Zitto anataka kusaliti CHADEMA?

Zitto anataka kusaliti CHADEMA?

Status
Not open for further replies.
Zitto alitaka awe KUB na misimamo yake hii kwa JK. Hebu fikiria: Spika Anna Makinda; NS Job Ndugai; tungekuwa na Bunge gani? Zitto jifunze kidogo ile dhana ya UWAJIBIKAJI wa PAMOJA. Usidhani kwamba hata huko kwenye CC ya CCM wote walikubaliana kumtosa Sitta. Haujamsikia hata mmoja akijitokeza hadharani kueleza msimamo wake tofauti na ule alooueleza Makamba.
 
Katika SIASA kupingana kimtamzamo na wenzake ni jambo la kawaida ila yeye kama kiongozi alipaswa kusimamia na kutetea maamuzi ya wengi bila kuujulisha umma kura yake iliegemea upande upi. Hata hivyo bado ana uhuru wa kuzungumza yeye kama Zitto na Mbunge wa Kigoma Kaskazini
 
Kutofautiana kupo ila kwa utaratibu unaoeleweka si kila mtu anaweza kuja kwenye public kutoa msimamo wake,kwani wengine hawana tofauti na mambo ndani ya chama?Kama ni amewakilisha maamuzi ya jimbo lake mbona hakusema kabla ikajulikana?na ni kwa nini yeye tu ndio awe anawakilisha maoni ya jimboni kwake?Kijana keshalewa itategemea maamuzi ya chama kitafanya nini ila ni ukweli dogo anaporomoka.Pia anahatarisha utulivu ndani ya chama.
 
Niliandika hapa https://www.jamiiforums.com/uchaguzi-tanzania-2010/71656-msaada-kwenye-kona.html kabla ya Uchaguzi.

Tatizo la zitto ni KUTANGULIZA MASLAHI BINAFSI MBELE ya yale ya UMMA kupitia mgongo wa MSIMAMO THABITI! Na kupitia huyu huyu, ccm inaingiza VIRUS CHADEMA. HAWEZI kuondoka kwa sababu sasa kwani hata wanaomtumia wanamaximize akiendelea kuwa ndani ya chama kuliko akiwa nje. Pamoja na ukweli kwamba PUBLIC TRUST Graph yake inashuka, lakini anamomonyoa sawia UMOJA katika chama na sura ya chama inapata MAWAA katika jamii.
 
Not suprised, Where is Warid Kaborou( whatever his name), he is political dead,like Tambwe Hiza, Msabaha,Masumbuko Lamwai and other traitors, Zito go,go, join them,the birds of the similar color fly together.
 
Sipendezwi na jinsi Zitto anavyoropoka hovyo, lakini ili asikichafue Chadema bora aachwe atajikuta mwenyewe yupo nje. Tukichukua mifano michache tangu wakati ule wa kugombea Uenyekiti wa Chama vyombo vya habari na hata CCM walionekana kumbeba Zitto kama vile wanaitakia mema Chadema. Wakati anagombea ubunge mwaka huu akasema 2015 anataka urais. juzi juzi tena akawa anataka kuwa Kiongozi wa kambi ya upinzani bungeni. Sasa amekuja na suala la kilichaamuliwa na kikao cha wabunge wa Chadema na kukiongea nje ya vikao wakati akijua yeye siyo msemaji wao. Kama walipiga kura hata kama alikuwa na mawazo tofauti anaendeleaje kupingana na mawazo ya Chama?
ni kweli.zitto aondolewe chadema.ukweli chadema isipofanya hivyo sasa itakuja kufanya hivyo ikiwa imechelewa.mbona tarime siyo ngome tena ya chadema? Kigoma ndo hiyo inaenda nccr.chadema ni chama cha kitaifa sasa.aache deko.wala hana chochote zaidi ya akina mdee na sasa ndo kabisa,nyerere,mnyika,lissu,zitto nini bana.nasisitiza aondolewe
 
ki ukweli yule jamaa huwa ana vielement ambavyo bado sijavielewa vizuri


kama wengi walishinda basi angeingia bungeni na kisha kutoka.

ANA KIBURI CHA ASILI
 
Akihojiwa na Kituo cha Televisheni cha TBC1, Bw. Kabwe alisema yeye asingeweza kuingia bungeni na kutoka wakati Rais Kikwete ambaye ni Amiri Jeshi Mkuu, na ambaye amefanya mambo mengine mkoani Kigoma kuliko marais wengine anahutubia. Source: Majira

Based on that inaonyesha kabisa Zitto alikua anamuunga mkono kikwete kama katika nafasi ya Urais na Siyo Dr maweapon hiyo ndiyo sababu ya kutoingia bungeni kabisa na kupinga hoja ya chama ya kutoka bungeni wakati Rais anahutubia. Zitto yupo CHADEMA kimaslahi binafsi sana na siyo ya kichama. Kama kweli haungi mkono ni bora angejiudhuru hata hiyo nafasi ya unaibu katibu mkuu awe mwanachama wa kawaida kabisa, Aige mfano wa Shitambala.

WELL DONE ZITTO, kwa kusema ukweli na kutokuwa mnafiki wa dhamira ya nafsi yako kwa kile ambacho unakiamini. Huo ndio ushujaa, usiogope mtu na sema ukweli sio kuburuzwa na wachache ndani ya CHADEMA
 
huyo bwana mdogo kaonja fedha za mafisadi na sasa ameanza kuwatumikia. Nikirejea chaguzi za ndani ya chama ninamwona kama ni kijana mwenye tamaa sana ya madaraka. Mimi sisemi chadema wamfukuze lakini ninawashauri wawe makini nae vinginevyo atakivuruga chama. Sisi wananchi wengi wengi wanyonge hapa nchini tumefurahi kupata chama tunachoona kuwa ni kimbilio letu yaani chadema. Bila chadema tungejuaje kama umaskini wetu umesababishwa na mafisadi wanaokumbatiwa na ccm!! Endapo chadema ikiachwa ivurugwe na wachumia tumbo na wenye tamaa ya madaraka kama zitto ni wazi kuwa chadema itaporomoka na hiyo itakuwa ndiyo furaha ya ccm na mafisadi wake. Wananchi wanyonge walioanza kuona mwanga wa matumaini wataangamia.


zitto amekuwa msaliti wa mabadiliko maana hata anayo yafanya tangu kuingizwa kwenye kamati ile ya madini zitto amekuwa mwanachama wa chadema lakini ki uhakisia zitto yuko ccm hana tofauti na mrema wa tlp!!!! Mifno inaendelea kudhihirika.


Chonde chonde zitto tunaomba kama unadhamira ya kweli usivuruge vuguvugu la mabadiliko maana hautabaki salaama kwani adhabu ya mungu dhidi ya udhalimu unaotaka kutufanyia itakuwa kubwa!!!!!!!!!!!!
 
Tatizo la zitto ni tamaa ya madaraka, na misifa na asipoangalia umaarufu wake utadondoka
 
hata kule jimboni kwake alishinda kwa tofauti ya kura chache sana


huyu angekuwa ndo mwenyekiti angeiuza chadema....... hana maana
 
Sumu. It is not the right time.... tolerance is important in this delicate situation. Play safe! If the changes are for the mass/public nobody can stop them. For he who instigates ill-conflicts will lose credibility before the mass/public. Until that time when public and majority of the members lose trust on such a leader he will disappear in the political arena automatically! The boat has different types of people you cant easily know them unless you give them freedom to speak and show their true colors.



Get lessons from the history.

God Bless Tanzania

I agree with you: Kwa sasa kuna agenda muhimu za kushughulikia kwa pamoja, wasihamishe focus kutoka kwenye kudai Tume huru, Katiba mpya kwenda kwa maoni binafsi ya Kiongozi mmoja mmoja
 
Jamani,
Hichi ni kipindi cha kuimarisha na kukijenga chama kiwe thabiti zaidi.

Ishu kama hiyo sidhani kama ina uzito kiasi hicho bali ni jambo la kumkalisha/kumwonya.

Tusikubali kumpa kunguru faida kwa kunyoosheana vidole hadharani.

Ni mtazamo wangu tuu.
 
Ninaamini UONGOZI wa juu wa CHADEMA unamfahamu ZITTO. Wasimfukuze. Watampa umaarufu kama ule alioupata BUngeni kwenye suala la Buzwagi.
 
Amri jesh mkuu ambae alishinda kwa wizi wa kura. Zitto, hoja ya kitoto. Sema nyingine.

Kwangu mimi Zito hajawahi kuwa hero kwa kuwa ni opportunist mkubwa sana. Maelezo yake ni ya kitoto sana
 
Zitto alitaka awe KUB na misimamo yake hii kwa JK. Hebu fikiria: Spika Anna Makinda; NS Job Ndugai; tungekuwa na Bunge gani? Zitto jifunze kidogo ile dhana ya UWAJIBIKAJI wa PAMOJA. Usidhani kwamba hata huko kwenye CC ya CCM wote walikubaliana kumtosa Sitta. Haujamsikia hata mmoja akijitokeza hadharani kueleza msimamo wake tofauti na ule alooueleza Makamba.

Ni kawaida kabisa kutofautiana kwenye baadhi ya mambo... Naamini hata ndani ya Baraza la Mawaziri huwa pia wanatofautiana. Lakini Sio busara kuongea "publically" kwenye kitu ambacho maamuzi yamefanyika tofauti na maoni yako., ni kuonyesha uchanga wa uhuru wa maamuzi ndani ya vikao. Naami CHADEMA wana "Code of Conduct" na hasa inapokuja namna ya kutoa matamko rasmi ya CHAMA na Maoni binafsi
 
Mi nadhani udhuru nao una threshold yake mkulu.

Nafahamu. Ataondoka mwenyewe atakapoona anatofautiana na wenzake karibu kwa kila jambo. Kaka yake, Dr Kabourou, hayuko CHADEMA. Hakufukuzwa. CHADEMA ni imara zaidi sasa kuliko wakati wowote. Misimamo ya watu wa KIGOMA, KAGERA, MBEYA,......inafahamika.
 
Zitto atueleze anaitaka CHADEMA haitaki siyo kila siku yeye tu, kama anataka kuwa mpiga debe aende huko CCM akaungane na Tabwe Hiza
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom