Yona na Mramba hawana kesi ya kujibu maana katika katiba yetu ya Tanzania kahuna sheria au kifungu chochote binding kinachomtaka Waziri au Niabu Waziri kufuata ushauri fulani katika kutoa maamuzi , ndio maana kuna collective cabinet responsibilities hivyo kama hawa walikosea, ni Cabinet nzima na Rais wao-Mkapa walikosea na kuitia serikali hasara hizo, pia hawawezi kufanywa scape goats maana sheria ina-operate uniformly btn citizens hivyo hata wengineo walioboronga inabidi waletwe mbele ya Pilato mkuu as soon as practically is possible. Labda akina yona na Mramba wa-argue hili ili watanzania wainuliwe macho..
Case hii ni Nzuri kama DPP akiishinda maana ina na ita-set precedent kwa wengineo kufanyiwa kweli, sio Magufuri, Megji (sorry spelling), kalamagi na hata Mkapa Mwenyewe.
Wanaosema kwamba tuna kinga ya Rais, nafikiri hao bado ni mbumbumbu au wavivu wa kufikiri na kutafakari mambo - kwani kinga hiyo haimkingi Rais anapofanya -criminal activities, sema kwa mfano Rais yuko likizo na katika Likizo hiyo akagombana na watu kijijini kwake au hata member wa familia yake, naye aka-mshuti, sheria itakuwa ni sheria tu haijari kama ana kinga, Lazima afikishwe kwa pilato. Au sema akiwa huko Holiday afanye tendo lolote ambalo ni criminal kama ku-mwibia nduguye chochote kile katika familia yao, na mtu huyo wa familia akamfungulia mashitaka, ni lazima ashitakiwe tu.
Nina maana ya kwamba sisi wa-Tanzania ndio wanafamilia ambao tumewathamini na kuwaweka madarakani viongozi mbalimbali wa serikali zetu. Wakati tunawaweka huko, wao waliahidi kwamba watawatumikia vema WaTanzania kwa kufutua misingi ya katiba. Sasa kwa ufupi ni kwamba wametukosea na kudai kwamba eti siku hizi wao ni wanafunzi na sio wanasiasa, hii inaonesha ni jinsi gani walivyo na madhalau ua upeo mdogo wa uelewa, na wanafikiri kwamba hata sisi pia tuko kama wao.
Kinachotakiwa ni DPP na wanasheria wake wawapeleke wote waliokuwa kwenye cabinet ya mkapa na waishitaki cabinet nzima ya mkapa-Kikwete akiwemo pia kwamba- wali-abuse powers as collective responsibility na pia kwamba wananchi wa Tz hawakuwatuma kwenda kufanya criminal activities bali ku-excute sheria zilizomo ndani ya katiba yetu.
Evidence zipo za akina Mwakyembe na Dr Slaa, kwa nini kusua sua, witness wapo na affidavits nyingine zipo sasa kwanini kuogopa ogopa kama kuku anayechinjwa?
Kama DPP anasua sua hata yeye mwenyewe ana harufu ya ka-ufisadi maana walikuwepo wakati haya yanatokea in some capacities, na tunachohitaji ni kuwa na independent judiciary iliyo kama federal Court ya USA kwamba Rais aweze kuwachagua majaji lakini asiwe na uwezo wa kuwafuta baada ya bunge kuwathibitisha, wao wawe independent na excutives pia legislature.. hii itasaidia kuwafikisha mahakamani wale wote wanaofanya uharifu. Pili ili kuthibiti Rushwa inabidi tuangaliwe wenzetu wanaipunguzaje katika mahakama na taasisi nyingine, angalia mfano wa SFO= SERIOUS FRAUD OFFICE au angalia JINSI Mapolisi wa UK wanavyokuwa wana-attend matukio na kuwahoji watu,
kWANZA huwatenganisha watu na kuchukua malelezo mbalimbali, hii inasaidia non colaboration ya ushahidi, pia hao police wa uk huwa wana vinasa sauti mpaka camera kwenye vichwa au masikio yao... kila kitu wakifanyacho kinakuwa documented hamna rushwa ndogo ndogo bwana. Pia anaglieni wenzetu China, ukipatikana na hatia ya Rushwa Lazima unyongwe tu baada ya appeal zote kufanyika, haya anagalieni Malaysia pia Singapore, if they say something they mean it. ukipitisha madawa, utanyongwa ukikamatwa, na hili linafanyika, kuna -less standard of proof katika makosa yanohusu public na this is a way to go in Tanzania sio kuanza kuwahurumia etu tume ama tunakusnya ushahidi, ushahidi waweza kukusanya mtuhumiwa akiwa rumande...
Watanzania tuamkeni na tuwachangamikie wote walioanya ufisadi na kuamua yafuatayo.
1. Dpp alisema kwamba ma-fisadi wote wakipelekwa mahakamani , nchi itayumba, basi afanye amnest kwa masharti ya kwamba mali zao zote zitaifishwe na ziletwe kwenye ujenzi wa taifa pia mafisadi hao badala ya kuachwa kwenda huru, waisadie serikali katika kutumia akili zao kuziba mianya ya ufisadi maana wao wanazifaham loopholes za grand corrption haswa.
2. Tusikubari kwamba inchi itayumba maana asemaye hivyo ni mvivu wa kufikiri naye pia ana -abuse authority yake kwa kutofanya anacholipwa afanye yaani kuwafikisha wote wahusika na watuhumiwa wa ufisadi na abuse of powers kwa mzee pilato.
3. Tufanye mchakato nchi nzima na tujue wananchi wanataka nini, maana ionekanvyo ni wabunge wachache sana wanaopigia kelele mambo hayo ya ufisadi na utendanji kazi, yawezekana labda hawajui au wamezidiwa na data na inabidi wanyamaze ili wao wanazozijua data wazilezee vizuri.
4. Nchi kama nchi inabidi iwe na malengo na kuyatimiza malengo hayo kwa muda fulani na sio endless malengo yasio isha, mfano, tunataka kuwa na motorways regardless of costs ambazo zitaunganisha mikoa yote ya Tanzania inyeshe Mvua, jua liwake barabara zipitike wakati wote, lengo hili lifanyike ndani ya miaka 5 Rais anapoingia madarakani, pia tuweze kuinua pato la mkulima kwa ku-commercialise kilimo within 3 years ya mungwana katika kazi.
4. Tuondokane na kasumba kwamba wawekezaji ndo wanaleta maendleo na ku-create jobs ingawaje hii is arguable both ways, wawekezaji hao ni lolongolongo tu maana Tanzania hatuna umeme wa uhakika, kama viwanda vyote alivyojenga nyerere, vikifufuriwa na kufanya kazi 24/7, basi hatutakuwa na uwezo wa kukidhi mahitaji ya umeme, pia kwamba kamam viwanda hivyo vyote vikifanya kazi , basi kazi zenyewe zitatafuta watu na sio watu kutafuta kazi, hata hao wakimbizi waliopo Kigoma kutakuwa hakuna haja ya kuwarushisha makwao bali ni tutawatumia kwa manufaa yao na kwetu.
Ni haya tu wakuu na najua kwamba uchangiaji wangu waweza kuwa na mapungufu fulani, uboleshini na nitaupokea ushauri wenu.
SMP- LLM London