Petro E. Mselewa
JF-Expert Member
- Dec 27, 2012
- 10,197
- 25,517
Kwa kiwango na uchezaji wa Simba hii, hakika michuano hii ingedharaulika na kutofuatiliwa. Simba imechoka na haina hata uwezo wa kupiga pasi tano.
Simba wamekuwa wakijipambanua kuwa wao ndiyo wacheza-klabu Bingwa Afrika. Wamekuwa wakiwabeza na kuwatweza Yanga kuwa michuano hiyo hawaiwezi na si level yao.
Kuanzia mechi ya Asec, Galaxy na hata ya jana ya Wydad, Simba wamekuwa na lengo moja tu: kuzuia kufungwa. Ni kuzuia tu mwanzo mwisho. Back-passes na kubutua kukatamalaki.
Wachezaji wako hoi na hawana maarifa yoyote. Yaani wenye viwango vya mashindano wawe na goli moja la penati katika mechi tatu!?
Haya sasa, Simba nao wanashika mkia kwenye kundi lao. Simba mjifunze kubakisha maneno. Na bahati mbaya iliyopo ni kuwa Wydad ndiyo kwanza wameanza kukusanya alama kwao.
Simba wamekuwa wakijipambanua kuwa wao ndiyo wacheza-klabu Bingwa Afrika. Wamekuwa wakiwabeza na kuwatweza Yanga kuwa michuano hiyo hawaiwezi na si level yao.
Kuanzia mechi ya Asec, Galaxy na hata ya jana ya Wydad, Simba wamekuwa na lengo moja tu: kuzuia kufungwa. Ni kuzuia tu mwanzo mwisho. Back-passes na kubutua kukatamalaki.
Wachezaji wako hoi na hawana maarifa yoyote. Yaani wenye viwango vya mashindano wawe na goli moja la penati katika mechi tatu!?
Haya sasa, Simba nao wanashika mkia kwenye kundi lao. Simba mjifunze kubakisha maneno. Na bahati mbaya iliyopo ni kuwa Wydad ndiyo kwanza wameanza kukusanya alama kwao.