Creative Hub
Member
- Dec 2, 2019
- 89
- 98
Sisi tunasubiri tuwaone tukipita hapo
Polis nao ni Tawi la CCM ,wanaogopa mpaka Bendera。
Na Mwanza na Dodoma je?Jana CCM tulikua na uchaguzi kwenye ukumbi wa mikutano wa AICC-Arusha.
Hatukuweka bendera hata moja njiani ila kulikua na wanachama wenye sare pekee.
Cecil Mwambe ni damu mbichi japo wahenga wanasema mpini mpya husababisha machacha na njia mpya haikosi visiki na miiba.
Freeman Mbowe ni damu ya mzee japo wahenga wanasema uzee si busara na ukiona nyani mzee ujue amekwepa mishale mingi.
Wakati tunasubiri matokeo rasmi, unadhani kwa siasa za awamu ya tano, nani anafaa kupeperusha bendera ya uenyekiti wa chama kikuu cha upinzani?
Wasije wakavamia mkutano wakasema ati hauna kibali na pia kuna harufu ya uvunjifu wa amani.
kweli maajabu ya karne, yaani bendera nayo inaogopwa!!Tanzania ya mauzauza Bendera zinatisha wenye mamulaka Maajabu ya chattels haya Sisi Kama Chadema tunasema Mbowe mi 5 tena Mwamba Tuvushe
Pamoja na mapungufu yake ila Mzee Kikwete ni Mkweli.. na ukweli unakuweka HURU. CCM bila Jeshi la Police ni walaini kama karatasi iliyonyeshewa mvua.
Hakuna mtu wa kumtoa Mbowe kwenye kiti anachotaka na baada ya Uchaguzi kumalizika, Mwambe atafukuzwa ndani ya CHADEMA!
Yaliyomkuta Zitto mwaka 2014 yanaenda kumpata Cecil Mwambe! Baada ya Uchaguzi wa ndani aanze kutafuta chama kingine mapema!
Pamoja na mapungufu yake ila Mzee Kikwete ni Mkweli.. na ukweli unakuweka HURU. CCM bila Jeshi la Police ni walaini kama karatasi iliyonyeshewa mvua.
Hivi CCM wanapochagua mwenyekiti wao Viongozi wa dini yanakuwapo? Naomba wa kunijuzaHapo msajili wa vyama vya siasa hawezi kutia neno. Anasubiri wafuasi wakatae uonevu ili atoe barua ya onyo kwa chadema. Viongozi wa dini nao wanashihudia kinachoendelea lkn wako kimya. Ngoja tusubiri kuona dini na madhehebu yake watatuma wawakilishi wa aina gani maana siku hizi nao wameshaunga juhudi.
Huku sisi tulishavuka waendelee kusubiri kuona kaburi la chadema kama wasira anavyo subiri kuonas kama alivyo sema miaka hiyo kuwa chadema itakufa matokeo yake kafa yeye..Kwa maelezo yako bango namba 4 wewe hutaki Mbowe aendelee,halafu inasema kuweni makini,na kutoa rai ya kuchagua mtu anaeweza kushinda hila za CCM wenzio,si munataka upinzani ufe ndiyo maana munalipigia debe pandikizi?inawauma nini Chadema ikifa wakati ndiyo kusudio lenu?Tunampigia Mbowe(MWAMBA)ili atuvushe kwenye mto wa hila zenu za mapandikizi.
Sent using Jamii Forums mobile app