Ndugu wana JF,
Kumekuwa na mada nyingi sna humu ndani ambazo zinajaribu kuonyesha kuwa mimi ni mkosaji na kunipaka matope sana. Nimejdiliwa mno katika jf na hata kuzushiwa mambo mengi sana. Kuna wanaonisema kwa dhati y moyo wao kwamba nimekosea hapa na pale na kuna wanaoona huu ndio wakati wa kumwangusha Zitto na hivyo kuendeleza propaganda za kila namna.
Hii makala imetoka katika gazeti la Mwanahalisi la wiki iliyopita. Imeandikwa na Ansbert Ngurumo, Mhariri wa Tanzania Daima na Press Secretary wa Mwenyekiti wa Taifa wa CHADEMA. MwanaHalisi linamilikiwa na Mkurugenzi wa Fedha na Utawala wa CHADEMA ndugu Antony Komu. MwanaHalisi limekuwa mstari wa mbele kunipaka matope na kutoa propaganda chafu dhidi yangu na sijui ni kwa faida ya nani.
Nadhani mmenijadili vya kutosha. Itoshe kusema nimesikia. Yale ambayo ni makosa nitajirekebisha maana mimi ni binaadamu. Yale ambayo ni uzushi, uwongo na propaganda nitayadharau.
Jambo moja nilisema na nimeshalisema huko nyuma ni kwamba, nimekuwa mwanachama wa CHADEMA toka nikiwa nina umri wa miaka 16 na sasa nina miaka 35, sijawahi kuwa mwanachama wa chama kingine chochote cha siasa. Sitegemei kuwa mwanachama wa chama kingine chochote cha siasa tofauti na CHADEMA. Sijawahi hata siku moja kusaliti chama changu na wala sitajaribu kufanya hivyo. Nina utii kwa Katiba ya chama changu na kwa chama kama Taasisi (Asasi). Pamoja na kutofautiana kimawazo na viongozi wenzangu (wote hatuwezi kufikiri sawasawa) sijawahi kukiuka maamuzi halali ya vikao vya chama kwa mujibu wa Katiba.
CHADEMA ni taasisi inayokua na hivyo changamoto zinaongezeka kila siku. Ni jukumu letu kuhakikisha kuwa tunazikabili changamoto hizi bila kuathiri kazi iliyombele yetu ya kujenga Tanzania yenye demokrasia ya kweli na yenye watu wenye fursa ya kuendeleza maisha yao.
Siasa za kupakana matope. Siasa za kumalizana. Siasa za maji taka, hazitasaidia nchi yetu wala chama chetu. Ifikapo mwaka 2015, wanachama wataamua nani atabeba bendera ya chama kwa njia za kidemokrasia. Hakuna sababu ya kuanza kumalizana sasa. Tukajenge chama wilayani na vijijini ili ifikapo uchaguzi ujao tuwe na mawakala kila kituo, walinde kura zetu na tuweze kushika Dola na kuongoza.
Watanzania mtusaidie katika jukumu hili. Jumamosi njema
Ni vizuri ulivyoweka msimamo wako Hadharani hivyo kuondoa maneno maneno ya watu ( marafiki wa CDM na MAADUI wa CDM na wananchi wa kawaida wenye mapenzi mema na nchi yao)
Lakini kwa upande wangu umeibua hisia za kuwepo mgogoro mkubwa ndani ya CDM maana umetubainishia kuwa
Ansbert Ngurumo ni Press Secretary wa Mwenyekiti wa Taifa wa
CHADEMA na pia MwanaHalisi linamilikiwa na Mkurugenzi wa Fedha na Utawala wa CHADEMA ndugu
Antony Komu katika POST yako umeonyesha kuwa gazeti la MWANAHALISI lipo mstari wa mbele ktk kukuchafua, nanukuu"MwanaHalisi limekuwa mstari wa mbele kunipaka matope na kutoa propaganda chafu dhidi yangu na sijui ni kwa faida ya nani". Hivyo kwa mtazamo wako na maelezo yako yanabainisha kuwa CHADEMA mnatafunana wenyewe kwa wenyewe kama SENENE swali kichawani mwangu mnatafunana kwa maslahi ya CHAMA au BINAFSI au ya Adui CCM?
Lakini ni vyema ufahamu na tufahamu kuwa
Ansbert Ngurumo ana haki ya kuwa na mawazo yake na msimamo wake tofauti na wa mwenyekiti, pia ana haki ya kutoa msimamo wake. Cha kujiuliza je msimamo alioutoa katika makala yake alilazimishwa na wenyekiti au una mlengo wa kumjenga mwenyekiti na kumualibia
ZITTO?
Je makala za kumchafua
ZITTO katika gazeti la Mwanahalisi(kama anavyolalamika ndugu yetu ZITTO) je ni maelekezo ya mmiliki wake
Antony Komu au ni maoni na misimamo ya waandishi wa Makala hizo?
Ni vyema Mpiganaji Mwenzetu
ZITTO akawa makini ktk suala hili maana kitendo chake cha kutoingia
BUNGENI kimewaumiza wanaharakati na wapiganaji wengi, Lakini maoni na ufafanuzi alioutoa TBC 1
huo umewaudhi na kuwa kwaza na kuwavunja imani wanaharakati, wapiganaji, wana CDM na WATANZANIA wengi wapenda mapadiliko. ZITTO kwa kiukweli umetuumiza na kutukwaza
mimi ni mmoja wa watu ambao tunakuamini na kuona wewe ni kiongozi shupavu na mkweli kwa CHAMA na NCHI yako. Lakini kwa maoni na utetezi wako TBC1 hapana je ungekaa kimya nini kingetokea, wajua kutoingia kwako Bungeni ilikuwa ni habari tosha kwa wanahabari je kabla ya kutoa utetezi wako na maoni yako ulipima kwanza? Je una kumbukumbu nzuri na TBC1 ilichokuwa inakifanya wakati wa kampeni kuidhoofisha CHADEMA? Je Kituo hicho cha TV yaani TBC1 uliona ndio kituo sahihi kwa wewe kutolea ufafanuzi au utetezi wako? Pia kusema kuwa kikao mlichokaa wabunge na kupiga kura ili kukubaliana kama mtoke bungeni au la wakati Rais anahutubia mliotaka msitoke mlishindwa hivyo waliotaka mtoke walishinda je wewe kutokufuata makubaliano ya kikao si ndio kukiuka DEMOKRASIA unayoihubiri siku zote? si kukisaliti CHAMA chako maana ni
CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO? kweli unadhamini
MAENDELEO unayosema yameletwa na
KIKWETE jimboni kwako na Kuikana
DEMOKRASIA ktk chama chako? Pia kusema ni kweli umefanya kosa kwa kushiriki ktk kutoka ktk Bunge kama mlivyo kubaliana na una subiri
ADHABU ya CHAMA, (ZITTO kiongozi wangu na mpiganaji wangu kweli ulikuwa serious) Huoni kuwa una watega viongozi wenzako kwa kufanya kosa makusudi halafu unasubiri wenzako wakuadhibu ili baadae ulalamike/uwashutumu kuwa wanakuadhibu kwa sababu hauko kundi lao (yaani wewe ni mpinzani wa mwenyekiti)?
Ninamaswali mengi juu yako Kiongozi/kamanda ambayo nahitaji majibu, lakini ustaharabu wako wa kukiri kosa na kutuelezea kwa kifupi nini kinachoendelea au anachohisi unatendewa kwangu naona hupo sahihi na bado upo nasi ktk mapambano.
USHAURI WANGU KWAKO, MBOWE NA CHADEMA
CHADEMA Kilianzisha mapambano ktk kipindi kigumu cha 1995 lakini hakuna aliyegungua kuwa chama hicho ni NURU na MKOMBOZI kwa watanzania HADI MWL. NYERER alipotubainishia kuwa amesoma sera za vyama vyote na amekubali kuwa sera za CHADEMA ni sera za CHAMA mbadala, watu bado walikuwa wazito kuelewa lakini mapambano mliyoyaendesha toka 2000 hadi 2010 yamebainisha ukweli. Katika kuijenga CHADEMA hakuna asiyeuona mchango wa MBOWE, SLAA, ZITTO,MTEI, BOB MAKANI, BAREGU, Late CHACHA WANGWE, ARFI, KOMU,REGIA MTEMA, KAFULILA(nahodha aliyejitosa baharini),NDESA,MDEE na wengi wengi toka waanzilishi hadi waliojiunga wakati wa kampeni kama kaka SHIBUDA, kila mmoja anamchango wake ktk ujenzi wa CHAMA.
Ni wazi kuwa chama ni kundi la watu waliokubaliana kiitikadi na kisera kugombea ili kuchukua madaraka ya kuongoza nchi. na si kundi la watu wenye mawazo sawa,akili sawa na waliokubaliana kiitikadi na kisera kugombea ili kutwaa madaraka ya kuongoza nchi kwakuwa mnatofautiana mawazo na akili hivyo ni wazi mnaweza kutofautiana ktk utekelezaji wa sera, au kuongoza chama husika, hivyo kutofautiana ni lazima pia kutofautiana kunaweza kupelekea chama kwenye migogoro (Disputes) na ni wazi kuwa migogoro ikitumiwa vyema uimarisha CHAMA hiyo ni positive effect ya Disputes hivyo si vyema kiunyesha Watanzania mna migogoro badala ya kuitatua ndani ya chama ili iweze kuimarisha chama, nje ya chama kuna watu wakila aina wenye mapenzi na wasio na mapenzi kwa chama.
JAMANI ACHENI KUCHEZA NA MEDIA KATIKA MASUALA SENSITIVE KWA CHAMA wanachama wamewapa uongozi hivy onyesheni uwezo wenu wa uongozi kwa kutatua migogoro ya ndani ya chama bila kuinadi ktk media.
Kuhusu nani agombee urais 2015 chama kama kawaida kipige utafiti wa kisayansi ili kumpata mgombea na si viongozi muanze kujijenga kwa kuchafuana ili muonekane mnafaa mbinu hizo ni za CCM acheni kuturudisha turikokimbia. PIA UCHAGUZI mkuu wa CHADEMA uonyeshe Demokrasia ya kweli na si kuombana kutoa majina mjenge mazoea ya ndani ya chama ya kukubali kushindwa au kushinda ili yakitokea hukunje ya chama ktk chaguzi za nchi tuwe kweli mfani wa DEMOKRASI kwa kukubali kushinda na kushindwa kama chaguzi ni za kidemokrasia na si mbinu ya CCM ya kupita bila kupingwa hapo dhana ya cham cha DEMOKRASIA itapoteza maana
ZITTO na viongozi wenzako kumbukeni kujikwaa si kuanguka(sio mimi wahenga ndivyo wasemavyo) jipangeni kuendeleza mapambano. JAMANI MUDA HUU NI VITA YA KUDAI KATIBA MPYA, TUME HURU YA UCHAGUZI, MGOMBEA BINAFSI na MAZINGIRA SAWA YA UENDESHAJI SIASA NCHINI, MGAWANYO SAWA WA RASILIMALI ZA NCHI, KUONDOA UMASIKINI ULIO TAMALAKI NCHINI na KUTOKOMEZA UFISADI.
NYINYI CHADEMA NDIO WAPIGANAJI MLIO MSTARI WA MBELE KUSITASITA NI KUTUSALITI( WAYAHUDI USEMA NI HERI MMOJA AFE KWA AJILI YA WENGI) ZITTO NA VIONGOZI WENZAKO Huu SIO wakati wa kuchagua silaha, eti silaha hii sio nzuri na hii ni nzuri suala lililopo ni kuwa kama silaha inauwezo wa kummaliza ADUI itumike hata kama ni KOMBEO
nawasilisha