Yaliyojiri katika kesi ya Freeman Mbowe -Inspector Lugawa ISSA Maulid atoa Ushahidi, Kesi yaahirishwa hadi Novemba 25, 2021

Mimi bado sielewi kitu, mbona naona kama madhahidi wa mashitaka ushahidi wao unafanana (kamata, kula, safirisha, weka ndani, andika) tofauti ni mashahidi, nini kinatafutwa maana sioni kutegwa kwa makombora, mabomu na mahandaki.
USHAHIDI WA UGAIDI BADO HATUUONI, Kinachoonekana ni taratibu za ukamataji, kusafiri toka Moshi hadi Dar, kunywa supu na MO energy, kuwekana mahabusu....Sasa ushahidi wa ugaidi tutaelezwa saa ngapi ili tujue?
 
Elimu ya mashahidi upande wa serikali ,wamesoma wapi,wamejiunga lini na jeshi la polisi na kuajiriwa rasmi,hilo mmelihoji ?
 
Sasa askari wa tazara anahusika nn wkt Shahid anakataaa kuwa akina Ling'wenya hakuwa huko ktk kituo Cha tazara? Hata mpubavu atagundua Kuna mchezoe una chezwa
 
USHAHIDI WA UGAIDI BADO HATUUONI, Kinachoonekana ni taratibu za ukamataji, kusafiri toka Moshi hadi Dar, kunywa supu na MO energy, kuwekana mahabusu....Sasa ushahidi wa ugaidi tutaelezwa saa ngapi ili tujue?
Endeleeni Kula Mtori nyama mtazikuta chini ya sufuria.
 
kesi ya kinafki hii, hapo hamna kesi na leo itahairishwa.

Ni kwania ya kufikia mchakato wa katiba mpya ulopangwa kufanyika 2022, na sio 2021 kama mbowe alivotaka.

Kwahio hapo watamwachia mwisho wa mwaka huu au mwanzoni mwa mwaka 2022.
Nakubaliana na wewe maana hata Wajawazito kurudi shule wamekubali Leo ili waanze mwakani.
 
USHAHIDI WA UGAIDI BADO HATUUONI, Kinachoonekana ni taratibu za ukamataji, kusafiri toka Moshi hadi Dar, kunywa supu na MO energy, kuwekana mahabusu....Sasa ushahidi wa ugaidi tutaelezwa saa ngapi ili tujue?
Bado unapikwa,ukiiva akina king'aa watapanda nao kwenye kizimba🤔.
 
Leo tarehe 24, Nov. 2021kesi ya ugaidi inayomkabili Mbowe na wenzake 3 inaendelea katika mahakama divisheni ya Uhujumu Uchumu na Rushwa ambapo leo Jamhuri italeta Shahidi Mwingine.

Kujua kesi ilipoishia, soma: Yaliyojiri katika kesi ya Freeman Mbowe - Novemba 23, 2021. Kesi yaahirishwa hadi Novemba 24, 2021

========

UPDATES:


Jaji naingia

Mahakamani Kesi namba 16/2021 Khalfani Bwire, Adam Kasekwa, Mohammed Ling'wenya na Freeman Mbowe inatajwa

Wakili wa Serikali: Robert Kidando anatambulisha Jopo la Mawakili wa Serikali

Pius Hilla
Abdallah Chavula
Jenitreza Kitali
Nassoro Katuga
Esther Martin
Tulimanywa Majige

Wakili Peter Kibatala anatambulisha Jopo la Mawakili wa Utetezi

Idd Msawanga
Nashon Nkungu
John Mallya
Fredrick Kihwelo
Dickson Matata

Jaji anaita Majina ya washtakiwa Wote wanne na wote wanaitika wapo.

Wakili wa Serikali: Ahsante Mheshimiwa Jaji, Shauri limekuja kwa ajili ya Kusikilizwa na Leo tuna shahidi Mwingine Mmoja na tupo tayari Kuendelea

Wakili Peter Kibatala: Na sisi kwa ruhusa yako pia Mheshimiwa Jaji tupo tayari kuendelea Jaji na atakuwa shahidi wa nne siyo?

Wakili wa Serikali: Ndiyo

Shahidi anaingia Moja kwa Moja Mahakamani, kijana amevaa kaunda suti..

Jaji: Majina yako

Shahidi: Inspector Lugawa ISSA Maulid

Jaji: Miaka

Shahidi: 42

Jaji: Kabila

Shahidi: Mluguru

Jaji: Dini Shahidi' Muislamu

Jaji: Thibitisha

Shahidi: Wallah wabillah watallah Nathibitisha Ushahidi nitakao toa Mbele ya Mahakama hii utakuwa ni Kweli, kweli tupu Eeh Mwenyezi Mungu Nisaidie

WS Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji nitamuongoza

Wakili wa Serikali: hebu rudia Majina yako

Shahidi: Naitwa Inspector Lugawa ISSA Maulid

Wakili wa Serikali: Unafanya Kazi gani

Shahidi: Ni Askari Polisi

Wakili wa Serikali: Kazi hizo za Uaskari Polisi unazifanyia Wapi?

Shahidi: Nazifanyia Kikosi cha Polisi Tazara Dar es Salaam

Wakili wa Serikali: Kikosi hiki kina husika na nini

Shahidi: Kinahusika na Usalama wa Mali zote zinazokuwa na Mamlaka ya Reli zinazomilikiwa na Mamlaka ya Reli ya Tanzania na Zambia

Wakili wa Serikali: Ambazo ni Mali gani

Shahidi: Majengo ya Mamlaka Ya Tazara, Mabehewa ya Mizigo na Abiria, Vichwa Vya Treni Pamoja na Miundo Mbinu na Raia..

Wakili wa Serikali: Kingine?

Shahidi: Kuzuia Uhalifu utakaotokea Pale, Ndani ya Mamlaka Ya Tazara

Wakili wa Serikali: Unaposema ndani ya Mamlaka Ya Eneo la Tazara Unamaanisha nini?

Shahidi: tunahusika zaidi Tazara, uhalifu unaofanyika ndani ya Treni, kwa Abiria na Majengo ya Tazara, NJE ya pale hatuhusiki

Wakili wa Serikali: Sasa umesema Upo Kikosi cha Polisi Tazara, Je Kituo chako Cha kazi ni Kipi?

Shahidi: Kituo cha Polisi Tazara, Pugu Road Kinachopatikana Tazara, Wilaya ya Temeke

Wakili wa Serikali: Kinaitwaj?

Shahidi: Kituo cha Polisi Tazara Pugu Road

Wakili wa Serikali: Una nafasi gani pale Kituo cha Tazara Pugu road

Shahidi: Kwa sasa ni kaimu Mkuu wa Kituo

Wakili wa Serikali: Eneo la kazi unaofanyika kazi linaukubwa gani

Shahidi: Kuanzia Dar es Salaam Mpaka Kisaki, Kilomita 223 ndiyo ninalohudumu Mimi

Wakili wa Serikali: Sasa Ukiwa Kaimu, Elezea Mahakamani Nafasi ya kaimu Mkuu wa Kituo umepata lini

Shahidi: Nimekabidhiwa Majukumu hayo Kuanzia Tarehe 03 June 2021

Wakili wa Serikali: Majukumu yako sasa Kama kaimu Mkuu wa Kituo cha Polisi Tazara ni nini?

Shahidi: yamegawanyika Sehemu Kuu tano

1.kusimamia nidhamu ya Askari ninao waongoza 2.Kusimamia Mpango Kazi wa Kituo

3.kuhakikisha Askari Wameingia Kazini kwa wakati kwa Maeneo Husika waliyopangiwa Kufanya Doria Maeneo yote ya Tazara

4.kusimamia na Kuzi Linda Mali zote za Serikali Yakiwemo Majengo, Magari ya Serikali, Office furniture pamoja na Silaha na Mali zingine zote

5.Kushughulikia Malalamiko yote yanayo fikishwa Kituoni, Ikiwemo Kufungua Kesi, Kupeleleza, na Kufikisha Mahakamani Watuhumiwa

6.Kuwasimamia Mahabusu Wote waliopo Kituoni Kwa Wakati huo Kuhakikisha wapo Salama Kiafya, Wamepata huduma za Chakula...

Wakili wa Serikali: Katika Jukumu la Kusimamia Mahabusu, Nini haswa ambacho wewe Unafanya

Shahidi: Kwa Mujibu wa Utaratibu kama Mkuu wa Kituo, Nikifika Kituoni cha Kwanza Naanza Kukagua Mahabusu kisha napitia REPORT BOOK Kuangalia Kesi zilozofunguliwa Kisha Nachukua Kitabu cha Detention Register Kuangalia Watu waliopo Mahabusu

Baada ya Kuchukua Detention Register, lazima niongozane Na Askari 1 au 2 Kutoka hapo CRO kwenda Mahabusu Kama Kuna Watuhumiwa Wa Kike nakuwa na Askari 1 wa kike na Wa kiume Na Fungua Detention Register Naanza Kuita Jina Moja Moja Ambao Wanakuwa wamo katika Kitabu Kile

Wakili wa Serikali: SUBIRI KWANZA JAJI ANAANDIKA

Shahidi: Ni kisha muita namuhoji Kosa linalo Mkabili alitaka, namuhoji tarehe ya Kuingia, baada ya Kumuhoji naenda Kwa Mtuhumiwa wa Pili

Wakili wa Serikali: TWENDE TARATIBU JAJI ANAANDIKA

Wakili wa Serikali: Umesema Kusimamia Mahabusu Unafanya nini

Shahidi: Kuhakikisha Hali zao Ki-Afaya, Wamepata Chakula kwa Wakati, na Status zao Kwa Ujumla

Wakili wa Serikali: Dhumuni ni nini?

Shahidi: Kutambua Reality ya Kinachofanana na Kwenye Detention Register

Wakili wa Serikali: Endelea Kueleza sasa

Shahidi: Baada ya Kukagua na Kujiridhisha nafunga ile Cello na Kurudi Charge Room Office nawakabidhi Ile Detention Register Kuendelea na Majukumu yao

Kama Upelelezi Haujakamilika Nawaamuru Waongeze Bidii kwa wakati Na Kama Upelelezi Haujakamilika na Makosa yanadhaminika basi Nawaamuru Mahabusu apewe Dhamana Hayo ndiyo Majukumu yangu ya Kila siku

Wakili wa Serikali: Malengo ya Kufanya Ukaguzi Mahabusu ni nini

Shahidi: Kuoanisha Taarifa za Report Book na Watu waliopo Kule Cello pia Kunirahisishia namna ya Kupanga Wapepelezi na Kama Wamekamilisha Upelelezi Nawaamuru Mtuhumiwa afikishwe Mahakamani Kwa Wakati

Wakili wa Serikali: Kwa Nafasi Yako ya Kaimu Mkuu wa Kituo Cha Tazara, Elezea ni Makosa gani ya Jinai Unayoshughulika nayo Kituo cha Polisi Tazara

Shahidi: Tunashughulika Makosa yote ya Jinai yatakayotokea Ndani ya eneo la Tazara

Wakili wa Serikali: Eneo la Tazara Unamaanisha nini?

Shahidi: Maeneo yote, (Within Compaund) kwenye Station Zake, Karakana zake na Ofisi zake

Wakili wa Serikali: Panapo Kituo cha Polisi Tazara, upo kwa Muda gani Mpaka Sasa

Shahidi: Mpaka Sasa nipo Kwa Miaka 17

Wakili wa Serikali: Ongeza Sauti.

Wakili wa Serikali: ulikuwa unatekeleza Majukumu Gani kama Operesheni Ofisa

Shahidi: Kuhakikisha Treni zote za Mizigo na Abiria Zinakuwa na Askari anayetembea na Treni, Kuhakikisha Doria zote zinazo takiwa kufanyika kwenye Reli ya Tazara Zina fanyika kwa wakati, Kupata Taarifa zote za Mahabusu

Wakili wa Serikali: Elezea Mwaka Jana Mwezi August 2020 katika Eneo lako la kazi

Shahidi: Nakumbuka Tarehe 03 August 2020, Ngoja Kidogo Mwezi May 10,2020 nilikuwa Operesheni Ofisa Wa Kituo Cha Polisi Tazara Nilikuwa nahudumu Kuanzia Dar es Salaam Mpaka Tunduma Kote

Vituo Vyote Kuanzia Tazara Dar es Salaam Mpaka Tunduma na nilipata Nampatia Mkuu wa Kikosi Kusimamia Mazoezi yote ya u tayari Kwa Askari

Wakili wa Serikali: Mazoezi ya Utayari Unamaanisha ni Yapi..?

Shahidi: parade na Medani za Kivita

Wakili wa Serikali: Unakumbuka Tarehe 03 ulikuwa unatekeleza Jukumu gani

Shahidi: Nakumbuka 03 August 2020 nilipewa Jukumu la kukaimu Ukuu Wa Kituo baada ya aliyekwepo Kwenda Likizo fupi ya Siku 28

Wakili wa Serikali: Baada ya Kupata hiyo Barua Tarehe hiyo Majukumu Yakianza Lini na Kuishia Lini

Shahidi: Kuanzia Tarehe 03 August 2020 Mpaka 06 September 2020

Wakili wa Serikali: Elezea hapa Mahakamani Kama Ulifanya Shughuli zinazohusu Mahabusu

Shahidi: Kama inavyopaswa na Mkuu wa Kituo, Nikifanya Ukaguzi Siku ya Tarehe 07, Mahabusu Yetu halikuwa na Mtuhumiwa Tarehe 08 Nikifanya Ukaguzi Kama Kawaida, Tarehe hiyo palikuwa na Mtuhumiwa Mmoja Mwanamume.

Wakili wa Serikali: Katika Kipindi Ulicho kuwa unakaimu Ukuubwa Kituo pale Tazara, Elezea Tarehe 07 Mpaka 09 August 2020 ulikuwa wapi

Shahidi: Nilikuwa kazini natekeleza Majukumu Yangu ya Kipolisi

Wakili wa Serikali: Wapi

Shahidi: Kituo Cha Polisi Tazara

Wakili wa Serikali: na Huyu Mkuu wa Kituo Cha a Polisi aliyekwepo na Kwenda Polisi anaitwa Nani

Shahidi: RICHARD OGUTU Superitendent wa Polisi

Wakili wa Serikali: Wakati Umekaimu ni Majukumu Gani ulikuwa unafanya

Shahidi: Yale Matano ya Awali

Wakili wa Serikali: Katika Kusimamia Mahabusu pale Kituoni ni Vitu gani mnafanya

Shahidi: Tuna Report Book, Tuna Detention Register Zinazotumika na Watuhumiwa Wote waliopo Mahabusu, na Tuna PPR ( Prisoner's property Report Book) Kitabu Kinachoonyesha Mali anazomiliki Mtuhumiwa

Wakili wa Serikali: Elezea Sasa Majukumu hayo Uliyo kaimu wakati Richard OGUTU ameenda Likizo yaliendelea Mpaka Lini

Shahidi: Yaliendelea Mpaka Tarehe 06 September 2020

Wakili wa Serikali: Siku hiyo nini Kilitokea

Shahidi: Alikuja Superitendent Richard OGUTU Nikamkabidhi Kituo chake

Wakili wa Serikali: Ulimkabidhi nini Na nini

Shahidi: Idadi ya silaha, Magari, Assets Kwa Maana ya Furnitures, Mahabusu wakiwa Salama, na Nyaraka zingine za Serikali

Wakili Serikali: Unasema Ulimkabidhi Mali kama Ulivyo orodhesha, Je Detention Register Ulifanyia nini

Shahidi: Detention Register ilikwepo CRO wakati wa Makabidhiano

Wakili wa Serikali: Alikuwa anatuhumiwa nini

Shahidi: Kujifanya Mtumishi wa Serikali

Shahidi: Tarehe 09 Palikuwa pana Watuhumiwa Wawili, Wanafunzi Wa Kiume, Ambao walikuwa Wanatuhumiwa Kuhatarisha Miundo Mbinu ya Reli, Tuliwakamata wakifungua Nati za Reli

Wakili wa Serikali: Ulibaini Vipi hao watuhumiwa

Shahidi: Kama Ilivyo Kawaida inapofika Asubuhi, Napitia Detention Register, na chukua Mtu wa CRO naenda Kufanya Check Up Mahabusu, kwa hilo niliwakauta Mahabusu

Wakili wa Serikali: Sasa Baada ya Kufanya Shughuli hiyo ya Ukaguzi wa Mahabusu, Wewe Unauthibitisho gani kama Watuhumiwa hao Walikwepo

Shahidi: Uthibitisho Mkubwa ni Detention Register ambayo pia Ilikuwa na Saini yangu baada ya Kufanya Ukaguzi

Wakili wa Serikali: Hiyo Detention Register Unavyosema Ndiyo Unauthibitisho huo, Wakati huo unakaimu ilikuwa inatunzwa Wapi

Shahidi: Kawaida huwa inatunzwa Charge Room Office, Kwa hiyo ilikuwa Charge Room Office

Wakili wa Serikali: Elezea Ni Kitu gani Kilitokea Baina yako na OGUTU

Kibatala: OBJECTION Mheshimiwa Jaji hatujasikia hayo

Jaji: hujasikia tarehe 03 Kibatala: Swali ni Leading

Wakili wa Serikali: Lini ukikabidhiwwa Majukumu hayo

SHAHIDI SP RICHARD OGUTU

Wakili wa Serikali: Makabidhiano hayo ya Majukumu yalifanyikaje

Shahidi: Kupitia Nyaraka Za Makabidhiano Wakili wa Serikali Katika Nyaraka hiyo ya Makabidhiano Mlikabidhiana nini

Shahidi: Nyaraka hiyo Ulionyesha Mali zilizopo Kituoni, Office Furniture, Mali zilipo Kituoni na Silaha, Nyaraka zingine Za Siri, Ikiwemo Nyaraka zilizo Kwishatumika ikiwepo Detention Register na Report Book

Wakili wa Serikali: ulijumuisha Detention Register zilizokwisha, Ni zipi hizo

Shahidi: Ikiwemo ile ya August 2020 ambayo nilikuwa nikikaimu Ukuu wa Kituo

Wakili wa Serikali: Baada ya Kukabidhiwa Detention Register iliyoisha, Uliyo itumia August 2020, Ulimpeleka wapi

Shahidi: Nilikuta Ikiwa imehifadhiwa Katika Ofisi yake

Wakili wa Serikali: Baada ya Tarehe 03 June 2021 ni lini tena Ulifanyika Kazi

Shahidi: Nakumbuka Tarehe 14 November 2021, alikuja Mtu Mmoja aliyejitambukisha kwamba ni Askari Polisi Kwa Jina la Inspector Swila, anatoka Ofisi Ya DCI

Wakili wa Serikali: alikuja wapi

Shahidi: Kituoni Tazara

Wakili wa Serikali: Saa ngapi!?

Shahidi: Majira ya Saa Tano, alifika Charge Room Office, akamuulizia Mkuu wa Kituo, Alikuja Askari Wa Charge Room Office akaniita kwamba nahitajika Chini kwamba Inspector Swila ananihitaji

Shahidi: Nikitoka Ofisini Kwangu Nikashuka Kwenda Chini Charge Room Office kwenda Kuonana naye ana kwa ana

Wakili wa Serikali: Baada ya Kuonana naye

Shahidi: akinihoji Kuhusu Detention Register Iliyotumika Mwezi August 2020

Wakili wa Serikali: Alikueleza ni ya Nini

Shahidi: Alinieleza Kwamba inahitajika Mahakamani Kwa ajili ya Ushahidi

Wakili wa Serikali: Wewe Ulifanya nini baada ya Kuwa Amekueleza hivyo

Shahidi: pale Ofisini Detention Register ilikuwa Mpya, Ile ambayo aliyokuwa anahitaji ilikuwa imeshatumika Mwisho Mwezi May, Kwa wakati huo haikuwepo pale Charge Room a office

Wakili wa Serikali: Ukafanya nini sasa

Shahidi: Nikamjulisha kwamba nitaitafuta Ofisini Kwangu kwenye Makabati ninayohifadhia Nyaraka Mbalimbali, yeye akaondoka Nikaenda Ofisni nikaikuta

Wakili wa Serikali: aliondoka kwenda wapi

Shahidi: Aliondoka Kituoni Miye nikarudi Ofisini kwenda Kuitafuta, nikaipata

Wakili wa Serikali: Ukakuta nini

Shahidi: Baada ya Kukagua nikamkuta Tarehe 06 na Tarehe 07 Hapakuwa na Mahabusu

Wakili wa Serikali: Sasa Hapa Mahakamani Pana Kesi na Nitakutajia Majina Uelezee Kama hizo Tarehe 7 na 8 kama yaliikuwepo Khalfani Bwire Adam Kasekwa Mohammed Ling'wenya

Shahidi: Kupitia Detention Register Majina hayo hayapo na Watuhumiwa hao hawakuwepo Kituoni Kwa Tarehe hizo Tajwa

Wakili wa Serikali: KWA SAUTI TAFADHALI

Shahidi: Kupitia Detention Register Majina hayo hayapo na Watuhumiwa hao hawakuwepo Kituoni Kwa Tarehe hizo Tajwa

Wakili wa Serikali: baada ya hapo Uliipeleka wapi?

Shahidi: Nilihifadhi na Mpaka Leo nimekuja nayo

Wakili wa Serikali: hiyo Detention Register Ilitumika Kipindi Gani?

Shahidi: Tangu January Mosi 2019 Mpaka Mwaka huu May 25

Wakili wa Serikali: na Hii Detention Register ambayo umekuwa ulielezea, Wewe Utaitambuaje

Shahidi: Detention Register Ina sehemu ya Nje na ya ndani kwa Sehemu ya Nje Nakumbuka tuliandika Kwa a maker Pen ya Blue Bahari WEF 01. 01 .2019 Chini kuna maandishi Madogo yameandikwa TANZANIA MINISTRY OF HOME AFFAIR TANZANIA POLICE FORCE na Maneno Madogo Sana ya PR20

Na Kwa ndani Inakuwa na Maandishi ya asomeka POL/TZR/PR/IR OR RB/MWAKA

Wakili wa Serikali: Kitu Kingine

Shahidi: Ni sahihi au Jina la Afisa aliye kagua Kipindi hicho

Wakili wa Serikali: Kitu gani Kina kuhusu Wewe

Shahidi: Kujua Idadi ya Polisi

Wakili wa Serikali: Katika Utambuzi wa hiyo Detention Register Kuna Kitu gani Kingine

Shahidi: Sahihi yangu, niliyo Saini Siku tofauti tofauti

Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji tunaomba Kumpatia Shahidi Kielelezo Kwa ajili ya Utambuzi

Jaji: Sawa

Wakili wa Serikali: Kitu gani Kingine

Shahidi: Kumbukumbu namba za Kesi zilizo andikwa kwa Kifupi P. O. L/TZR/PR na Zingine

Wakili wa Serikali: Ungependa Mahakama ifanye nini na hiyo Detention Register

Shahidi: Mahakama Ipokee Kama Kielelezo Katika Ushahidi Wangu

Wakili wa Serikali: Kama Umetambua hiyo ni Kitu gani

Shahidi: Hii ni Detention Register

Wakili wa Serikali:
Detention Register Ya wapi

Shahidi: Police Tazara, Pugu Road

Wakili wa Serikali: Umeitambuaje

Shahidi: Nimeitambua Kwa Maandishi Yalipo Nje

Wakili wa Serikali: Yataje

Shahidi: Maandishi ya Blue Bahari Tarehe 01.01 2019 ni Detention Register Inayomilikiwa na Jeshi la Polisi

Wakili wa Serikali: Umeitambuaje.

Shahidi: Ndani Kuna Sahihi yangu

Wakili wa Serikali: Kitu gani Kingine

Shahidi: Kumbukumbu namba za Kesi zilizo andikwa kwa Kifupi P. O. L/TZR/PR na Zingine

Wakili wa Serikali: Ungependa Mahakama ifanye nini na hiyo Detention Register

Shahidi: Mahakama Ipokee Kama Kielelezo Katika Ushahidi Wangu

Wakili wa Serikali: Tutajie Serial Namba

Mtobesya: OBJECTION amevuka mipaka yake

Wakili wa Serikali: Ulisema Mwanzo Kuna Vitu Vitavyofanya uitambue

Shahidi: Maandishi PF 20 MINISTRY OF HOME AFFAIR TANZANIA POLICE FORCE PF 20

Mawakili wa utetezi wanapelekewa nyaraka Wameizunguka Kwa pamoja, wanaifungua mbele nyuma kwa kasi, wanaigeuza geuza hapa, wanaangalia kwa mbali kidogo, Mtobesya anavaa miwani yake vizuri hapa Malya anachukua katarasi na Pen, Ku' Note Vitu Kibatala anafungua begi lake kubwa

Jaji: napokea kama Kielelezo p3 kwenye Kesi Ndogo Ndani ya Kesi kubwa ya Upande wa Mashtaka Mawakili Wa pande zote mbili wanakubaliana na Jaji kwa kusimama

Jaji: asome sehemu ambayo ni Relevant

Wakili wa Serikali: Soma Tarehe 8 na 9 ya August 2020

Shahidi: 08/8 palikuwa na Mtuhumiwa anaitwa Godfrey Kilimba anaishi Mbezi Juu, PPR 0627 aliingia 08/8 saa 5 na Nusu Usiku akatolewa Siku ya tarehe 10 August 2020, Saa 6 Na Dakika 45, NJE kwa Upelelezi

Shahidi: Tarehe 09 Palikuwa na Mtuhumiwa John Gerald, kabila Mfipa, Mwanamume Mwenye Afya Njema, Mwanafunzi wa Yombo Sekondari PIA palikuwa na Mtuhumiwa Lucas Jovin wa Miaka 12, alitoka tarehe 10

Wakili wa Serikali: Shahidi Nenda sasa Katika Kielelezo hicho Kwa Tarehe 7,8 na 9 ya Mwezi August 2020

Shahidi: Tarehe 7 Hakuna Mahabusu

Wakili wa Serikali: Sasa Mahabusu uliyemsoma kwenye Entry 257 Soma Jina lake na Tuhuma zake

Shahidi: Geoffrey Kilimba, kabila Mhaya

Wakili wa Serikali: Alikuwa na Tuhuma gani

Shahidi: Kujifanya Mtumishi Wa Serikali

Wakili wa Serikali: Kwenye Entry namba 258 ni nani

Shahidi: John Gerald, Kuhatarisha Miundo Mbinu ya Reli

Wakili wa Serikali: Tutajie pia na Entry namba 259

Shahidi: Lucas Jovin, Kuhatarisha Miundo Mbinu ya Reli

Wakili wa Serikali: Katika Eneo hilo Kuna kitu kinaonyesha kwamba Ulikagua

Shahidi: Kuna Saini yangu hapo ambayo nilikagua

Wakili wa Serikali: Kitabu hicho Kilitumika Kuanzia Lini hadi lini

Shahidi: Kuanzia 01.01.2019 Mpaka 29 May 2021 WS: Ahsante, ni hayo tu Mheshimiwa

Mtobesya anaenda Shahidi alipo

Mtobesya: naweza Kuendelea Mheshimiwa Jaji

Jaji: Sawa

Mtobesya: Shahidi Tusaidie Kwanza Unafahamu PGO ni Kitu gani

Shahidi: Kitabu cha Ufanyaji kazi na Taratibu za Polisi

Mtobesya: Nitakuwa Sahihi nikisema Kitabu hiki Kinakuhusu

Shahidi: Sahihi

Mtobesya: Kwa Mujibu wa Kifungu cha 353 cha PGO nani anatakiwa Kukagua Mahabusu

Shahidi: Kuna Makundi Manne, kuanzia Mkuu wa Kituo

Mtobesya: Kwa PGO gani

Shahidi: Hiyo kuanzia 353 nafikiri

Mtobesya: Nitakuwa sahihi Nikisema Kwamba Wakati Mwaka Jana unakagua wewe Hukuwa NCO

Shahidi: Ndiyo

Mtobesya: unafahamu Kitu kinaitwa OCCURANCE BOOK

Shahidi: Ndiyo

Mtobesya: Nitakuwa sahihi nikisema Kwamba Ukienda Kukagua Mahabusu Unatakiwa Kusaini Station Diary

Shahidi: Siyo kweli

Mtobesya: Na umesema Kwamba Unaifahamu PGO

Shahidi: Ndiyo

Mtobesya: Na Kwamba haina Matakwa hayo

Shahidi: Sikumbuki Kidogo

MTOBESYA: Mkuu wa Kituo, Kamanda wa Kikosi Waziri husika, Watu wa Haki za Binadamu... Je Charge Room Officer Harusiwi?

Shahidi: anaruhusiwa

Mtobesya: Kuna watu wa naitwa Wa naitwa NCO ni akina nani

Shahidi: Coplo, sergeant na sergeant Major

Mtobesya: Kwamba Kama Ungekuja na Station Diary ndiyo tungeamini Kwamba Ulikwepo Siku hiyo

Shahidi: Ndiyo

Mtobesya: Tungeona Saini yako

Shahidi: Mimi huwa si saini

Mtobesya: Lakini Unatakiwa Kusaini kuanzia Mkuu wa Kituo Mpaka Chini

Shahidi: Ndiyo Natakiwa kusaini

Jaji: Mmeniacha Kidogo Mlinzi kuwa mnazungumzia Prison Inspection hapa naona unazungumzia Prison Visit

Mtobesya: Kwenye PGO hawana Inspection Wanaita Prison Visit

Jaji: Ok Sawa!

Mtobesya: Shahidi Station Diary Inachukua Taarifa gani

Shahidi: Askari wanaoingia na kutoka Kazini

Mtobesya: Wakati Unatambua Kitabu Ulitaja WEF, Je Ulieleza hii WEF ni Kitu gani

Shahidi: Sikueleza

Mtobesya: Wakati Uliongozwa na Wakili Wa Serikali Robert Kidando, Ulielezea Kuhusu Hii namba Ilisha andikwa lakini ikaonekana Ikarudiwa..?

Shahidi: sikumueleza

Mtobesya: Nilisikia pia unasema Kwamba Ulikabidhiwa kituo na Mtu anaitwa Richard OGUTU

Shahidi: Ndiyo

Mtobesya: Mlikabidhiana Kwa maandishi

Shahidi: Hapana

Mtobesya: Ikitokea Detention Register Imeisha Muda wake Mnaiweka wapi

Shahidi: Ina chukuliwa kutoka Charge Room Office Kwenda Kwenye Cabinet Ofisi ya Mkuu wa Kituo

Mtobesya: Kwenye hizo Entry Mlinzi Shughulikia Mwisho Lini

Shahidi: Tarehe 10 September 2020

Mtobesya: Baada ya hapo Kitabu Kilibakia wapi

Shahidi: Charge Room Office

Mtobesya: Baada ya Kuliacha Mara ya Mwisho 6 September 2020 ulikiona tena lini

Shahidi: Sikukitumia Mpaka Leo

Mtobesya: Wakati Superitendent wa Polisi OGUTU anakukabidhi bila Maandishi nani alikuwa ana kihifadhi

Shahidi: Superitendent OGUTU

Mtobesya: Wakati Msomi Kaka Yangu Wakili wa Serikali Robert Kidando anakuongoza, ulitaja namba hapa, Je Ulieleza zipo wapi

Shahidi: Nilileza

Mtobesya: Ndiyo Record zinavyoonyesha?

Jaji: Ukisema Record wakati alikuwa aandiki inakuwa Ngumu kwake

Mtobesya: naomba Kurudia Swali

Mtobesya: Wakati pia Msomi Kaka Yangu Wakili wa Serikali Robert Kidando +anakuongoza, ulitaja namba hapa, Je Ulieleza zipo wapi

Shahidi: Nilisema Kitabu Kina Nje na Ndani

Mtobesya: Ulisema Kituo cha Polisi ambacho Kipo Pugu Road kina Abbreviation gani

Shahidi: P.O.L/TZR

Mtobesya: Hakuna Sehemu inaelekeza kwamba Kituo cha Polisi Tazara Kinatakiwa Kiitwe TPG?

Shahidi: sijui

Mtobesya: akitokea mtu akasema Kituo cha Polisi Tazara Kinatakiwa Kutamkwa kwa Kifupi cha TPG ni Muongo au Mkweli?

Shahidi: atakuwa Muongo

Mtobesya: nimemaliza

Mallya: We Shahidi Unajua Kwamba Ugaidi ni Makosa Serious

Shahidi: Ndiyo

Mallya: hii Serious Crime ni sahihi kwa Polisi Kui attend kwa dharula kabla haitatokea

Shahidi: Ndiyo inawezekana na Ndiyo kazi zetu

Mallya: Najua umesoma Polisi Moshi, au Popote nataka Kujua Kama Una elimu Nje ya Nchi

Shahidi: Hapana

Mallya: Ulishawahi Kusikia Kwamba Magaidi Wameng'oa Reli au Kufanya Ugaidi Kwenye Treni

Shahidi: Nimesikia Kupitia BBC huko Pakistan

Mallya: Kama nimekuelewa Kwamba Jambo Linashughulikiwa Tazara ndiyo linaonekana humu, Kama Jambo siyo la Tazara haliwezi Kuonekana humu

Shahidi: Ndiyo

Mallya: Uliulizwa Majukumu yako na Kaka yangu Kidando, Ukasema ni uhalifu ulikuwa Unafanyika ndani ya Treni na Sehemu zenu

Shahidi: Ndiyo

Mallya: Kuna Majukumu Mengine shahidi Ujayataja, Pale Inapotokea Kusaidia Jeshi la Polisi Namna Nyie Mnauwezo huo, Ni lazima Mtayafanya

Shahidi: Ndiyo

Mallya: Ikitokea Kwamba DCI anasema Kwamba ana dharula akaomba Watuhumiwa Wawekwe Pale Tazara Utakubali au utakataa, Pia, DCI anakusikia huko alipo..

Jaji: Sijui Kama tupo Live huko

Mallya: sijamaanisha hivyo Mh Jaji, Namsaidia Shahidi ajue baada ya Kesi Mambo yatakuwa wazi

Shahidi: Kwa Mamlaka ya DCI Vituo Vyote Vya Polisi Vipo Chini ya DCI, nitamkubalia with Condition

Mallya: Kuhusu Condition yako Mimi sina Interest nazo

Shahidi: Katika Condition nitakao Mpa DCI nitamwambia Kwamba DCI anipe Case number

Mallya: Kwenye Hii DR zinaingia Kesi za Tazara tu, Je utawaandika humu

Shahidi: Lazima niwaandike

Mallya: lakini Mwanzo Tumekubaliana Kinachoandikwa humu ni Tazara tu

Shahidi: atanipa IR za alikofungulia nayo case

Mallya: Kama atakupa..?

Shahidi: Nita andika, Kama hatonipa sitoandika

Mallya: naomba nipewe Kielelezo Cha P2

Mallya: Sasa Sisi tunafaida ya Kuwa na Detention Register mbili, Mwenzio Polisi alileta hapa na Bila shaka zinatakiwa kufanana

Shahidi: Ndiyo zinatakiwa Kufanana

Mallya: Sasa hii Detention Register Ya Central na Hii Detention Register Ya Kwako, Hazifanani kabisa hapa Juu

Shahidi: Kwenye nini

Mallya: Soma hapa Juu hii na hii, Ya Kwako ina WEF 20

WS Robert Kidando: OBJECTION. Mheshimiwa Jaji Wakili anachofanya anakiuka kaomba Kielelezo Ghafla anampatia Shahidi bila Kujenga Misingi

Jaji: Kuna Sheria Kavunja..?

WS Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji ataanza Chavula Kisha nitamalizia..

WS Abdallah Chavula: Mheshimiwa Jaji Tunauliza Maswali, pale ambapo hujasema ameshughulika Vipi, Swali atakalo Jibu ni Opinion na Huyu ni Shahidi Wa Fact huyu siyo Mtaalamu wa PGO Leo anakuja Kaimu Kituo unamwambia afanye Comparison, Siyo sahihi

WS Robert Kidando: Inatosha Mheshimiwa Jaji

Mallya: naona Mtobesya anataka Kunisaidia,

Mtobesya: Mimi ni Afisa wa Mahakama, natakiwa nisaidie Mahakama, Mheshimiwa Jaji Shahidi kaulizwa Kwamba Detention zinatakiwa zifanane akasema Ndiyo, Sasa wanataka Wakili alay foundation gani? Kama Maswali hayamvunjii Heshima Shahidi, Maswali Yanaruhusiwa!

Wakili Nashon Nkungu: Sijajua Hoja ya Kujenga Msingi Kwenye Cross Examination inatokea wapi, Nawakumbusha Wenzangu kwamba Hear Say ni Kutoka Third party, Sijaona hapo Third party inatoka wapi....

John Mallya: kwa Maneno Ya shahidi Kwamba hizi ni Polisi form, na imeingia kwenye Rekodi, Huenda Hoja yao ilikuwa ni Kunikatisha Mzuka wangu Ukatike....

Jaji: Niseme Jambo Moja kwamba Kielelezo Chochote Kinachotolewa Mbele ya Mahakama Kinaweza Kutumika na Kielelezo anachotumia ni Kielelezo P2

Jaji: Kwa hiyo, kwa namna hiyo alichofanya Bwana Mallya sijaona alipokesea, Isipokuwa Mr Mallya Shahidi alijibu ndiyo Jibu lake...

Wakili Mallya: Haya tuonyeshe Sasa

Shahidi: Katika Exhibit P2 Kuna

Mallya: Hapo WEF ipo au Haipo

Shahidi: Hapa Haipo

Mallya: hii Nyaraka Ya P3, umeleta wewe ina karatasi imeondolewa

Shahidi: Hapana

Shahidi: Ila inakaratasi imeunganishwa

Shahidi: Kimyaaaaaaaaaa

Mallya: Wakati Unaongozwa na Kaka yangu Kidando Ulieza Kwamba Kuna Karatasi Imeunganishwa?

Shahidi: Hapana Sikusema

Mallya: Muonyeshe au Msomee Mheshimiwa Jaji ni Entry ipi ambayo imeunganishwa

Shahidi: ni Entry namba 275 Mpaka 277

Mallya: Uliongozwa na kaka yangu Robert Kidando Ulisema Kwamba Mnashughulika na nini

Shahidi: Makosa yote ya Reli yatakayotokea Katika Mazingira yetu ya Tazara

Mallya: Mheshimiwa Jaji Ya kwangu ni hayo tu Anasimama wakili Fredrick Kihwelo

Fredrick: Ni sahihi Nafasi Uliyo nayo sasa ulikaimu 03/6/2021

Shahidi: Ndiyo

Fredrick Kihwelo Ni sahihi Kwamba Hujaonyesha Hapa Mahakamani Nyaraka Kwamba Ulikaimu nafasi hiyo

Shahidi: Ndiyo Sijaonyesha Nyaraka Yoyote

Fredrick Kihwelo: Ni sahihi Kwamba Unaonyesha Nyaraka Yoyote hapa Mahakamani Kwamba Wewe ni Askari polisi

Fredrick: ni sahihi wewe Kama Askari Polisi Unapokea Maelekezo Kutoka Juu yako

Shahidi: Ndiyo

Fredrick PGO ya ngapi

Shahidi: Sikumbuki, ila Ndiyo Utaratibu Kupokea Malekezo Kutoka Juu Kupeleka Chini

Shahidi: Nimeonyesha Detention Register na Pili Kiapo nilichoapa hapa Mahakamani

Fredrick Kihwelo: Kiapo ni Nyaraka

Shahidi Hapana, ila Nimeonyesha Detention Register

Fredrick Kihwelo: Ni sahihi Ulitembelewa Ofisini kwako na Inspector Swila

Shahidi: Ndiyo

Fredrick Kihwelo: Mwambie Mheshimiwa Jaji siku ambayo alikutembelea Inspector Swila ilikuwa siku gani..

Shahidi: Siku siwezi kukumbuka aisee!

Shahidi: Lakini Mpaka nikumbuke kwenye kalenda

Fredrick Kihwelo: Mimi nasema Ilikuwa Jumapili

Shahidi: Exactly..... ilikuwa Jumapili

Mahakama:Hahahaaaa

Fredrick Kihwelo: Nimesikia Kwamba Toka tarehe 06/9/2020, Leo ndiyo Mara ya Kwanza unaiona

Shahidi: Leo ndiyo nimewasilisha Mahakamani, nilitafuta Nikaipata Baada ya Kupata Maelezo kwa Inspector Swila...

Fredrick: Ukipewa Maagizo kutoka Kwa Mabosi zako Utatekeleza au Hautotekeleza

Shahidi: Nitatekeleza

Fredrick: Nitakuwa Sahihi nikisema kwamba Mnamo Mwaka 2020, 08/8/2020 ulipewa Maagizo ya Kuwahifadhi Watuhumiwa Adam Kasekwa na Mohamed Ling'wenya

Shahidi: Hapana Sikupewa

Fredrick Kihwelo Kwa hiyo Unafualta Neno kwamba Leo ndiyo umeona Mahakamani

Shahidi: Kimyaaaaaaaaaa

Fredrick Kihwelo: Nimesikia Kwamba Umesema Kuna Mshtakiwa alishitakiwa kwa kosa la Kujifanya ni Mtumishi wa Serikali

Shahidi: Ndiyo

Fredrick Kihwelo: Mwambie Mheshimiwa Jaji Kwamba Hilo lina husika Vipi na Masuala ya Tazara

Shahidi: Aliwaambia Askari Kwenye Treni kwamba yeye ni Kamishina wa Polisi, Wakamfuatilia wakagundua Siyo wakamleta Kituoni

Fredrick Kihwelo: Kwa hiyo Uliambiwa au ulishuhudia

Shahidi: Walimleta Kituoni

Fredrick Kihwelo: ni hayo tu Mheshimiwa Jaji

Kibatala: Mheshimiwa Jaji Kwakuwa Muda wetu wa Break Umekaribia, Basi naomba twende Break Kwanza

Jaji: itakuwa Muda gani

Kibatala: pia Mheshimiwa Jaji hata kama hapa hapa ndani Chini ya uangalizi wa Mahakama naomba Ruhusa ya Kukipitia Kielelezo p3

Jaji: Upande wa Serikali

WS Robert Kidando: Kwanza hakuna la Msingi ATAKALOGUNDUA, Suala la Kuomba Kielelezo ni Suala la Wakati wa Mahakama, Sioni kama ana sababu za Msingi

Jaji: ulitaka Kukiangalia Kwa Dakika Ngapi

Kibatala: hata 10, pia nilikuwa na Kuomba wewe siyo wao

Jaji: Sawa ila Mimi Ndiyo niliwapa nafasi wajibu, Basi nakupa Dakika 5 Mbele ya Afisa wa Mahakama..

Jaji: Tutarudi Saa 8 Kamili Jaji anatoka!

----------

Jaji amerejea

Mahakamani Kesi namba 16 ya Mwaka 2021 Khalfani Bwire, Adam Kasekwa, Mohammed Ling'wenya na Freeman Mbowe inatajwa tena

Wakili wa Serikali; Mheshimiwa Jaji Quorum yetu ipo Vilevile tupo tayari Kuendelea

Kibatala; pia Mheshimiwa Jaji Quorum yetu ipo Vilevile tupo tayari Kuendelea

Kibatala: Wakati Mawakili Wa Utetezi wanakuuliza Kuhusu Siku ya Inspector Swila Kuhusu Tarehe 14 November 2021 Ukasema Hukumbuki

Shahidi: Ndiyo sikumbuki

Kibatala: Ngoja Nikupe hiki kitu

Shahidi: hii ni kalenda

Kibatala: Kalenda ya Taasisi gani

Shahidi: Mahakama

WS Pius Hilla: OBJECTION. Shahidi anaonyeshwa Kitu ambacho hata sisi Mawakili hatujaona na Kuanza Kumuonyesha Shahidi

Kibatala: Kwa Heshima na Taadhima, Sijaona Hoja ya Msingi

Jaji: ni Sahihi Kumpatia Nyaraka Shahidi na Kuanza Kusoma, Ndiyo Hoja yake

Kibatala: Ndiyo hivyo sasa aniambie ni Sheria gani inakataza

Jaji: Mimi nafikiri hata Mahakama ingetaarifiwa ni Kitu gani iweze Ku' Note

Kibatala: Sawa Mheshimiwa Jaji nakubalina na hilo, Ngoja Niichukue nmpatie tena

Kibatala: Mheshimiwa Jaji Kwakuwa Shahidi aliulizwa Kuhusu Tarehe 14 November 2021 ni lini na Wakili Fredrick Kihwelo akasema hakumbuki Mpaka atizame kalenda, Hapa Mkononi ni kalenda nimeomba Ofisi ya Msajili Mahakama Mbayo Imetolewa na Mtendaji Mkuu wa Mahakama, Naomba Kuitumia

Kuuliza Swali Kwa Shahidi Kuhusiana Na Siku ya tarehe 14 November 2021

Jaji: naiomba Kwanza Huku,

Jaji: Upande Wa Mashtaka? Mawakili wa pande wa Mashitaka Wanaijadili Kidogo Wanaizunguka

WS Pius Hilla: hatuna pingamizi Na Shahidi Kuonyeshwa hii Nyaraka

Kibatala: Asante Mheshimiwa Jaji

Kibatala: Sasa Shahidi Nimeomba Ruhusa Mahakamani naomba uniambie Kwa Ushahidi Wako Siku ya tarehe 14 November 2021 kwamba ilikuwa Siku gani

Shahidi: Siku ya Jumapili

Kibatala: Kwamba Ilikuwa Majira ya Saa ngapi

Shahidi: Saa 5:30 Asubuhi

Kibatala: Wakati Unaongozwa na Wakili Msomi Mr. Robert Kidando, Uiliiambia Mahakama au Jaji Kwamba Mimi huwa nafanya kazi Siku ya Jumapili?

Shahidi: Katika Majukumu yangu Nilisema Kwamba Mimi Kama Mkuu wa Kituo Natakiwa Kufika Kituoni Siku zote

Kibatala: Ulitaja Neno Jumapili au Hukutaja

Shahidi: Sikutaja

Kibatala: Mtu akifika Tazara Kama anataka Kumuona Mkuu wa Kituo

Shahidi: Utafika CRO Kuna Mambo Mawili Kama Shida ya Ofisi Utaruhusiwa Kuniona.

Kibatala: Kama Shida ya Kiofisi naruhusiwa Kuja Ofisini kwako?

Shahidi: ndiyo

Kibatala: Na Inspector Swila ilikuwa Kwa shida ya Kiofisi

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: Basi nahama hapo, Inspector Swila alikwambia nini

Shahidi: Kwamba Kuna Complains zimejitokeza Kwenye kesi ya Mheshimiwa Mbowe na Kwamba Mimi Kama MKuu wa Kituo natatakiwa Kuja Kutoa Ushahidi

Kibatala: kwa hiyo Swila kwambia Kwamba Detention Register Inahitajika

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: Kwa hiyo Wewe tangu Siku hiyo ulikuwa unajua Unakuja na Kithibiti kuja Kutoa Ushahidi

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: Kwamba Bila Swila Leo hii Usingekuwa Mahakamani Kutoa Ushahidi

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: Inspector Swila alikwambia anatoka wapi

Shahidi: Ofisi ya DCI

Kibatala: DCI yupi?

Shahidi: Camilius Wambura

Kibatala: Inspector Swila alikupa Barua Kwamba Detention Register

Shahidi: Hapana

Kibatala: Unafahamu Kitu kinaitwa Chain of Custody katika Kuchukua Vielelezo

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: Kwa hiyo kuna sehemu umeandika unachukua Kielelezo

Shahidi: Kwa cheo, nafasi na majukumu yangu naweza kuchukua kielelezo chochote wakati wowote

Kibatala: kwani shahidi vielelezo vinatolewa kwa mujibu wa sheria au kwa namna mnavyotaka?

Shahidi: Kwa mujibu wa sheria

Kibatala: PGO hiyo hapo nionyeshe sehemu kama Kuna kifungu chochote kinachokuruhusu wewe kama Afisa wa Polisi kuchukua kielelezo (Detention Register) bila kusaini kwenye Exhibit Register

Shahidi: Mimi sifahamu

Kibatala: Wakati Unaitoa Detention Register Ulishafahamu tangu tarehe 14 November kwamba Itatumika kama Kielelezo Cha Ushahidi?

Shahidi: Naomba Kuku Jibu Kwa Ufahamu wangu, Kwamba Detention Register Ilikuwa Imeshatumika na Baada ya Miaka 03 tutafanya Disposal

Kibatala: Nikumbushe tafadhali Afisa wa Polisi Anafanya kazi Kwa Kuongozwa na PGO au Kwa Utashi wake

Shahidi: Kwa Kuongozwa na PGO

Kibatala: Hivi Vituo Vya Polisi Vinafanyiwa Ukaguzi?

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: OCD wa Temeke anaweza kwenda Kufanya Inspection Tazara?

Jaji: Tazara inajitegemea kwa Maelezo yake

Kibatala: Sawa, Ngoja Nibadili swali, Je Kamanda wako wa Vikosi wa Tazara anaweza Kufanya Ukaguzi wa Ghafla Kituoni kwako?

Shahidi: anaweza

Kibatala: je akija sasa Kwenye Ukaguzi atajua Kidhibiti Kipo wapi?

Shahidi: Mimi kabla sijatoka au Kufanya Jambo lazima nimuarifu Mkuu wangu

Kibatala: Hapo Swali Je wakati Uliongozwa na Wakili Wa Serikali Robert Kidando, Ulizungumzia Kuhusu Kumtaarifu Mkuu wako wa Vikosi?

Shahidi: Hapana Sikusema

Kibatala: Je Boss Wako anayefuatia anaruhusiwa na Yeye Kwenda Kufanya Ukaguzi?

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: akienda atajua kwa Maandishi Kwamba Kielelezo Kimeenda wapi

Shahidi: atanisubiri Mpaka nirudi..
Yaani mpaka wewe urudi ndio Boss ajue cha kufanya
 
Yaani tangu mlolongo wa kesi uanze sijaona shahidi hata mmoja aliyethibitisha namna ugaidi ungefanywa
Ni kweli bado kesi inaonekana kama vile kitu cha kufikirika kuliko uhalisia, Sasa wangeondoka huko kwenye hilo dude lililokama set up au flaming kama wahusika wanavyodai Sasa waanze kutuletea fact za ugaidi maana ndo kitu wengi tunasubiri.
 
Haa Mawakili wa Mbowe"wamesomea" kazi yao, Mtobesya yuko smart! Jaji anaongozwa na Mtobesya!!

Kuna wakati Jaji anavaa jezi lakini vibendera wanamvua na kumpa joho lake kwa lazima...naona kwa mbali na hukumu itakuwa na mauzauza kama tunavyoona kwenye tamthilia pendwa
 
Kibatala: Cheo chako wewe ni nani?

Shahidi: Inspector Wa Polisi

Kibatala: Kwenye Mambo yenu Iliandikwa A! inspector Maana yake nini?

Shahidi: kimyaaaa

Kibatala: Mwaka Jana ulikuwa nani vile?

Shahidi: Inspector

Kibatala: na Mwaka huu ni Inspector eeh?

Kibatala: nimekuuliza Mwanzo KUWA Mwaka Jana ulikuwa nani Ukajibu ni Inspector hapa Umejaza in Assistant Inspector Je Ulimwambia Mheshimiwa Jaji?

Shahidi: Sikufafanua
kimeumana.🤣🤣🤣🤣
 
Back
Top Bottom