Zanzibar ni member wa SADC?

Zanzibar ni member wa SADC?

CCM unaitaja ili iweje haswa.. kama unashida nao nenda Lumumba ukawasalimu. Inaonyesha una mawazuuuuu na hicho chama chao.. na bado utaendelea kuisoma namba maana Mwenyekiti wao ni bonge la Jembe..
Tena inakuwaje Mwenyekiti wenu hamumupambi bali muko bizi na Jembe kila wakati na Chama chake?
Hopeless
 
Nimeelewa watu hupendekeza katiba na kuitumia. Zanzibar kwenye masuala hayo haipo. Haitambuliki kwasababu sio nchi bali kikoloni cha Tanganyika
 
Scotland,Northern Ireland,England and Wales all of these are nations with their own rules but united together to bring up a one strong nation called United kingdom.And the strongest arm overtaking all is England.
Na hilo je unalizungumziaje???
Na hapa kinachoitwa muungano ni nini???
Tanganyika inajulikana km Tanzania bara.
Ukisikia Tanzania bara basi ujue Tanganyika tayari hyo.
Kila muungano wa mataifa una policies zake unaozitengeneza kuhusiana na hiyo Union.
Mnh.. Huu mfano sidhani kama uko relevant...
 
p
Tanzania ni JMT ya TZ Bara na TZ Visiwani, Rais wa Zanzibar ni mmoja wa viongozi 5 wakuu wa JMT wakiongozwa na President, VP, PM, Rais wa Zanzibar na Waziri Kiongozi kwa mujibu wa katiba ya JMT, au Makamo wa I na II kwa mujibu wa katiba ya Zanzibar ambapo rais wa Zanzibar ni mjumbe wa cabinet ya JMT kama Waziri asiye na Wizara maalum. Hivyo amehudhuria kama kiongozi wa kitaifa.
P
Pascal hiko sio kikao cha CCM pale chimwaga au lumumba sema tuna mazuzu wengi Sana awam hii ya chattels ndohu tabu nyanda
 
Yani Zanzibar kama wanajielewa wangesepa tu..
Muungano Wa nchi mbili ila Rais ni mmoja!!

Rais Wa Jamuhuri ya Muungano Wa Tanzania. JPM

She ni kama RC tu Zanzibar.
 
Muungano Ni UKOLONI TUU FULL STOP
Mkuu Dega, muwe angalau na shukrani japo kidogo kwa sababu ni muungano ndio umewafanya baadhi yenu mpo hadi leo, ingekuwa sio muungano kuna watu fulani , baada ya yale Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, wangekuwa wiped kwenye uso wa dunia, the wiper alikuwa ana wipe tuu, lakini ni kupitia Muungano huu adhimu Nyerere akazuia watu fulani wasiwe wiped.
Shukuru kwa hilo.

P
 
Mnajichanganya kwenye katiba cheo cha waziri kina teuliwa na rais tu na ndiye anaye weza kutengua, je Shein kateuliwa na nani
Dr. Shein aliteuliwa Waziri wa JMT na rais Magufuli na aliapishwa Ikulu jijini Dar es Salaam.
P
 
Sasa hapo anaepaswa kudai taifa lake ni mtanganyika au mzanzibar?
Maana Zanzibar INA exist ila Tanganyika haipo popote, nani amepunjwa?
hizi ndio kero za muungano , kama zanzibar iliungana na Tanganyika na bado ipo je Tanganyika iko wapi ? au Tanzania ndio Tanganyika , kwanini ? ndio maana wazanzibar wanataka kero zitatuliwe , kumbuka wanasema Zanzibar ni Nchi , ina bendera na wimbo wake wa Taifa , sasa kinachoitwa muungano ni nini ?
 
Kiukweli elimu ya uraia inahitajika sana. Kumbe watu hamjui kuwa rais wa Zanzibar ni mjumbe wa cabinet ya JMT kama Waziri asiye na Wizara maalum na alifanikiwa na JPM. Nchi yetu Ina viongozi wakuu 5 wa kisiasa wanaotembea na msafara wa vingora.
  1. Rais wa JMT
  2. Makamo wa Rais
  3. Waziri Mkuu
  4. Rais wa Zanzibar
  5. Makamo wa Zanzibar
P.
CDF anatembea na king’ora, haya naye muweke hapo kama king’ora ni sifa ya kuwa kiongozi mkuu!
 
Asa atakuaje mwanachama wa CAF ilhali Tanzania yawakilisha serikali zote????
Nikuulize na ww,kwan Zanzibar kama Zanzibar ipo ktk wanachama wa UN???
Kwani wizara ya michezo ipo katika mambo ya Muungano?
 
CDF anatembea na king’ora, haya naye muweke hapo kama king’ora ni sifa ya kuwa kiongozi mkuu!
Spika, Jaji Mkuu, CDF, boss wa TISS, IGP, wao wana vingora vya escorts kuwasafishia tuu njia lakini sio kusimamishiwa magari. Hawa watano traffic wanawekwa kuziba njia gari zinasimamishwa, hawa wengine hakuna traffic bali wanapishwa tuu njia kama fire au ambulance.

Hizo escorts hata mtu wa kawaida unaweza omba unalipia unaletewa, kwenye misiba, ugeni au matukio muhimu, unaomba escort unapewa.
P
 
Tanzania ni JMT ya TZ Bara na TZ Visiwani, Rais wa Zanzibar ni mmoja wa viongozi 5 wakuu wa JMT wakiongozwa na President, VP, PM, Rais wa Zanzibar na Waziri Kiongozi kwa mujibu wa katiba ya JMT, au Makamo wa I na II kwa mujibu wa katiba ya Zanzibar ambapo rais wa Zanzibar ni mjumbe wa cabinet ya JMT kama Waziri asiye na Wizara maalum. Hivyo amehudhuria kama kiongozi wa kitaifa.
P
Kiungo mwakilishi kutoka ZNZ ni SAMIA na aliteuliwa kutoka znz kuwa makamu wa rais kuiwakilisha ZNZ kwenye muungano huu TATA.
Kwa SHENI kuhudhuria naona ni kujikomba kwa wahusika kuficha aibu ya utata wa muungano feki.
 
Kiungo mwakilishi kutoka ZNZ ni SAMIA na aliteuliwa kutoka znz kuwa makamu wa rais kuiwakilisha ZNZ kwenye muungano huu TATA.
Kwa SHENI kuhudhuria naona ni kujikomba kwa wahusika kuficha aibu ya utata wa muungano feki.
Mkuu Mwala, kwanza uheshimu muungano usiuite feki, bali una changamoto.

Makamo wa rais ni structural issue kuwa rais akitoka upande mmoja wa muungano Makamo lazima atoke upande mwingine, hivyo Samia sio mwakilishi wa Zanzibar kwenye serikali ya JMT ni rais mwenza wa JMT, in case of anything, kama kutimia kwa ile ndoto ya Lema, yeye ndiye anaapishwa kuwa rais wa JMT.

In case rais akitoka Zanzibar, makamu atatoka Bara huwezi sema makamu ni mwakilishi wa bara ndani ya serikali ya JMT.

Mwakilishi halali wa Zanzibar ndani ya serikali ya JMT ni rais wa Zanzibar anayeingia kwenye cabinet ya JMT kama Waziri asiye na Wizara maalum.
P
 
Back
Top Bottom