rodrick alexander
JF-Expert Member
- Feb 12, 2012
- 15,206
- 20,191
Kwa wale wanaofatilia Azam TV, kuna mahojiano na mashabiki kuelekea mechi ya Yanga na Simba. Katika mahojiano hayo kuna shabiki mmoja wa Yanga anatamka bila wasiwasi na Azam TV kumuweka hewani kuwa, Simba hawawezi kufunga Yanga bila makandokando na hata walipomfunga nne walimhonga Yondani.
Yondani bado anacheza mpira kama ajira yake, kitendo cha kumhusisha na hongo kitamfanya asiaminike hata pale inapotokea akafanya kosa kwa bahati mbaya. Pia kitawapa mashaka waajiri wake hata kutomuongezea mkataba.
Katika ile mechi, Yondani aliingia mwishoni wakati timu imeshafungwa, kwanini sasa wamhusishe na hongo? Kwa TV kama Azam sikutegemea kama wanaweza kukosa weledi na kurusha kipindi bila kufanya uhariri, hivyo ni muda sahihi wa Yondanj kuchukua hatua za kisheria dhidi yao.
Yondani bado anacheza mpira kama ajira yake, kitendo cha kumhusisha na hongo kitamfanya asiaminike hata pale inapotokea akafanya kosa kwa bahati mbaya. Pia kitawapa mashaka waajiri wake hata kutomuongezea mkataba.
Katika ile mechi, Yondani aliingia mwishoni wakati timu imeshafungwa, kwanini sasa wamhusishe na hongo? Kwa TV kama Azam sikutegemea kama wanaweza kukosa weledi na kurusha kipindi bila kufanya uhariri, hivyo ni muda sahihi wa Yondanj kuchukua hatua za kisheria dhidi yao.