hivi ndugu huamini CCM inaweza kuanguka? Rais Mkapa aliacha misingi mizuri sana ya uchumi wa nchi. Professor Kikwete ameivunja yote. Leo hii tunavyoongea shilingi ya tanzania imeporomoka Kwa mujibu wa tovuti ya Benki kuu ya Tanzania dola moja ni shilingi 1718. Hii ni mbaya sana kwa uchumi wa nchi. Ufisadi unaofumbiwa macho umesababisha wahisani kuzuia dola 449 million na majuzi tu Serikali ya marekani imetangaza ku freeze msaada wa MCC takribani dola million 700....Professor kikwete alijipambanua sana kutegemea wahisani badala ya kujenga misingi ya kujitegemea kwenye bajeti. Leo hii ni vigumu kwa serikali kufanya matumizi ya kila siku...inalazimika kutumia ubabe kukopa kwenye mabenki ya ndani ili kulipa mishahara na matumizi mengine. Haya yote yanatokana na misingi mibovu na utawala mbovu wa Professor Kikwete. Kuna siku aliwahi kwenda kufanyiwa check up New York halaf siku anarudi wasaidizi waka wakamshauri aende kutembelea wagonjwa muhimbili. Haya yote wananchi wanayaona na kwa kuwa technolojia ya habari imekua watu hawadanganyiki tena! David kafulia aliinuka bungeni na kusema serikali ya marekani imesitisha msaada, waziri wa fedha bila chembe ya aibu anainuka na hijabu yake kusema si kweli...leo hii balozi wa marekani anathibitisha...Katibu mkuu kiongozi anasema ni jambo la kawaida duniani kote......hakika Professor Kikwete ameiharibu kabisa nchi hii.......