Zitto anataka kusaliti CHADEMA?

Zitto anataka kusaliti CHADEMA?

Status
Not open for further replies.
Nafikiri kufanya maamuzi ya haraka kama haya yanaweza kureta mgogoro kwenye chama.Cha msingi ni kumvumilia na kuishi naye kwa akili sana!
 
kutokana na kichefuchefu (haswa baada ya kusema anamtambua jk ni amiri jeshi mkuu na alama ya bunge na hivyo si vizuri kutoka bungeni na kwa kiburi kabisa kusema anasubiria hatma yake chamani kutokana na uamuzi wake huo) ambacho mh. Zitto kabwe ameendelea kuleta ndani ya chadema wana jf wenzangu nilikuwa ninatoa mapendekezo kuwa huyu jamaa ni wa kuogopwa kama ukoma, na ni kidudu hatari kuliko kirusi cha ukimwi kwa wana upinzani, wapigania haki na kwa wananchi wa tanzania waliodhulumiwa haki zao kwa muda mrefu na chama tawala cha ccm. Kwangu mimi namwona ni msaliti mkubwa wa watanzania na upinzani. Hivyo ni nilikuwa napendekeza aondolewe chadema haraka kwani amepandikizwa na ccm. Nakishauri chadema kimvue uanachama ili kunusuru upinzani wa ukweli ambao umebaki peke yake chadema. Je wana jf wenzangu mnaonaje? Je aendelee kubaki chadema au aondolewe. Ushauri utakaopatikana hapa ukiambatana na sababu za msingi, naomba chadema waufanyie kazi.


kwani nani alikuambia kuwa mhe jakaya kikwete sio raisi wa nchi inayoitwa tanzania, sio amiri jeshi mkuu wa majeshi ya tanzania n.k. Kaa chini usome nini hasa chadema wanasema ndio uweze kuanzisha mada yenye mashiko. Kwa kifupi chadema inasema kuwakatiba na sheria mbovu zinawalazimisha watanzania kukubali motokeo ua kura za uraisi yanayotangazwa na tume ya uchaguzi pasipo sheria hizo kutoa fursa ya kupinga matokeo hayo katika vyombo vya sheria kama ilivyo kwa ubunge na udiwani.

hivyo kitendo walichafanya wao kama wabunge ni kusimama wakati wa rais wa jamhuri ya muungano wa tanzania anaingia katika ukumbi wa bunge halafu kutoka nje kwa maana ya kususia kusikiliza hotuba yake kama njia ya kuonyesha kutokukubali kwao kwa mfumo huo wa katiba na sheria zilizopitwa na wakati.

kuhusu suala la zitto sioni kama kuna tatizo kubwa kwa kuwa anatumia uhuru wake wa kutoa maoni, tunaikata ccm kwa kuwa mambo yaote huamuliwa na wa tu wachache na kubaki ni siri yao hao wateule wachache.

Badala ya kumuvua uanachama zitto anatakiwa kupatiwa ushauri tu kuwa kuendelea kuwa anasema sema katika vyombo vya habari vinampunguzia hadhi na heshima aliyo nayo. Kwani wangapi walipiga kura ya kutotoka nje ya ukumbi wa bunge na wameamua kunyamaza?
haiwezekani kikwa chama cha kufukuzana hakuna kuvumiliana.
 
Niliwahi kusema siku moja wakati tukijadili Post ya Mabere Marando kuwa ni UWT; Nilieleza katika watu ambao mie siwahofii ni Marando na nikabainisha kuwa mtu ambaye namuona Hatari kwa CDM ni Zitto Kabwe. Ngoja niitafute hiyo post niwawekee humu au kama kuna ambaye anakumbuka aiweke hapa.
 
Zitto ni mkweli sana , na mkimtoa CDM mmejimaliza. Aliisha wahi kuwaambia juu ya kumfukuza Kafulila, leo madhara yake mmeyaona amewahenyesha kwenye ubunge na ameupata. Msiwazibe wana mapinduzi ya kweli km wakina zitto kusema ukweli wao, hiyo siyo demokrasia. Na ndio maana hapa twasema CDM sio shwari kwa sasa kuna mazongozongo mengi sana ndani ya Chama. Wakina Mbowe wanataka watukuzwe km mungu mtu, sasa watu makini km wakina zitto hawakubali. Kuweni wapole mwacheni atoe mawazo yake.


Na Ubaguzi wa kimaeneo na udini tu ndo unaendelea sasa
 
Mara nyingi nimekuwa nikisoma habari za Zitto zinazohusiana na maamuzi mbalimbali yanayotolewa chedema kupitia vikao vyao na ameonekana mara nyingi kuwa na mtazamo tofauti na maamuzi hayo. Rejea issue ya mzee wa kufulia na mengineyo mengi na akitoka hapo anakwenda kwenye media kutangaza msimamo wake? Je hii inaonyesha huyu bwana yupo pale kwa manufaa yake binafsi. Hebu wanajamii wenzangu tujadili mie nimewasilisha.
 
mbona wenye mawazo km ya zito wakati wa malumbano kabla ya kuingia bungeni walikuwa wengi ,akiwemo ndesa kahigi .
mbona wewe umemlenga zito pekee
 
HUYU DOGO ANADHANI YEYE NI BIGGER THAN CHADEMA.....! imekuwa tooo much...!

DAWA NI KUMFUKUZA TU..! chadema ni chama kikubwa already..!
 
Ndg zangu lazima tutambue kuwa siasa ni gharama, lakini kuhusu hili la Zitto nimekuwa na doubt. Anyway, ninaamini chama kitatujuza ni nini hasa kinachoendelea kuliko kujenga hoja ambazo ni hasi kwa Zitto.
 
Skeleton!

Sasa hivi sio muda muafaka wa kufukuzana kwenye chama CDM wako kwenye kipindi muafaka cha kutengeneza hatima ya nchi yetu miaka mingi ijayo, hao ndio wawakilishi wa kweli na hiyo ni moja ya mambo ambayo sisi tuliwatuma wakatuwakilishe.Tunataka mfumo wa uchaguzi huru na unaoleweka sio huu uliopo wa kutumia IT kuhesabu kura kwa siku tatu na kutumial manual kwa siku chini ya moja.
 
One of the strategic of CCM is always to make sure Chadema stape down by any means Zitto nowdays is one of the weak point where by our anemy may use it.kumfukuza is not any issue ,cha msingi ni Chama kuangalia njia sahihi za kukosoana pale mtu anapokwenda against.unapojenga Chama chenye lengo la kuongoza Nchi lazima utakutana na changamoto kubwa na ndogo na tena watakaokuletea changamoto ni wale watu mnaowategemea la msingi ni kutulia kumaliza tofatuti zenu bila kuathiri uhai,utendaji na uwajibikaji wa chama.Hongera sana CHADEMA kwa uamuzi mlomuonyehsa JK,ni watu kama CHILIGATI na wale wasiopenda kutawaliwa watapingana nanyi .mwisho UJUMBE WANGU KWA CHILIGATI Usivyoipenda CHadema hata sisi hatupendi hata kuiona sura yako wewe na watu wote wenye misimamo kama yako wasiopenda mabadiliko.WE ALL STAND BEHIND YOU CHADEMA MP.
 
Zitto ni mkweli sana , na mkimtoa CDM mmejimaliza. Aliisha wahi kuwaambia juu ya kumfukuza Kafulila, leo madhara yake mmeyaona amewahenyesha kwenye ubunge na ameupata. Msiwazibe wana mapinduzi ya kweli km wakina zitto kusema ukweli wao, hiyo siyo demokrasia. Na ndio maana hapa twasema CDM sio shwari kwa sasa kuna mazongozongo mengi sana ndani ya Chama. Wakina Mbowe wanataka watukuzwe km mungu mtu, sasa watu makini km wakina zitto hawakubali. Kuweni wapole mwacheni atoe mawazo yake.

nilipolisoma jina hapo juu nilidhani mjenga hoja wa maana, kumbe pumba zimekujaa kichwani.
 
mkuu leo asubuhi kwenye jambo tz tbc1 ndi alichosema kwamba mimi sikuchaguliwa na slaa/mbowe bali na wanakigoma kwa hiyo ridhaa yao ilikuwa yamhimu sana ili kuwalk out.
Halafu wanasema nini? Kumfukuza, thubutu, walifanya hivyo kwa kafulila na mwenzake siunaona yaliyowafika, siwamepoteza majimbo yote mawili? Au hawajifunzi?
Kwa taarifa yako chadema haina nguvu wala mvuto kwa majimbo ambayo yana waislamu wengi, zaidi ya umaarufu wa mgombea husika ndo maana hata akina kafulila walipoondoka chadema na mwenzake bado walipata hayo majimbo kupitia nccr mageuzi
leo hii natamani imfukuze zitto ili kifo chao kiwadie kwani watachaguliwa mbeya na kilimanjaro na sehemu zinazofanana na hizo tu.
Trust me.
Solution, (binafsi siipendi ccm lakini siipendi chadema zaidi ndo maana hata kura yangu nilikuwa tayari kuwapa ccm kuliko chama hicho cha kikabila/kidini/kifamilia.
Dr. Slaa you are the hores, i trust you, kupitia uongozi mwanana wa kikwete umeweza kupata nafasi ya kuananika mengi ambayo tulikuwa hatuyafahamu na vyombo vya habari vikapewa nafasi ya kuyaandika, thats big thanks kwa slaa,
lakini ndugu yandu slaa hao watu waliokuzunguka wengi si watu wazuri we know them and we can not trust them anytime hata leo kuwapa nchi, ndo maana hata wabunge wakuteuliwa wamewekana ndugu tu ni tofauti kabisi na cuf ambapo hatuoni ndugu yake seif au lipumba akipendelewa kupewa viti maalum.
Watch it out au fanya hima uungani na watu wa cuf hao wamekomaa kisiasa na hawanatamaa na madaraka then itakuwa easy kuwapeni nchi, other no and go to hell.
See you next time.
Hivi hayo majimbo mawili waliyoshinda kafulila na huyo mwenzake yalikua yanashikiliwa na CHADEMA au CCM?Sasa nani kapoteza jimbo hapo?ni CCM au CHADEMA?
 
Atimuliwe ama ajiuzulu mwenyewe, anaonekana analenga zaidi maslahi binafsi na anajidanganya kwamba yeye ni mkubwa kuliko cdm. hana maana Zitto akakae na akina Rostama tujue moja.
 
Zitto siyo roho ya CHADEMA, hata akiondoka chama kitaendelea kukua tu. Waliondoka akina Kabourou yeye nani? Apeleke unafiki wake kwa wanaoupenda.
 
Zitto ni mkweli sana , na mkimtoa CDM mmejimaliza. Aliisha wahi kuwaambia juu ya kumfukuza Kafulila, leo madhara yake mmeyaona amewahenyesha kwenye ubunge na ameupata. Msiwazibe wana mapinduzi ya kweli km wakina zitto kusema ukweli wao, hiyo siyo demokrasia. Na ndio maana hapa twasema CDM sio shwari kwa sasa kuna mazongozongo mengi sana ndani ya Chama. Wakina Mbowe wanataka watukuzwe km mungu mtu, sasa watu makini km wakina zitto hawakubali. Kuweni wapole mwacheni atoe mawazo yake.

Madhara gani imeyapata CHADEMA Kwa kuwaengua hao ndugu zake zitto?mbona huyo zitto wako alishadadia na kuwa mstari wa mbele kumshughulikia marehemu CHACHA WANGWE?Kiufupi humu JF watu walikua wanamuona Zitto kama malaika,last year ilikua ukimgusa tu zitto humu ndani utajuta kuzaliwa,kila mtu atakushambulia,nakumbuka ile issue ya zitto kumsafisha dr.IDRISA wa TANESCO Ilivyosumbua humu ndani baada ya watu kujaribu kuonyesha zitto anatumiwa na mafisadi kuwasafisha wateule wao,pia mnakumbuka issue ya MREMA wa TANROADS ambae nae zitto alituhumiwa kumsafisha?ka Zitto ni Kuwadi ka mafisadi Japo wengi bado mnakapenda,mi sikapendi,kalihongwa dola 50,000 na ROSTAM kaifagilie mitambo ya DOWANS.
 
Zitto alitaka awe KUB na misimamo yake hii kwa JK. Hebu fikiria: Spika Anna Makinda; NS Job Ndugai; tungekuwa na Bunge gani? Zitto jifunze kidogo ile dhana ya UWAJIBIKAJI wa PAMOJA. Usidhani kwamba hata huko kwenye CC ya CCM wote walikubaliana kumtosa Sitta. Haujamsikia hata mmoja akijitokeza hadharani kueleza msimamo wake tofauti na ule alooueleza Makamba.
Kweli kabisa Ishu ya kumtosa Sitta haikuungwa mkono na member wote wa kamati kuu ila mwisho wa yote jibu moja tu lilitolewa.....Tatizo la Zitto anatafuta cheap politics tu. kwani angekaa kimya kipi kingeharibika? Wengi wape hata kama inakuuma hiyo ndo demokrasia... na kama wengi wangepinga kutoka nje leo Zitto angesema nn?
 
Zitto kwa JK ni kama MBWA kwa CHATU. Lolote utalojaribu kulifanya linalombomoa JK Zito hatakubaliana nawe.
 
Zitto kwa JK ni kama MBWA kwa CHATU. Lolote utalojaribu kulifanya linalombomoa JK Zito hatakubaliana nawe.

Kuna post hapa niliipitiaga kipindi fulani, ya Zitto, anasema alikuwa ateuliwe uwaziri.nadhani katikati kwene kile kipindi cha vuguvugu la Richmond au Buzwagi .Nways taratibu mwanga unajitenga na kiza.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom