa uchumi wa Taifa letu haufiki chini na hivyo hauendani kabisa na kupungua kwa umasikini. Ajenda hii imesahaulika sana sana. Baada ya kupata sheria mpya ya madini (bado ina mapungufu kidogo), napeleka nguvu kwenye kuhakikisha kuwa Gesi Asilia na Mafuta yanafaidisha nchi yetu. Lengo ni kusukuma kuwe na Sheria mpya ya Gesi na Mafuta ili kuepuka yaliyotukuta kwenye sekta ya Madini. Nina muswada wa sheria nilioandika ili kubadili sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma na Serikali kukataa kuuchapisha. Ninadhamiria kuhakikisha kuwa muswada ninaurudisha Bungeni. Lengo ni kutenganisha Biashara na siasa kwa kuanzisha blind trusts. Pia lengo ni kufanya sheria ya maadili iwe effective na wananchi wawe na uhuru zaidi wa kukagua mali za viongozi wao.

Mabo mengine ni masuala ya chama mfano suala la Katiba mpya nk.

Kwenye red ilikujenga imani kwa wengi,hoja hii ungeipendekeza kuwa Sera ya chama chako mkaijadili na kuipitisha na viongozi wote wa Chadema mkafanya hivyo (kuonyesha njia)na mwisho ukaipeleka Mjengoni.
 
Hapo naona kama unatupa taarifa ambazo hatukuhitaji kuzijua, isitoshe, kwa kusema hivyo unataka kutupa ujumbe gani? Na kwanini?

Kweli kama ni kijambo kimepata mjambaji..........

Ha ha ha ha!
 
Sijawahi kuomba Kikwete aongezewe muda. Tanzania Daima waliandika habari hiyo kwa lengo maalumu na nililalamika rasmi kwa Mhariri mtendaji. Unaona sasa unanihukumu kwa habari iliyotungwa? Ndio maana nimetaja Tanzania Daima na Mhariri wake maana hii ni scheme ya muda mrefu na nimelalamika sana kimya kimya. Hata suala la mimi kutangaza nitagombea 2015 liliandikwa na Tanzania Daima peke yake tena kati kati ya kampeni. Hakuan aliyejiuliza ni kwa nini gazeti linalomilikiwa na Kiongozi wa CHADEMA linaweza kuandika kitu kama kile katikati ya kampeni.

Zitto umejadiliwa sana hapa JF kwa mazuri na mabaya yako kwa sababu wewe ni public figure na kama mwanasiasa kijana umeinspire wengi binafsi nikiwemo. Hongera kwa kudeclare wazi kwa wale tuliokasirishwa na kitendo chako cha kutoingia bungeni na then kwenda kuongea na TBC1, wengi bila shaka watakuelewa kuwa lile tukio limeshapita na umeapologize kwa yale yaliyosababishwa na kitendo kile, uliyoyafanya ndani ya CDM ni mengi na mchango wako kila mtanzania anautambua. Haya mengine ni vema nyinyi viongozi wakuu mkajihadhari sana maana baada ya uchaguzi kwisha mkakati wa CCM ni kuhakikisha CDM inasambaratika kwa gharama zozote zile na watajaribu kutumia vyombo vya habari ili kuonyesha kuwa kuna mgogoro ndani ya chama hata inapotokea watu wakatofautiana mawazo kwao hilo litakuwa mgogoro.

Zitto na wenzako tunahitaji zile operation sangara zirudi, tujenge chama. Ile support mliyoipata wakati wa uzaguzi isipoendelezwa itapotea.
Hawa Tz daima na mwanahalisi wamejijengea heshima kwa sababu ya umakini wa habari zao na bahati nzuri wasomaji wale wa haya magazeti ni watu wenye upeo na wachambuzi wa mambo, kama watabadilika na kuanza kuandika habari zisizo na utafiti yuatakayo wakuta ni kama ya yale yaliyowakuta rai na mtanzania.
 
Zitto yuko juu wanaslaa na mbowe msiwe wanafiki huyu akili zimo sana sio kama mbowe na uchaguzi ujao wa chadema lazima awe mwenyekiti
 
Jamani, Zitto amefanya kosa na amekiri ya kuwa amefanya kosa, kwa hiyo tumsamehe kwa hilo. Ni lazima tutambue ya kuwa hakuna mwanadamu ambaye yuko perfect. Suala sio kuanguka, bali unafanya ni nini badala ya kuanguka. JF inamuhitaji Zitto na Mheshimiwa pia anaiitaji JF, kwani vitu alivyoambiwa hapa asingeweza kuambiwa sehemu yeyote.

CHADEMA ni chama kichanga, na kinachohitaji nguvu zetu katika kukijenga. Ushauri wangu tuzungumzie jinsi ya kukijenga chama na jinsi gani tutaanza kupanga mipango ya kuiondoa CCM madarakani mwaka 2015.
 
Nikusahihishe kidogo. Mnyika na Halima hawakuwepo kabisa Dodoma siku ya tukio au walikuwepo lakini hawakuja kwenye kikao na kisha Bungei. Mimi nilikuwepo kwenye kikao na kusema wazi mawazo yangu kuwa sioni kama ku walk out ni mkakati mzuri. Kwa kuwa sikuunga mkono maamuzi hayo niliamua kutokwenda kabisa Bungeni. Nimeshalisemea hilo na kulitolea maelezo hapa JF. Sikutaka kuwa mnafiki na kujificha katika pazia la wengine. Sasa kama ni uamuzi wa makos umeshatokea, muhimu ni kusahihisha makosa na kwenda mbele. Nawaomba radhi wale wote niliowaudhi kwa msimamo niliochukua na hivyo mkaumia. Mimi niliona ndio msimamo sahihi (kutokwenda Bungeni kabisa na kama kwenda kuto walk out). Wengi mmeona haukuwa msimamo sahihi. Nimesikia. Tupige mstari na tuendelee na kazi nyingine.
at least umeona kosa! ndo ukomavu wa kisias Mh
 
Sijafanya kikao chochote na Lowasa. Kulikuwa na kikao cha Lowasa na Mbowe ambacho mimi nilishiriki kama Naibu wa Mbowe Bungeni. Hata hivyo sijafanya kikao kingine chochote.
Punguza kutaja majina hasa ya kiongozi wako(hasa kwa mwelekeo wa kushoto) hapa unaonyesha kikao kilikuwa si cha chama ni cha Mbowe ulitakiwa kusema kulikuwa na kikao cha chama na wewe ulishiriki kama mmoja wa viongozi wakuu wa chama. Usiwe una-personalize vitendo vya chama.
 
Zitto back to the point je suala la transparency unaonaje liwe mpaka kwenye mishahara ya waheshimiwa wote pamoja na mikataba yote iwe transparent kwa any layman kuweza kuiona kwa urahisi. We need to know how much of our hard earned cash zinawalipa waheshimiwa
 
Mada ifungwe kwa kuwa ina jadili mgogoro wa chadema?Ingekuwa inahusu wana ccm hapa ungekuwa unapiga zumari!acheni hizo wanachadema acha mjadala uendelee!

Nani kakuambia CHADEMA kuna mgogoro? Mjadala ulimhusu Zitto, na tunashukuru amejitokeza kujieleza na sie tumeujua ukweli. CHADEMA hakuna MGOGORO! Shame on you Leem!
 
Na kutotabirika ni sifa njema eee!

Chadema nzima haitabiri lakini tusimlaumu sana kwa hilo. Leo Slaa anasema hatumtambui rais, siku ya pili Mbowe anauliza dhana ya kutomtambua rais imetoka wapi

Leo mtu analilia ubunge kwa nguvu zote mpaka kuwaaibisha viongozi wengine wa chama, baada ya siku 7 za ubunge anasema kaboreka.

Mwengine anajisifu kwenye post ya juu kuwa kazi ya uteuzi wa viti vya wanawake alitunukiwa yeye, baada ya post 20 anasema demokrasia ilitumika.

Natengeneza database ya Political Analysts na Policy Analysts nchini, naomba CV yako!
 
..niliwahi kueleza kwamba Zitto is not radical enough, or too soft, when it comes to dealing with CCM.

..mawazo na mitizamo yake iko tofauti na what Chadema's base support wants.

..binafsi nilianza kushtukia misimamo na mitizamo yake wakati wa Tume ya Afrika Mashariki ya Prof Wangwe. baada ya hapo akaja na misimamo ya ajabu ktk suala la dowans, then suala la Dr.Rashidi, tume ya Jaji Bomani, suala la gavana wa bot.


..it is very frustrating, kwasababu huyu ni kiongozi wa Chadema, and he wants to be the Chairman of the party, lakini mawazo,mitizamo,na hoja zake, ni as if you r dealing na kiongozi wa CCM.

..in my opinion, kinachoendelea baina ya Zitto na mahasimu wake ni MISTRUST. sasa ili waweze kufanya kazi kwa pamoja na kusonga mbele ktk kujenga chama inabidi upande mmoja ubadilike. ama Zitto aachane ni hii misimamo na hoja zake ambazo ni pro-CCM, au Zitto aamue kutetea na kusimamia kwa nguvu zote msimamo na mawazo ya wakereketwa wa Chadema.

..katika kufuatilia kwangu siasa sijaona chama chochote kile kikaongozwa na mtu ambaye haungi mkono hoja za party base/wakereketwa wa chama.
 
Zitto
Jiangalie sana unapofanya maamuzi ya kuongea na vyombo vya habari kwasababu watanzania Wanamtazamo hasi juu yako.........huu ndio ukweli you need to be careful.Otherwise your political capital will be eroded soon.................
 
Hapana Mkuu although i dont agree with people Bashing lakini banning thread itakuwa ni kuingilia freedom of speech, Hapo ndio credibility ya JF itakwenda out of the window.... Believe it or not most things ambazo zinaongelewa hapa na ndizo watu wanaongea mitaani... JF is just a reflection of what people think... am sure readers are bright enough kuchuja pumba na mchele.... lets not insult the intelligence of our readers
noted with thanks

But i think hakuna uhuru usio na mipaka na hakuna intelligence kwenye kurudiarudia post zinazofanana kwa mtu huyohuyo ilmradi zimeletwa na member mwingine


To me stalking/bashing has been synonymous these days

Hebu jiulize ndugu yangu, kama watu wanaongea mitaani kuhusu kitu fulani basi ni heri kila siku tuwe na thread hiyohiyo lakini inaanzishwa na mtu tofauti? why not working on one thread? to that would bring continuity in the communication, consistency and easy to follow thread/subject

We would rather have one or two threads than having a new one everyday
 
Ni vyema ikajulinana kuwa Zitto amekuwa "Zitto" kwa sababu ni mtu mwenye msimamo na anayependa kuweka wazi misimamo yake. Misimamo hiyo inapokuwa kupinga utendaji mbovu wa serikali sote hujarijika na kumpongeza. Hata hivyo, ni vyema tukatambua kuwa utendaji mbovu au makosa hayako serikalini tu. Yako kwa kila mmoja wetu popote tulipo. Na Zitto akiona atasema. Na ninaamini kwa asilimia 100 kuwa hufanya hivyo kwa maslahi ya Taifa.

Sasa basi tusimtake Zitto awe "Zitto kamili" kwenye hoja zinazohusu serikali, huku tukimtaka awe "nusu- Zitto" kwenye hoja za kichama.Kwa maslahi ya Taifa Zitto na watu wenye tabia kama zake wanapaswa kupongezwa, kuungwa mkono na kuongezewa nguvu. Ni kwa jinsi hii tu,tunaweza kupata utawala bora unaojali sheria. Zitto akiogopa kusema maoni yake kwa kisingizio cha maslahi ya Chama ilhali Taifa linahujumiwa, hawezi kuwa Zitto tunayejivunia.
 
Zitto
Jiangalie sana unapofanya maamuzi ya kuongea na vyombo vya habari kwasababu watanzania Wanamtazamo hasi juu yako.........huu ndio ukweli you need to be careful.Otherwise your political capital will be eroded soon.................

Swala siyo Zitto kuwa careful. Swala ni kwetu sisi kujiuliza kwa nini watanzania wana mtazamo hasi? Je, huo mtazamo ni natural au induced?
 
Sijawahi kusema mahala popote kuwa ndani ya CHADEMA kuna udini. Ninaomba clip ya TBC iwekwe hapa jamvini na mtu anionyeshe wapi nimesem kuwa ndai ya CHADEMA kuna udinni. Tafadhali usinywe sumu unazopewa.

Kweli hukusema CHADEMA kuna udini but kulisema nchi hii ina uchaguzi wa kidini.. Je ni agenda ya chama chako? ni kweli?
 
..niliwahi kueleza kwamba Zitto is not radical enough, or too soft, when it comes to dealing with CCM.

..mawazo na mitizamo yake iko tofauti na what Chadema's base support wants.

..binafsi nilianza kushtukia misimamo na mitizamo yake wakati wa Tume ya Afrika Mashariki ya Prof Wangwe. baada ya hapo akaja na misimamo ya ajabu ktk suala la dowans, then suala la Dr.Rashidi, tume ya Jaji Bomani, suala la gavana wa bot.


..it is very frustrating, kwasababu huyu ni kiongozi wa Chadema, and he wants to be the Chairman of the party, lakini mawazo,mitizamo,na hoja zake, ni as if you r dealing na kiongozi wa CCM.

..in my opinion, kinachoendelea baina ya Zitto na mahasimu wake ni MISTRUST. sasa ili waweze kufanya kazi kwa pamoja na kusonga mbele ktk kujenga chama inabidi upande mmoja ubadilike. ama Zitto aachane ni hii misimamo na hoja zake ambazo ni pro-CCM, au Zitto aamue kutetea na kusimamia kwa nguvu zote msimamo na mawazo ya wakereketwa wa Chadema.

..katika kufuatilia kwangu siasa sijaona chama chochote kile kikaongozwa na mtu ambaye haungi mkono hoja za party base/wakereketwa wa chama.

Joka Kuu,
Tatizo moja linaweza kuwa na njia mbalimbali ya kulitatua. Naamini Zitto anatamani angeweza kuitisha referendum leo na katiba mpya ikaundwa na by Dec 2011 tukawa tuna katiba mpya. Lakini reality anayokutana nayo Zitto inashape jinsi anavyodeal na matters. Hii ni busara. Hakuna haja ya kuwa radical tu hata kama unaona kuwa radical hakutabadili chochote. Tufanye vitu hatua kwa hatua, na tujitahidi zaidi kuwajenga waliojitolea kwenye hili badala ya kutafuta mianya ya kuwabomoa.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom