Mkuu wangu na ndugu yangu kipenzi
Ngongoseke kiukweli hamu ya mabidiliko kwa vijana wengi ni kubwa sana hasa ukizingatia wakati kama huu nchi hii imezidi kuzama katika kila aina ya unyonyaji kwa wananchi wake lakini hawa tunaowaita wanamabadiliko wenyewe wapohoi bin taabani aka wasakatonge walilokosa tonge hilo kutoka CCM au wanaosaka chanci ya kuwapiga watz kama watawala wanavyofanya. Kwa mtindo huu tutake tusitake bado sana mpaka kuja kuwang'oa CCM.
Nimekuwapo hivi karibuni maeneo ya kusini mwa nchi hii ambako angalau kwamba CUF inapigapiga kelele lakini nimeshuhudia maisha ya watu huko niya mashaka sana na wengi wao wanachagua viongozi hasa kutokana na kidogo kitu wanachopata.
Safari ni ndefu sana ukizingatia waendeshaji wenyewe wa harakati hizi si wamoja.