Zitto anataka kusaliti CHADEMA?

Zitto anataka kusaliti CHADEMA?

Status
Not open for further replies.
Sijawahi kuomba Kikwete aongezewe muda. Tanzania Daima waliandika habari hiyo kwa lengo maalumu na nililalamika rasmi kwa Mhariri mtendaji. Unaona sasa unanihukumu kwa habari iliyotungwa? Ndio maana nimetaja Tanzania Daima na Mhariri wake maana hii ni scheme ya muda mrefu na nimelalamika sana kimya kimya. Hata suala la mimi kutangaza nitagombea 2015 liliandikwa na Tanzania Daima peke yake tena kati kati ya kampeni. Hakuan aliyejiuliza ni kwa nini gazeti linalomilikiwa na Kiongozi wa CHADEMA linaweza kuandika kitu kama kile katikati ya kampeni.

Please mimi kama Mtanzania, who had lost hope kama kweli kutakuwa na upinzani wa kweli, mpaka Chadema ilipokuja na kufika hapa ilipo sasa, ninawaomba mkae nyote and sort out your differences behind the scenes, and make sure they are sorted.... Remember we are fighting the same battle, small differences zisitutenganishe, na kama kuna mchawi ndani ya chama basi aonywe na aadhibiwe.
 
Sijawahi kusema mahala popote kuwa ndani ya CHADEMA kuna udini. Ninaomba clip ya TBC iwekwe hapa jamvini na mtu anionyeshe wapi nimesem kuwa ndai ya CHADEMA kuna udinni. Tafadhali usinywe sumu unazopewa.,Umewaudhi wapenda mageuzi, hata wapigakura wako, kwa tabia yako ya kuonekana kigeugeu, kwa kuwa umejitokeza, tunachokuomba uyafanye mambo kwa vitendo kuturudishia imani. Vile vile kama kuna tofauti kati yako na uongozi, take action to solve, tuendeleze CHADEMA yetu. Ndani ya CHADEMA hakuna udini, kama ulipitiwa siku unahojiwa TBC, ifute ile kauli yako humu. Asante sana kwani kidogo nimeanza kupata imani na wewe.

Kaka zitto fanya kazi wananchi walokutuma achana na majungu, na kama hukukubaliana na mgomo wa Wenzako ungekuwa mwenye akili kama ungekaa kimya than kupayuka TBC, ulichemsha kaka hapo, ulionekana Kiherehere mbele ya CCM na Makamba au JK mwenyewe, ulionekana KIKOMEDY fulani kwa wanamageuzi halisia kama wewe, ulionekana nadhamilia kusema CHIZI kwa walio wengi wetu tunaokufahamu ndugu MPIGANIA ZITTO WA KABWE...TUBU MTU WANGU na ukubali ulichemsha otherwise hatutakuelewa hapo
 
Huwezi kutegemea ufanye makosa kisha usiandikwe kwa sababu tu gazeti linamilikiwa na mwenyekiti wa chama

Na kama unaona kuna tatizo kwenye hilo ulitakiwa uwasiliane na mwenyekiti wa chama na mjadiliane mpaka mpate suluhu. Kama msimamo wake ni hasi kwako, kwa faida ya chama unatakiwa umezee tu ufe kisabuni.

Hii ya kuja kuweka malalamiko ya kuonyesha kuwa kuna mvurugiko kwenye chama is not a good look kwako wala chama chako.

sikufanya makosa. Nimesema nimeandikwa ndivyo sivyo. Ningekuwa nimefnya makosa magazeti mengi zaidi yangeandika lakini liliandika moja tu. Sijaja kuweka malalamiko hapa JF. Kufa kisabuni yaweza kuwa ushauri mzuri lakini nimeukataa. Kufa kisabuni ni unafiki uliozidi kipimo. I am sorry for that.
 
Sijawahi kuomba Kikwete aongezewe muda. Tanzania Daima waliandika habari hiyo kwa lengo maalumu na nililalamika rasmi kwa Mhariri mtendaji. Unaona sasa unanihukumu kwa habari iliyotungwa? Ndio maana nimetaja Tanzania Daima na Mhariri wake maana hii ni scheme ya muda mrefu na nimelalamika sana kimya kimya. Hata suala la mimi kutangaza nitagombea 2015 liliandikwa na Tanzania Daima peke yake tena kati kati ya kampeni. Hakuan aliyejiuliza ni kwa nini gazeti linalomilikiwa na Kiongozi wa CHADEMA linaweza kuandika kitu kama kile katikati ya kampeni.
Si kweli tukio lili ripotiwa na TBC1 ukiongea.
 
Naona Zitto amesema vizuri yale anayofikiri. Nafikiri hakuna haja ya kuendeleza malumbano. Tukumbuke, we need to think about developing this nation. Halitaendelea hili Taifa kama bado tunaendelea kupoteza muda kwenye mambo yasiyo na tija. We have a part to play to contribute to our well being as JF members throught ideas that we throw everyday in the forums.
 
It looks like you guys don't even know the meaning of freedom. My take Zitto only exercises his freedom of choice of expression etc. He doesn't offend anyone. You can also exercise yours if you like. I think this is what all of JF members have been fighting for, what is strange there?.

Consider CHADEMA wins election what will happen to people who dares like Zitto?!, all complaints you are laying here are just meant to express your true characters.

Macho yangu mwaka huu!!!!!
 
Kaka zitto fanya kazi wananchi walokutuma achana na majungu, na kama hukukubaliana na mgomo wa Wenzako ungekuwa mwenye akili kama ungekaa kimya than kupayuka TBC, ulichemsha kaka hapo, ulionekana Kiherehere mbele ya CCM na Makamba au JK mwenyewe, ulionekana KIKOMEDY fulani kwa wanamageuzi halisia kama wewe, ulionekana nadhamilia kusema CHIZI kwa walio wengi wetu tunaokufahamu ndugu MPIGANIA ZITTO WA KABWE...TUBU MTU WANGU na ukubali ulichemsha otherwise hatutakuelewa hapo

Kukaa kimya ni unafiki. sikuona kosa kujibu swali nililoulizwa kwa nini sikwenda Bungeni. Hata hivyo nimeshasema, hili limeonekama kuudhi wengi. Ninaoba radhi.
 
Si kweli tukio lili ripotiwa na TBC1 ukiongea.

weka clip y TBC1 inayoonyesha kuwa nilisema nitagombea Urais. Tanzania Daima nao walisema nilisema hivyo TBC na source yao ilikuwa TBC. Wangeweza hata kunitafuta ni balance kama wasemavyo wenyewe waandishi lakini hawakufanya hivyo. Walijua wanafanya nini. Magazeti mengine yangeweza kuandika toka TBC pia. Mwananchi waliniuliza na nikawaeleza what happened, hawakuandika. Tanzania Daima?
 
Zito
kumbuka upinzani hata wale wa canada, Norway, Australia bado kazi yao ni kukosoa serikali.

Je una mipango gani yenye priority kwako kuhusu mfuko wa jimbo ?
je katika serikali hii utajikita kuban utendaji wa wizara gani hasa? Tunaweza kukusaidia kukupa baadhi ya data za kuhoji

Otherwse nakutakia U MP mwema
 
sikufanya makosa. Nimesema nimeandikwa ndivyo sivyo. Ningekuwa nimefnya makosa magazeti mengi zaidi yangeandika lakini liliandika moja tu. Sijaja kuweka malalamiko hapa JF. Kufa kisabuni yaweza kuwa ushauri mzuri lakini nimeukataa. Kufa kisabuni ni unafiki uliozidi kipimo. I am sorry for that.

Basi usilalame tukikunukuu kuwa umesema kuna mvurugiko ndani ya chama kwa sababu ndo ulichokisema leo.

Kuwa huwezi kufa kisabuni kwa hiyo umeamua ufe pamoja na wengine.

Umeamua kusema kuwa kuna watu wanaokuhujumu, tena ni watu wa karibu sana na mwenyekiti wako, ili usitupiwe lawama peke yako, bora 'uoza' wa chama wote uuanike nje.

Hao mentors wako ndo walivyokufundisha hivyo? Kuwa faida na image yako lazima iwe mbele, chama baadae?
 
Zito ushauri wangu let your job do the talking, am sure ukianza kufight for the people na kuwabana mafisadi kama long time all this will go away..... No one will dare talk bad about you. Kwahiyo please ungana na vijana wetu wengine na uwape support, Wenje, Sugu etc, ili chadema iwe tishio
 
mkuu zitto

Ninakuelewa vizuri sana na umekua makini..... msisitizo wangu ni kwamba ... kwakuwa tayari umeshaonyesha dhahiri kwamba magazeti haya mawili ambayo yanamahusiano ya karibu na kina na uongozi wa CHADEMA hususan menyekiti wako... nadhani huu sio muda wa wewe kusema sijui kwanini magazeti haya yananichafua.... itakuwa ni adabu ya woga ndani ya chama.... dont be and ignorant of law..... as it is not an excuse, unaonyesha haujui taratibu na vifungu vya sheria za chama chako kwa jambo hili...... hivi hakuna discplinary organs za ngazi ya juu ndani ya chama ukayafikisha haya direct na mkamaliza ........ very silent.... hatupendi muwe na malumbano we are behind you as our endeavors of change and true democracy
 
Nashukuru sana kwa ushauri wako. Wakati mwingine ukikaa kimya maadui zako huona kama ndio umekiri. Nimekaa kimya sana sana. Nilisimama kabisa kuja hapa nikadhani itapunguza chuki za watu. Hata hivyo haikukoma. Hata hivyo ushauri wako nimeuchukua kwa mikono miwili. Asante sana sana

Kama bahati tu.
Mh.Zitto huo ushauri huyo bwana kwa kweli ukiusoma unaoneka kutoka moyoni.
Napenda kuongezea kuwa si humu JF tu ambapo unafaa kuchunga na kuwa makini kuongelea mambo ya Chama Chako au ya kwako binafsi hasa pale ambapo unadhani yanaweza husishwa na Chama au status yako ya Kisiasa bila ya kuyapima kwa umakini mkubwa.
Sisi wengine unatuumiza na hasa wanachama wa Chama Chako pale ambapo unakuwa mbele kuliko chama chako katika kutoa habari kwa vyombo vya habari ili hali Chama kama Taasisi bado haijatoa habari husika.
Ni kweli kuwa tunafaa kuwa na Uhuru wa kusema lakini tunafaa kuwa makini kupima tunayosema maadui zetu wanafaidika namna gani au tunaendelea kuwabomoa kiasi gani
Asante na endelea kuwatumikia wana Kigoma na TZ kwa uadilifu mkubwa na Mungu akujaze hekima na busara ili Mafisadi wasikuchote na kukuweka kwenye hima yao.
 
Basi usilalame tukikunukuu kuwa umesema kuna mvurugiko ndani ya chama kwa sababu ndo ulichokisema leo.

Kuwa huwezi kufa kisabuni kwa hiyo umeamua ufe pamoja na wengine.

Umeamua kusema kuwa kuna watu wanaokuhujumu, tena ni watu wa karibu sana na mwenyekiti wako, ili usitupiwe lawama peke yako, bora 'uoza' wa chama wote uuanike nje.

Hao mentors wako ndo walivyokufundisha hivyo? Kuwa faida na image yako lazima iwe mbele, chama baadae?

Gaijin
Zitto akioga wengine wanachafuka na wengine wakioga uchafu unamrukia zito.

Sioni tatizo kwa zitto kujaribu kujisafisha. mradi tu uwe ukweli. Kama akijisfishakwa ukwelihtakama mwenyekiti atachafuka ni haki yake. Ila jambo lililo wazi vyombo vya habri tanzania vinatumika na vinatumiwa vibaya. few days back i saw one face of zitto. 2 day I see anaother face. Huruma inanijia kwa zitto na CHADEMA. ila sijajua ukweli ni upi
 
Zito
kumbuka upinzani hata wale wa canada, Norway, Australia bado kazi yao ni kukosoa serikali.

Je una mipango gani yenye priority kwako kuhusu mfuko wa jimbo ?
je katika serikali hii utajikita kuban utendaji wa wizara gani hasa? Tunaweza kukusaidia kukupa baadhi ya data za kuhoji

Otherwse nakutakia U MP mwema

Mwaka 2010 - 2011 nimeamua kujikita kwenye Rural Growth, Gas and Petroleum sub-sectors and Leadership Ethics. Rural growth kwa ajili ya kusukuma nguvu katika cutting poverty levels vijijini. Bado ukuaji wa uchumi wa Taifa letu haufiki chini na hivyo hauendani kabisa na kupungua kwa umasikini. Ajenda hii imesahaulika sana sana. Baada ya kupata sheria mpya ya madini (bado ina mapungufu kidogo), napeleka nguvu kwenye kuhakikisha kuwa Gesi Asilia na Mafuta yanafaidisha nchi yetu. Lengo ni kusukuma kuwe na Sheria mpya ya Gesi na Mafuta ili kuepuka yaliyotukuta kwenye sekta ya Madini. Nina muswada wa sheria nilioandika ili kubadili sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma na Serikali kukataa kuuchapisha. Ninadhamiria kuhakikisha kuwa muswada ninaurudisha Bungeni. Lengo ni kutenganisha Biashara na siasa kwa kuanzisha blind trusts. Pia lengo ni kufanya sheria ya maadili iwe effective na wananchi wawe na uhuru zaidi wa kukagua mali za viongozi wao.

Mabo mengine ni masuala ya chama mfano suala la Katiba mpya nk.
 
Basi usilalame tukikunukuu kuwa umesema kuna mvurugiko ndani ya chama kwa sababu ndo ulichokisema leo.

Kuwa huwezi kufa kisabuni kwa hiyo umeamua ufe pamoja na wengine.

Umeamua kusema kuwa kuna watu wanaokuhujumu, tena ni watu wa karibu sana na mwenyekiti wako, ili usitupiwe lawama peke yako, bora 'uoza' wa chama wote uuanike nje.

Hao mentors wako ndo walivyokufundisha hivyo? Kuwa faida na image yako lazima iwe mbele, chama baadae?


Nionyeshe wapi nimesema kuna mvurugano ndani ya chama. Sijasema hivyo. Hiyo ni tafsiri yako na una haki ya kuweka tafsiri ya jambo lolote. Siwezi kukuingilia uhuru wako wa kutafsiri.
 
Mwaka 2010 - 2011 nimeamua kujikita kwenye Rural Growth, Gas and Petroleum sub-sectors and Leadership Ethics. Rural growth kwa ajili ya kusukuma nguvu katika cutting poverty levels vijijini. Bado ukuaji wa uchumi wa Taifa letu haufiki chini na hivyo hauendani kabisa na kupungua kwa umasikini. Ajenda hii imesahaulika sana sana. Baada ya kupata sheria mpya ya madini (bado ina mapungufu kidogo), napeleka nguvu kwenye kuhakikisha kuwa Gesi Asilia na Mafuta yanafaidisha nchi yetu. Lengo ni kusukuma kuwe na Sheria mpya ya Gesi na Mafuta ili kuepuka yaliyotukuta kwenye sekta ya Madini. Nina muswada wa sheria nilioandika ili kubadili sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma na Serikali kukataa kuuchapisha. Ninadhamiria kuhakikisha kuwa muswada ninaurudisha Bungeni. Lengo ni kutenganisha Biashara na siasa kwa kuanzisha blind trusts. Pia lengo ni kufanya sheria ya maadili iwe effective na wananchi wawe na uhuru zaidi wa kukagua mali za viongozi wao.

Mabo mengine ni masuala ya chama mfano suala la Katiba mpya nk.

Hapo penye red ninakuunga, na isiishie hapo tu kuwe na trasparency ya kuweza kujua chochote kinachohusu serikali, iwe mishahara ya maraisi, wabunge, mawaziri, na mikataba iwe open kwa mwananchi yoyote aweze kuona. Hizi secrecy sitatufikisha pabaya
 
Gaijin
Zitto akioga wengine wanachafuka na wengine wakioga uchafu unamrukia zito.

Sioni tatizo kwa zitto kujaribu kujisafisha. mradi tu uwe ukweli. Kama akijisfishakwa ukwelihtakama mwenyekiti atachafuka ni haki yake. Ila jambo lililo wazi vyombo vya habri tanzania vinatumika na vinatumiwa vibaya. few days back i saw one faceof zitto 2 day I see anaother face. Huruma inanijia kwa zitto na CHADEMA. ila sijajua ukweli

Nakubaliana na wewe kuwa vyombo vya habari vinatumiwa na watu kwa ajili ya manufaa yao.

Lakini bado tunabaki na mshangao kuona mgogoro mkubwa namna hii wa kufika kumchafua mara kwa mara kwenye magazeti umeshindwa kupatiwa ufumbuzi ndani ya chama.

Kwa nini asipeleke malalamiko rasmi kwa uongozi wa chama? Hili lingejadiliwa na uongozi wa juu lingepatiwa ufumbuzi au anataka kutwambia kuwa uongozi wa juu wote hauko pamoja nae?

Na akitwambia hivyo tutaanza tena kuja na masuali ya 'kwa nini?'

Hapo ndo watu wanapopewa mwanya wa kutunga sababu zao lukuki na amini kuwa kila upande utapata washabiki wa kutosha kiasi cha kusambaratisha chama.

Namshauri awe na mipaka kwa yale anayoyasema mbele ya jamii hata kama ni katika kujisafisha hasa akiona kujisafisha huko kutaleta masuala mengi zaidi ya majibu.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom