Zitto anataka kusaliti CHADEMA?

Zitto anataka kusaliti CHADEMA?

Status
Not open for further replies.
Zitto je tuko pamoja kwenye kudai katiba mpya na kuisarambatisha nec

Madai ya Katiba mpya nchini sio madai mapya. Toka mfumo wa vyama vingi umeanza kwa nyakati tofauti kumekuwa na madai ya Katiba mpya. Yanaibuka na kupotea. Nimeshiriki katika madai haya toka nikiwa shuleni. Mwaka 1998 nikiwa nimemaliza kidato cha Sita Tosamaganga na kupita Dar es Salaam nikielekea Kigoma nilihudhuria mkutano ulioandaliwa na Busineness times kuhusu Katiba Mpya na kuzungumza. Mwaka 1999 nilishiriki kutoa maoni katika Kamati ya Jaji Kisanga kuhusu Katiba Mpya. Mwaka 2001 nilishiriki maandamano ya vyama vya upinzai kudai Katiba mpya na Tume huru ya Uhaguzi. Mwaka 2005 Februari nikiwa sio Mbunge nilishiriki katika vikao vya kamati ya Bunge ya sheria na Katiba kuhusu madai ya Katiba mpya. Nilipochaguliwa tu niliandika barua kwa Rais kuhusu umuhimu wa kuandika katiba na kubadili mfumo wa uchaguzi. Nina rekodi ya madai ya Katiba hapa nchini.

Ili Tanzania ikue kidemokrasia na kiuchumi ni lazima tujiangalie tunavyojitawala. Mchakato wa kuandika Katiba mpya unapaswa kuanza mara moja. Katiba mpya iweke Tume Huru ya uchaguzi na kutatua tatizo la kero za Muungano na mfumo gani wa Muungano ufuatwe. Ninapenda kuona Tanzania yenye Katiba Mpya wakati wa kusherehekea miaka 50 ya Uhuru wa Taifa letu mwezi Disemba mwaka 2011.
 
Why are you so obsessed with Ms. Mtema? Regina hajawahi kulalamika juu ya Kitila.

Regia Mtema ndiye aliyekuja hapa kumlalamikia Kitila in a rather disgraceful way.

Kitila hakujibu, sasa mtu ninayeshutumu migogoro ya chama, hususan kuanikwa hadharani, nitamlaumu nini hapo Kitila ?

Kama unaongelea kumshutumu Kitila sehemu nyingine, angalia kule kwenye thread ya uteuzi wa wabunge wa viti maalum CHADEMA nimemsema Kitila vizuri tu.

Usitake kujifanya una uwezo wa kusoma threads zote hapa, unataka tuanze kufukua threads hapa?
 
Ndugu Zitto nikupongeze kwa kujitokeza kuelezea msimamo wako pamoja na kutuahidi utiifu wa maamzi ya vikao vya Chama hapo umenena.

Napenda nikueleze tu kuwa ukiona threads nyingi kwenye JF zikiandikwa kinyume chako hapo ujue kuwa umekengeuka au umeenda kinyume na matarajio ya watu waliowengi. Kumbuka kuwa sisi wanaJF wengi wetu nirahia wakawaida(siyo viongozi ndani ya vyama) Hivyo hattatafumbia macho kitendo chochote chenye lengo la kuturudisha nyuma au kuhatarisha umoja ndani ya chama bila kujali kimefanywa na nani? Hata kama ni Mbowe,Lisu,Zitto,Mnyika au hata Rais wetu mtarajiwa Dr wa ukweli Slaa.Tutakemea jambo hilo kwa nguvu zetu zote bila kujali kama limefanywa kwa bahati mbaya au makusudi

Nikishasema hayo napenda kukueleza kuwa mimi ni miongoni mwa Tanzania ambao wanakukubali kwa jinsi unavyojenga hoja na kusimamia haki lakini kitendo cha kushindwa kuungana na akina Lisu,Mnyika Mdee,Mbowe na wabunge wengine wa CDM kususia hotuba ya Rais ulinivunja moyo sana unajua pale ulisababisha mgawanyiko mkubwa sana.

Ladba tu ndugu yangu Zitto nikueleze ukweli kuwa mimi ni miongoni mw Watanzania ambao wanakuamini kama mpigania haki za wanyonge kwa jinsi ulivyo makini katika kujenga hoja na kuzisimamia lakini kitendo cha kukatataa kuungana na wapiganajipya akina Lisu,Munyika,Mdee, Mbowe na wabunge wengine wa Chadema kiliniuma sana na nilianza kuhisi kuwa sasa wewe unamalengo yako tofauti kwakweli mtu mzima lazima ukubali ulipotoka na kama hilo hujalikubali basi sasa tambua kuwa yawezekana umeamua kuchukua
uelekeo wa peke yako na wala siyo wa Chama unajua nalazimika kukueleza hayo kwakuwa kile kitendo chako cha kuchukua msimamo wa peke yako(Shibuda Simsemei Kunaphylosophy nikitaka mzungumzia) kiliwavunja wapenda mabadiriko wengi na athali yake ndoo hizo thread nyingi ambazo ziko negative kwako. Ila maadamu umejitokeza hadharani with objective dirrection sina budi kusema nimekusamehe
 
Pole sana Zitto kwa madongo unayotupiwa, tambua tu umekuwa ni mwanga na tumaini kwa vijana wengi (mimi mmoja wapo) lakini kwa siku za hivi karibuni tumaini la vijana hawa limeanza kufifia hata kufikia kusema kwamba Tanzania mabadiliko hayawezekani iwapo hata Zitto "kanunuliwa". Mie sina ushahidi wa hayo unayotuhumiwa na sidhani kama kuna mtu yeyote mwenye ushahidi 100% isipokuwa dhamira yako wewe mwenyewe ndio inayojua ukweli ni upi, brother, you are one of the icons of the Tanzanian youths, a hope to the young ones, hakuna pesa utakayopokea kutoka kwa mafisadi itakuwa na thamani kubwa kuliko imani yetu sisi kwako. Lisemwalo lipo, kama halipo linakuja, tafakari na uchukue hatua, kama ulipotoka, huo ni ubinadamu, rudi kwenye mstari tuendeleze mapambano.

Take all these allegations thrown against you as an incentive to work hard and get rid of your controversial moves which of recent have made most of us suspicious about your trustworthness and intergrity!

Dhamira yangu ni nyeupe. Sijanunuliwa maana sina bei. Haya yote baada ya muda yatajulikana ni uwongo, uzushi na siasa za maji taka. Kama Mwanasiasa nina wajibika kwa maamuzi yote nifanyayo, mazuri na mabaya. Kama binaadamu ninijifunza kwa maamuzi mabaya niliyofaya huko nyuma ili nisirudie maamuzi hayo.
 
Ile ilikuwa mbaya. Bora hata hii, mwandishi kaficha jina.

Wanaaibisha jina la chama tu.

Hivi mpaka Zitto aje ajitetee na kujaza information zote hizo kuwa linamilikiwa na nani na kuonyesha ugomvi ndani ya chama?

Angejitetea bila ya kutaja majina ya watu wa ndani ya chama angepungua wapi?


Haya ndio mambo yanayonifanya nianze kuhisi kumbe Tanzania kila anayejifanya anapigania haki ni muongo, ukweli ni kwamba watu

wanapigania matumbo yao, na ikitokea kasimama kutetea maslahi ya umma basi ujue nyuma ya hiyo ajenda kuna maslahi yake binafsi.

Ubinafsi utatuangamiza mpaka siku ya mwisho wa dunia.
 
Dhamira yangu ni nyeupe. Sijanunuliwa maana sina bei. Haya yote baada ya muda yatajulikana ni uwongo, uzushi na siasa za maji taka. Kama Mwanasiasa nina wajibika kwa maamuzi yote nifanyayo, mazuri na mabaya. Kama binaadamu ninijifunza kwa maamuzi mabaya niliyofaya huko nyuma ili nisirudie maamuzi hayo.

Kuna watu wanasema una ego kubwa na katika kujifanya muwazi sana, ukweli ni kwamba una satisfy ego yako tu, na kujipromote at the expense of party cohesion, unasema mengi ambayo hutakiwi kusema, loose lips sinks ships.

Swala la kutounga mkono kumsusia rais bungeni kwa mfano, ilikuwa lazima kuliongelea na kuonyesha tofauti binafsi ndani ya chama wakati chama kilishaamua? Au ulitumwa na chama?

Unasemaje kuhusu hili ?
 
Ndugu wana JF,
Kumekuwa na mada nyingi sna humu ndani ambazo zinajaribu kuonyesha kuwa mimi ni mkosaji na kunipaka matope sana. Nimejdiliwa mno katika jf na hata kuzushiwa mambo mengi sana. Kuna wanaonisema kwa dhati y moyo wao kwamba nimekosea hapa na pale na kuna wanaoona huu ndio wakati wa kumwangusha Zitto na hivyo kuendeleza propaganda za kila namna.

Hii makala imetoka katika gazeti la Mwanahalisi la wiki iliyopita. Imeandikwa na Ansbert Ngurumo, Mhariri wa Tanzania Daima na Press Secretary wa Mwenyekiti wa Taifa wa CHADEMA. MwanaHalisi linamilikiwa na Mkurugenzi wa Fedha na Utawala wa CHADEMA ndugu Antony Komu. MwanaHalisi limekuwa mstari wa mbele kunipaka matope na kutoa propaganda chafu dhidi yangu na sijui ni kwa faida ya nani.

Nadhani mmenijadili vya kutosha. Itoshe kusema nimesikia. Yale ambayo ni makosa nitajirekebisha maana mimi ni binaadamu. Yale ambayo ni uzushi, uwongo na propaganda nitayadharau.

Jambo moja nilisema na nimeshalisema huko nyuma ni kwamba, nimekuwa mwanachama wa CHADEMA toka nikiwa nina umri wa miaka 16 na sasa nina miaka 35, sijawahi kuwa mwanachama wa chama kingine chochote cha siasa. Sitegemei kuwa mwanachama wa chama kingine chochote cha siasa tofauti na CHADEMA. Sijawahi hata siku moja kusaliti chama changu na wala sitajaribu kufanya hivyo. Nina utii kwa Katiba ya chama changu na kwa chama kama Taasisi (Asasi). Pamoja na kutofautiana kimawazo na viongozi wenzangu (wote hatuwezi kufikiri sawasawa) sijawahi kukiuka maamuzi halali ya vikao vya chama kwa mujibu wa Katiba.

CHADEMA ni taasisi inayokua na hivyo changamoto zinaongezeka kila siku. Ni jukumu letu kuhakikisha kuwa tunazikabili changamoto hizi bila kuathiri kazi iliyombele yetu ya kujenga Tanzania yenye demokrasia ya kweli na yenye watu wenye fursa ya kuendeleza maisha yao.

Siasa za kupakana matope. Siasa za kumalizana. Siasa za maji taka, hazitasaidia nchi yetu wala chama chetu. Ifikapo mwaka 2015, wanachama wataamua nani atabeba bendera ya chama kwa njia za kidemokrasia. Hakuna sababu ya kuanza kumalizana sasa. Tukajenge chama wilayani na vijijini ili ifikapo uchaguzi ujao tuwe na mawakala kila kituo, walinde kura zetu na tuweze kushika Dola na kuongoza.

Watanzania mtusaidie katika jukumu hili. Jumamosi njema
Ungesema hiyo habari imeandikwa na Ansbert Ngurumo kupitia Mwanahalisi,kuliwa na umuhimu gani wa kusema mwandishi ni Press secretary wa Mbowe.

Unaendelea na siasa zako za maji taka kumtaja Antony Komu ni mmiliki wa Mwanahalisi na kuwaacha wamiliki wengine wenye hisa nyingi kama Kubenea kwasababu sio wachaga.
Hii si mara ya kwanza kuihusisha Chadema na ukabila ni wazi unataka wakufukuze ili ukaseme Wachaga wamekufuza.Cha kushangaza mpaka sasa hivi haujui Watanzania wengi wameshaelewa Chadema hakuna ukabila na hakuna atakaye kufukuza.
 
Ndugu Zitto nikupongeze kwa kujitokeza kuelezea msimamo wako pamoja na kutuahidi utiifu wa maamzi ya vikao vya Chama hapo umenena.

Napenda nikueleze tu kuwa ukiona threads nyingi kwenye JF zikiandikwa kinyume chako hapo ujue kuwa umekengeuka au umeenda kinyume na matarajio ya watu waliowengi. Kumbuka kuwa sisi wanaJF wengi wetu nirahia wakawaida(siyo viongozi ndani ya vyama) Hivyo hattatafumbia macho kitendo chochote chenye lengo la kuturudisha nyuma au kuhatarisha umoja ndani ya chama bila kujali kimefanywa na nani? Hata kama ni Mbowe,Lisu,Zitto,Mnyika au hata Rais wetu mtarajiwa Dr wa ukweli Slaa.Tutakemea jambo hilo kwa nguvu zetu zote bila kujali kama limefanywa kwa bahati mbaya au makusudi

Nikishasema hayo napenda kukueleza kuwa mimi ni miongoni mwa Tanzania ambao wanakukubali kwa jinsi unavyojenga hoja na kusimamia haki lakini kitendo cha kushindwa kuungana na akina Lisu,Mnyika Mdee,Mbowe na wabunge wengine wa CDM kususia hotuba ya Rais ulinivunja moyo sana unajua pale ulisababisha mgawanyiko mkubwa sana.

Ladba tu ndugu yangu Zitto nikueleze ukweli kuwa mimi ni miongoni mw Watanzania ambao wanakuamini kama mpigania haki za wanyonge kwa jinsi ulivyo makini katika kujenga hoja na kuzisimamia lakini kitendo cha kukatataa kuungana na wapiganajipya akina Lisu,Munyika,Mdee, Mbowe na wabunge wengine wa Chadema kiliniuma sana na nilianza kuhisi kuwa sasa wewe unamalengo yako tofauti kwakweli mtu mzima lazima ukubali ulipotoka na kama hilo hujalikubali basi sasa tambua kuwa yawezekana umeamua kuchukua
uelekeo wa peke yako na wala siyo wa Chama unajua nalazimika kukueleza hayo kwakuwa kile kitendo chako cha kuchukua msimamo wa peke yako(Shibuda Simsemei Kunaphylosophy nikitaka mzungumzia) kiliwavunja wapenda mabadiriko wengi na athali yake ndoo hizo thread nyingi ambazo ziko negative kwako. Ila maadamu umejitokeza hadharani with objective dirrection sina budi kusema nimekusamehe

Nikusahihishe kidogo. Mnyika na Halima hawakuwepo kabisa Dodoma siku ya tukio au walikuwepo lakini hawakuja kwenye kikao na kisha Bungei. Mimi nilikuwepo kwenye kikao na kusema wazi mawazo yangu kuwa sioni kama ku walk out ni mkakati mzuri. Kwa kuwa sikuunga mkono maamuzi hayo niliamua kutokwenda kabisa Bungeni. Nimeshalisemea hilo na kulitolea maelezo hapa JF. Sikutaka kuwa mnafiki na kujificha katika pazia la wengine. Sasa kama ni uamuzi wa makos umeshatokea, muhimu ni kusahihisha makosa na kwenda mbele. Nawaomba radhi wale wote niliowaudhi kwa msimamo niliochukua na hivyo mkaumia. Mimi niliona ndio msimamo sahihi (kutokwenda Bungeni kabisa na kama kwenda kuto walk out). Wengi mmeona haukuwa msimamo sahihi. Nimesikia. Tupige mstari na tuendelee na kazi nyingine.
 
Also to Zitto, Mbowe and Chadema please sort out any problems about Chadema behind the scenes no need kuwapa wapinzani ammunition

I love this. Zitto this is important for growth of CDM!!! Please.
 
Nilimtetea huko nyuma, lakini kwa hili inabidi nilisema kama lilivyo. Zitto, jaribu kuwa makini na kile unachozungumza. Kama una tatizo peleka kwenye vikao vya chama na sio hapa JF. Hakuna chama kisicho na matatizo, lakini matatizo ya chama hayatolewi nje au kwenye blogs, yanatatuliwa ndani ya chama. Kuna wakati Kikwete alisema watu ndani ya CCM walikuwa hawaaminiani kiasi cha kushindwa hata kula chakula pamoja, lakini hatukuwahi kusikia mwanachama akiongea kwenye vyombo vya habari mambo yao, ingawaje matatizo yalifahamika ndani ya chama.

Ushauri wangu kwako, sio kila habari inayokuzungumzia wewe lazima uijibu, wewe ni public figure kwa hiyo tegemea kuandikwa; isitoshe hayo magazeti yanafanya biashara na labda wameona habari zako zinauza. Pili, jifunze jinsi ya kuongea, mahali pa kuongea na wakati wa kuongea. Tatu, jifunze kuwaweka maadui wako karibu kuliko marafiki zako. Nne, tambua ya kuwa kwenye huu msuguano unaoendelea one might win the battle, but lose the war (2015). Tano, majibu mengi unayoyatoa hapa yana too much information ambazo nyingine watu wa sio ndani ya chama hawastahili kuzijua.
 
Je hili suala la wewe kugombea uraisi 2015 ni la kweli... sio vibaya kila mtu ana rights za kugombea ila i have heard (am not sure kama ni kweli) kwamba uliwaaga wapiga kura wako kwamba ni mara ya mwisho wewe kwenda kuomba kura zao za ubunge... Je bado una dhamira hiyo ya kugombea 2015
 
Ungesema hiyo habari imeandikwa na Ansbert Ngurumo kupitia Mwanahalisi,kuliwa na umuhimu gani wa kusema mwandishi ni Press secretary wa Mbowe.

Unaendelea na siasa zako za maji taka kumtaja Antony Komu ni mmiliki wa Mwanahalisi na kuwaacha wamiliki wengine wenye hisa nyingi kama Kubenea kwasababu sio wachaga.
Hii si mara ya kwanza kuihusisha Chadema na ukabila ni wazi unataka wakufukuze ili ukaseme Wachaga wamekufuza.Cha kushangaza mpaka sasa hivi haujui Watanzania wengi wameshaelewa Chadema hakuna ukabila na hakuna atakaye kufukuza.

samahani kama nimekukosea. Hizo tafsiri za uchaga ni zako. Sio zangu hata kidogo. Niwie radhi lakini. Pole
 
Je hili suala la wewe kugombea uraisi 2015 ni la kweli... sio vibaya kila mtu ana rights za kugombea ila i have heard (am not sure kama ni kweli) kwamba uliwaaga wapiga kura wako kwamba ni mara ya mwisho wewe kwenda kuomba kura zao za ubunge... Je bado una dhamira hiyo ya kugombea 2015

2015 nitakuwa nina umri wa miaka 39. Katiba inasema kuwa Rais lazima awe na miaka 40. Hata hivyo, sio kosa kwa Mtanzania yeyote kusema anataka kuwa Rais ya Jamhuri yetu tukufu.
 
:A S crown-1: Lisemwalo lipo... kama halipo laja.... Kwenye msafara wa mamba hata kenge huwemo.....
 
I think Jamaa amekili kuwa kuna makosa kafanya kama kila binadamu anavyofanya... na amesema tuko bado pamoja, kwahiyo kuliko kupigana wenyewe kwa wenyewe tumpe chance aendelee kutuwakilisha. Na kama alifanya makosa huko nyuma, tuyaache and lets start a new chapter
 
Watanzania imekula kwetu, viongozi tunaowategemea hawaoni hata maneno yao yatachukuliwaje na jamii.

Hapa tukifungua thread tukamnukuu, tukaanza kujadili kwa nini Zitto anahujumiwa ndani ya Chadema atakuja kusema "thread sikuanzisha mie na maneno hayo nilikuwa najibu thread nyengine kwa hiyo yasitumiwe" au?

Hebu fikirini kidogo kabla ya kuja kupayukwa ya ndani ya chama huko.

My man Kuhani angeipenda hii.
 
ila kunamengine Zitto ukubali kuwa unakosea kwanini watu wamakujadili wewe sana ndani ya CHADEMA wakati wapo wengi pale? kwanini hasiwe Mdee?
Mkuu, Mh. Zitto kisha sema yeye ni binadamu kama kuna sehemu kakosea atajirekebisha na kama kuna watu wamemzushia yeye atadharau. Nadhani ujumbe hapo kautoa naomba ufike.
 
2015 nitakuwa nina umri wa miaka 39. Katiba inasema kuwa Rais lazima awe na miaka 40. Hata hivyo, sio kosa kwa Mtanzania yeyote kusema anataka kuwa Rais ya Jamhuri yetu tukufu.
Tuko pamoja ushauri wangu ni kuwa just wait your time will come.... Am sure uwezo unao jenga Chama one day your time will come you are still young
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom