duh.. hapa hata sijaribu kuelimisha. Basi nimekubali maana kama mtu haelewi summons na subpoena kati ya sheria za Kiingereza na Kimarekani basi tuna kazi.
Sawa: Mahakama zetu katika kesi za madai hazina uwezo wa kumuita shaidi au ushahidi kama kwa uamuzi wake au kwa kuomba na pande yoyote katika kesi usiku.
Sawa: Washtakiwa katika kesi za madai hawana haki ya kuwaita mashahidi wa watakao kutetea upande na hawawezi kufanya hivyo kwa sababu Jaji atawashangaa.
Sawa: Katika kesi za madai za Tanzania mshtakiwa hana haki ya kuita mashahidi na mahakama haiwezi kulazimisha mashahidi hao kuja mahakamani.
Nimekubali sijui sheria kwa sababu nasoma kama novel!! Nimekubali kushindwa handedly.
Mzee Mwanakijiji,
Na wewe kwa upotoshaji kweli umekubuhu, ukija pewa nafasi sitashangaa nikiona unakuwa worse kuliko hata hao akina Rweyemamu. Katika mjadala wote huu sijaona mahali popote palipokufanya uje na conclusion kama hiyo unless kama lengo ni ku SPIN.
Kama nilivyosema mimi sio mwanasheria ila nimeona cases nyingi tu ambazo mashahidi wanaotakiwa na upande mmoja au mwingine hawafiki mahakamani na case inaendelea.
Mfano juzi tu hapa case ya prof. Mahalu ambayo mashahidi mbalimbali wa serikali wameshindwa kwenda mahakani na hakimu akaamua case iendelee.
Angalia pia Milosovic naye alitaka mashahidi kibao lakini akaambiwa wao sio relevant kwenye cases husika.
Mimi nakumbuka hata wakati wa case ile ya wale waliotaka kumpindua Nyerere, mashahidi wengi ambao waliomba waje mahakamani, hawakwenda.
Sasa nitashangaa kweli kwenye case ya madai kama utaweza kumuita mtu yeyote unayemtaka bila kuonyesha sababu za msingi za kuwepo kwake. Kwa mfano ili uweze kusema Manji ndiye alirudisha pesa za Kagoda lazima uwe na ushahidi kuonyesha hivyo, ushahidi ambao umepatikana kwa njia halali. Hapo ni bank iliyopokea au wale waliokuwa wanapokea hizo pesa, vinginevyo mahakama itakataa kumwita shahidi huyo.
Case ya mafisadi ingekuwa na maana kama Mengi na wengine tunaopinga mafisadi ndio tungeifungua case na sio vinginevyo. Kwasasa kazi kubwa ya kuhakikisha madai ya ufisadi iko kwa Mengi na wala sio kwa hao mafisadi.
Pia Mengi ni wrong person kupigana hii vita ya ufisadi kwasababu ni rahisi sana kuonyesha kwamba kwa njia moja ama nyingine kuna ugomvi na wahusika hasa Manji. Huo ugomvi wao binafsi whether ni kwenye biashara au huko Yanga, sio tu unawagawa watu bali pia unashusha uzito wa case.
Hawa mafisadi ilitakiwa wafikishwe mahakamani na watu ambao wako clean kwenye suala zima.
Ninakuwa na wasiwasi kweli na hawa watu wanaowashauri viongozi wetu au wafanyabiashara maarufu. Huenda kwasababu hao viongozi wetu hawaambiliki au washauri wetu ni opportunists na wanaangalia boss anataka nini kisha kwenda na wazo kama hilo. Mshauri ambaye ni huru angeweza kabisa kumwambia Mengi timing sio nzuri.
Vinginevyo hata mimi nasubiri hiyo case. Tatizo tu Mengi akishindwa tayari atakuwa ameua case nzima na hawa mafisadi na itakuwa ngumu sana kwa mtu mwingine kuwavaa.