Ni vyema ikajulinana kuwa Zitto amekuwa "Zitto" kwa sababu ni mtu mwenye msimamo na anayependa kuweka wazi misimamo yake. Misimamo hiyo inapokuwa kupinga utendaji mbovu wa serikali sote hujarijika na kumpongeza. Hata hivyo, ni vyema tukatambua kuwa utendaji mbovu au makosa hayako serikalini tu. Yako kwa kila mmoja wetu popote tulipo. Na Zitto akiona atasema. Na ninaamini kwa asilimia 100 kuwa hufanya hivyo kwa maslahi ya Taifa.
Sasa basi tusimtake Zitto awe "Zitto kamili" kwenye hoja zinazohusu serikali, huku tukimtaka awe "nusu- Zitto" kwenye hoja za kichama.Kwa maslahi ya Taifa Zitto na watu wenye tabia kama zake wanapaswa kupongezwa, kuungwa mkono na kuongezewa nguvu. Ni kwa jinsi hii tu,tunaweza kupata utawala bora unaojali sheria. Zitto akiogopa kusema maoni yake kwa kisingizio cha maslahi ya Chama ilhali Taifa linahujumiwa, hawezi kuwa Zitto tunayejivunia.