Zanzibar kuendelea kunufaika na karafuu ya Morogoro, wakatazwa isiuzwe kwa ushindani, Waziri wa Kilimo, viwanda SMZ yuko Morogoro leo

nokwenumuya

JF-Expert Member
Jun 29, 2019
810
2,851
Juhudi za Mkoa wa Morogoro kuwakwamua wakulima wa karafuu kupata mnunuzi mwenye bei nzuri zimegonga mwamba baada ya kulazimishwa kuwa lazima karafuu inayozalishwa Morogoro basi iuzwe kwa SMZ ili wao wauze nje kwa bei kubwa zaidi.

Kwa wasiojua, Morogoro vijijini wanazalisha karafuu nyingi kuliko Zanzibar yote. Uongozi wa Morogoro kwa muda mrefu umekuwa ukipambana ili ipate wanunuzi watakaoshindana badala ya kuendelea kulanguliwa na SMZ na wao kupata bei kubwa katika soko la dunia.

Siku ya leo Waziri wa Viwanda, Kilimo na Biashara wa Zanzibar anafanya ziara huko Morogoro vijijini wanakolima karafuu. Awali walilazimisha Uongozi wa Mkoa wa Morogoro uingie nao mkataba wa kuwa hakuna mtu mwingine kununua karafuu ya Morogoro isipokuwa wao SMZ.

Ikumbukwe karafuu ni zao ghali sana duniani. bei yake kimataifa ni kubwa sana. Siku zote SMZ ilikuwa inajificha chini ya mawakala kuinunua lakini sasa wamekuja wenyewe.

sasa huu Muungano ni kama hauna maana kama utakuwa unanufaisha kasehemu kadogo huku majority wakiumia. haya maagizo kutoka juu yanatuumiza watanganyika. Walianza kukopa pesa nyingi kupeleka kwao, wamekuja kubinafsisha bandari zetu zote, wakasema wana ardhi yao Bagamoyo huku watu wa bara hawaruhusiwi kumiliki ardhi kule, sasa leo wamekuja kwenye karafuu Morogoro.
 
Karafuu ya Morogoro usiifananishe na karafuu ya Pemba. Its about quality.

Kuna nchi nyingi zinazalisha karafuu duniani, lakini Zanzibar ni number one by quality.
 
Nina shamba hapo Morogoro la Karafuu. Mwaka wa jana walikuja wa indonesia (Barozi wa Indonesia Tanzania), kuingia mkataba Kijiji cha Konde Matombo Morogoro, Mkataba uliingiwa mbele ya Mkurugenzi wa Halimashauri Rehema Bwasi, Mkuu wa Wilaya(Albert Msando) na Wanasheria wa Ubarozi na Halimashauri wa indonesia hao pia wamewekeza Zanzibar kwahiyo wamekuja na Wazanzibar wengi. Mkataba unataja ujenzi wa kiwanda cha majani ya Karafuu kuzalisha mafuta, na Ununuzi wa Karafuu yenyewe.

Utekelezaji wa mradi hauweleweki mpaka sasa. Kuna benki ilikuja kutoka Mikopo, pia nayo ikaingia mkataba na wanakijiji ikawaadaa ikaondoka. Naona hata waziri wa Zanzibar anaenda nae atawapiga kiswahili pia ataondoka.

Morogoro Milima ya Uluguru (Matombo) kwa sasa wanaongoza kulima mazao ya viungo (Karafuu) kwa Tanzania, na miaka 3 ijayo itatoa karafuu mara 4 ya Zanzibar, lakini Serikali imewaacha wakulima, ambao kwa nguvu zao na kujitafuta wamebuni Njia za kulima zao hilo bila msaada wa serikali wala ushauri wao.

Wanaofaidika na karafuu ya Morogoro ni Kenya, ambao utumia madalali wa kitanzania kukodisha Miti kabla haijazaa na kuwanyonya wakulima huku Serikali ikiangalia. Karafuu hiyo uenda Kenya sababu madalali wameshika soko. Nini cha kufanya.

i. Kuanzisha chama cha ushirika ambacho wakulima watauza, watapata mikopo, na watapata ushauri wa kilimo, Mkurugenzi na Mkuu wa Wilaya walisema wataanzisha mbele ya mkutano wa wananchi lakini hakuna kilichoanzishwa yalikuwa maneno.

ii. Wananchi wanajitaidi kulima lakini moundombinu ni duni, Barabara ya Matombo - Konde KM 4 ni mbovu na Injinia wa Halimashauri aliwaambia wananchi kwamba ataijenga lakini hakuna kinachoendelea.

iii. Umeme umevutwa kijijini na transfoma zimefungwa 2 lakini huu ni mwaka wa 3 haujawashwa kwahiyo wananchi wamechoka.

iv. Wananchi wameongopewa sana na wanasiasa kwa namna nyingine wamechoka. Kijiji kimoja kinatoa tani 300 za karafuu, kg 1 inauzwa 14,000/. hadi elf 22,000/. Lakini kijiji barabara mbovu, zahanati hakuna, shule msingi mbovu, sekondari hakuna na Umeme hakuna.

Serikali vikumbukeni vijiji watu wanapambana lakini msaada hakuna. Vijiji vinavyolima Karafuu Milima ya Uluguru ni Konde, Lubwe, Tegetero, Kinore, Sanzani, Kitungwa, Lugogo, Kibwege, na vinginevyo.
 
Hivi MVIWATA ilikufa, makao makuu yake si yapo Morogoro? Au wakulima wa Matombo hawamo kwenye vikundi vya MVIWATA?
 
Karafuu ya Morogoro usiifananishe na karafuu ya Pemba. Its about quality.
Kuna nchi nyingi zinazalisha karafuu duniani, lakini Zanzibar ni number one by quality.
Quality? Karafuu ya Morogoro ni kali sana by quality na inatoa harufu kubwa( Sting Aroma). Inawasha sana kwa sababu inazalishwa katika eneo la baridi kiasi na joto la wastani ( Muinuko1,200 M - 1,500 M juu ya Milima ya Uluguru yenye urefu wa 2,800M, kutoka usawa wa bahari), kwahiyo karafuu inayozalishwa kwenye Mid - climate au baridi na joto kidogo uwa kali sababu ya baridi uongeza ubora wa mazao. Karafuu ya Zanzibar haiwashi sana kwa sababu ya joto kali zanzibar (Mansoon type of climate) na hali ya mvuke wa pwani, pia haina harufu kali, sababu joto huadhiri ubora na ukuaji wa mazao.

Mikarafuu ya Morogoro ukaa miaka 80 hadi 100 maana hao wahindi wa Indonesia walpokuja Morogoro walikagua mkarafuu wa 1 ambao una miaka 80 na bado unazaa, wakasema Mikarafuu yote ya Zanzibar na Morogoro ilitoka Indonesia ikaja Mauritius halafu ikalwetwa Zanzibar na Wafaransa ndipo wamisionari wa katoliki Wakaileta Milima ya Uluguru, walisema Indonesia na Zanzibar ni visiwa vyenye joto ubora wa karafuu upo chini kuliko Morogoro ambapo karafuu ulimwa kwenye hari ya uvuguvugu (Mid climate) na milimani.

Pia indonesia na Zanzibar Mikarafuu mwisho miaka 40 hadi 50 wakati Morogoro hukaa miaka 100. Ndio maana Karafuu Morogoro ugombaniwa na madarali ili wakachanganye na ya Zanzibar au ya Mueza Tanga.
 
Nina shamba hapo Morogoro la Karafuu. Mwaka wa jana walikuja wa indonesia (Barozi wa Indonesia Tanzania), kuingia mkataba Kijiji cha Konde Matombo Morogoro, Mkataba uliingiwa mbele ya Mkurugenzi wa Halimashauri Rehema Bwasi, Mkuu wa Wilaya(Albert Msando)...
Nchi ya kiduwanzi saana hii
 
Quality? Karafuu ya Morogoro ni kali sana by quality na inatoa harufu kubwa( Sting Aroma). Inawasha sana kwa sababu inazalishwa katika eneo la baridi kiasi na joto la wastani ( Muinuko1,200 M - 1,500 M juu ya Milima ya Uluguru yenye urefu wa 2,800M, kutoka usawa wa bahari)...
Mkuu umemwaga madini muhimu, natamani kuingia kwenye hiki kilimo naomba nije pm kwa maongezi zaidi.
 
Juhudi za Mkoa wa Morogoro kuwakwamua wakulima wa karafuu kupata mnunuzi mwenye bei nzuri zimegonga mwamba baada ya kulazimishwa kuwa lazima karafuu inayozalishwa Morogoro basi iuzwe kwa SMZ ili wao wauze nje kwa bei kubwa zaidi...
Duh! Jamaa wanatafuta weeee kutuchonganisha but where! Hawatoweza.
 
Juhudi za Mkoa wa Morogoro kuwakwamua wakulima wa karafuu kupata mnunuzi mwenye bei nzuri zimegonga mwamba baada ya kulazimishwa kuwa lazima karafuu inayozalishwa Morogoro basi iuzwe kwa SMZ ili wao wauze nje kwa bei kubwa zaidi...
Naona Zanzibar wanataka kututawala wa Tanganyika tuwarudishe kwao.
 
Aisee, kumbe Mambo mazuri hivi. Basi wananchi wajitahidi kulimabkwa ukubwa ili iwaokoe washing maisha Bora. Wasiingize siasa kwenye hili Jambo lao. Mie naamini wakizalisha soko litapatikana tu

Sent from my SM-G977B using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom