Yanga imetoa funzo kubwa kwa Simba na wengineo. Italiandika tena kwenye msimu ujao wa Klabu Bingwa?

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Dec 27, 2012
10,197
25,517
Mwanzo mwanzoni nitamke wazi kuwa mimi ni mshabiki wa Yanga tangu utoto wangu. Lakini, kila ninapotazama mechi ya mpira(nilianza kufuatilia tangu miaka ya 90), huwa nauweka ushabiki wangu pembeni.

Daima huwa naitazama mechi kiufundi na kunasa cha kuondoka nacho, achilia mbali matokeo. Huwa naondoka na hali ya maandalizi; mbinu za benchi la ufundi; uwezo wa wachezaji; figisu zitokeazo na kadhalika. Kinapofanyika kila kitu na timu kukosa matokeo mazuri huwa naumia lakini nafarijika.

Yanga imetoa somo la kuwa matokeo ya soka yanaweza kupatikana popote-nyumbani au ugenini. Msimu huu wa Kombe la Shirikisho Afrika Yanga imesare, imeshinda na kushindwa nyumbani na ugenini. Lakini, rekodi yake ya kushinda ugenini imetamalaki.

Yanga imeshinda kwenye viwanja vigumu kupata matokeo. Ilishinda kwa Rivers ambako Wydad alipotea. Ikashinda kwa Marumo ambako Pyramids aliuwawa; ikashinda kwa USMA ambako hata sare kabla ya jana haikutoka. Nimeacha pale Lubumbashi kwa Mazembe makusudi.

Yanga imetoa somo na kutuma ujumbe kwa wapinzani wajao wa michuano ya CAF. Kuwa hakuna cha nyumbani wala ugenini watakapokutana na Yanga. Simba wajifunze. Wafike mbali zaidi na zaidi.

Najua na nakiri kuwa rekodi ya Simba kwenye Klabu Bingwa Afrika ni kubwa kuliko ya Yanga. Ila wanapaswa kuvuka robo fainali kwa somo la Yanga. Waachane na kufukua mambo bishani ya 1974 na mengineyo. La kweli ni la fainali ya CAF mwaka 1993 na walizabwa 2 kwa 0 Uwanja wa Uhuru baada ya sare ya kule Abidjan. Wakaponzwa na uwanja wa nyumbani.

Pamoja na figisu za jana za USMA, Yanga wakalipa kisasi cha kufungwa nyumbani. Uongozi wa CAF ulikuwepo na kuona ukali wa Yanga. Waarabu wanakuwa wanaiogopa Yanga popote watakapokutana nayo.

Wachambuzi walichambua na kutisha kwa rekodi za nyumbani za wapinzani wa Yanga kila mechi. Yanga proved them wrong. Mpira hauna nyumbani wala ugenini. Ni kiwango na maandalizi tu. Faraja yetu ni kuwa tumemaliza mashindano ya Afroka kwa ushindi. Na tumekuwa Makamu Bingwa wa Shirikisho tukitoa Mfungaji bora na Golikipa bora wa mashindano hayo. Tukutane msimu ujao wa michuano ya CAF!
 
Mwanzo mwanzoni nitamke wazi kuwa mimi ni mshabiki wa Yanga tangu utoto wangu. Lakini, kila ninapotazama mechi ya mpira(nilianza kufuatilia tangu miaka ya 90), huwa nauweka ushabiki wangu pembeni.

Daima huwa naitazama mechi kiufundi na kunasa cha kuondoka nacho, achilia mbali matokeo. Huwa naondoka na hali ya maandalizi; mbinu za benchi la ufundi; uwezo wa wachezaji; figisu zitokeazo na kadhalika. Kinapofanyika kila kitu na timu kukosa matokeo mazuri huwa naumia lakini nafarijika.

Yanga imetoa somo la kuwa matokeo ya soka yanaweza kupatikana popote-nyumbani au ugenini. Msimu huu wa Kombe la Shirikisho Afrika Yanga imesare, imeshinda na kushindwa nyumbani na ugenini. Lakini, rekodi yake ya kushinda ugenini imetamalaki.

Yanga imeshinda kwenye viwanja vigumu kupata matokeo. Ilishinda kwa Rivers ambako Wydad alipotea. Ikashinda kwa Marumo ambako Pyramids aliuwawa; ikashinda kwa USMA ambako hata sare kabla ya jana haikutoka. Nimeacha pale Lubumbashi kwa Mazembe makusudi.

Yanga imetoa somo na kutuma ujumbe kwa wapinzani wajao wa michuano ya CAF. Kuwa hakuna cha nyumbani wala ugenini watakapokutana na Yanga. Simba wajifunze. Wafike mbali zaidi na zaidi.

Najua na nakiri kuwa rekodi ya Simba kwenye Klabu Bingwa Afrika ni kubwa kuliko ya Yanga. Ila wanapaswa kuvuka robo fainali kwa somo la Yanga. Waachane na kufukua mambo bishani ya 1974 na mengineyo. La kweli ni la fainali ya CAF mwaka 1993 na walizabwa 2 kwa 0 Uwanja wa Uhuru baada ya sare ya kule Abidjan. Wakaponzwa na uwanja wa nyumbani.

Pamoja na figisu za jana za USMA, Yanga wakalipa kisasi cha kufungwa nyumbani. Uongozi wa CAF ulikuwepo na kuona ukali wa Yanga. Waarabu wanakuwa wanaiogopa Yanga popote watakapokutana nayo.

Wachambuzi walichambua na kutisha kwa rekodi za nyumbani za wapinzani wa Yanga kila mechi. Yanga proved them wrong. Mpira hauna nyumbani wala ugenini. Ni kiwango na maandalizi tu. Faraja yetu ni kuwa tumemaliza mashindano ya Afroka kwa ushindi. Na tumekuwa Makamu Bingwa wa Shirikisho tukitoa Mfungaji bora na Golikipa bora wa mashindano hayo. Tukutane msimu ujao wa michuano ya CAF!
usisahau kilichowaponza yanga(kukosa kombe la CAF confederation) ni kufungwa mechi ya nyumbani.

NB: medali bila kombe ni kama shanga tu.

Sent from my TECNO BA2 using JamiiForums mobile app
 
"Makamu Bingwa wa Shirikisho" Hii mpya hii ila sishangai kuisikia kutoka kwa Mwanayanga.
Tuwasamehe bure tu
FB_IMG_1682646137959.jpg
FB_IMG_1682646171032.jpg
 
Somo kubwa Simba wanalotakiwa kujifunza ni kuwa making kuanzia kuchagua viongozi na katiba ambayo haimfanyi mtu mmoja kuwa na maamuzi ya mwisho.
Yanga mpaka wamefika hapa waliiga na kujifunza vitu vingi Toka kwa Simba walichukua mazuri ya Simba na kuyaboresha.Simba ndio ilianza kuajili CEO wao wakamchukua, wakati Simba inaajili CEO wa kwanza ilifanya mchakato wa wazi lakini CEO aliyefuata hakupitia mchakato wowote na ndie aliyechangia Simba kutoendelea pale alipoikuta kwani yeye alijikita kubana matumizi na kujitangaza binafsi. Hata CEO wa kwanza hakufanya makubwa kwani alipoikuta Simba ndipo alipoiacha ila uwepo wa watu kama marehemu Hanspope ulichangia pakubwa.
Bada ya Simba kutolewa na Ud Songo kocha alifukuzwa haraka bila kutafakari kwanini tulitolewa na kosa hilohilo lilijurudia pale tulipotolewa na timu ya Botswana likafukuzwa karibia benchi lite ikiwamo kocha wa makipa ambaye ni kama tuliwapa yanga, kocha wa viungo bila kujali kama alihusika au la.
Ni aibu timu kama Simba kucheza nusu msimu bila kuwa na kocha wa viungo Wala makipa Lisa kubana matumizi.
Timu ya Simba ni nzuri wasikurupuke kuacha wachezaji wengi pia waepuke kujaza wachezaji wengi wa nafasi Moja
 
1. Kaka ungepangilia hoja zako hata kwa namba tuhesabu hayo masomo.

2. MPIRA una MATOKEO Matatu
Kushinda, kupata SARE, Kufungwa.
Unaposema matokeo tukueleweje?????..

3. Ukasisktiza mpira hauna nyumbani Wala UGENINI unachezwa popote.

4.Kumbuka timu nyingi zilizocheza kombe la shirikisho nyingine zimeshukala Daraja, nyingine ni ngeni kwenye mashindano ya kimataifa,
USMA walikuwa nafasi ya Tisa Hadi Jana.

YANGA imefungwa na Timu inashika nafasi ya Tisa. 9 ALGERIA.


TUSUBIRI MSIMU UJAO KAMA HAO YANGA WATAFURUKUTA UPANDE WA WANAUME CAFCL.

TUJIFUNZE KUFICHA UJINGA.
 
Mwanzo mwanzoni nitamke wazi kuwa mimi ni mshabiki wa Yanga tangu utoto wangu. Lakini, kila ninapotazama mechi ya mpira(nilianza kufuatilia tangu miaka ya 90), huwa nauweka ushabiki wangu pembeni.

Daima huwa naitazama mechi kiufundi na kunasa cha kuondoka nacho, achilia mbali matokeo. Huwa naondoka na hali ya maandalizi; mbinu za benchi la ufundi; uwezo wa wachezaji; figisu zitokeazo na kadhalika. Kinapofanyika kila kitu na timu kukosa matokeo mazuri huwa naumia lakini nafarijika.

Yanga imetoa somo la kuwa matokeo ya soka yanaweza kupatikana popote-nyumbani au ugenini. Msimu huu wa Kombe la Shirikisho Afrika Yanga imesare, imeshinda na kushindwa nyumbani na ugenini. Lakini, rekodi yake ya kushinda ugenini imetamalaki.

Yanga imeshinda kwenye viwanja vigumu kupata matokeo. Ilishinda kwa Rivers ambako Wydad alipotea. Ikashinda kwa Marumo ambako Pyramids aliuwawa; ikashinda kwa USMA ambako hata sare kabla ya jana haikutoka. Nimeacha pale Lubumbashi kwa Mazembe makusudi.

Yanga imetoa somo na kutuma ujumbe kwa wapinzani wajao wa michuano ya CAF. Kuwa hakuna cha nyumbani wala ugenini watakapokutana na Yanga. Simba wajifunze. Wafike mbali zaidi na zaidi.

Najua na nakiri kuwa rekodi ya Simba kwenye Klabu Bingwa Afrika ni kubwa kuliko ya Yanga. Ila wanapaswa kuvuka robo fainali kwa somo la Yanga. Waachane na kufukua mambo bishani ya 1974 na mengineyo. La kweli ni la fainali ya CAF mwaka 1993 na walizabwa 2 kwa 0 Uwanja wa Uhuru baada ya sare ya kule Abidjan. Wakaponzwa na uwanja wa nyumbani.

Pamoja na figisu za jana za USMA, Yanga wakalipa kisasi cha kufungwa nyumbani. Uongozi wa CAF ulikuwepo na kuona ukali wa Yanga. Waarabu wanakuwa wanaiogopa Yanga popote watakapokutana nayo.

Wachambuzi walichambua na kutisha kwa rekodi za nyumbani za wapinzani wa Yanga kila mechi. Yanga proved them wrong. Mpira hauna nyumbani wala ugenini. Ni kiwango na maandalizi tu. Faraja yetu ni kuwa tumemaliza mashindano ya Afroka kwa ushindi. Na tumekuwa Makamu Bingwa wa Shirikisho tukitoa Mfungaji bora na Golikipa bora wa mashindano hayo. Tukutane msimu ujao wa michuano ya CAF!
Soka haliendi exponentially kuna uwezekana yanga mwaka ujao wa mashindano akaishia kwenye round zile za qualification. Sababu kubwa ni wachezaji wao wengi kufikia kwenye hatua ya kurudi nyuma kiufanisi na umri kuwatupa mkono. Sababu nyingine ni uwezo mdogo wa kocha wao - profesa wa mchongo, ndugu nabi na yule mrundi
 
1. Kaka ungepangilia hoja zako hata kwa namba tuhesabu hayo masomo.

2. MPIRA una MATOKEO Matatu
Kushinda, kupata SARE, Kufungwa.
Unaposema matokeo tukueleweje?????..

3. Ukasisktiza mpira hauna nyumbani Wala UGENINI unachezwa popote.

4.Kumbuka timu nyingi zilizocheza kombe la shirikisho nyingine zimeshukala Daraja, nyingine ni ngeni kwenye mashindano ya kimataifa,
USMA walikuwa nafasi ya Tisa Hadi Jana.

YANGA imefungwa na Timu inashika nafasi ya Tisa. 9 ALGERIA.


TUSUBIRI MSIMU UJAO KAMA HAO YANGA WATAFURUKUTA UPANDE WA WANAUME CAFCL.

TUJIFUNZE KUFICHA UJINGA.
Mkùu, naamini wewe ni mfuatiliaji mzuri wa mpira. Ligi za nchi hazina maana yoyote kwenye mashindano ya vilabu katika bara husika.

Liverpool na Chelsea waliwahi kutwaa UCL wakiwa nje ya nne bora. Juzi tu Sevilla ametwaa Europa akiwa nje ya 10 bora ya La Liga. Kushuka kwa Marumo na nafasi ya USMA si kigezo cha kuiona Yanga haikufanya lolote.

Marumo alimfunga Pyramids anayeshika nafasi ya pili kwenye ligi, bora kuliko yetu,ya Misri. Tena, Marumo aliongoza kundi alimokuwamo Bingwa wa Shirikisho.

Raja Casablanca aliyempiga Simba nje ndani Klabu Bingwa, mwakani hatashiriki michuano hiyo. Na anaweza asishiriki hata Shirikisho kulingana na nafasi yake.

Yanga wamefanya makubwa na lazima mkubali. Ukweli wa kisoka hautaki ushabiki...
 
Back
Top Bottom