Zimbabwe Election: Progress & Results

..kitila,

..mwisho wa mugabe unakuja,haitakuwa this election year,but unakuja!

..castro yuko wapi? sasa ona cuba inavyobadilika taratibu!
 
A lot of people will be disappointed baada ya matokeo ya huu uchaguzi. Mugabe against the world and guess who is going to win!!!??
 
Pengine wengine hawajaona Red card ambazo Bob Karigamombe anazoonyeshwa. Akishinda jamaa watachinjana ile ya Kenya itakuwa ni mchezo wa mdundiko.
 
Ningekuwa Mzimbabwe ningempa kura yangu Mugabe kwa mbwembwe zote bila kusita.
Ukiangalia kwa undani sana utaona matatizo ndani ya Zimbabwe yameanza pale tu mgogoro wa Ardhi ulivyoanza. Lakini kabla ya mgogoro huo Zimbabwe ilikuwa shwari na ilikuwa kipenzi kikubwa cha nchi za Magharibi.
Hapa inaonesha wazi kwamba nchi za magharibi zinaangalia masilahi yao zaidi kuliko masilahi ya wananchi wa nchi husika. Nasisi Waafrica kama hatutaamka na kufungua macho katika hilo basi tujue wazi kwamba bado hatuko huru kama tunavyodhani. Tulipigania uhuru hapo awali ili tuweze kuwa na mamalaka ya kuendesha nchi zetu bila ya kuingiliwa na nchi nyingine, ila tutashirikiana na nchi nyingine tutakazo taka kushirikiana nazo bila ya kushurutishwa na mtu ama hali fulani.

Tuwe makini sana na vyombo vya habari vya nchi za magharibi kwani vinapenda sana kupotosha na kupaka matope yale yaliyo mazuri katika Africa ili yaonekane mabaya na tuanze kuichukia Africa yetu. Na hapo ndipo hawa watu wa magharibi wanapopata mwanya wa kutugombanisha sisi wenyewe kwa wenyewe, huku wakituuzia silaha zao.
Nimefika Zimbabwe miezi mitatu iliyopita, hakuna njaa kama vyombo vya habari vya nchi za magharibi vinavyotangaza. Chakula kipo ila kama kawaida ni pesa yako ndiyo inayoweza kukuchagulia nini ule na kwa wakati gani kama sehemu yoyote ile Duniani. Kila nchi duniani kuna watu masikini na pia kuna sehemu ambazo zinakaliwa na watu wenye kipato cha chini. Vyombo vya habari vya nchi za magharibi mara nyingi sana vinapenda kuonesha ama kutangaza sehemu hizo mbaya na masikini, havipendi kuonesha sehemu nzuri na safi. Hayo ndiyo yanayotendeka huko Zimbabwe.
Zimbabwe inaweza kuwa na uhaba wa chakula kuliko Somalia na Sudani?, hamwoni kama hii yote ni propaganda ya hawa watu wa magharibi?
Mnafikiri kwanini nchi nyingi duniani na wala si Africa tu zina muunga mkono na kumtambua Mugabe?. Kwanini Nelson Mandela amekaa kimya kuhusu suala hili?, kwani lingekuwa baya linalohusisha ubaguzi mzee huyu asingeona haya hata kidogo kumwambia ukweli Mugabe.

Hii yote ni kampeni ya nchi za magharibi zikiongozwa na UK+USA kuichafua Zimbabwe na kumchafua Mugabe, huku zikijaribu kuwataka na wengine pia kufuata mkondo huo.

Kumbukeni tulitawaliwa kiasi cha kutosha, tulinyanyaswa kiasi cha kutosha na sasa ni wakati muafaka wa kukataa mambo hayo.
 
Mtambo: Pamoja na maelezo yako marefu na mazuri, hebu tuambie, ina maana huko Zimbabwe au humo ndani ya ZANU-PF hakuna mwingine wa kutetea hiyo ardhi unayodia isipokuwa Robert Gabriel Mugabe? Ina maana Zimbabwe haiwezi kuwepo bila Mugabe au namna gani? Why Mugabe tu?
 

Sikiliza Kitila, Tatizo lilipo hapa ni kwamba kwanini wananchi wa Zimbabwe wampe kura Mugabe na wala si kwanini ZANU-PF waendelee kumsimamisha Mugabe kuwa mgombea wa kiti cha Uraisi kwa tiketi ya ZANU-PF.
Hayo ni mambo yanayo kihusu chama cha ZANU-PF na wanachama wake, kwani bila shaka wana katiba na itikadi zao.
Kama wao wameona Mugabe anafaa kuendelea kugombea kiti hicho kwa tiketi ya chama chao sasa kelele za nini?.
Watu wa nchi za magharibi wanachotaka ni kutawala Zimbabwe kwa remote control kwa faida yao na wala si kwa faida ya wazimbabwe.
Hata huyu wanayempa support kwa sasa kama hatafuata yale wanayotaka basi elewa kwamba watafanya kama wanavyofanya sasa ama zaidi ya haya. Kwanini tusijifunze kwa yaliyomtokea Sadamu Hussain, Charles Taylor, Mabutu, Musharaf na wengineo?.
Tuwe makini sana na watu wa nchi za magharibi muda wote wanajaribu kutafuta njia mpya za kubeba na kuhamisha rasilimali zetu kwa ajili ya maendeleo yao. Wanatutumia sisi wenyewe kufanikisha malengo yao.
 
Ninaogopa kusema lakini ni ukweli usiopingika kwamba Mugabe ni kichaa. Huwezi kuongoza nchi yenye inflation rate ya 100,000% na bado unataka kuendelea kuwepo madarakani hadi kifo. Hivi kweli ni nchi za magharibi ziliwapiga wapinzani? Ni nchi za magharibi zimefungia vyombo vyote vya habari na kubakiza viwili tu vya serikali? Hivi ni mjinga gani asiyejua mashamba walinyang'anywa weupe wachache wakapewa viongozi wezi wachache wa ZANU na ndugu zake Mugabe?

Mugabe ni kichaa na wanaomsapoti wajiulize mara mbili mbili> Huwezi kuwasema wazungu vibaya wakati kila mtu anajua Mugabe ndio anayewaletea mateso watu wake. Mbona waafrika tunajiaibisha hivi jamani? hatuwezi kutumia akili zetu na kufikiri? Mugabe yuko pale kwa ajili yake yeye binafsi na sio kwa ajili ya wazimbabwe au kwa ajili ya kupambana na wazungu. Hizo ni sababu tu za kuwavutia wavivu wa kufikiri ili wamsapoti. Grrrrrrr!
 
Mugabe ni kiongozi ambae kwa kweli sitmuonea aibu usoni mwake iwapo nitaonana nae ! Nina guts kweli kweli juu ya huyu mzee !

i cant even put words into sentences maana nina mengi ya kusema juu ya huyu mzee !
 
Kura za wapinzani wawili ambao wameshindwa kuungana na kuwa pamoja ili kumng'oa Mugabe zitakuwa ni nyingi kuliko atakazopata Mugabe. Hivyo wasipopata kura zaidi ya asilimia 50 (combined) wamekwisha.
 
Either way he should be thoroughly rejected by the people of Zimbabwe but then again this is Africa we are talking about here....typical Africans will elect him again...
 
Zimbabwe election facts

FOLLOWING are some key facts on Zimbabwe's elections.

* Zimbabwe has a total of 5,934,768 registered voters from a population estimated at over 13 million.

* At stake in the parliamentary election are 210 House of Assembly seats and 60 seats in the Senate, the upper house.

* Vote counting starts immediately after polls close. Parliamentary results will be announced in constituency centres and the presidential result in the capital Harare.

* The main election observer mission is from the Southern African Development Community. Monitors from Western countries critical of Mugabe were barred.

* The winner needs more than 51 percent in the presidential election to avoid a run-off.

* President Robert Mugabe got 56 percent in the last election in 2002. Main rival Morgan Tsvangirai got 42 percent then.

* In the 2005 parliamentary election, Mugabe's ruling Zanu PF won 78 of 120 contested seats while Tsvangirai's MDC won 41 seats. One seat went to an independent

Source: Reuters

Mahali walipochemsha wapinzani ni pale waliposhindwa kukubaliana kushirikiana. Nimeshangaa kusikia kwamba wanafanya majadiliano ya ushirikiano ikiwa round ya kwanza hatapatikana mshindi. Hivi kwanini wasikubaliane kuanzia round ya kwanza ili waongeze chances za kushinda. Wanapogawanyika ndiyo wanampa nguvu zaidi Mugabe.

Kilichotokea Kenya kitarudiwa Zimbabwe na tena with full information. Matokeo ya round ya kwanza yatatoa picha ni wapi waibe na watumie njia gani kuiba kura. Haya mambo ya wote kung'ang'ania kuingia Ikulu ndiyo yanafanya upinzani ushindwe kwenye chaguzi.
 
Kwani Tanzania Ina Tofauti Gani Za Zimbabwe Au Kwa Sababu Nyie Mnakaa Mijini Hamjui Yanayoendelea Vijijini Tangu Hawa C.c.m Watutawale Tuna Nini Kipya Kwani Ni Lazima Tutawaliwe Na C.c.m Angalieni Maendeleo Ya Mikoa Na Wilaya Yaliyokuwepo Zamani Halafu Ufananishe Na Sasa Angalieni Maendeleo Ya Miji Iliyokuwepo Zamani Usafi Wa Miji Taa Za Barabarani Na Bustani Nzuri Halafu Leo Hii Angalia Bustani Zile Ziko Wapi Taa Ziko Wapi Eti Barabaraya Morogoro Kuanzia Pale Faya Mpaka Makutano Ya Sam Nujoma Ndiyo Bustani Zetu Mpya Baada Ya Uhuru.aibu.halafu Ati Mji Una Meya Na Huwa Sijui Ni Elimu Gani Au Kigezo Gani Kinahitajika Ili Mtu Awe Meya Maana Nawaona Kama Vichekesho Tu
 
Prof Baregu unahabari nyingi sana za Zimbabwe,hebu tupatie taarifa ya mgogoro wa aridhi kule zimbabwe maana naamini wewe uliishi kule miaka kadhaa.

Lakini hivi huu Umoja,sijui niseme muungano wa africa(AU)wanafanyaga nini wanapokwenda Ethiopia?Mimi nadhani matatizo ya Zimbabwe yangekua miongoni mwa agenda za mikutano yao lakini utakuta ndio wa kwanza kumtetea Mugabe anapowekewa vikwazo.
 
Q&A: everything you need to know about the elections



What's happening?


Mugabe akishinda AU waende kumng'oa bana kama walivyofanya Comoro maana mwenyekiti wa AU hana mchezo ati?.
 

Sawa kabisa Maj gen, Tusiwalaumu hawa Wazimbambwe they know what they are doing...the one wears the shoes knows where it hurts, they might not be stupid as most us think of. We Tanzanians have been doing the same for many years..with the late Nyerere even now with CCM.....mnakumbuka tulikuwa tunapigia kura kivuli ama picha ya mtu, baadaye ikawa jembe na nyundo wakati tunafahamu hatuwezi ongozwa na kivuli ama Nyundo ukizingatia 80% of the population walikuwa wakulima mlitegemea nini? CCM imekuwa ikideclare winner even before registration for voting !!!the diference in Tanzania CCM do not public announce....they usually prepare the swearing party way before we vote, acheni propaganda...za kijinga, hivi unataka niambia wananchi Rukwa Mbunge wao Mzindikakaya wanatofauti gani na Wazimbabwe? Jimbo la Makweta, RA, wabunge wa maisha hadi Mungu awachukue, CCM itatawala milele Tanzania, tuache wasingizia Wazimbabwe nasisi tuko hivyo hivyo Mugabe juuuuuuuuuuuuuuuuuuuuu hongera kuwa raisi wa Zimbabwe huru.....
 
Either way he should be thoroughly rejected by the people of Zimbabwe but then again this is Africa we are talking about here....typical Africans will elect him again...

This is scary but the fact. And here is what the so called defence forces are saying:

"Defense Forces commander Gen. Constantine Chiwenga has said his soldiers will not serve anyone but Mugabe and on Friday the chiefs of the police, army, air force, prison service and intelligence agency told reporters the armed forces were "up to the task in thwarting all threats to national security."
And there are people even in this forum who are so daring that they still support Mugabe! If you can unshamedly support Mugabe, what moral authority do you have to question what CCM is doing? Hii dunia ina mambo kwa kweli!
 
Hii yote ni kampeni ya nchi za magharibi zikiongozwa na UK+USA kuichafua Zimbabwe na kumchafua Mugabe, huku zikijaribu kuwataka na wengine pia kufuata mkondo huo.

Ina maana kaka (samahani kama ni dada), yale matatizo ya Zimbabwe huamini kama ni ya kweli? Hapo ulipo hujakutana kabisa na wazimbabwe wakwambia yanayoendelea Zimbabwe? Tutaendelea lini kuwalaumu wazungu kwa matatizo tunayojisababishia wenyewe? Hakuna mzungu aliyemwambia Kibaki aibe kura wala hakuna aliyewaamuru wakenye wauane au sio?

Mugabe kaichafua Zimbabwe kwa mikono yake mwenyewe na inabidi awajibike kwa hilo, kuwalaumu wazungu ni kukwepa kuwajibika na ni utoto wa hali ya juu!
 
Kitila
Lazima tukubaliane na Democracy. Hata Tanzania mpaka sasa bado kuna watu wanaona kuwa CCM ina devine right ya kutawala, ragadless of all the mess they have caused, ni uelewa tu wa watu kwa hiyo wanaomsupport Mugabe, tuwaheshimu. Mimi leo nikiitwa mwafrika mpumbavu kwa kiasi fulani nakubali, kwa sababu mambo kama haya ya Zimbabwe yanaprove kuwa sisi na watu wa namna hiyo. Zimbabwe kuwa raisi kwa mara nyingine tena is in the interest Bob and his Cronies, not in the Interest of Zimbabweans, neighbors na kwa ujumla ni shame kwa Africa nzima.
Nimeangalia clip moja inaonekana kuwa kuna watu tayari wamekufa toka mwaka 1901 lakini wameingizwa kwenye karatasi ya wapiga kura na watampigia Mugabe, na kuna voting center ambayo iko shambani hakunua kibanda wala hakuna njia ya kwena huko, clearly ukijumlisha na kaluli za wana usalama utaona kuwa Mugabe atashinda tu, kama alivyoshinda Kibaki!
 
Bongolander, hata yule adversary wa Mugabe marehemu Smith yupo kwenye register book, halafu tukiambiwa sisi tuna matatizo tunavimba!
 
Wazimb kwa sasa naweza kuwapa nafasi kama ya wale wa kiteto majuzi walio vaa maguo na makofia ya CCM wakati ukweli uko mezanoi lakini wakaimba Kidumu Chama chao .
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…