Yona na Mramba: Mashtaka na yatokanayo

Yona na Mramba: Mashtaka na yatokanayo

Mheshimiwa Mwakenja hongera. Unaijua kazi yako na unaifanya kwa umakini. Jamii ya Watanzania ina imani nawe. Sheria ifuate mkondo wake.

wewe na mimi hatukuwepo wakati mramba na yona wakifanya madudu yaliyowafikisha mahakamani, ila tumemtwaa tu-try kwa sheria zetu, kwa sheria iliyoko yule ni mtuhumiwa tu na hajawa convicted, kwa hiyo anayo haki ya dhamana.

inapotokea hakimu anamkomoa mtu anyemtuhumu kwa kuzima simu na kukimbil;ia bagamoyo ili asiandike removal order tumsifu kwa lipi? kama yeye ameshawahukumu ya nini sasa waendelee kuitwa watuhumiwa? nadhani huyu hakimu ni mkomoaji, na hastahili kuitwa mtoa haki, yeye ni sawa na mafisadi wengine, tofauti tu yeye anaifisadi sheria tuliyoitunga wenyewe(kwa kuwakilishwa na bunge letu)

asipotenda haki kwa hawa una hakika gani kuwa atatenda haki kwa mjomba wako aliyekamatwa na kubambikiziwa kesi na polisi? au siku kikwete atakapombakizia kesi dr slaa akapelekwa kwake una hakika gani atatenda haki?

tusimame kwenye haki na tujue kuwa mahakama ni mahali pekee panapotolewa haki, hakutakiwi watu wanaoendeshwa kwa utashi na ushabiki wao kama mwankenja bali wenye uadilifu na kuifuta sheria
 
wewe na mimi hatukuwepo wakati mramba na yona wakifanya madudu yaliyowafikisha mahakamani, ila tumemtwaa tu-try kwa sheria zetu, kwa sheria iliyoko yule ni mtuhumiwa tu na hajawa convicted, kwa hiyo anayo haki ya dhamana.

inapotokea hakimu anamkomoa mtu anyemtuhumu kwa kuzima simu na kukimbil;ia bagamoyo ili asiandike removal order tumsifu kwa lipi? kama yeye ameshawahukumu ya nini sasa waendelee kuitwa watuhumiwa? nadhani huyu hakimu ni mkomoaji, na hastahili kuitwa mtoa haki, yeye ni sawa na mafisadi wengine, tofauti tu yeye anaifisadi sheria tuliyoitunga wenyewe(kwa kuwakilishwa na bunge letu)

asipotenda haki kwa hawa una hakika gani kuwa atatenda haki kwa mjomba wako aliyekamatwa na kubambikiziwa kesi na polisi? au siku kikwete atakapombakizia kesi dr slaa akapelekwa kwake una hakika gani atatenda haki?

tusimame kwenye haki na tujue kuwa mahakama ni mahali pekee panapotolewa haki, hakutakiwi watu wanaoendeshwa kwa utashi na ushabiki wao kama mwankenja bali wenye uadilifu na kuifuta sheria


Mkuu Mwikimbi
Ni kweli tunategemea sheria lakini kama hawa waheshimiwa wenyenchi hawakuona kero za mahakama na kilio cha wananchi kutendewa haki mahakamani, utamweleza nini mdai haki wa karibu miaka 50 akuelewe mbele ya mwenye kunyimwa haki kwa wiki? Kusimama kwenye haki kunahitaji haki pia
 
.... kama yeye ameshawahukumu ya nini sasa waendelee kuitwa watuhumiwa? nadhani huyu hakimu ni mkomoaji, na hastahili kuitwa mtoa haki, yeye ni sawa na mafisadi wengine, tofauti tu yeye anaifisadi sheria tuliyoitunga wenyewe(kwa kuwakilishwa na bunge letu)...asipotenda haki kwa hawa una hakika gani kuwa atatenda haki kwa mjomba wako aliyekamatwa na kubambikiziwa kesi na polisi? au siku kikwete atakapombakizia kesi dr slaa akapelekwa kwake una hakika gani atatenda haki?
Mkuu,hebu fanya kama unacheza mchezo wa 'SCRABLE' na hizo BOLD alafu nambiye kama utaelekea kufikiri ninavyofikiri mimi....ntaomba maoni yako mkuu....
My Take:Hizo thubutu za hao uliyowaita mahakimu zinabaraka kutoka mkono wa kuume wa serikali.
 
kinachofurahisha hapa ni kuwa hata baba wa bwana harusi elvis msiba ameshawahi kufungwa miaka ya nyuma kwa tuhuma za wizi... Tena alifungwa keko hapo hapo alipo mramba

watoto wa mafisadi wafunga ndoa!!!!!!! ..... 🙂
 
Jamani, sidhani kama Mramba na Yona wameonewa. Alichokifanya Mwankenja nadhani ni sahihi kwa sababu alikuwa bado hajapokea nakala ya hukumu ya Mahakama Kuu na awali aliipangia kesi hiy kuja tarehe 2 yaani kesho. Hivyo watuhumiwa hawa hawakupaswa kuja mahakamani leo unlss kama Mahakama kuu ingekuwa imeshaleta nakala ya hukumu ambamo ingekuwepo amri ya kumtaka hakimu awaite watuhumiwa leo na kuwapatia dhamana.
Mwankenja alipokea nakala mchana leo haikuwa na amri ya kumtaka asikilize ksi hiyo leo. Hivyo alikuwa sahihi kabisa 'kuwafukuza' watuhumiwa hao hadi kesho. Hii haimaanishi kuwa hawana haki ya dhamana, lakini haki yao lazima ifuate matakwa ya kanuni na taratibu-kama kesi imepangwa kesho, basi waje kesho na watakipata hicho wanachokihitaji.
kama Mwankenja angekiuka taratibu hizi na kuwapatia dhamana leo, watu wangemshangaa sana kwamba amefanya hivyo kwa kukiuka kanuni
 
Hii ni vita ya wakubwa wacha nyasi ziungue kwa joto kali maana si mchezo hapa .
 
Hii ni vita ya wakubwa wacha nyasi ziungue kwa joto kali maana si mchezo hapa .

Mkuu kwa hili tupo pamoja kwani ukiangalia Hakimu alikosea hata kupiga hesabu za dhamana, na aka demand cash instead of immovable asset of that value
Bodo tuu kesi immenda kwake tena
Mbona wale mafisadi walikuwa wanaend mahakamani pindi wanapokamilisha masharti ya dhamana
Huyu hakimu lazima atakuwa fisadi
 
Mkuu kwa hili tupo pamoja kwani ukiangalia Hakimu alikosea hata kupiga hesabu za dhamana, na aka demand cash instead of immovable asset of that value
Bodo tuu kesi immenda kwake tena
Mbona wale mafisadi walikuwa wanaend mahakamani pindi wanapokamilisha masharti ya dhamana
Huyu hakimu lazima atakuwa fisadi

Kama unadhani ni fisadi basi jaribu kumpelekea pesa ili amalize kesi hiyo uone kama na wewe ukulala Keko. Yeye alikuwa anatimiza wajibu wake kama alivyoona sheria inamtaka. Kama kakosea hiyo ndio kazi ya mahakama kuu. Kwani Majaji watafanya kazi gani?
 

Kama mtakumbuka wakati walimu walipogoma hukumu ya kusimamisha mgomo wao ilitolewa saa ngapi?Je ilikuwa ni siku ya kazi?au kuna kina kipengele kinachoruhusu kazi za mahakama kuendelea kama ni serikali itakuwa inahusika?


kwa taarifa ambaoz ninadho mpaka sasa,mambo ni magumu sana katika chama na kwa sasa hata mkulu anatumia inteligensia ya Jeshi kuhandle ishu zake.Hakuna kuaminiana kwa sasa kati ya mtandao kwa kuwa watu hawaeleweki leo wanataka Mkulu afanye hli kesho wanamwambia amekosea hivyo mkulu kaamua kufanya anavyoona ni sahihi ili kuwaridhisha wananchi.

Hili la saa ya kazi kuisha, hakuna kukomoana ni utaratibu na hebu jiulize kama Mramba na mwenzake wangepata dhamana baada ya muda wa kazi kuisha si mngeanzisha lawama nyingine. Kuna mahabusu wangapi huko nyuma walifanyiwa kama Mramba na mwenzake na hakuna aliyelalamika?

Kuhusu Mgomo wa walimu, Serikali ina haki ya kuchukua tahadhari kwa jambo lolote inayoona linaweza hatarisha ufanisi wake, hivyo kutoa hukumu usiku inategemeana na uzito wa jambo, Dhamana ya Mramba na mwenzake haiakuwa na umuhimu wowote katika uendeshaji nchi hivyo hakukuwa na haja ya kuchukua tahadhari. Kumbuka serikali hailali watu ndiyo wanalala na ndiyo maana kuna wengine wanakesha ili kukufanya wewe ulale usingizi. Sasa usilinganishe watu wawili na serikali (Iliyopo kwa ajili ya watu 40 million).
 
Hili la saa ya kazi kuisha, hakuna kukomoana ni utaratibu na hebu jiulize kama Mramba na mwenzake wangepata dhamana baada ya muda wa kazi kuisha si mngeanzisha lawama nyingine. Kuna mahabusu wangapi huko nyuma walifanyiwa kama Mramba na mwenzake na hakuna aliyelalamika?

Kuhusu Mgomo wa walimu, Serikali ina haki ya kuchukua tahadhari kwa jambo lolote inayoona linaweza hatarisha ufanisi wake, hivyo kutoa hukumu usiku inategemeana na uzito wa jambo, Dhamana ya Mramba na mwenzake haiakuwa na umuhimu wowote katika uendeshaji nchi hivyo hakukuwa na haja ya kuchukua tahadhari. Kumbuka serikali hailali watu ndiyo wanalala na ndiyo maana kuna wengine wanakesha ili kukufanya wewe ulale usingizi. Sasa usilinganishe watu wawili na serikali (Iliyopo kwa ajili ya watu 40 million).

Duh, nchi ya wadanganyika, poleni - mahakama + serikali = usanii.
 
Jamani kwa wale wanaomsema Hakimu, wakati walikwenda kwenye vikao vya michango ya dhamana automatically au mnaweza kuonekana ni bias. Hiyo ni moja. Pili mali isiyo hamishika inaweza kukubaliwa, lakini uthaminishaji wa mali Tanzania una matatizo, moja ya ku-inflate thamani, pili ya hiyo dhamana kuweza kuuzika. na hasa wakati huu ambapo ufisadi umepungua, hivyo huyo wakuweza kununua nyumba hiyo atapatikana wapi?. Hivyo dhamana yenye 99.9% ni cash/ Bond, lakini ukitoa hiyo Bond ambayo huandikwa na Bank kwenda Mahakamani, still ni lazima hiyo Pesa iwepo in the account, maana Bank hawawezi kukupa Bond, ikiwa huna hela huko Bank. Sasa utakuta wengi waliofanya Ufisadi hiyo hela haipo Tanzania au haipo kwenye Bank Zetu, na usipokuwa mwangalifu unaweza kupewa Bond feki, toka kwenye Ma-Bank huko Amerika ya Kusini, Mauritius, Dubai etc. Pili lazima mumpe Hakimu heshima yake, sio a-dance kutokana na uwezo au wasifu wa mtuhumiwa.
 
Dhamana ya akina Yona yabaki fumbo
Shadrack Sagati
Daily News; Monday,December 01, 2008 @21:15

Mambo yameendelea kuwa magumu kwa mawaziri wawili wa zamani Basil Mramba na Daniel Yona baada ya juhudi za kuwatoa rumande kukwama tena jana. Washitakiwa hao wawili ambao wanadaiwa kuitia hasara ya Sh bilioni 11. 7 serikali, walishindwa kupata dhamana baada ya Mahakama ya Kisutu kugoma kusikiliza shauri lao kwa maelezo kuwa taratibu za mahakama zilikiukwa.

Hakimu Hezron Mwankenja ambaye anasikiliza kesi hiyo, hakuthubutu kuwapandisha kizimbani washitakiwa hao, baada ya kung'amua kuwa hakukuwa na hati ya kuwapeleka mahakamani hapo (Remove Order). Hakimu huyo pia alisema hata jalada ambalo lilitoka Mahakama Kuu, halikuwa na amri ya Msajili au ya Jaji inayomtaka yeye kusikiliza shauri hilo kwa siku ya jana, kitendo ambacho kilimfanya kugoma kusikiliza shauri hilo.

Jana haikuwa siku ambayo washitakiwa hao walipangiwa kwenda mahakamani, ila kwa washitakiwa ambao dhamana zao ziko wazi huwa wanafikishwa mahakamani kutoka rumande kwa hati maalumu ya hakimu. Lakini kwa Mramba na Yona mahakama hiyo haikuwa na habari za wao kufikishwa kuendelea na mchakato wa dhamana.

Badala yake kesi hiyo ilishapangwa leo kwa ajili ya kutajwa tena; fursa ambayo washitakiwa wanaweza kuitumia kuendelea na mchakato wa dhamana zao. Hata agizo la msajili wa Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam Lameck Mlacha, alilolitoa siku ya Ijumaa kuwa mchakato wa kupata dhamana kwa washitakiwa hao ungeendelea jana Kisutu, halikuwekwa kwa maandishi.

Ni kwa sababu hiyo, Hakimu Mwankenja hakuwa na njia nyingine; bali kuwaeleza kwa kina mawakili wa pande zote kuwa hawezi kuendelea na shauri hilo kwa vile taratibu za mahakama hazikufuatwa hasa za kuwapeleka washitakiwa hao mahakamani hapo jana. Aliwaeleza kuwa yeye hakutoa hati ya kuwapeleka mahakamani washitakiwa kuendelea na mchakato wa kupata dhamana, hivyo hawezi kusikiliza shauri hilo.

Kutokana na msimamo huo wa hakimu, mawakili wa upande wa utetezi na wale wa upande wa mashitaka walilazimika kurudi katika ukumbi namba moja wa mahakama na kuchukua nyaraka zao na kuondoka ukumbini. Kitendo hicho kiliwaduwaza ndugu wa washitakiwa ambao tayari walishajazana katika ukumbi huo, kwa matumaini kuwa taratibu za dhamana zingekamilika na kujumuika nao uraiani.

Ndugu hao baada ya kuona mawakili wanaondoka, nao walitoka nje ya ukumbi wakiwa na shauku ya kilichotokea. Hata mawakili wa washitakiwa hawakuwapa maelezo ya sababu ya kesi hiyo kutoendelea jana. Badala yake ndugu hao sasa wakataka kujua habari hizo kutoka kwa wanahabari "Jamani twambieni ni nini kinaendelea, maana tumeona mawakili wanatoka nje ya ukumbi wa mahakama bila kutuambia kilichotokea."

Mmoja wa mawakili wa utetezi alipoulizwa na wanahabari kuhusiana na hali hiyo alijibu "hata mimi sijui ninachosubiri hapa ni kuitwa mahakamani kuendelea na kesi, hayo unayoniuliza siyajui." Mwendesha Mashitaka wa Serikali Boniface Stanslaus alipoulizwa sababu ya kesi hiyo kutoendelea jana naye alijibu. "Mimi sio msemaji wa suala hilo, ila niko hapa nasubiri tuitwe mahakamani."

Mmoja wa ndugu wa Yona alipoulizwa kama mahakama iliwataarifu kinachoendelea naye alijibu "kwa kweli ndugu yangu na sisi tumebaki tunashangaa, hatujui kinachoendelea hapa mahakamani." Baadaye waandishi wa habari walimfuata Hakimu Mwankenja kupata ufafanuzi wa suala hilo, ndipo alipotoa ufafanuzi wa namna taratibu zilivyokiukwa.

Kutokana na msimamo huo wa Hakimu Mwankenja, washitakiwa waliondolewa eneo la Mahakama ya Kisutu saa 7.10 na basi la Magereza lenye namba za usajili STK 4373 huku wakisindikizwa na magari mengine manne. Walionekana watu wasio na furaha, tofauti na siku zingine wakati wanaondolewa katika eneo hilo la mahakama. Katika basi hilo walipanda pamoja na washitakiwa wengine.

Kabla ya tukio hilo la kesi yao kutosikilizwa jana, washitakiwa hao mara tu baada ya kufikishwa mahakamani hapo saa mbili asubuhi, waliondolewa katika eneo hilo la mahakama na kupelekwa Mahakama Kuu. Baadaye tena saa tatu walirudishwa Kisutu na kufikishiwa rumande kusubiri taratibu zao za kupata dhamana.

Asubuhi Hakimu Mwankenja alipoulizwa kama alikuwa na taarifa za washitakiwa hao kupelekwa mahakamani hapo alijibu "Hapa nilipo sijapata jalada kutoka Mahakama Kuu, tusubiri tuone kitakachokuja kimeandikwa kwenye jalada hilo." Ila alisisitiza kuwa yeye hakuwa ametoa hati ya kuwapeleka Kisutu, ila yuko tayari kuendelea na shauri hilo kama jalada litakuwa na amri ya Mahakama Kuu ya kumtaka aendelee kulisikiliza shauri hilo kwa siku ya jana.

Mramba na Yona wanashitakiwa kwa makosa 13 ambayo ni kuipendelea kampuni ya Alex Stewart kwa kuipa mkataba bila kufuata sheria za ununuzi na kuisamehe kodi hivyo kuisababishia serikali hasara ya Sh bilioni 11.7. Mramba katika kesi hiyo anaguswa na mashitaka yote 13 wakati Yona anagushwa na mashitaka sita. Mashitaka yanayomgusa Yona ni yale ya kushiriki kuipendelea kampuni ya Alex Stewart kwa kuipa nyongeza ya mkataba.

Lakini pia Waziri huyo wa zamani wa nishati na madini anatuhumiwa kuipendelea kampuni hiyo na kuiachia suala la ukaguzi wa hesabu za kampuni zinazochimba madini nchini kufanywa kiholela na kampuni hiyo bila kuishirikisha ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali. Kutokana na kutokuwa makini Yona anahusishwa kuchangia kuisababishia hasara ya Sh bilioni 11.7 Serikali ya Tanzania. Mramba licha ya kuguswa na mashitaka hayo; lakini pia anatuhumiwa kutoa misamaha mbalimbali ya kodi kwa kampuni ya Alex Stewart na kusababisha hasara hiyo ya Sh bilioni 11.7.
 
Mkuu kwa hili tupo pamoja kwani ukiangalia Hakimu alikosea hata kupiga hesabu za dhamana, na aka demand cash instead of immovable asset of that value
Bodo tuu kesi immenda kwake tena
Mbona wale mafisadi walikuwa wanaend mahakamani pindi wanapokamilisha masharti ya dhamana
Huyu hakimu lazima atakuwa fisadi

Hakimu Mwankenja anajua hasa uhakimu mtu huwezi kuiba hela Cash halafu dhamana unaweka jengo la kufugia kuku.Umeiba cash lete thamana cash zetu.Wallahi washtakiwa walioweka dhamana majengo badala ya kuleta cash wakitoroka halafu hayo majengo yakashindwa kuuzika kulingana na hiyo Cash waliyokwiba mimi naapa nitararua joho la jaji aliyepingana na uamuzi wa hakimu Mwankenja.

Huyu mama ni mtetezi wa pesa za umma zilizopotea.Dhamana ya washtakiwa waliolikosesha taifa pesa kudhaminiwa kwa majengo sikubaliani nalo kabisa.Kazi ya sheria na jaji iwe ni kuokoa hela la umma zilizopotea lakini kama kazi yake ni kuvaa joho na kupoteza hela za umma hapo lazima vita ihamie kwao kama likitokea tatizo.

Wameiba cash lazima dhamana iwe cash.Mama Mwankeja I salute you for your decision.

Mama pia kuwatimua jana alikuwa sahihi.Mawakili na watu wa magereza ilibidi wajue taratibu za sheria kama mama Mwankenja badala ya kukurupuka tu na ving`ora kama wehu kuwapeleka kisutu.Ona sasa wamepoteza mafuta ya umma bure kwa kulitia hasara jeshi la magereza kwa kesi ambayo haisikilizwi.
 
..mramba na yona wametumia madaraka vibaya....na kusababisha hasara..tatizo hapa mashtaka hayajaweka wazi kuiba..,tofauti na kina JEETU patel ambao wameiba live,.....imekuwaje wale wa EPA wamekubaliwa kuweka bond hadi mali zisizoamishika...na kwa hawa kuinakuwa na kigugumizi.....

thats why pamoja na uamuzi huu ambao utakuwa funzo kwa wanasiasa wetu....nachelea kusema pia ndani ya hii kesi kuna hidden agenda vile vile..ningependa kusubiri hadi mwisho...nione.Lakini labda tutahadharishe tu kuwa kama kuna nguvu ya ziada inatumika chini kwa chini ..iachwe kwani ita jeopedise ..good will ya president...katika hii vita!!..,mwisho itasababisha sympethisers kuona kama kuna kukomoana kwenye hii kesi...

na pia la muhimu rais tunamtegemea sana kwenye kuwashughulikia waliotutia hasara ya RICHMOND...kwani ushahidi wake ni wa moto zaidi na wa kuaminika .....
 
Yule mke wa fisadi mashuhuri mh yona aliekuwa keko amezirai jana gafla baada ya kuaandaa shampeni na viburudisho kibao kufurahia kurudi kwa mumewe
habari kamili mama alipata taarifa mbofumbofu mzee anaweza shuka muda wowote leo na kuachiwa mama ndipo alipojipanga haswaa kumrudisha darling kundini!!!gafla alipoambiwa hawatolewi ndipo mama alipoonyesha kwamba kweli kammiss mavituz ya mzee kupita kiasi na kuanguka gafla!!!!polen sana hata sisi f twamtakia atoke leo!!!!ila mramba aendelee kujifua huko mpaka mwanae atakapozalishwa!!!!kwapicha za harusi ya mramba sa hapo chini
 
aliemponza mwenzake mramba alipeleka hati ya nyumba kumbe ina bond kama bank 2!!1wakaishtukia mahakamani!!!pole mzee wetu
 
Katika kile kinachoonekana mchakato mbovu kabisa wa upatikanaji haki watuhumiwa wa kesi za Jinai ambao waliwahi kuwa Mawaziri wa Muungano Bw. Basil Mramba na Bw. Daniel Yona wamerudishwa rumande leo baada ya Hakimu anayesikiliza kesi yao Bw. Hezron Mwankenja kukataa kuwaona kwani hakuwa ameipanga kesi hiyo leo na hakukuwa na agizo lolote la kuwatoa huko rumande kuwaleta mahakamani. "Kwanza wametokaje mahubusu kuja hapa bila ya 'removal order'?" alihoji Bw. Mwankenja.
Katika kesi yao ya msingi watuhumiwa hao ambao wanadaiwa kulisabababishia taifa hasara ya karibu bilioni 11 kutokana na uzembe na matumizi mabaya ya ofisi zao walinyimwa dhamana kesi hiyo ilipotajwa mara ya kwanza. Jaribio lao la kukata rufaa siku ya Ijumaa iliyopita liligonga mwamba na taarifa zote za awali siku hiyo zilisema kuwa uamuzi kuhusu rufaa yao utakamilika baada ya kukamilika kwa uhakiki wa hati za kumiliki nyumba (title deeds) ambako kulitakiwa kukamilishwa asubuhi ya leo huko Kisutu. Uamuzi huo ulitolewa na Jaji Mwaikugile wa Mahakama Kuu.

Hivyo maamuzi kuhusu dhamana yao yaweza kutolewa na kukamilishwa kesho wakati wa kutajwa tena kwa kesi yao ya msingi.
 
Yule mke wa fisadi mashuhuri mh yona aliekuwa keko amezirai jana gafla baada ya kuaandaa shampeni na viburudisho kibao kufurahia kurudi kwa mumewe
habari kamili mama alipata taarifa mbofumbofu mzee anaweza shuka muda wowote leo na kuachiwa mama ndipo alipojipanga haswaa kumrudisha darling kundini!!!gafla alipoambiwa hawatolewi ndipo mama alipoonyesha kwamba kweli kammiss mavituz ya mzee kupita kiasi na kuanguka gafla!!!!polen sana hata sisi f twamtakia atoke leo!!!!ila


2994-mke-wa-fisadi-yona-azirai-1-mramba.jpg


Maisha kweli sio lelemama...
 
Kweli nimeamini na wanadamu ni mashaidi kwa unayoyafanya ama yawe mazuri ama mabaya na pia ukifanya mabaya kelele za wanadamu zinatosha kukuadhiri na pengine hapa nduniani, Nikikumbuka usemi huu huwa machozi yanakaribia kudondoka "Hata mkila majani ................ Itanunuliwa" Je Nikweli usemi huu ulisemwa na kiongozi wa umma ama mtawala wa umma.Na haya ni malipo ya usemi huu.
 
Back
Top Bottom