Eng. Zezudu
JF-Expert Member
- Aug 23, 2012
- 7,813
- 10,831
Kwa Nini makaratasi yanachanwa na kuunganishwa
Haa Mawakili wa Mbowe"wamesomea" kazi yao, Mtobesya yuko smart! Jaji anaongozwa na Mtobesya!!Jaji: Mmeniacha Kidogo Mlinzi kuwa mnazungumzia Prison Inspection hapa naona unazungumzia Prison Visit
Mtobesya: Kwenye PGO hawana Inspection Wanaita Prison Visit
Jaji: Ok Sawa!
USHAHIDI WA UGAIDI BADO HATUUONI, Kinachoonekana ni taratibu za ukamataji, kusafiri toka Moshi hadi Dar, kunywa supu na MO energy, kuwekana mahabusu....Sasa ushahidi wa ugaidi tutaelezwa saa ngapi ili tujue?Mimi bado sielewi kitu, mbona naona kama madhahidi wa mashitaka ushahidi wao unafanana (kamata, kula, safirisha, weka ndani, andika) tofauti ni mashahidi, nini kinatafutwa maana sioni kutegwa kwa makombora, mabomu na mahandaki.
Yaan mawakili wa utetezi Wana kazi kweli kweli, wamuongeze Shahidi wamuongoze ma jaji pia.Haa Mawakili wa Mbowe"wamesomea" kazi yao, Mtobesya yuko smart! Jaji anaongozwa na Mtobesya!!
umeona eh!Yaan mawakili wa utetezi Wana kazi kweli kweli, wamuongeze Shahidi wamuongoze ma jaji pia.
Yaani tangu mlolongo wa kesi uanze sijaona shahidi hata mmoja aliyethibitisha namna ugaidi ungefanywaUSHAHIDI WA UGAIDI BADO HATUUONI, Kinachoonekana ni taratibu za ukamataji, kusafiri toka Moshi hadi Dar, kunywa supu na MO energy, kuwekana mahabusu....Sasa ushahidi wa ugaidi tutaelezwa saa ngapi ili tujue?
Endeleeni Kula Mtori nyama mtazikuta chini ya sufuria.USHAHIDI WA UGAIDI BADO HATUUONI, Kinachoonekana ni taratibu za ukamataji, kusafiri toka Moshi hadi Dar, kunywa supu na MO energy, kuwekana mahabusu....Sasa ushahidi wa ugaidi tutaelezwa saa ngapi ili tujue?
Nakubaliana na wewe maana hata Wajawazito kurudi shule wamekubali Leo ili waanze mwakani.kesi ya kinafki hii, hapo hamna kesi na leo itahairishwa.
Ni kwania ya kufikia mchakato wa katiba mpya ulopangwa kufanyika 2022, na sio 2021 kama mbowe alivotaka.
Kwahio hapo watamwachia mwisho wa mwaka huu au mwanzoni mwa mwaka 2022.
Bado unapikwa,ukiiva akina king'aa watapanda nao kwenye kizimba🤔.USHAHIDI WA UGAIDI BADO HATUUONI, Kinachoonekana ni taratibu za ukamataji, kusafiri toka Moshi hadi Dar, kunywa supu na MO energy, kuwekana mahabusu....Sasa ushahidi wa ugaidi tutaelezwa saa ngapi ili tujue?
mkuu mbona kama umejikoroga, kwahiyo na wewe ni mjamzito?Nakubaliana na wewe maana hata Wajawazito kurudi shule wamekubali Leo ili waanze mwakani.
Yaani mpaka wewe urudi ndio Boss ajue cha kufanyaLeo tarehe 24, Nov. 2021kesi ya ugaidi inayomkabili Mbowe na wenzake 3 inaendelea katika mahakama divisheni ya Uhujumu Uchumu na Rushwa ambapo leo Jamhuri italeta Shahidi Mwingine.
Kujua kesi ilipoishia, soma: Yaliyojiri katika kesi ya Freeman Mbowe - Novemba 23, 2021. Kesi yaahirishwa hadi Novemba 24, 2021
========
UPDATES:
Jaji naingia
Mahakamani Kesi namba 16/2021 Khalfani Bwire, Adam Kasekwa, Mohammed Ling'wenya na Freeman Mbowe inatajwa
Wakili wa Serikali: Robert Kidando anatambulisha Jopo la Mawakili wa Serikali
Pius Hilla
Abdallah Chavula
Jenitreza Kitali
Nassoro Katuga
Esther Martin
Tulimanywa Majige
Wakili Peter Kibatala anatambulisha Jopo la Mawakili wa Utetezi
Idd Msawanga
Nashon Nkungu
John Mallya
Fredrick Kihwelo
Dickson Matata
Jaji anaita Majina ya washtakiwa Wote wanne na wote wanaitika wapo.
Wakili wa Serikali: Ahsante Mheshimiwa Jaji, Shauri limekuja kwa ajili ya Kusikilizwa na Leo tuna shahidi Mwingine Mmoja na tupo tayari Kuendelea
Wakili Peter Kibatala: Na sisi kwa ruhusa yako pia Mheshimiwa Jaji tupo tayari kuendelea Jaji na atakuwa shahidi wa nne siyo?
Wakili wa Serikali: Ndiyo
Shahidi anaingia Moja kwa Moja Mahakamani, kijana amevaa kaunda suti..
Jaji: Majina yako
Shahidi: Inspector Lugawa ISSA Maulid
Jaji: Miaka
Shahidi: 42
Jaji: Kabila
Shahidi: Mluguru
Jaji: Dini Shahidi' Muislamu
Jaji: Thibitisha
Shahidi: Wallah wabillah watallah Nathibitisha Ushahidi nitakao toa Mbele ya Mahakama hii utakuwa ni Kweli, kweli tupu Eeh Mwenyezi Mungu Nisaidie
WS Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji nitamuongoza
Wakili wa Serikali: hebu rudia Majina yako
Shahidi: Naitwa Inspector Lugawa ISSA Maulid
Wakili wa Serikali: Unafanya Kazi gani
Shahidi: Ni Askari Polisi
Wakili wa Serikali: Kazi hizo za Uaskari Polisi unazifanyia Wapi?
Shahidi: Nazifanyia Kikosi cha Polisi Tazara Dar es Salaam
Wakili wa Serikali: Kikosi hiki kina husika na nini
Shahidi: Kinahusika na Usalama wa Mali zote zinazokuwa na Mamlaka ya Reli zinazomilikiwa na Mamlaka ya Reli ya Tanzania na Zambia
Wakili wa Serikali: Ambazo ni Mali gani
Shahidi: Majengo ya Mamlaka Ya Tazara, Mabehewa ya Mizigo na Abiria, Vichwa Vya Treni Pamoja na Miundo Mbinu na Raia..
Wakili wa Serikali: Kingine?
Shahidi: Kuzuia Uhalifu utakaotokea Pale, Ndani ya Mamlaka Ya Tazara
Wakili wa Serikali: Unaposema ndani ya Mamlaka Ya Eneo la Tazara Unamaanisha nini?
Shahidi: tunahusika zaidi Tazara, uhalifu unaofanyika ndani ya Treni, kwa Abiria na Majengo ya Tazara, NJE ya pale hatuhusiki
Wakili wa Serikali: Sasa umesema Upo Kikosi cha Polisi Tazara, Je Kituo chako Cha kazi ni Kipi?
Shahidi: Kituo cha Polisi Tazara, Pugu Road Kinachopatikana Tazara, Wilaya ya Temeke
Wakili wa Serikali: Kinaitwaj?
Shahidi: Kituo cha Polisi Tazara Pugu Road
Wakili wa Serikali: Una nafasi gani pale Kituo cha Tazara Pugu road
Shahidi: Kwa sasa ni kaimu Mkuu wa Kituo
Wakili wa Serikali: Eneo la kazi unaofanyika kazi linaukubwa gani
Shahidi: Kuanzia Dar es Salaam Mpaka Kisaki, Kilomita 223 ndiyo ninalohudumu Mimi
Wakili wa Serikali: Sasa Ukiwa Kaimu, Elezea Mahakamani Nafasi ya kaimu Mkuu wa Kituo umepata lini
Shahidi: Nimekabidhiwa Majukumu hayo Kuanzia Tarehe 03 June 2021
Wakili wa Serikali: Majukumu yako sasa Kama kaimu Mkuu wa Kituo cha Polisi Tazara ni nini?
Shahidi: yamegawanyika Sehemu Kuu tano
1.kusimamia nidhamu ya Askari ninao waongoza 2.Kusimamia Mpango Kazi wa Kituo
3.kuhakikisha Askari Wameingia Kazini kwa wakati kwa Maeneo Husika waliyopangiwa Kufanya Doria Maeneo yote ya Tazara
4.kusimamia na Kuzi Linda Mali zote za Serikali Yakiwemo Majengo, Magari ya Serikali, Office furniture pamoja na Silaha na Mali zingine zote
5.Kushughulikia Malalamiko yote yanayo fikishwa Kituoni, Ikiwemo Kufungua Kesi, Kupeleleza, na Kufikisha Mahakamani Watuhumiwa
6.Kuwasimamia Mahabusu Wote waliopo Kituoni Kwa Wakati huo Kuhakikisha wapo Salama Kiafya, Wamepata huduma za Chakula...
Wakili wa Serikali: Katika Jukumu la Kusimamia Mahabusu, Nini haswa ambacho wewe Unafanya
Shahidi: Kwa Mujibu wa Utaratibu kama Mkuu wa Kituo, Nikifika Kituoni cha Kwanza Naanza Kukagua Mahabusu kisha napitia REPORT BOOK Kuangalia Kesi zilozofunguliwa Kisha Nachukua Kitabu cha Detention Register Kuangalia Watu waliopo Mahabusu
Baada ya Kuchukua Detention Register, lazima niongozane Na Askari 1 au 2 Kutoka hapo CRO kwenda Mahabusu Kama Kuna Watuhumiwa Wa Kike nakuwa na Askari 1 wa kike na Wa kiume Na Fungua Detention Register Naanza Kuita Jina Moja Moja Ambao Wanakuwa wamo katika Kitabu Kile
Wakili wa Serikali: SUBIRI KWANZA JAJI ANAANDIKA
Shahidi: Ni kisha muita namuhoji Kosa linalo Mkabili alitaka, namuhoji tarehe ya Kuingia, baada ya Kumuhoji naenda Kwa Mtuhumiwa wa Pili
Wakili wa Serikali: TWENDE TARATIBU JAJI ANAANDIKA
Wakili wa Serikali: Umesema Kusimamia Mahabusu Unafanya nini
Shahidi: Kuhakikisha Hali zao Ki-Afaya, Wamepata Chakula kwa Wakati, na Status zao Kwa Ujumla
Wakili wa Serikali: Dhumuni ni nini?
Shahidi: Kutambua Reality ya Kinachofanana na Kwenye Detention Register
Wakili wa Serikali: Endelea Kueleza sasa
Shahidi: Baada ya Kukagua na Kujiridhisha nafunga ile Cello na Kurudi Charge Room Office nawakabidhi Ile Detention Register Kuendelea na Majukumu yao
Kama Upelelezi Haujakamilika Nawaamuru Waongeze Bidii kwa wakati Na Kama Upelelezi Haujakamilika na Makosa yanadhaminika basi Nawaamuru Mahabusu apewe Dhamana Hayo ndiyo Majukumu yangu ya Kila siku
Wakili wa Serikali: Malengo ya Kufanya Ukaguzi Mahabusu ni nini
Shahidi: Kuoanisha Taarifa za Report Book na Watu waliopo Kule Cello pia Kunirahisishia namna ya Kupanga Wapepelezi na Kama Wamekamilisha Upelelezi Nawaamuru Mtuhumiwa afikishwe Mahakamani Kwa Wakati
Wakili wa Serikali: Kwa Nafasi Yako ya Kaimu Mkuu wa Kituo Cha Tazara, Elezea ni Makosa gani ya Jinai Unayoshughulika nayo Kituo cha Polisi Tazara
Shahidi: Tunashughulika Makosa yote ya Jinai yatakayotokea Ndani ya eneo la Tazara
Wakili wa Serikali: Eneo la Tazara Unamaanisha nini?
Shahidi: Maeneo yote, (Within Compaund) kwenye Station Zake, Karakana zake na Ofisi zake
Wakili wa Serikali: Panapo Kituo cha Polisi Tazara, upo kwa Muda gani Mpaka Sasa
Shahidi: Mpaka Sasa nipo Kwa Miaka 17
Wakili wa Serikali: Ongeza Sauti.
Wakili wa Serikali: ulikuwa unatekeleza Majukumu Gani kama Operesheni Ofisa
Shahidi: Kuhakikisha Treni zote za Mizigo na Abiria Zinakuwa na Askari anayetembea na Treni, Kuhakikisha Doria zote zinazo takiwa kufanyika kwenye Reli ya Tazara Zina fanyika kwa wakati, Kupata Taarifa zote za Mahabusu
Wakili wa Serikali: Elezea Mwaka Jana Mwezi August 2020 katika Eneo lako la kazi
Shahidi: Nakumbuka Tarehe 03 August 2020, Ngoja Kidogo Mwezi May 10,2020 nilikuwa Operesheni Ofisa Wa Kituo Cha Polisi Tazara Nilikuwa nahudumu Kuanzia Dar es Salaam Mpaka Tunduma Kote
Vituo Vyote Kuanzia Tazara Dar es Salaam Mpaka Tunduma na nilipata Nampatia Mkuu wa Kikosi Kusimamia Mazoezi yote ya u tayari Kwa Askari
Wakili wa Serikali: Mazoezi ya Utayari Unamaanisha ni Yapi..?
Shahidi: parade na Medani za Kivita
Wakili wa Serikali: Unakumbuka Tarehe 03 ulikuwa unatekeleza Jukumu gani
Shahidi: Nakumbuka 03 August 2020 nilipewa Jukumu la kukaimu Ukuu Wa Kituo baada ya aliyekwepo Kwenda Likizo fupi ya Siku 28
Wakili wa Serikali: Baada ya Kupata hiyo Barua Tarehe hiyo Majukumu Yakianza Lini na Kuishia Lini
Shahidi: Kuanzia Tarehe 03 August 2020 Mpaka 06 September 2020
Wakili wa Serikali: Elezea hapa Mahakamani Kama Ulifanya Shughuli zinazohusu Mahabusu
Shahidi: Kama inavyopaswa na Mkuu wa Kituo, Nikifanya Ukaguzi Siku ya Tarehe 07, Mahabusu Yetu halikuwa na Mtuhumiwa Tarehe 08 Nikifanya Ukaguzi Kama Kawaida, Tarehe hiyo palikuwa na Mtuhumiwa Mmoja Mwanamume.
Wakili wa Serikali: Katika Kipindi Ulicho kuwa unakaimu Ukuubwa Kituo pale Tazara, Elezea Tarehe 07 Mpaka 09 August 2020 ulikuwa wapi
Shahidi: Nilikuwa kazini natekeleza Majukumu Yangu ya Kipolisi
Wakili wa Serikali: Wapi
Shahidi: Kituo Cha Polisi Tazara
Wakili wa Serikali: na Huyu Mkuu wa Kituo Cha a Polisi aliyekwepo na Kwenda Polisi anaitwa Nani
Shahidi: RICHARD OGUTU Superitendent wa Polisi
Wakili wa Serikali: Wakati Umekaimu ni Majukumu Gani ulikuwa unafanya
Shahidi: Yale Matano ya Awali
Wakili wa Serikali: Katika Kusimamia Mahabusu pale Kituoni ni Vitu gani mnafanya
Shahidi: Tuna Report Book, Tuna Detention Register Zinazotumika na Watuhumiwa Wote waliopo Mahabusu, na Tuna PPR ( Prisoner's property Report Book) Kitabu Kinachoonyesha Mali anazomiliki Mtuhumiwa
Wakili wa Serikali: Elezea Sasa Majukumu hayo Uliyo kaimu wakati Richard OGUTU ameenda Likizo yaliendelea Mpaka Lini
Shahidi: Yaliendelea Mpaka Tarehe 06 September 2020
Wakili wa Serikali: Siku hiyo nini Kilitokea
Shahidi: Alikuja Superitendent Richard OGUTU Nikamkabidhi Kituo chake
Wakili wa Serikali: Ulimkabidhi nini Na nini
Shahidi: Idadi ya silaha, Magari, Assets Kwa Maana ya Furnitures, Mahabusu wakiwa Salama, na Nyaraka zingine za Serikali
Wakili Serikali: Unasema Ulimkabidhi Mali kama Ulivyo orodhesha, Je Detention Register Ulifanyia nini
Shahidi: Detention Register ilikwepo CRO wakati wa Makabidhiano
Wakili wa Serikali: Alikuwa anatuhumiwa nini
Shahidi: Kujifanya Mtumishi wa Serikali
Shahidi: Tarehe 09 Palikuwa pana Watuhumiwa Wawili, Wanafunzi Wa Kiume, Ambao walikuwa Wanatuhumiwa Kuhatarisha Miundo Mbinu ya Reli, Tuliwakamata wakifungua Nati za Reli
Wakili wa Serikali: Ulibaini Vipi hao watuhumiwa
Shahidi: Kama Ilivyo Kawaida inapofika Asubuhi, Napitia Detention Register, na chukua Mtu wa CRO naenda Kufanya Check Up Mahabusu, kwa hilo niliwakauta Mahabusu
Wakili wa Serikali: Sasa Baada ya Kufanya Shughuli hiyo ya Ukaguzi wa Mahabusu, Wewe Unauthibitisho gani kama Watuhumiwa hao Walikwepo
Shahidi: Uthibitisho Mkubwa ni Detention Register ambayo pia Ilikuwa na Saini yangu baada ya Kufanya Ukaguzi
Wakili wa Serikali: Hiyo Detention Register Unavyosema Ndiyo Unauthibitisho huo, Wakati huo unakaimu ilikuwa inatunzwa Wapi
Shahidi: Kawaida huwa inatunzwa Charge Room Office, Kwa hiyo ilikuwa Charge Room Office
Wakili wa Serikali: Elezea Ni Kitu gani Kilitokea Baina yako na OGUTU
Kibatala: OBJECTION Mheshimiwa Jaji hatujasikia hayo
Jaji: hujasikia tarehe 03 Kibatala: Swali ni Leading
Wakili wa Serikali: Lini ukikabidhiwwa Majukumu hayo
SHAHIDI SP RICHARD OGUTU
Wakili wa Serikali: Makabidhiano hayo ya Majukumu yalifanyikaje
Shahidi: Kupitia Nyaraka Za Makabidhiano Wakili wa Serikali Katika Nyaraka hiyo ya Makabidhiano Mlikabidhiana nini
Shahidi: Nyaraka hiyo Ulionyesha Mali zilizopo Kituoni, Office Furniture, Mali zilipo Kituoni na Silaha, Nyaraka zingine Za Siri, Ikiwemo Nyaraka zilizo Kwishatumika ikiwepo Detention Register na Report Book
Wakili wa Serikali: ulijumuisha Detention Register zilizokwisha, Ni zipi hizo
Shahidi: Ikiwemo ile ya August 2020 ambayo nilikuwa nikikaimu Ukuu wa Kituo
Wakili wa Serikali: Baada ya Kukabidhiwa Detention Register iliyoisha, Uliyo itumia August 2020, Ulimpeleka wapi
Shahidi: Nilikuta Ikiwa imehifadhiwa Katika Ofisi yake
Wakili wa Serikali: Baada ya Tarehe 03 June 2021 ni lini tena Ulifanyika Kazi
Shahidi: Nakumbuka Tarehe 14 November 2021, alikuja Mtu Mmoja aliyejitambukisha kwamba ni Askari Polisi Kwa Jina la Inspector Swila, anatoka Ofisi Ya DCI
Wakili wa Serikali: alikuja wapi
Shahidi: Kituoni Tazara
Wakili wa Serikali: Saa ngapi!?
Shahidi: Majira ya Saa Tano, alifika Charge Room Office, akamuulizia Mkuu wa Kituo, Alikuja Askari Wa Charge Room Office akaniita kwamba nahitajika Chini kwamba Inspector Swila ananihitaji
Shahidi: Nikitoka Ofisini Kwangu Nikashuka Kwenda Chini Charge Room Office kwenda Kuonana naye ana kwa ana
Wakili wa Serikali: Baada ya Kuonana naye
Shahidi: akinihoji Kuhusu Detention Register Iliyotumika Mwezi August 2020
Wakili wa Serikali: Alikueleza ni ya Nini
Shahidi: Alinieleza Kwamba inahitajika Mahakamani Kwa ajili ya Ushahidi
Wakili wa Serikali: Wewe Ulifanya nini baada ya Kuwa Amekueleza hivyo
Shahidi: pale Ofisini Detention Register ilikuwa Mpya, Ile ambayo aliyokuwa anahitaji ilikuwa imeshatumika Mwisho Mwezi May, Kwa wakati huo haikuwepo pale Charge Room a office
Wakili wa Serikali: Ukafanya nini sasa
Shahidi: Nikamjulisha kwamba nitaitafuta Ofisini Kwangu kwenye Makabati ninayohifadhia Nyaraka Mbalimbali, yeye akaondoka Nikaenda Ofisni nikaikuta
Wakili wa Serikali: aliondoka kwenda wapi
Shahidi: Aliondoka Kituoni Miye nikarudi Ofisini kwenda Kuitafuta, nikaipata
Wakili wa Serikali: Ukakuta nini
Shahidi: Baada ya Kukagua nikamkuta Tarehe 06 na Tarehe 07 Hapakuwa na Mahabusu
Wakili wa Serikali: Sasa Hapa Mahakamani Pana Kesi na Nitakutajia Majina Uelezee Kama hizo Tarehe 7 na 8 kama yaliikuwepo Khalfani Bwire Adam Kasekwa Mohammed Ling'wenya
Shahidi: Kupitia Detention Register Majina hayo hayapo na Watuhumiwa hao hawakuwepo Kituoni Kwa Tarehe hizo Tajwa
Wakili wa Serikali: KWA SAUTI TAFADHALI
Shahidi: Kupitia Detention Register Majina hayo hayapo na Watuhumiwa hao hawakuwepo Kituoni Kwa Tarehe hizo Tajwa
Wakili wa Serikali: baada ya hapo Uliipeleka wapi?
Shahidi: Nilihifadhi na Mpaka Leo nimekuja nayo
Wakili wa Serikali: hiyo Detention Register Ilitumika Kipindi Gani?
Shahidi: Tangu January Mosi 2019 Mpaka Mwaka huu May 25
Wakili wa Serikali: na Hii Detention Register ambayo umekuwa ulielezea, Wewe Utaitambuaje
Shahidi: Detention Register Ina sehemu ya Nje na ya ndani kwa Sehemu ya Nje Nakumbuka tuliandika Kwa a maker Pen ya Blue Bahari WEF 01. 01 .2019 Chini kuna maandishi Madogo yameandikwa TANZANIA MINISTRY OF HOME AFFAIR TANZANIA POLICE FORCE na Maneno Madogo Sana ya PR20
Na Kwa ndani Inakuwa na Maandishi ya asomeka POL/TZR/PR/IR OR RB/MWAKA
Wakili wa Serikali: Kitu Kingine
Shahidi: Ni sahihi au Jina la Afisa aliye kagua Kipindi hicho
Wakili wa Serikali: Kitu gani Kina kuhusu Wewe
Shahidi: Kujua Idadi ya Polisi
Wakili wa Serikali: Katika Utambuzi wa hiyo Detention Register Kuna Kitu gani Kingine
Shahidi: Sahihi yangu, niliyo Saini Siku tofauti tofauti
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji tunaomba Kumpatia Shahidi Kielelezo Kwa ajili ya Utambuzi
Jaji: Sawa
Wakili wa Serikali: Kitu gani Kingine
Shahidi: Kumbukumbu namba za Kesi zilizo andikwa kwa Kifupi P. O. L/TZR/PR na Zingine
Wakili wa Serikali: Ungependa Mahakama ifanye nini na hiyo Detention Register
Shahidi: Mahakama Ipokee Kama Kielelezo Katika Ushahidi Wangu
Wakili wa Serikali: Kama Umetambua hiyo ni Kitu gani
Shahidi: Hii ni Detention Register
Wakili wa Serikali: Detention Register Ya wapi
Shahidi: Police Tazara, Pugu Road
Wakili wa Serikali: Umeitambuaje
Shahidi: Nimeitambua Kwa Maandishi Yalipo Nje
Wakili wa Serikali: Yataje
Shahidi: Maandishi ya Blue Bahari Tarehe 01.01 2019 ni Detention Register Inayomilikiwa na Jeshi la Polisi
Wakili wa Serikali: Umeitambuaje.
Shahidi: Ndani Kuna Sahihi yangu
Wakili wa Serikali: Kitu gani Kingine
Shahidi: Kumbukumbu namba za Kesi zilizo andikwa kwa Kifupi P. O. L/TZR/PR na Zingine
Wakili wa Serikali: Ungependa Mahakama ifanye nini na hiyo Detention Register
Shahidi: Mahakama Ipokee Kama Kielelezo Katika Ushahidi Wangu
Wakili wa Serikali: Tutajie Serial Namba
Mtobesya: OBJECTION amevuka mipaka yake
Wakili wa Serikali: Ulisema Mwanzo Kuna Vitu Vitavyofanya uitambue
Shahidi: Maandishi PF 20 MINISTRY OF HOME AFFAIR TANZANIA POLICE FORCE PF 20
Mawakili wa utetezi wanapelekewa nyaraka Wameizunguka Kwa pamoja, wanaifungua mbele nyuma kwa kasi, wanaigeuza geuza hapa, wanaangalia kwa mbali kidogo, Mtobesya anavaa miwani yake vizuri hapa Malya anachukua katarasi na Pen, Ku' Note Vitu Kibatala anafungua begi lake kubwa
Jaji: napokea kama Kielelezo p3 kwenye Kesi Ndogo Ndani ya Kesi kubwa ya Upande wa Mashtaka Mawakili Wa pande zote mbili wanakubaliana na Jaji kwa kusimama
Jaji: asome sehemu ambayo ni Relevant
Wakili wa Serikali: Soma Tarehe 8 na 9 ya August 2020
Shahidi: 08/8 palikuwa na Mtuhumiwa anaitwa Godfrey Kilimba anaishi Mbezi Juu, PPR 0627 aliingia 08/8 saa 5 na Nusu Usiku akatolewa Siku ya tarehe 10 August 2020, Saa 6 Na Dakika 45, NJE kwa Upelelezi
Shahidi: Tarehe 09 Palikuwa na Mtuhumiwa John Gerald, kabila Mfipa, Mwanamume Mwenye Afya Njema, Mwanafunzi wa Yombo Sekondari PIA palikuwa na Mtuhumiwa Lucas Jovin wa Miaka 12, alitoka tarehe 10
Wakili wa Serikali: Shahidi Nenda sasa Katika Kielelezo hicho Kwa Tarehe 7,8 na 9 ya Mwezi August 2020
Shahidi: Tarehe 7 Hakuna Mahabusu
Wakili wa Serikali: Sasa Mahabusu uliyemsoma kwenye Entry 257 Soma Jina lake na Tuhuma zake
Shahidi: Geoffrey Kilimba, kabila Mhaya
Wakili wa Serikali: Alikuwa na Tuhuma gani
Shahidi: Kujifanya Mtumishi Wa Serikali
Wakili wa Serikali: Kwenye Entry namba 258 ni nani
Shahidi: John Gerald, Kuhatarisha Miundo Mbinu ya Reli
Wakili wa Serikali: Tutajie pia na Entry namba 259
Shahidi: Lucas Jovin, Kuhatarisha Miundo Mbinu ya Reli
Wakili wa Serikali: Katika Eneo hilo Kuna kitu kinaonyesha kwamba Ulikagua
Shahidi: Kuna Saini yangu hapo ambayo nilikagua
Wakili wa Serikali: Kitabu hicho Kilitumika Kuanzia Lini hadi lini
Shahidi: Kuanzia 01.01.2019 Mpaka 29 May 2021 WS: Ahsante, ni hayo tu Mheshimiwa
Mtobesya anaenda Shahidi alipo
Mtobesya: naweza Kuendelea Mheshimiwa Jaji
Jaji: Sawa
Mtobesya: Shahidi Tusaidie Kwanza Unafahamu PGO ni Kitu gani
Shahidi: Kitabu cha Ufanyaji kazi na Taratibu za Polisi
Mtobesya: Nitakuwa Sahihi nikisema Kitabu hiki Kinakuhusu
Shahidi: Sahihi
Mtobesya: Kwa Mujibu wa Kifungu cha 353 cha PGO nani anatakiwa Kukagua Mahabusu
Shahidi: Kuna Makundi Manne, kuanzia Mkuu wa Kituo
Mtobesya: Kwa PGO gani
Shahidi: Hiyo kuanzia 353 nafikiri
Mtobesya: Nitakuwa sahihi Nikisema Kwamba Wakati Mwaka Jana unakagua wewe Hukuwa NCO
Shahidi: Ndiyo
Mtobesya: unafahamu Kitu kinaitwa OCCURANCE BOOK
Shahidi: Ndiyo
Mtobesya: Nitakuwa sahihi nikisema Kwamba Ukienda Kukagua Mahabusu Unatakiwa Kusaini Station Diary
Shahidi: Siyo kweli
Mtobesya: Na umesema Kwamba Unaifahamu PGO
Shahidi: Ndiyo
Mtobesya: Na Kwamba haina Matakwa hayo
Shahidi: Sikumbuki Kidogo
MTOBESYA: Mkuu wa Kituo, Kamanda wa Kikosi Waziri husika, Watu wa Haki za Binadamu... Je Charge Room Officer Harusiwi?
Shahidi: anaruhusiwa
Mtobesya: Kuna watu wa naitwa Wa naitwa NCO ni akina nani
Shahidi: Coplo, sergeant na sergeant Major
Mtobesya: Kwamba Kama Ungekuja na Station Diary ndiyo tungeamini Kwamba Ulikwepo Siku hiyo
Shahidi: Ndiyo
Mtobesya: Tungeona Saini yako
Shahidi: Mimi huwa si saini
Mtobesya: Lakini Unatakiwa Kusaini kuanzia Mkuu wa Kituo Mpaka Chini
Shahidi: Ndiyo Natakiwa kusaini
Jaji: Mmeniacha Kidogo Mlinzi kuwa mnazungumzia Prison Inspection hapa naona unazungumzia Prison Visit
Mtobesya: Kwenye PGO hawana Inspection Wanaita Prison Visit
Jaji: Ok Sawa!
Mtobesya: Shahidi Station Diary Inachukua Taarifa gani
Shahidi: Askari wanaoingia na kutoka Kazini
Mtobesya: Wakati Unatambua Kitabu Ulitaja WEF, Je Ulieleza hii WEF ni Kitu gani
Shahidi: Sikueleza
Mtobesya: Wakati Uliongozwa na Wakili Wa Serikali Robert Kidando, Ulielezea Kuhusu Hii namba Ilisha andikwa lakini ikaonekana Ikarudiwa..?
Shahidi: sikumueleza
Mtobesya: Nilisikia pia unasema Kwamba Ulikabidhiwa kituo na Mtu anaitwa Richard OGUTU
Shahidi: Ndiyo
Mtobesya: Mlikabidhiana Kwa maandishi
Shahidi: Hapana
Mtobesya: Ikitokea Detention Register Imeisha Muda wake Mnaiweka wapi
Shahidi: Ina chukuliwa kutoka Charge Room Office Kwenda Kwenye Cabinet Ofisi ya Mkuu wa Kituo
Mtobesya: Kwenye hizo Entry Mlinzi Shughulikia Mwisho Lini
Shahidi: Tarehe 10 September 2020
Mtobesya: Baada ya hapo Kitabu Kilibakia wapi
Shahidi: Charge Room Office
Mtobesya: Baada ya Kuliacha Mara ya Mwisho 6 September 2020 ulikiona tena lini
Shahidi: Sikukitumia Mpaka Leo
Mtobesya: Wakati Superitendent wa Polisi OGUTU anakukabidhi bila Maandishi nani alikuwa ana kihifadhi
Shahidi: Superitendent OGUTU
Mtobesya: Wakati Msomi Kaka Yangu Wakili wa Serikali Robert Kidando anakuongoza, ulitaja namba hapa, Je Ulieleza zipo wapi
Shahidi: Nilileza
Mtobesya: Ndiyo Record zinavyoonyesha?
Jaji: Ukisema Record wakati alikuwa aandiki inakuwa Ngumu kwake
Mtobesya: naomba Kurudia Swali
Mtobesya: Wakati pia Msomi Kaka Yangu Wakili wa Serikali Robert Kidando +anakuongoza, ulitaja namba hapa, Je Ulieleza zipo wapi
Shahidi: Nilisema Kitabu Kina Nje na Ndani
Mtobesya: Ulisema Kituo cha Polisi ambacho Kipo Pugu Road kina Abbreviation gani
Shahidi: P.O.L/TZR
Mtobesya: Hakuna Sehemu inaelekeza kwamba Kituo cha Polisi Tazara Kinatakiwa Kiitwe TPG?
Shahidi: sijui
Mtobesya: akitokea mtu akasema Kituo cha Polisi Tazara Kinatakiwa Kutamkwa kwa Kifupi cha TPG ni Muongo au Mkweli?
Shahidi: atakuwa Muongo
Mtobesya: nimemaliza
Mallya: We Shahidi Unajua Kwamba Ugaidi ni Makosa Serious
Shahidi: Ndiyo
Mallya: hii Serious Crime ni sahihi kwa Polisi Kui attend kwa dharula kabla haitatokea
Shahidi: Ndiyo inawezekana na Ndiyo kazi zetu
Mallya: Najua umesoma Polisi Moshi, au Popote nataka Kujua Kama Una elimu Nje ya Nchi
Shahidi: Hapana
Mallya: Ulishawahi Kusikia Kwamba Magaidi Wameng'oa Reli au Kufanya Ugaidi Kwenye Treni
Shahidi: Nimesikia Kupitia BBC huko Pakistan
Mallya: Kama nimekuelewa Kwamba Jambo Linashughulikiwa Tazara ndiyo linaonekana humu, Kama Jambo siyo la Tazara haliwezi Kuonekana humu
Shahidi: Ndiyo
Mallya: Uliulizwa Majukumu yako na Kaka yangu Kidando, Ukasema ni uhalifu ulikuwa Unafanyika ndani ya Treni na Sehemu zenu
Shahidi: Ndiyo
Mallya: Kuna Majukumu Mengine shahidi Ujayataja, Pale Inapotokea Kusaidia Jeshi la Polisi Namna Nyie Mnauwezo huo, Ni lazima Mtayafanya
Shahidi: Ndiyo
Mallya: Ikitokea Kwamba DCI anasema Kwamba ana dharula akaomba Watuhumiwa Wawekwe Pale Tazara Utakubali au utakataa, Pia, DCI anakusikia huko alipo..
Jaji: Sijui Kama tupo Live huko
Mallya: sijamaanisha hivyo Mh Jaji, Namsaidia Shahidi ajue baada ya Kesi Mambo yatakuwa wazi
Shahidi: Kwa Mamlaka ya DCI Vituo Vyote Vya Polisi Vipo Chini ya DCI, nitamkubalia with Condition
Mallya: Kuhusu Condition yako Mimi sina Interest nazo
Shahidi: Katika Condition nitakao Mpa DCI nitamwambia Kwamba DCI anipe Case number
Mallya: Kwenye Hii DR zinaingia Kesi za Tazara tu, Je utawaandika humu
Shahidi: Lazima niwaandike
Mallya: lakini Mwanzo Tumekubaliana Kinachoandikwa humu ni Tazara tu
Shahidi: atanipa IR za alikofungulia nayo case
Mallya: Kama atakupa..?
Shahidi: Nita andika, Kama hatonipa sitoandika
Mallya: naomba nipewe Kielelezo Cha P2
Mallya: Sasa Sisi tunafaida ya Kuwa na Detention Register mbili, Mwenzio Polisi alileta hapa na Bila shaka zinatakiwa kufanana
Shahidi: Ndiyo zinatakiwa Kufanana
Mallya: Sasa hii Detention Register Ya Central na Hii Detention Register Ya Kwako, Hazifanani kabisa hapa Juu
Shahidi: Kwenye nini
Mallya: Soma hapa Juu hii na hii, Ya Kwako ina WEF 20
WS Robert Kidando: OBJECTION. Mheshimiwa Jaji Wakili anachofanya anakiuka kaomba Kielelezo Ghafla anampatia Shahidi bila Kujenga Misingi
Jaji: Kuna Sheria Kavunja..?
WS Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji ataanza Chavula Kisha nitamalizia..
WS Abdallah Chavula: Mheshimiwa Jaji Tunauliza Maswali, pale ambapo hujasema ameshughulika Vipi, Swali atakalo Jibu ni Opinion na Huyu ni Shahidi Wa Fact huyu siyo Mtaalamu wa PGO Leo anakuja Kaimu Kituo unamwambia afanye Comparison, Siyo sahihi
WS Robert Kidando: Inatosha Mheshimiwa Jaji
Mallya: naona Mtobesya anataka Kunisaidia,
Mtobesya: Mimi ni Afisa wa Mahakama, natakiwa nisaidie Mahakama, Mheshimiwa Jaji Shahidi kaulizwa Kwamba Detention zinatakiwa zifanane akasema Ndiyo, Sasa wanataka Wakili alay foundation gani? Kama Maswali hayamvunjii Heshima Shahidi, Maswali Yanaruhusiwa!
Wakili Nashon Nkungu: Sijajua Hoja ya Kujenga Msingi Kwenye Cross Examination inatokea wapi, Nawakumbusha Wenzangu kwamba Hear Say ni Kutoka Third party, Sijaona hapo Third party inatoka wapi....
John Mallya: kwa Maneno Ya shahidi Kwamba hizi ni Polisi form, na imeingia kwenye Rekodi, Huenda Hoja yao ilikuwa ni Kunikatisha Mzuka wangu Ukatike....
Jaji: Niseme Jambo Moja kwamba Kielelezo Chochote Kinachotolewa Mbele ya Mahakama Kinaweza Kutumika na Kielelezo anachotumia ni Kielelezo P2
Jaji: Kwa hiyo, kwa namna hiyo alichofanya Bwana Mallya sijaona alipokesea, Isipokuwa Mr Mallya Shahidi alijibu ndiyo Jibu lake...
Wakili Mallya: Haya tuonyeshe Sasa
Shahidi: Katika Exhibit P2 Kuna
Mallya: Hapo WEF ipo au Haipo
Shahidi: Hapa Haipo
Mallya: hii Nyaraka Ya P3, umeleta wewe ina karatasi imeondolewa
Shahidi: Hapana
Shahidi: Ila inakaratasi imeunganishwa
Shahidi: Kimyaaaaaaaaaa
Mallya: Wakati Unaongozwa na Kaka yangu Kidando Ulieza Kwamba Kuna Karatasi Imeunganishwa?
Shahidi: Hapana Sikusema
Mallya: Muonyeshe au Msomee Mheshimiwa Jaji ni Entry ipi ambayo imeunganishwa
Shahidi: ni Entry namba 275 Mpaka 277
Mallya: Uliongozwa na kaka yangu Robert Kidando Ulisema Kwamba Mnashughulika na nini
Shahidi: Makosa yote ya Reli yatakayotokea Katika Mazingira yetu ya Tazara
Mallya: Mheshimiwa Jaji Ya kwangu ni hayo tu Anasimama wakili Fredrick Kihwelo
Fredrick: Ni sahihi Nafasi Uliyo nayo sasa ulikaimu 03/6/2021
Shahidi: Ndiyo
Fredrick Kihwelo Ni sahihi Kwamba Hujaonyesha Hapa Mahakamani Nyaraka Kwamba Ulikaimu nafasi hiyo
Shahidi: Ndiyo Sijaonyesha Nyaraka Yoyote
Fredrick Kihwelo: Ni sahihi Kwamba Unaonyesha Nyaraka Yoyote hapa Mahakamani Kwamba Wewe ni Askari polisi
Fredrick: ni sahihi wewe Kama Askari Polisi Unapokea Maelekezo Kutoka Juu yako
Shahidi: Ndiyo
Fredrick PGO ya ngapi
Shahidi: Sikumbuki, ila Ndiyo Utaratibu Kupokea Malekezo Kutoka Juu Kupeleka Chini
Shahidi: Nimeonyesha Detention Register na Pili Kiapo nilichoapa hapa Mahakamani
Fredrick Kihwelo: Kiapo ni Nyaraka
Shahidi Hapana, ila Nimeonyesha Detention Register
Fredrick Kihwelo: Ni sahihi Ulitembelewa Ofisini kwako na Inspector Swila
Shahidi: Ndiyo
Fredrick Kihwelo: Mwambie Mheshimiwa Jaji siku ambayo alikutembelea Inspector Swila ilikuwa siku gani..
Shahidi: Siku siwezi kukumbuka aisee!
Shahidi: Lakini Mpaka nikumbuke kwenye kalenda
Fredrick Kihwelo: Mimi nasema Ilikuwa Jumapili
Shahidi: Exactly..... ilikuwa Jumapili
Mahakama:Hahahaaaa
Fredrick Kihwelo: Nimesikia Kwamba Toka tarehe 06/9/2020, Leo ndiyo Mara ya Kwanza unaiona
Shahidi: Leo ndiyo nimewasilisha Mahakamani, nilitafuta Nikaipata Baada ya Kupata Maelezo kwa Inspector Swila...
Fredrick: Ukipewa Maagizo kutoka Kwa Mabosi zako Utatekeleza au Hautotekeleza
Shahidi: Nitatekeleza
Fredrick: Nitakuwa Sahihi nikisema kwamba Mnamo Mwaka 2020, 08/8/2020 ulipewa Maagizo ya Kuwahifadhi Watuhumiwa Adam Kasekwa na Mohamed Ling'wenya
Shahidi: Hapana Sikupewa
Fredrick Kihwelo Kwa hiyo Unafualta Neno kwamba Leo ndiyo umeona Mahakamani
Shahidi: Kimyaaaaaaaaaa
Fredrick Kihwelo: Nimesikia Kwamba Umesema Kuna Mshtakiwa alishitakiwa kwa kosa la Kujifanya ni Mtumishi wa Serikali
Shahidi: Ndiyo
Fredrick Kihwelo: Mwambie Mheshimiwa Jaji Kwamba Hilo lina husika Vipi na Masuala ya Tazara
Shahidi: Aliwaambia Askari Kwenye Treni kwamba yeye ni Kamishina wa Polisi, Wakamfuatilia wakagundua Siyo wakamleta Kituoni
Fredrick Kihwelo: Kwa hiyo Uliambiwa au ulishuhudia
Shahidi: Walimleta Kituoni
Fredrick Kihwelo: ni hayo tu Mheshimiwa Jaji
Kibatala: Mheshimiwa Jaji Kwakuwa Muda wetu wa Break Umekaribia, Basi naomba twende Break Kwanza
Jaji: itakuwa Muda gani
Kibatala: pia Mheshimiwa Jaji hata kama hapa hapa ndani Chini ya uangalizi wa Mahakama naomba Ruhusa ya Kukipitia Kielelezo p3
Jaji: Upande wa Serikali
WS Robert Kidando: Kwanza hakuna la Msingi ATAKALOGUNDUA, Suala la Kuomba Kielelezo ni Suala la Wakati wa Mahakama, Sioni kama ana sababu za Msingi
Jaji: ulitaka Kukiangalia Kwa Dakika Ngapi
Kibatala: hata 10, pia nilikuwa na Kuomba wewe siyo wao
Jaji: Sawa ila Mimi Ndiyo niliwapa nafasi wajibu, Basi nakupa Dakika 5 Mbele ya Afisa wa Mahakama..
Jaji: Tutarudi Saa 8 Kamili Jaji anatoka!
----------
Jaji amerejea
Mahakamani Kesi namba 16 ya Mwaka 2021 Khalfani Bwire, Adam Kasekwa, Mohammed Ling'wenya na Freeman Mbowe inatajwa tena
Wakili wa Serikali; Mheshimiwa Jaji Quorum yetu ipo Vilevile tupo tayari Kuendelea
Kibatala; pia Mheshimiwa Jaji Quorum yetu ipo Vilevile tupo tayari Kuendelea
Kibatala: Wakati Mawakili Wa Utetezi wanakuuliza Kuhusu Siku ya Inspector Swila Kuhusu Tarehe 14 November 2021 Ukasema Hukumbuki
Shahidi: Ndiyo sikumbuki
Kibatala: Ngoja Nikupe hiki kitu
Shahidi: hii ni kalenda
Kibatala: Kalenda ya Taasisi gani
Shahidi: Mahakama
WS Pius Hilla: OBJECTION. Shahidi anaonyeshwa Kitu ambacho hata sisi Mawakili hatujaona na Kuanza Kumuonyesha Shahidi
Kibatala: Kwa Heshima na Taadhima, Sijaona Hoja ya Msingi
Jaji: ni Sahihi Kumpatia Nyaraka Shahidi na Kuanza Kusoma, Ndiyo Hoja yake
Kibatala: Ndiyo hivyo sasa aniambie ni Sheria gani inakataza
Jaji: Mimi nafikiri hata Mahakama ingetaarifiwa ni Kitu gani iweze Ku' Note
Kibatala: Sawa Mheshimiwa Jaji nakubalina na hilo, Ngoja Niichukue nmpatie tena
Kibatala: Mheshimiwa Jaji Kwakuwa Shahidi aliulizwa Kuhusu Tarehe 14 November 2021 ni lini na Wakili Fredrick Kihwelo akasema hakumbuki Mpaka atizame kalenda, Hapa Mkononi ni kalenda nimeomba Ofisi ya Msajili Mahakama Mbayo Imetolewa na Mtendaji Mkuu wa Mahakama, Naomba Kuitumia
Kuuliza Swali Kwa Shahidi Kuhusiana Na Siku ya tarehe 14 November 2021
Jaji: naiomba Kwanza Huku,
Jaji: Upande Wa Mashtaka? Mawakili wa pande wa Mashitaka Wanaijadili Kidogo Wanaizunguka
WS Pius Hilla: hatuna pingamizi Na Shahidi Kuonyeshwa hii Nyaraka
Kibatala: Asante Mheshimiwa Jaji
Kibatala: Sasa Shahidi Nimeomba Ruhusa Mahakamani naomba uniambie Kwa Ushahidi Wako Siku ya tarehe 14 November 2021 kwamba ilikuwa Siku gani
Shahidi: Siku ya Jumapili
Kibatala: Kwamba Ilikuwa Majira ya Saa ngapi
Shahidi: Saa 5:30 Asubuhi
Kibatala: Wakati Unaongozwa na Wakili Msomi Mr. Robert Kidando, Uiliiambia Mahakama au Jaji Kwamba Mimi huwa nafanya kazi Siku ya Jumapili?
Shahidi: Katika Majukumu yangu Nilisema Kwamba Mimi Kama Mkuu wa Kituo Natakiwa Kufika Kituoni Siku zote
Kibatala: Ulitaja Neno Jumapili au Hukutaja
Shahidi: Sikutaja
Kibatala: Mtu akifika Tazara Kama anataka Kumuona Mkuu wa Kituo
Shahidi: Utafika CRO Kuna Mambo Mawili Kama Shida ya Ofisi Utaruhusiwa Kuniona.
Kibatala: Kama Shida ya Kiofisi naruhusiwa Kuja Ofisini kwako?
Shahidi: ndiyo
Kibatala: Na Inspector Swila ilikuwa Kwa shida ya Kiofisi
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Basi nahama hapo, Inspector Swila alikwambia nini
Shahidi: Kwamba Kuna Complains zimejitokeza Kwenye kesi ya Mheshimiwa Mbowe na Kwamba Mimi Kama MKuu wa Kituo natatakiwa Kuja Kutoa Ushahidi
Kibatala: kwa hiyo Swila kwambia Kwamba Detention Register Inahitajika
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Kwa hiyo Wewe tangu Siku hiyo ulikuwa unajua Unakuja na Kithibiti kuja Kutoa Ushahidi
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Kwamba Bila Swila Leo hii Usingekuwa Mahakamani Kutoa Ushahidi
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Inspector Swila alikwambia anatoka wapi
Shahidi: Ofisi ya DCI
Kibatala: DCI yupi?
Shahidi: Camilius Wambura
Kibatala: Inspector Swila alikupa Barua Kwamba Detention Register
Shahidi: Hapana
Kibatala: Unafahamu Kitu kinaitwa Chain of Custody katika Kuchukua Vielelezo
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Kwa hiyo kuna sehemu umeandika unachukua Kielelezo
Shahidi: Kwa cheo, nafasi na majukumu yangu naweza kuchukua kielelezo chochote wakati wowote
Kibatala: kwani shahidi vielelezo vinatolewa kwa mujibu wa sheria au kwa namna mnavyotaka?
Shahidi: Kwa mujibu wa sheria
Kibatala: PGO hiyo hapo nionyeshe sehemu kama Kuna kifungu chochote kinachokuruhusu wewe kama Afisa wa Polisi kuchukua kielelezo (Detention Register) bila kusaini kwenye Exhibit Register
Shahidi: Mimi sifahamu
Kibatala: Wakati Unaitoa Detention Register Ulishafahamu tangu tarehe 14 November kwamba Itatumika kama Kielelezo Cha Ushahidi?
Shahidi: Naomba Kuku Jibu Kwa Ufahamu wangu, Kwamba Detention Register Ilikuwa Imeshatumika na Baada ya Miaka 03 tutafanya Disposal
Kibatala: Nikumbushe tafadhali Afisa wa Polisi Anafanya kazi Kwa Kuongozwa na PGO au Kwa Utashi wake
Shahidi: Kwa Kuongozwa na PGO
Kibatala: Hivi Vituo Vya Polisi Vinafanyiwa Ukaguzi?
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: OCD wa Temeke anaweza kwenda Kufanya Inspection Tazara?
Jaji: Tazara inajitegemea kwa Maelezo yake
Kibatala: Sawa, Ngoja Nibadili swali, Je Kamanda wako wa Vikosi wa Tazara anaweza Kufanya Ukaguzi wa Ghafla Kituoni kwako?
Shahidi: anaweza
Kibatala: je akija sasa Kwenye Ukaguzi atajua Kidhibiti Kipo wapi?
Shahidi: Mimi kabla sijatoka au Kufanya Jambo lazima nimuarifu Mkuu wangu
Kibatala: Hapo Swali Je wakati Uliongozwa na Wakili Wa Serikali Robert Kidando, Ulizungumzia Kuhusu Kumtaarifu Mkuu wako wa Vikosi?
Shahidi: Hapana Sikusema
Kibatala: Je Boss Wako anayefuatia anaruhusiwa na Yeye Kwenda Kufanya Ukaguzi?
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: akienda atajua kwa Maandishi Kwamba Kielelezo Kimeenda wapi
Shahidi: atanisubiri Mpaka nirudi..
Ni kweli bado kesi inaonekana kama vile kitu cha kufikirika kuliko uhalisia, Sasa wangeondoka huko kwenye hilo dude lililokama set up au flaming kama wahusika wanavyodai Sasa waanze kutuletea fact za ugaidi maana ndo kitu wengi tunasubiri.Yaani tangu mlolongo wa kesi uanze sijaona shahidi hata mmoja aliyethibitisha namna ugaidi ungefanywa
AAaa wapi, nyama za kwenye mtori tukaziibuaga mapema tu kwa kijiko ‘uji’ tunamwachia waitress!Endeleeni Kula Mtori nyama mtazikuta chini ya sufuria.
Hahahahaha nimecheka hadi mbavu zinauma mieYaan mawakili wa utetezi Wana kazi kweli kweli, wamuongeze Shahidi wamuongoze ma jaji pia.
Haa Mawakili wa Mbowe"wamesomea" kazi yao, Mtobesya yuko smart! Jaji anaongozwa na Mtobesya!!
kimeumana.🤣🤣🤣🤣Kibatala: Cheo chako wewe ni nani?
Shahidi: Inspector Wa Polisi
Kibatala: Kwenye Mambo yenu Iliandikwa A! inspector Maana yake nini?
Shahidi: kimyaaaa
Kibatala: Mwaka Jana ulikuwa nani vile?
Shahidi: Inspector
Kibatala: na Mwaka huu ni Inspector eeh?
Kibatala: nimekuuliza Mwanzo KUWA Mwaka Jana ulikuwa nani Ukajibu ni Inspector hapa Umejaza in Assistant Inspector Je Ulimwambia Mheshimiwa Jaji?
Shahidi: Sikufafanua