Kuna viongozi wakuu wa aina mbili, kisiasa na kiutawala, kisiasa watu wanaitwa viongozi wakuu kitaifa ni watano. Rais, VP, PM, Rais wa Zanzibar na CM.
Kimamlaka nchi ina mihimili mikuu mitatu ambao ni rais Mkuu wa the executive, serikali, Spika Mkuu wa the legislature , Bunge na Jaji Mkuu, Mkuu wa the Judiciary, Mahakama. Hawa wakuu wa mihimili ndio the top kwenye mihimili yao.
Hawa wakuu wa mihimili wako sawa Kimamlaka. Rais, Spika na Jaji Mkuu wana hadhi na mamlaka sawa kupitia kanuni ya usawa wa mihimili "the principal of separation of powers, checks and balances. Rais ndiye mkuu wa wote, huu ndio mhimili uliojichombia chini zaidi,analiunda Bunge analivunja na kuteua mtendaji mkuu wa Bunge. Ndie anateua Jaji Mkuu. Spika ni mkubwa kuliko Waziri Mkuu ndani ya Bunge. Bunge nalo lina ukubwa kuliko rais wa JMT linaweza kumuondoa rais madarakani.
Japo rais anamteua Jaji Mkuu hawezi kumtengua na rais akivunja katiba Jaji Mkuu ndio anamchunguza na kuliarifu Bunge linamuondoa rais madarakani.
P