Zanzibar yaridhia mwaka mpya wa kiislamu kuwa siku ya kitaifa

Muuza Kangala

JF-Expert Member
Jul 21, 2021
1,126
4,169
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi ametangaza Siku ya Mwaka Mpya wa Kiislamu kuwa Sikukuu ya Kitaifa Zanzibar.

Dkt. Mwinyi ametangaza siku ya Jumatano ya Julai 19, 2023 sawa na Mwezi Mosi Muharram kuwa siku ya mapumziko Kitaifa Zanzibar ili kuadhimisha siku ya mwaka mpya wa Kiislamu.


1689618087881.png

---
Raisi wa Zanzibar, Dkt. Hussein Mwinyi amesema serikali itatoa tamko kuifanya siku ya mwaka wa kiislamu kuwa ya mapumziko, Dk Hussein Mwinyi alisema hayo Julai 31, 2022 katika kongamano lililofanyika msikiti wa Jamiu Zanzubar, Mazizini, mkoa wa Mjini Magharibi.

Rais Mwinyi alisema maadhimisho hayo yatafanyika kwa mzunguko kati ya Unguja na Pemba ili kutoa nafasi kwa waislamu kushiriki. Alisema utaratibu wa kuadhimisha mwaka mpya wa kiislamu utawasaidia waislamu kuujua mwaka wao kidini.

Waislamu wanatumia Kalenda ya Hijiri ambayo miezi yake huanza na kuisha kulingana na mbalamwezi. Kutoweka kwa mwezi kunaashiria mwisho wa mwezi. Kalenda hii iliundwa rasmi mwaka 622AD wakati wa utawala wa Khalifa Umar ibn al-Khattab. Kalenda hii inatumika kuashiria matukio na tarehe muhimu za kiislamu kama vile Ramadhani, Eid al-Fitr, Eid al-Adha na mwanzo wa msimu wa Hija.

Mwaka wa Hijiri una miezi kumi na miwili; Muharram, Safar, Rabi’Al-Awal, Rabee’Al-Akhir, Jumada Al Ula, Jumada Al-Akhirah, Rajab, Shaabani, Ramadhani, Shawwal, Dhu Al Qa’da na Dhu Al Hijja.

Waislamu husherekea mwaka mpya wa Hijiri (unao chukuliwa kuwa likizo rasmi katika baadhi ya nchi za kiislamu) katika mwezi wa kwanza wa kalenda ya kiislamu ya Muharram kila mwaka.
 
OIC mliwakatalia bure kwani hata Uganda wamo na Suriname, Guyana, hata Guinea pia
Sio waislam tu kwenye jumuiya hiyo

Kuhusu mwaka mpya ni sawa kwani wanasema wengi wape na asilimia kubwa ni Waislam hivyo hatuoni shida

Ila kama utaangalia kwa husda na ubaya lazima upinge

Hata wakifanya Mwezi wa Ramadhani wamalize kazi saa 7 sawa tu
 
CCm Ili kushinda Zanzibar,lazima wajifanye wao ndio waislamu zaidi..it is a political tactic,zile hoja za uzanzibari na uTanganyika hamtazisikia,zinakuwa replaced na udini...expect a docile Zanzibar in the next 5 yrs,watakuwa kama watu wa bara.
CCM hata waipambe misikiti kwa dhahabu na wadhikiri uchi kwa Zanzibar haiwezi kushinda uchaguzi wowote huru na wa haki.

Hichi chama kilishajifia zamani, kinabebwa na Jeshi la uvamizi la Tanganyika pamoja na usalama wao wa Taifa waliojiingiza kwa wingi sana hadi wengine wanavaa rubega za kimasai
 
CCM hata waipambe misikiti kwa dhahabu na wadhikiri uchi kwa Zanzibar haiwezi kushinda uchaguzi wowote huru na wa haki . Hichi chama kilishajifia zamani , kinabebwa na Jeshi la uvamizi la Tanganyika pamoja na usalama wao wa Taifa waliojiingiza kwa wingi sana hadi wengine wanavaa rubega za kimasai
Huwajui ndg zetu wakina Ishmael
 
Huwajui ndg zetu wakina Ishmael

Kwa hali hii hata siku moja.

Ishmaeli wengine kutoka jeshi la Burundi waliletwa kuja kupiga watu hapa wakati wa Uchaguzi

wengine ndio hawa wa jeshi la Tanganyika sikiliza walivyotufanyaia uchaguzi uliopita





 
Ili kwenda sawa, na wakristo wa Zanzibar waongezewe siku moja ya Sikukuu, mfano Jumatano ya Majivu au Alhamisi Kuu ifanywe kuwa Sikukuu ya Kitaifa na siku ya mapumziko
Wakristo wa Zanzibar tokea enzi na enzi hawana fujo na mtu , matatizo yameanza baada kuvamiwa na Tanganyika na kuanza kuletwa vijikanisa vya ajabu ajabu na hivi ndivyo vinaweza kujaribu kuleta chokochoko hiyo
 
Back
Top Bottom