Zitto anataka kusaliti CHADEMA?

Zitto anataka kusaliti CHADEMA?

Status
Not open for further replies.
Hii makala imetoka katika gazeti la Mwanahalisi la wiki iliyopita. Imeandikwa na Ansbert Ngurumo, Mhariri wa Tanzania Daima na Press Secretary wa Mwenyekiti wa Taifa wa CHADEMA. MwanaHalisi linamilikiwa na Mkurugenzi wa Fedha na Utawala wa CHADEMA ndugu Antony Komu. MwanaHalisi limekuwa mstari wa mbele kunipaka matope na kutoa propaganda chafu dhidi yangu na sijui ni kwa faida ya nani.

Kwa mantiki hii unanilazimisha kuamini kuwa una mgogoro Binafsi na mmoja wa uliowataja hapo juu. Kwa faida ya nani huo mgogoro? mimi sijui....

Sijafanya kikao chochote na Lowasa. Kulikuwa na kikao cha Lowasa na Mbowe ambacho mimi nilishiriki kama Naibu wa Mbowe Bungeni. Hata hivyo sijafanya kikao kingine chochote.

Makala hii imeandikwa kwa lengo baya na ndio maana mwandishi kaficha jina lake.
Kama ana guts aweke jina lake wazi na aje na ushahidi wa haya aliyoyaandika.

Inawezekana, swali langu kwako: kwa nini kila kukicha unaandikwa wewe tu? isitoshe sioni tatizo la mwandishi kuficha jina, kwa uzoefu wangu hii si mara ya kwanza kuona makala imeandikwa na mwandishi maalumu, labda tuseme analinda usalama wake.. Hivyo hapo penye nyekundu sidhani kama kuna ulazima wa huyo mwandishi kufanya hivyo.


Sijawahi kusema mahala popote kuwa ndani ya CHADEMA kuna udini. Ninaomba clip ya TBC iwekwe hapa jamvini na mtu anionyeshe wapi nimesem kuwa ndai ya CHADEMA kuna udinni. Tafadhali usinywe sumu unazopewa.

Hapo umenena. Kama kuna mwenye hiyo clip waungwana itasaidia kwa wale ambao hatujabahatika kuona kauli ya Mheshimiwa sana Zitto kuwa CHADEMA kuna udini..

Labda kwa kuongezea tu, Ndugu yangu Zitto jitahidi kuepuka kuwapatia watu nafasi ya kukuhukumu kwa maneno yako mwenyewe. Au kama huwezi kuvumilia basi tafuta mtu awe mshauri wako wa kisiasa ambaye atakuwa anakupa mwongozo wa nini useme na nini usiseme au ukiseme kwa kutumia maneno yapi, Siasa nayo ni sanaa wandugu. na neno likishatoka basi halirudi.

Silence can be misinterpreted but never misquoted, Even a stubborn fool is thought to be wise if he keeps silent.
 
too many zitto threads

probably you could just paste this one in the other trhead started yesterday

why are we giving this dude too much promo? are we losers or something... out of 40M we only talk of one young boy who cant even tell what he wants?

Lets be serious guys
hatuna umeme
hatuna maji
bei ya vitumbua imepanda
quality ya elimu hairidhishi
braza kubwa mno

Heri wewe umesema. Zitto siyo mustakabali wa Taifa letu.Na anayo hiari ya kujiunga na chama chochote. We are wasting time to discuss about him everyday.
 
Viongozi vijana hususan mna matatizo ya kuweka ego mbele mpaka mnaaibisha.

Hivi chama huwa hakijawafundisha namna ya kukabiliana na kuwa public figure au?
 
Nilimtetea huko nyuma, lakini kwa hili inabidi nilisema kama lilivyo. Zitto, jaribu kuwa makini na kile unachozungumza. Kama una tatizo tumia peleka kwenye vikao vya chama na sio hapa JF. Hakuna chama kisicho na matatizo, lakini matatizo ya chama hayatolewi nje au kwenye blogs, yanatatuliwa ndani ya chama. Kuna wakati Kikwete alisema watu ndani ya CCM walikuwa hawaaminiani kiasi cha kushindwa hata kula chakula pamoja, lakini hatukuwahi kusikia mwanachama akiongea kwenye vyombo vya habari mambo yao, ingawaje matatizo yalifahamika ndani ya chama.

Ushauri wangu kwako, sio kila habari inayokuzungumzia wewe lazima uijibu, wewe ni public figure kwa hiyo tegemea kuandikwa; isitoshe hayo magazeti yanafanya biashara na labda wameona habari zako zinauza. Pili, jifunze jinsi ya kuongea, mahali pa kuongea na wakati wa kuongea. Tatu, jifunze kuwaweka maadui wako karibu kuliko maadui wako. Nne, tambua ya kuwa kwenye huu msuguano unaoendelea one might win the battle, but lose the war (2015). Tano, majibu mengi unayoyatoa hapa yana too much information ambazo nyingine watu wa sio ndani ya chama hawatakiwi kuzijua.

Nashukuru sana kwa ushauri wako. Wakati mwingine ukikaa kimya maadui zako huona kama ndio umekiri. Nimekaa kimya sana sana. Nilisimama kabisa kuja hapa nikadhani itapunguza chuki za watu. Hata hivyo haikukoma. Hata hivyo ushauri wako nimeuchukua kwa mikono miwili. Asante sana sana
 
samahani kama nimekukosea. Hizo tafsiri za uchaga ni zako. Sio zangu hata kidogo. Niwie radhi lakini. Pole
Kulikuwa na umuhimu gani wa kuandika Ansbert Ngurumo ni Secretary wa Mbowe?
Kwa nini umemtaja Komu mmiliki wa Mwanahalisi ukawaacha wengine wenye share kubwa kama Kubenea?
 
Ndugu wana JF,
Kumekuwa na mada nyingi sna humu ndani ambazo zinajaribu kuonyesha kuwa mimi ni mkosaji na kunipaka matope sana. Nimejdiliwa mno katika jf na hata kuzushiwa mambo mengi sana. Kuna wanaonisema kwa dhati y moyo wao kwamba nimekosea hapa na pale na kuna wanaoona huu ndio wakati wa kumwangusha Zitto na hivyo kuendeleza propaganda za kila namna.

Hii makala imetoka katika gazeti la Mwanahalisi la wiki iliyopita. Imeandikwa na Ansbert Ngurumo, Mhariri wa Tanzania Daima na Press Secretary wa Mwenyekiti wa Taifa wa CHADEMA. MwanaHalisi linamilikiwa na Mkurugenzi wa Fedha na Utawala wa CHADEMA ndugu Antony Komu. MwanaHalisi limekuwa mstari wa mbele kunipaka matope na kutoa propaganda chafu dhidi yangu na sijui ni kwa faida ya nani.

Nadhani mmenijadili vya kutosha. Itoshe kusema nimesikia. Yale ambayo ni makosa nitajirekebisha maana mimi ni binaadamu. Yale ambayo ni uzushi, uwongo na propaganda nitayadharau.

Jambo moja nilisema na nimeshalisema huko nyuma ni kwamba, nimekuwa mwanachama wa CHADEMA toka nikiwa nina umri wa miaka 16 na sasa nina miaka 35, sijawahi kuwa mwanachama wa chama kingine chochote cha siasa. Sitegemei kuwa mwanachama wa chama kingine chochote cha siasa tofauti na CHADEMA. Sijawahi hata siku moja kusaliti chama changu na wala sitajaribu kufanya hivyo. Nina utii kwa Katiba ya chama changu na kwa chama kama Taasisi (Asasi). Pamoja na kutofautiana kimawazo na viongozi wenzangu (wote hatuwezi kufikiri sawasawa) sijawahi kukiuka maamuzi halali ya vikao vya chama kwa mujibu wa Katiba.

CHADEMA ni taasisi inayokua na hivyo changamoto zinaongezeka kila siku. Ni jukumu letu kuhakikisha kuwa tunazikabili changamoto hizi bila kuathiri kazi iliyombele yetu ya kujenga Tanzania yenye demokrasia ya kweli na yenye watu wenye fursa ya kuendeleza maisha yao.

Siasa za kupakana matope. Siasa za kumalizana. Siasa za maji taka, hazitasaidia nchi yetu wala chama chetu. Ifikapo mwaka 2015, wanachama wataamua nani atabeba bendera ya chama kwa njia za kidemokrasia. Hakuna sababu ya kuanza kumalizana sasa. Tukajenge chama wilayani na vijijini ili ifikapo uchaguzi ujao tuwe na mawakala kila kituo, walinde kura zetu na tuweze kushika Dola na kuongoza.

Watanzania mtusaidie katika jukumu hili. Jumamosi njema

Mkuu Zitto umeandika Vizuri sana, lakini hapo kwenye nyekundu kidogo kunaonyesha kuna kitu kinafukuta kati yako na Mwenyekiti Mbowe,
Lakini mkuu pamoja na hayo yote kama ulivyosema kwenye bandiko lako, unahitaji mabadiliko makubwa ili kurudisha imani ya watu walioijenga kwako, Licha ya hayo magazeti unayoyaona yanakutuhumu, lakini pia kuna malalamishi mengi ambayo hayatokani na hayo magazeti

Nimeipenda sana hii signature yako mpya“Ukweli haupendi kupuuzwa puuzwa - TUJISAHIHISHE, Nyerere 1962.”

na mimi namalizia kwa kusema "yana mwisho"
 
too many zitto threads

probably you could just paste this one in the other trhead started yesterday

why are we giving this dude too much promo? are we losers or something... out of 40M we only talk of one young boy who cant even tell what he wants?

Lets be serious guys
hatuna umeme
hatuna maji
bei ya vitumbua imepanda
quality ya elimu hairidhishi
braza kubwa mno

Zitto ni mfano mmoja mdogo tu katika crisis ya uongozi, hata huko upinzani tulikofikiri kungetupa mbadala.

Hapa tunaongelea zaidi ya Zitto, huu ni mfano katika swala zima la uongozi Tanzania. Na kwa sababu viongozi wengine hawaji hapa, si vibaya kuwapa nafasi wale wanaokuja wajieleze vizuri.
 
Nashukuru sana kwa ushauri wako. Wakati mwingine ukikaa kimya maadui zako huona kama ndio umekiri. Nimekaa kimya sana sana. Nilisimama kabisa kuja hapa nikadhani itapunguza chuki za watu. Hata hivyo haikukoma. Hata hivyo ushauri wako nimeuchukua kwa mikono miwili. Asante sana sana

Usikae kimya lakini think twice (no think three times and rethink) before you answear, BECAUSE SILENCE CAN BE INTERPRETED THAT YOU ARE GUILTY
 
2015 nitakuwa nina umri wa miaka 39. Katiba inasema kuwa Rais lazima awe na miaka 40. Hata hivyo, sio kosa kwa Mtanzania yeyote kusema anataka kuwa Rais ya Jamhuri yetu tukufu.
Sio ndiyo maana ukaomba Kikwete aongezewe muda.
 
Nashukuru sana kwa ushauri wako. Wakati mwingine ukikaa kimya maadui zako huona kama ndio umekiri. Nimekaa kimya sana sana. Nilisimama kabisa kuja hapa nikadhani itapunguza chuki za watu. Hata hivyo haikukoma. Hata hivyo ushauri wako nimeuchukua kwa mikono miwili. Asante sana sana

Hata kuja na kuandika hapa haiwezi kupunguza chuki kwa sababu ukiandika unaongezea na taarifa nyengine ambazo ni za kichochezi.


As long as hujui unapaswa kuongea nini mbele ya watu hizo chuki haziwezi kumalizika.
 
Hata kuja na kuandika hapa haiwezi kupunguza chuki kwa sababu ukiandika unaongezea na taarifa nyengine ambazo ni za kichochezi.


As long as hujui unapaswa kuongea nini mbele ya watu hizo chuki haziwezi kumalizika.

I beg to differ, suala sio kwamba aache kuja hapa, bali ajibu majibu diplomatically na asiongee jambo ambalo linaweza kukiumiza chama chake
 
I beg to differ, suala sio kwamba aache kuja hapa, bali ajibu majibu diplomatically na asiongee jambo ambalo linaweza kukiumiza chama chake

Nisome vizuri. Sijamkataza kuja hapa kuandika.

Yeye anasema 'alinyamaza kimya' lakini chuki zikaendelea ndio akaamua aje ajieleze.

Sasa kama kujieleza kwenyewe ndo kwa namna hii ya leo, chuki haziwezi kuondoka kamwe. Manake kaanzisha jengine jipya leo, kuwa ndani ya chama kuna mtu au watu wanamhujumu.

SMH
 
Sio ndiyo maana ukaomba Kikwete aongezewe muda.


Sijawahi kuomba Kikwete aongezewe muda. Tanzania Daima waliandika habari hiyo kwa lengo maalumu na nililalamika rasmi kwa Mhariri mtendaji. Unaona sasa unanihukumu kwa habari iliyotungwa? Ndio maana nimetaja Tanzania Daima na Mhariri wake maana hii ni scheme ya muda mrefu na nimelalamika sana kimya kimya. Hata suala la mimi kutangaza nitagombea 2015 liliandikwa na Tanzania Daima peke yake tena kati kati ya kampeni. Hakuan aliyejiuliza ni kwa nini gazeti linalomilikiwa na Kiongozi wa CHADEMA linaweza kuandika kitu kama kile katikati ya kampeni.
 
Wana Jf hii mada ifungwe, Zitto amejibu kwa ufasaha bila kuwa na jazba pamoja na madongo yote, at least nimeona jinsi kiongozi anavyotakiwa kuwa.
 
Kulikuwa na umuhimu gani wa kuandika Ansbert Ngurumo ni Secretary wa Mbowe?
Kwa nini umemtaja Komu mmiliki wa Mwanahalisi ukawaacha wengine wenye share kubwa kama Kubenea?

MwanaHalisi linamilikiwa na watu wawili wenye hisa sawa. Hakuna mwenye hisa nyingi kumzidi mwenzie kati ya Komu na Kubenea. Vile vile Komu na Kubenea wameoa nyumba moja. Kwenye MwanaHalisi Komu na Kubenea ndio wamiliki pekee. Kama wewe unajua wamiliki wengine tuambie.
 
Madai ya Katiba mpya nchini sio madai mapya. Toka mfumo wa vyama vingi umeanza kwa nyakati tofauti kumekuwa na madai ya Katiba mpya. Yanaibuka na kupotea. Nimeshiriki katika madai haya toka nikiwa shuleni. Mwaka 1998 nikiwa nimemaliza kidato cha Sita Tosamaganga na kupita Dar es Salaam nikielekea Kigoma nilihudhuria mkutano ulioandaliwa na Busineness times kuhusu Katiba Mpya na kuzungumza. Mwaka 1999 nilishiriki kutoa maoni katika Kamati ya Jaji Kisanga kuhusu Katiba Mpya. Mwaka 2001 nilishiriki maandamano ya vyama vya upinzai kudai Katiba mpya na Tume huru ya Uhaguzi. Mwaka 2005 Februari nikiwa sio Mbunge nilishiriki katika vikao vya kamati ya Bunge ya sheria na Katiba kuhusu madai ya Katiba mpya. Nilipochaguliwa tu niliandika barua kwa Rais kuhusu umuhimu wa kuandika katiba na kubadili mfumo wa uchaguzi. Nina rekodi ya madai ya Katiba hapa nchini.

Ili Tanzania ikue kidemokrasia na kiuchumi ni lazima tujiangalie tunavyojitawala. Mchakato wa kuandika Katiba mpya unapaswa kuanza mara moja. Katiba mpya iweke Tume Huru ya uchaguzi na kutatua tatizo la kero za Muungano na mfumo gani wa Muungano ufuatwe. Ninapenda kuona Tanzania yenye Katiba Mpya wakati wa kusherehekea miaka 50 ya Uhuru wa Taifa letu mwezi Disemba mwaka 2011.


Nakuomba tu kwenye hiyo katiba mpya kuweke kifungu kitakacho fafanua matumizi ya TISS na vyombo vingine vya ulinzi na usalama kwa manufaa ya taifa sio kwa kulinda manufaa ya viongozi na maslahi yao na hasa pale inapokuwa maslahi ya kiongozi ndio maslahi ya mafisadi na familia yake si ya wananchi wala nchi yao.
 
Wana Jf hii mada ifungwe, Zitto amejibu kwa ufasaha bila kuwa na jazba pamoja na madongo yote, at least nimeona jinsi kiongozi anavyotakiwa kuwa.
Mada ifungwe kwa kuwa ina jadili mgogoro wa chadema?Ingekuwa inahusu wana ccm hapa ungekuwa unapiga zumari!acheni hizo wanachadema acha mjadala uendelee!
 
Sijawahi kuomba Kikwete aongezewe muda. Tanzania Daima waliandika habari hiyo kwa lengo maalumu na nililalamika rasmi kwa Mhariri mtendaji. Unaona sasa unanihukumu kwa habari iliyotungwa? Ndio maana nimetaja Tanzania Daima na Mhariri wake maana hii ni scheme ya muda mrefu na nimelalamika sana kimya kimya. Hata suala la mimi kutangaza nitagombea 2015 liliandikwa na Tanzania Daima peke yake tena kati kati ya kampeni. Hakuan aliyejiuliza ni kwa nini gazeti linalomilikiwa na Kiongozi wa CHADEMA linaweza kuandika kitu kama kile katikati ya kampeni.

Huwezi kutegemea ufanye makosa kisha usiandikwe kwa sababu tu gazeti linamilikiwa na mwenyekiti wa chama

Na kama unaona kuna tatizo kwenye hilo ulitakiwa uwasiliane na mwenyekiti wa chama na mjadiliane mpaka mpate suluhu. Kama msimamo wake ni hasi kwako, kwa faida ya chama unatakiwa umezee tu ufe kisabuni.

Hii ya kuja kuweka malalamiko ya kuonyesha kuwa kuna mvurugiko kwenye chama is not a good look kwako wala chama chako.
 
Mada ifungwe kwa kuwa ina jadili mgogoro wa chadema?Ingekuwa inahusu wana ccm hapa ungekuwa unapiga zumari!acheni hizo wanachadema acha mjadala uendelee!

Brother, hakuna mgogoro CHADEMA!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom