Zitto anataka kusaliti CHADEMA?

Zitto anataka kusaliti CHADEMA?

Status
Not open for further replies.
Ninaamini UONGOZI wa juu wa CHADEMA unamfahamu ZITTO. Wasimfukuze. Watampa umaarufu kama ule alioupata BUngeni kwenye suala la Buzwagi.

Kama mtu anakuwa ndiye chanzo cha mizozo ndani ya chama ni kufungua mlango atoke kwa hiari yake mwenyewe, vinginevyo ni kumtimua.

WildCard, ndiyo maana vitu unavyotupa wewe jalalani, kwa watu wengine ni mali ndiyo maana kila siku watu wanapita majalalani kuokota uchafu, Zito akitupwa nje kwa wengine ni mtaji jalala.
 
I agree with you: Kwa sasa kuna agenda muhimu za kushughulikia kwa pamoja, wasihamishe focus kutoka kwenye kudai Tume huru, Katiba mpya kwenda kwa maoni binafsi ya Kiongozi mmoja mmoja

Sure, that should be the target, tusianze kuonyesha uzaifu
 
Napenda kuchukua nafasi hii kumpongeza Zitto Kabwe kama independent thinkers. Hawi - drowned na mob decisions hasa zile ambazo anaamini kuwa zina mushkeli ndani yake. He got the principles. Anasimamia anachokiamini, ana good know how of protocols. Hakurupuki.

Zitto is a true politician of his generations.
 
Nafahamu. Ataondoka mwenyewe atakapoona anatofautiana na wenzake karibu kwa kila jambo. Kaka yake, Dr Kabourou, hayuko CHADEMA. Hakufukuzwa. CHADEMA ni imara zaidi sasa kuliko wakati wowote. Misimamo ya watu wa KIGOMA, KAGERA, MBEYA,......inafahamika.
Lakini huyu ni kiongozi wa ngazi ya juu Chadema,anajua mengi na anashiriki mengi. Inaeza kufikia mahali sasa akawa anaeka tundu kwa kusudi kwene meli ya Chadema kwa udhahiri na kwa uwazi, Je aachwe tu mpaka damage itapokuwa irreversible?
 
Kutokana na kichefuchefu (haswa baada ya kusema anamtambua JK ni amiri jeshi mkuu na alama ya bunge na hivyo si vizuri kutoka bungeni na kwa kiburi kabisa kusema anasubiria hatma yake chamani kutokana na uamuzi wake huo) ambacho mh. Zitto Kabwe ameendelea kuleta ndani ya CHADEMA wana JF wenzangu nilikuwa ninatoa mapendekezo kuwa huyu jamaa ni wa kuogopwa kama ukoma, na ni kidudu hatari kuliko KIRUSI CHA UKIMWI kwa wana upinzani, wapigania haki na kwa wananchi wa Tanzania waliodhulumiwa haki zao kwa muda mrefu na chama tawala cha CCM. Kwangu mimi namwona ni msaliti mkubwa wa Watanzania na upinzani. Hivyo ni nilikuwa napendekeza aondolewe CHADEMA haraka kwani amepandikizwa na CCM. Nakishauri CHADEMA kimvue uanachama ili kunusuru upinzani wa ukweli ambao umebaki peke yake CHADEMA. Je wana JF wenzangu mnaonaje? Je aendelee kubaki CHADEMA au aondolewe. Ushauri utakaopatikana hapa ukiambatana na sababu za msingi, naomba CHADEMA waufanyie kazi.

Zitto ni mkweli sana , na mkimtoa CDM mmejimaliza. Aliisha wahi kuwaambia juu ya kumfukuza Kafulila, leo madhara yake mmeyaona amewahenyesha kwenye ubunge na ameupata. Msiwazibe wana mapinduzi ya kweli km wakina zitto kusema ukweli wao, hiyo siyo demokrasia. Na ndio maana hapa twasema CDM sio shwari kwa sasa kuna mazongozongo mengi sana ndani ya Chama. Wakina Mbowe wanataka watukuzwe km mungu mtu, sasa watu makini km wakina zitto hawakubali. Kuweni wapole mwacheni atoe mawazo yake.
 
Kutokana na kichefuchefu (haswa baada ya kusema anamtambua JK ni amiri jeshi mkuu na alama ya bunge na hivyo si vizuri kutoka bungeni na kwa kiburi kabisa kusema anasubiria hatma yake chamani kutokana na uamuzi wake huo) ambacho mh. Zitto Kabwe ameendelea kuleta ndani ya CHADEMA wana JF wenzangu nilikuwa ninatoa mapendekezo kuwa huyu jamaa ni wa kuogopwa kama ukoma, na ni kidudu hatari kuliko KIRUSI CHA UKIMWI kwa wana upinzani, wapigania haki na kwa wananchi wa Tanzania waliodhulumiwa haki zao kwa muda mrefu na chama tawala cha CCM. Kwangu mimi namwona ni msaliti mkubwa wa Watanzania na upinzani. Hivyo ni nilikuwa napendekeza aondolewe CHADEMA haraka kwani amepandikizwa na CCM. Nakishauri CHADEMA kimvue uanachama ili kunusuru upinzani wa ukweli ambao umebaki peke yake CHADEMA. Je wana JF wenzangu mnaonaje? Je aendelee kubaki CHADEMA au aondolewe. Ushauri utakaopatikana hapa ukiambatana na sababu za msingi, naomba CHADEMA waufanyie kazi.

Je CHADEMA mnapenda wanachama 'ndio mzee'?

Hamtaki challenges, hamtaki kuwa uhuru wa mawazo katika chama chenu, hamruhusu makosa, je ninyi ni malaika?

Kuna udhaifu mkubwa wa upeo kwa baadhi ya wanachadema, wa kufuata mkumbo kwa kila mnaloambiwa.
 
Je CHADEMA mnapenda wanachama 'ndio mzee'?

Hamtaki challenges, hamtaki kuwa uhuru wa mawazo katika chama chenu, hamruhusu makosa, je ninyi ni malaika?

Kuna udhaifu mkubwa wa upeo kwa baadhi ya wanachadema, wa kufuata mkumbo kwa kila mnaloambiwa.

Challenges wamesema hawataki? unawanukuu kutoka wapi?
 
Lakini huyu ni kiongozi wa ngazi ya juu Chadema,anajua mengi na anashiriki mengi. Inaeza kufikia mahali sasa akawa anaeka tundu kwa kusudi kwene meli ya Chadema kwa udhahiri na kwa uwazi, Je aachwe tu mpaka damage itapokuwa irreversible?
Unadhani kaanza leo kuwabadilikia wenzake? Wanamfahamu sana. Dr Kabourou alikuwa na cheo kikubwa zaidi ndani ya CHADEMA. Walimvumilia hadi alipoondoka na kurudi CCM.
 
Wakuu hii habari ni mpya kwangu nilikuwa nje ya mji unajua tena mawasilianao vijijini mgogoro.Nimesoma baadhi ya mabandiko nimepata picha kidogo kwamba Zitto aliamua kuchukua msimamo binafsi dhidi ya chama chake.

Sijui kwanini kila wakati issue za Bwana Mdogo Zitto zinapewa umuhimu wa juu usiostahili hata kidogo.Nakumbuka issue ya Dowans alikuwa na msimamo wa ajabu kiasi hata wabunge wa CCM wakamshangaa.Ikaja issue ya EAC akachukua msimamo tofauti na watanzania wengi kabla mambo hayajatulia akataka kugombea uenyekiti wa chama taifa mara akataka cheo cha KUB ilihali mwenyekiti wake yuko bungeni.

Zitto ataendelea kuwa mwiba wa CHADEMA kama hali ya mambo haitabadilishwa mara moja.
 
to me Zitto is a coward, a traitor and an impostor.
So he must go out of cdm.

You are right. he is a hero to stupid but to the cleaver ones no - Let him join CCM because he is one of them
 
Unadhani kaanza leo kuwabadilikia wenzake? Wanamfahamu sana. Dr Kabourou alikuwa na cheo kikubwa zaidi ndani ya CHADEMA. Walimvumilia hadi alipoondoka na kurudi CCM.

Dah, basi ni wanyonge sana na wanalea maradhi wao wenyewe.

Kumkopesha mtu ambaye haoni responsibility ya kichama ni kujirundikia matatizo huko mbeleni.
 
Chadema hamna guts wala balls za kumlet Zitto go. He got principles, stands on what he believes is right not drown by mob psychology.

Zitto knows what democracy is all about.
 
Chadema hamna guts wala balls za kumlet Zitto go. He got principles, stands on what he believes is right not drown by mob psychology.

Zitto knows what democracy is all about.

Wewe ndio vuvuzela yake JF? kuna kipindi alikimbia hiki kijiwe.
 
Nitamshangaa sana JK kama atamwacha Zitto kwenye Cabinet yake ya leo(kesho)?
 
Kwangu Zitto sasa naona kama angepewa uhuru wa kuchagua anataka nini.
Sioni kama ana manufaa kwa Chama tena ,sio mwanasiasa machachari kama alivyokuwa mwanzo sasa amekuwa kama kifaranga kinachojificha ndani ya mbawa za *****
Kama ameamua kurudi CCM ama ameamua kujiunga na CUF aende kwa amani ndo mambo ya siasa haya
 
Kutokana na kichefuchefu (haswa baada ya kusema anamtambua JK ni amiri jeshi mkuu na alama ya bunge na hivyo si vizuri kutoka bungeni na kwa kiburi kabisa kusema anasubiria hatma yake chamani kutokana na uamuzi wake huo) ambacho mh. Zitto Kabwe ameendelea kuleta ndani ya CHADEMA wana JF wenzangu nilikuwa ninatoa mapendekezo kuwa huyu jamaa ni wa kuogopwa kama ukoma, na ni kidudu hatari kuliko KIRUSI CHA UKIMWI kwa wana upinzani, wapigania haki na kwa wananchi wa Tanzania waliodhulumiwa haki zao kwa muda mrefu na chama tawala cha CCM. Kwangu mimi namwona ni msaliti mkubwa wa Watanzania na upinzani. Hivyo ni nilikuwa napendekeza aondolewe CHADEMA haraka kwani amepandikizwa na CCM. Nakishauri CHADEMA kimvue uanachama ili kunusuru upinzani wa ukweli ambao umebaki peke yake CHADEMA. Je wana JF wenzangu mnaonaje? Je aendelee kubaki CHADEMA au aondolewe. Ushauri utakaopatikana hapa ukiambatana na sababu za msingi, naomba CHADEMA waufanyie kazi.

Chama kikikataa mawazo mbadala ndio mwanzo wa udikteta. Kosa la Zito kwa mtazamo wangu ni kuongea tofauti yake na vyombo vya habari. Alitakiwa akae kimya ingetosha. Japo ni haki yake kwa yote aliyofanya lakini ukweli uanabaki kuwa Zito anataka kutuambia kuwa chadema kuna taswira 2. Lakini big up napenda anavyofanya japo ni wachache watamwelewa. Long live chadema!
 
kutokana na kichefuchefu (haswa baada ya kusema anamtambua jk ni amiri jeshi mkuu na alama ya bunge na hivyo si vizuri kutoka bungeni na kwa kiburi kabisa kusema anasubiria hatma yake chamani kutokana na uamuzi wake huo) ambacho mh. Zitto kabwe ameendelea kuleta ndani ya chadema wana jf wenzangu nilikuwa ninatoa mapendekezo kuwa huyu jamaa ni wa kuogopwa kama ukoma, na ni kidudu hatari kuliko kirusi cha ukimwi kwa wana upinzani, wapigania haki na kwa wananchi wa tanzania waliodhulumiwa haki zao kwa muda mrefu na chama tawala cha ccm. Kwangu mimi namwona ni msaliti mkubwa wa watanzania na upinzani. Hivyo ni nilikuwa napendekeza aondolewe chadema haraka kwani amepandikizwa na ccm. Nakishauri chadema kimvue uanachama ili kunusuru upinzani wa ukweli ambao umebaki peke yake chadema. Je wana jf wenzangu mnaonaje? Je aendelee kubaki chadema au aondolewe. Ushauri utakaopatikana hapa ukiambatana na sababu za msingi, naomba chadema waufanyie kazi.

kwani nani alikuambia kuwa mhe jakaya kikwete sio raisi wa nchi inayoitwa tanzania, sio amiri jeshi mkuu wa majeshi ya tanzania n.k. Kaa chini usome nini hasa chadema wanasema ndio uweze kuanzisha mada yenye mashiko. Kwa kifupi chadema inasema kuwakatiba na sheria mbovu zinawalazimisha watanzania kukubali motokeo ua kura za uraisi yanayotangazwa na tume ya uchaguzi pasipo sheria hizo kutoa fursa ya kupinga matokeo hayo katika vyombo vya sheria kama ilivyo kwa ubunge na udiwani.

hivyo kitendo walichafanya wao kama wabunge ni kusimama wakati wa rais wa jamhuri ya muungano wa tanzania anaingia katika ukumbi wa bunge halafu kutoka nje kwa maana ya kususia kusikiliza hotuba yake kama njia ya kuonyesha kutokukubali kwao kwa mfumo huo wa katiba na sheria zilizopitwa na wakati.

kuhusu suala la zitto sioni kama kuna tatizo kubwa kwa kuwa anatumia uhuru wake wa kuto maoni, tunaikata ccm kwa kuwa mambo yaote huamuliwa na wa tu wachache na kubaki ni siri yao hao wateule wachache. Zitto anatakiwa kupatiwa ushauri tu kuwa kuendelea kuwa anasema sema katika vyombo vya habari vinampunguzia hadhi na heshima aliyo nayo. Kwani wangapi walipiga kura ya kutotoka nje ya ukumbi wa bunge na wameamua kunyamaza?
 
Katika kila kundi kutofautiana kupo. Nashawishika kuhisi Ndg. Kabwe ana ka-tamaa na papara ya kupata madaraka...!! naamini wakongwe wa CHADEMA watamweka china nia kumwelimisha
 
Hii forum ni ya watu wenye weledi na uwezo mkubwa wa kuchambua mambo.
Ngwendu anasema haipendi CDM kwa sababu ni chama cha kikabila/kidini anamaanisha nini? Tukiachana upotoshaji wa mada ni vizuri kama mtu ana hoja uelezee kw vielelezo watu wakuelewe. Huu upuzi wa kushabikia ajenda wakati huielewi vizuri ni aibu sana.

Nashauri tena watu kutochanganya ajenda. Thread inazungumzia behavior ya Zitto baada ya walkout. Tunaomba kama mtu ana wazo zuri la kujenga afanye hivyo. Kama una wazo zuri pia soma na ukae kimya.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom