Zitto
Former MP Kigoma Urban
- Mar 2, 2007
- 1,562
- 10,890
Zitto je tuko pamoja kwenye kudai katiba mpya na kuisarambatisha nec
Madai ya Katiba mpya nchini sio madai mapya. Toka mfumo wa vyama vingi umeanza kwa nyakati tofauti kumekuwa na madai ya Katiba mpya. Yanaibuka na kupotea. Nimeshiriki katika madai haya toka nikiwa shuleni. Mwaka 1998 nikiwa nimemaliza kidato cha Sita Tosamaganga na kupita Dar es Salaam nikielekea Kigoma nilihudhuria mkutano ulioandaliwa na Busineness times kuhusu Katiba Mpya na kuzungumza. Mwaka 1999 nilishiriki kutoa maoni katika Kamati ya Jaji Kisanga kuhusu Katiba Mpya. Mwaka 2001 nilishiriki maandamano ya vyama vya upinzai kudai Katiba mpya na Tume huru ya Uhaguzi. Mwaka 2005 Februari nikiwa sio Mbunge nilishiriki katika vikao vya kamati ya Bunge ya sheria na Katiba kuhusu madai ya Katiba mpya. Nilipochaguliwa tu niliandika barua kwa Rais kuhusu umuhimu wa kuandika katiba na kubadili mfumo wa uchaguzi. Nina rekodi ya madai ya Katiba hapa nchini.
Ili Tanzania ikue kidemokrasia na kiuchumi ni lazima tujiangalie tunavyojitawala. Mchakato wa kuandika Katiba mpya unapaswa kuanza mara moja. Katiba mpya iweke Tume Huru ya uchaguzi na kutatua tatizo la kero za Muungano na mfumo gani wa Muungano ufuatwe. Ninapenda kuona Tanzania yenye Katiba Mpya wakati wa kusherehekea miaka 50 ya Uhuru wa Taifa letu mwezi Disemba mwaka 2011.