Yaliyojiri Harambee ya CHADEMA live ITV - Oktoba 31, 2014

Yaliyojiri Harambee ya CHADEMA live ITV - Oktoba 31, 2014

Ndesamburo amechanga sh. ngapi? Ndesamburo kwenye harambee ya M4C iliyopita alichanga pesa zake Lema akaenda kufanyia ubakaji London.
 
Hotuba ya mbowe inaonyesha kuwa hana elimu..hakuna tangible issues

Nakushangaa ww mwenye elimu uko mbele kutetea upumbavu unaofanywa na ccm hapo ww ndo utakua zero kabisa we need changes ili watu wajifunze sio mnawapa vibur tu kama nchi ni yakwao peke yao wanafanya wanavyotaka but no action
 
Gharama inayotumika kurusha matangazo ya chadema itv na vyombo vingine vya habari kwa saa moja ni sawa na kununa madawa ktk hospitali za rufaa na wilaya kote nchini. Ni sawa na kujenga shule 20 za sekondari kusomesha yatima na maskini nchini, je chadema haina uchungu kwa watz wanaokosa elimu kwa kukosa shule? Wanaokufa kwa kukosa madawa? Kweli hii ni timu madaraka

Billion 90 za MSD zimeenda wapi. We nawe uwage unawaza kabla kuropoka
 
Tatizo siyo kuchangia tatizo ni jinsi gani fedha hizo zitatumika! Maana hawa CDM ni wajanja wajanja sana maneno mengi kumbe wanalao jambo!

Tupeni mrejesho wa harambee za nyumba kwanza then tuanze kuchangia!
 
Mimi siyo mpenzi wa chama chochote ila nimejikuta nanogewa na program ya leo ya uchangiaji,swali langu ni je huu mchango na program kwa ujumla ni ya CHADEMA AU UKAWA.nauliza kwa sababu kwenye hotuba inatajwa UKAWA lakini Nembo iliyoonyeshwa kwenye runinga ni ya CHADEMA.Je hii haiwezi kuwafanya CUF na NLD kuona wamemezwa na CHADEMA?.Nauliza kwa nia njema msinitukane tafadhali maana humu uchelewi kurushiwa makonde.

Pamoja nakutiliana Saini ya Ushirikiano lkn pia wamekubaliana kila chama kijijenge kitengeneza BASE,,kwasababu ktkt umoja huo chama kitaungwa mkono na UKAWA pale itapoonekana chama hucka kina nguvu kwenye Eneo hilo so hata kwenye kutafuta Pesa za Kampeni ya UKAWA nadhani kila chama kitawajibika
 
Tuache ubahili kwa kuchangia m4c maana tunahitaji ukombozi ambao unahitaji gharama kutoka mkoloni mweusi.
Tukishinda shule nyingi zitajengwa na elimu bora itatolewa tusiangalie gharama iliyotumika kurusha matangazo. Tuangalie faida yake (the effect) ya kurusha matangazo. m4c pqmoja daima. people' power.
 
Anajichanganya kwa kusema waasisi wametoka kona zote za Tanzania na hivyo si chama cha kaskazini? Mbona hajatuambia kwa nini wenyeviti wote ni wachagga?

Hivi pia Bob Makani kumbe naye ni mchaga eeeh?
 
Gharama inayotumika kurusha matangazo ya chadema itv na vyombo vingine vya habari kwa saa moja ni sawa na kununa madawa ktk hospitali za rufaa na wilaya kote nchini. Ni sawa na kujenga shule 20 za sekondari kusomesha yatima na maskini nchini, je chadema haina uchungu kwa watz wanaokosa elimu kwa kukosa shule? Wanaokufa kwa kukosa madawa? Kweli hii ni timu madaraka

wajinga hawataisha. hivi chadema ni serikali?kama ccm imeshindwa kufanya hayo mambo wakiwa serikalini kwanini tuwape kura kama serikali wanazidiwa na chama kimoja cha upinzani tena kinachoendeshwa kwa ruzuku na michango ya wananchi ndo ujiulize kodi zetu zinaenda wapi.
 
Ahsante kwa taarifa nimechangia Tsh 10,000/-

Kutoa ni MOYO, Usambe ni UTAJIRI
 
Back
Top Bottom