Yupo wapi dereva teksi alyefichua njama za kumpindua Nyerere mwaka 1982? Je, alilipwa chochote kama ‘asante’?

Na yeye sijui kwa nini alitibua mpango wa wenzie bora angeacha tu hiki chama cha lumumba kisingekuwa madarakani leo hii ona sasa tulipo fika...
Comment yako imenifikirisha mno...

Kweli sisi vijana ni watu wa muhemko...

Yaani umepata "likes" 19?!!!

It's terrible

Tunalijenga taifa la aina gani ?!!!

Ni kutopenda umaana wa SOMO LA URAIA?!!!

Sijui ni kipi haswa?!!

Watu 19 wanashabikia MAPINDUZI YA KIJESHI ?!!! HAVOC HAVOC HAVOC

Hivi unadhani salama ya nchi ni kupinduana kijeshi?!!!! wanajeshi unawajua kwa kuwaona tu wamevaa sare huku mitaani ?!!! (

Kuiondoa "status quo" kijeshi ni kujiingiza katika "Moto wa duniani"...kwani "wakionja" huwa inafanywa ADA....

Wacha maskhara wewe
 
Khalafu utakuta anayeota mapinduzi analikitambi hata kutembea mita 500 hawezi. Angalie huko Kongo mkimbizi anakimbia na kutembea mamia ya km na rti mbuzi na safuri mgongoni. Acha kabisa hayo mambo. Na Miungu apishie mbali.
....apishie mbali ,aaamen aaamen aaamen

Amani ni kila kitu....
 
Ukiwa na mkosi hata ufanye jambo la kishujaa kiasi gani "hupati".

Jiulize watu wachache waliopigana vita vya Tanzania vs Uganda leo hata yebo hawavai sababu ya umasikini lkn waliokombolewa Dar - Dubai kula bata
 
Wamakonde wa pale Msasani nao wana mchango wao mkubwa katika kufanikisha kufichua uovu huo.

Zamani Idara ilijua kuchomeka watu na wakavaa uhalisia pasipo kufichua uficho wao!

Eti kila chuo maarufu lazima awepo mwehu wa kuzunguka majalalani. Mastelingi na maproduza wa hizo muvi walikuwa kiboko.
 
Ukiwa na mkosi hata ufanye jambo la kishujaa kiasi gani "hupati".

Jiulize watu wachache waliopigana vita vya Tanzania vs Uganda leo hata yebo hawavai sababu ya umasikini lkn waliokombolewa Dar - Dubai kula bata

Mfumo ndio unaotakiwa uyafanyie kazi hayo yote kwa kuweka taratibu za mafao yanayoeleweka kwa wahusika. Kama ni kusubiri fadhila na hizani, matokeo ndio hayo wahusika wanabakia na simulizi za kuvutia za kukusanya watu viembe gahawa huku wakipigwa na njaa kali. Yaani utasikia tulipotia buti Arua aah eya!!!
 
Historia ya serikali ya nchi hii ina Mengi na Mengi hayo hatuyajui.

Kina Hanspope, Maganga, Tamimu na wengine wengi walipanga kumuua na kuipundua serikali ya Mwl Nyerere.

Inadaiwa dereva teksi aliyekuwa akiwasafarisha wapanga mapinduzi kuhudhuria vikao vyao vya Siri alibaini mpango wao na kuripoti kwa vyombo vya usalama.

Muda umeenda Sasa, huyu dereva teksi ni nani? Yupo wapi Sasa? Alilipwa nini na serikali Kama shukurani ya kuinusuru nchi?
Mohamed Said anaweza kueleza hili vizuri
 
Hatukuwepo....

Ila yameandikwa vitabuni na magazetini....

Nilipokuwa shule ya msingi nilikuwa najisomea nakala ya gazeti la RAI kila wiki....nikapata kuwajua akina LUTENI LUGAKINGIRA ,EUGENE MAGANGA ,UNCLE TOM ,TAMIMU ,HATTY MC GHEE na wengineo.....

Tupende kujisomea....

Maarifa hupatikana humo....

#SiempreJMT
Ni lweli maarifa yapo kwenye maandishi. Kuna umuhimu mkubwa sana wa kuziendea maktaba.
 
Historia ya serikali ya nchi hii ina Mengi na Mengi hayo hatuyajui.

Kina Hanspope, Maganga, Tamimu na wengine wengi walipanga kumuua na kuipundua serikali ya Mwl Nyerere.

Inadaiwa dereva teksi aliyekuwa akiwasafarisha wapanga mapinduzi kuhudhuria vikao vyao vya Siri alibaini mpango wao na kuripoti kwa vyombo vya usalama.

Muda umeenda Sasa, huyu dereva teksi ni nani? Yupo wapi Sasa? Alilipwa nini na serikali Kama shukurani ya kuinusuru nchi?
Huyo alikuwa ni Shushushu. Enzi zile walikuwa wakiendesha vile vigari vya Kirusi.... Jina nimelisau.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom