Yaliyojiri katika Uchaguzi Serikali za Mitaa - Dec 14, 2014

Yaliyojiri katika Uchaguzi Serikali za Mitaa - Dec 14, 2014

Attachments

  • 1418558162171.jpg
    1418558162171.jpg
    50.3 KB · Views: 306
Migombani hapa Segerea kuna rapsha muda huu wanataka kuahirisha uchaguzi.Vijana hawataki
 
Kata ya madunga wilayani Babari, kijiji cha gidng'ata. Kuna wagombea wameondolewa wananchi wamekomaa hadi magari ya ffu kujazana pale
 
Mburura walipewa semina kujiangamiza wenyewe.Mjinga huwa anafikiria hapo alipo ni sawa na kuku akipoteza kifaranga chake hakumbuki.
 
Taarifa kutoka kwa Mwangalizi wetu Mr. Abuu Abdalah aliyeko Nzega anaripoti: Ndala kijiji cha Buhemeli hadi sasa bado hawajapiga kura na wala hawajaambiwa chochote.


Taarifa kutoka kwa Mwangalizi wetu Ms.Grace Mwangamila kutoka Mbeya, kata ya Iwambi anaripoti: Zoezi linaenda taratibu sana, majina yameandikwa na peni hayaonekani imelazimu wasimamizi kuita majina zoezi linachelewa. wanawake wamesubiri sana wameamua kukaa chini.
10685527_315218802005427_9080997790397668253_n.jpg

Chanzo:LHRC‬
 
Kongowe nimekuta wanajeshi 2 na migambo 6 kwenye kituo cha kupigia kura
 
Wakuu, leo, Disemba 14, 2014 Watanzania wanapiga kura kuchagua viongozi wao wa Serikali za Mitaa, Tanzania Bara (Tanganyika).

Viongozi wanaochaguliwa leo ni katika nafasi za Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa, Wenyeviti wa Vitongoji, Wajumbe 6 wa Serikali ya Mtaa (Halmashauri) na wajumbe wa Viti Maalum wa Mtaa/Kijiji.

Kama ilivyo ada JamiiForums itakuwa ikikujuza yanayojiri, katika uzi huu utapata/utaleta updates zinazohusiana na uchaguzi huu.

Karibuni sana

========
UPDATES MUHIMU:

attachment.php

attachment.php

Hapa ni Mtaa wa Kijitonyama
- Eneo la Shariff Shamba, Ilala jijini Dar uchaguzi umeahirishwa mpaka Jumapili ijayo baada ya vifaa kutopatikana ndani ya muda. Vyama vyote vinavyoshiriki vimeafikiana


- Mgombea wa CHADEMA Kijiji cha Darajani huko Liwale, M. Manakwa amepigwa na watu wasiojulikana usiku wa kuamkia leo, amelazwa hospitali



-Mkuu wa Wilaya ya Kilindi mkoani Tanga, Suleiman Liwowa ametangaza kuwa katika vitongoji 613 vya Wilaya hiyo vyama vya Upinzani vimeshindwa kusimamisha wagombea.



wilaya Mkinga uchaguzi, haukufanyika kwa sababu fomu za kura zimewachanganya wagombea
 
Leo uchaguzi wa serikali za mitaa slaa yupo karatu na mbowe yupo ujerumani wote hao hawapigi kura alafu wana taka chadema ishinde kila siku mtabaki na ngonjera kuwa ccm imewaibia kura

Tupo Makamanda na tumepiga kura,hizo porojo zako peleka lumumba!
 
Mbona KIKWETE na yeye hapigi kura hilo haulizungumzii? kwani wakati uandikishaji unafanyika alikuwa kwenye TEZI DUME

Watu wanajiandikisha Kikwete alikuwa matibabu. Ndio maana hata kampen kafanya mke wake tu!
 
namshukuru YESU KRISTO nimepiga kura yangu salama. Wasimamizi wana lugha ya hovyo sana
 
vifaa vinafichwa kwanza karibu na vituo ili kuona hari ikoje then ikionekana watu wameondoka wanapigiana simu vifaa vinaletwa waliopo wachache wanapiga alafu mda unaisha fasta wanafunga ..kwahyo msiondoke vituoni
 
Mkuu kwenye post zako za kuku nakufuatilia sana. Nimeleta kuchi 20 na wote wako vizuri. Napenda pia harakati zako za ukombozi. Safi Sana kamanda

Asante mkuu! Mie saa hizi nasomeka 100 hahahah
 
Nimetoka kula pilau yangu hapa Magomeni Butiama mara naona timbwili katika kituo cha kupigia kura pale. Nikachukua video clip faster nikasepa zangu wasije nikwapulia simu. Nimeshindwa ku-upload hizi clips kutoka kwenye simu
 
wakuu hawa ukawa wametubana sana hata vile vi tiktak vyetu wana viotea siamini kitaeleweka tu jioni wakichoka doria au mnaonaje wakuu
 
Back
Top Bottom