Brooklyn
JF-Expert Member
- Mar 17, 2009
- 1,459
- 286
Nawashangaa sana watu wanaosema eti Zitto ni mwana demokrasia, demokrasia gani aliyonayo Zitto ya kutoheshimu kura za wengi? Aesema kwamba walipiga kura, na wengi wakachagua kutoka nje wakati 'Rais' akianza kuhutubia, sasa yeye kama mpenda demokrasia si alitakiwa aheshimu mawazo ya wengi?
Misingi ya utawala bora inasema kama Zitto bado alikuwa na shaka angeomba dissenting opinion yake irekodiwe au hata kuamua kujiuzuru kama anaona jambo analolisimia ni la msingi kiasi kwamba hawezi kuendelea kuishi katika mfumo huo.
Kitendo cha Chadema kupiga kura na kura za wengi kuheshimiwa ni ishara tosha kwamba ndani ya chama kuna demokrasia, kwa hiyo hoja ya kwamba eti ooh Mh. Mbowe anakiburuza Chama haina mashiko.
Katika hili la kwenda kwenye vyombo vya habari na 'kuropoka' kunadhihirisha Zitto asivyopenda demokrasia, na pengine anapenda chama kiwe kinamsikiliza yeye tu. Lazima tukiri kwamba Zitto either bado ni mchanga sana katika masuala ya uongozi na uwajibikaji ama anatumika na kundi au watu fulani kuchafua hali ya hewa ndani ya Chadema.
Binafsi nilipoteza imani kwa Zitto toka kipindi kile cha mijadala ya kununua mitambo ya Dowans!! Bwana mdogo ana tamaa sana ya madaraka na pia ni mtu wa kupenda sana sifa binafsi. Mtu kama huyu hawezi kuwa na mchango wa maana katika kambi ya upinzani.
Somo kwa Zitto: Kwa mtizamo wake, je kufikia uamuzi wa kumuengua Mh. Sitta kugombea uspika kupitia tiketi ya CCM ni wajumbe wote walikubaliana? Na ni wote waliafiki kuwaengua wagombea wanaume na kuafiki kuwasimamisha wanawake tu?
Naamini atajibu si wote. Je kwa nini hakuna mjumbe zaidi ya Katibu Mkuu wa CCM aliyetoka na kwenda kwenye vyombo vya habari kueleza kwamba yeye hakukubaliana na uamuzi wa wengi?
Kuhusu kwamba eti aliwasiliana na wapiga kura wake kujua msimamo wao kuhusu kutoka nje ya ukumbi wa bunge, ni hoja ambayo inaonyesha dhahiri kwamba Zitto ni muongo. Kwa hali halisi ya kimawasiliano ya jimbo la Zitto, aliwasiliana vipi na wapiga kura wake (idadi ya wapiga kura) na kufikia uamuzi kwamba wengi hawakukubakiana na uamuzi wa Chama?
Zitto anasema yuko tayari kusubiri adhabu atakayopewa na chama kwa utovu wa nidhamu, hiki ni kichekesho cha mwaka......badala ya mtu wa ngazi yake (Naibu Katibu Mkuu wa Chama) kusema anaomba radhi kwa kuwa amefanya kosa yeye analeta jeuri kwamba anasubiri adhabu atakayopewa!! Ni kama anawatishia Chadema..!!
Huyu bwana mdogo anaonyesha jeuri na kiburi ambacho hakina maana kabisa!! Binafsi naona angevuliwa uongozi na kubaki kama mwanachama wa kawaida. Chadema isiogope kuwatosa wanachama wasio na nidhamu kama hawa, ni mzigo kwa chama na ukuaji wa demokrasia.
Misingi ya utawala bora inasema kama Zitto bado alikuwa na shaka angeomba dissenting opinion yake irekodiwe au hata kuamua kujiuzuru kama anaona jambo analolisimia ni la msingi kiasi kwamba hawezi kuendelea kuishi katika mfumo huo.
Kitendo cha Chadema kupiga kura na kura za wengi kuheshimiwa ni ishara tosha kwamba ndani ya chama kuna demokrasia, kwa hiyo hoja ya kwamba eti ooh Mh. Mbowe anakiburuza Chama haina mashiko.
Katika hili la kwenda kwenye vyombo vya habari na 'kuropoka' kunadhihirisha Zitto asivyopenda demokrasia, na pengine anapenda chama kiwe kinamsikiliza yeye tu. Lazima tukiri kwamba Zitto either bado ni mchanga sana katika masuala ya uongozi na uwajibikaji ama anatumika na kundi au watu fulani kuchafua hali ya hewa ndani ya Chadema.
Binafsi nilipoteza imani kwa Zitto toka kipindi kile cha mijadala ya kununua mitambo ya Dowans!! Bwana mdogo ana tamaa sana ya madaraka na pia ni mtu wa kupenda sana sifa binafsi. Mtu kama huyu hawezi kuwa na mchango wa maana katika kambi ya upinzani.
Somo kwa Zitto: Kwa mtizamo wake, je kufikia uamuzi wa kumuengua Mh. Sitta kugombea uspika kupitia tiketi ya CCM ni wajumbe wote walikubaliana? Na ni wote waliafiki kuwaengua wagombea wanaume na kuafiki kuwasimamisha wanawake tu?
Naamini atajibu si wote. Je kwa nini hakuna mjumbe zaidi ya Katibu Mkuu wa CCM aliyetoka na kwenda kwenye vyombo vya habari kueleza kwamba yeye hakukubaliana na uamuzi wa wengi?
Kuhusu kwamba eti aliwasiliana na wapiga kura wake kujua msimamo wao kuhusu kutoka nje ya ukumbi wa bunge, ni hoja ambayo inaonyesha dhahiri kwamba Zitto ni muongo. Kwa hali halisi ya kimawasiliano ya jimbo la Zitto, aliwasiliana vipi na wapiga kura wake (idadi ya wapiga kura) na kufikia uamuzi kwamba wengi hawakukubakiana na uamuzi wa Chama?
Zitto anasema yuko tayari kusubiri adhabu atakayopewa na chama kwa utovu wa nidhamu, hiki ni kichekesho cha mwaka......badala ya mtu wa ngazi yake (Naibu Katibu Mkuu wa Chama) kusema anaomba radhi kwa kuwa amefanya kosa yeye analeta jeuri kwamba anasubiri adhabu atakayopewa!! Ni kama anawatishia Chadema..!!
Huyu bwana mdogo anaonyesha jeuri na kiburi ambacho hakina maana kabisa!! Binafsi naona angevuliwa uongozi na kubaki kama mwanachama wa kawaida. Chadema isiogope kuwatosa wanachama wasio na nidhamu kama hawa, ni mzigo kwa chama na ukuaji wa demokrasia.