X Boyfriend anataka kumuoa wifi yangu

X Boyfriend anataka kumuoa wifi yangu

Wazima wapendwa, jamani X boyfriend wangu anataka kumuoa wifi yangu, walikkutana vp sifaham, wana uhusiano mda gani sifaham lakini juzi ndio tumetabulishwa rasmi nikiangalia mgeni ni Xboyfriend bado kidogo nizimie maana nilijikaza tu jamani mume wangu akijua yule alikuwa x wangu itakuwaje? vp nimwambie wifi yangu kama jamaa alikuwa x? ama kweli bongo kijiji sikulitegemea hili kabisa. Naombeni mawazo yenu naona huu mtihani utakuja kunikorofisha na familia mbeleni japo sina wazo wala siwezi kudate tena na huyo X na wala hatukuwa na mawasiliano kwa almost 6 yrs.

nakushauri usimwambie mumeo kwan kwa vyovyote vile hatakuwa na iman na wewe kila mara utapokuwa upo karibu na huyo jamaa na ndoa utaanza kuiona chungu na wifi akijua uliwah kudo na mumewe hapo ndo balaa na undugu unakufa.mi naona panga cku tena mapema onana na x wako mwambie kama mnaamua kuwa cool iwe hivyo manake we unaweza kaa kimya mwenzio akaropoka na hao ndugu wakisema ila nyie wahusika mlichokipanga kiwe msimamo mfano mnaweza amua wewe ukamwambia mumeo huyu kaka na x wangu walikuwa pete na kidole hadi ikafikia hatua watu walikuwa hawajui nani nado nae na upande wa pili akiulizwa msipishane maneno hapo mtajenga undugu wewe na wifi yako mmeo na x wako bila hivyo kwa kuwa wengi wanaamin x huwa anakula hamtaaminiwa na yeyote hata familia nzima ya wifio.
 
Ex kumuoa wifi yako hayakuhusu. Just to be on the safe side mwambie mume wako akae akijua. As for wifi, huna haja ya kumwambia, mtu wake atamwambia mwenyewe akiona kuna umuhimu wa yeye kujua.
Because he was your ex and he is now part of the family ni bora ku-avoid kua nae karibu, kuzungumza nae in private na mengine kama hayo. Soon utasahau kua mliwahi ku-date.
Thanx, nimeupenda huu ushauri ingawa sijui mumewe atamchukuliaje huyo jamaa baada ya kuingia kwenye hiyo familia. Kama hatakuwa na upeo wa kufikiria sawa sawa kuna hatari ya kuja kuhisi anaibiwa huko baadaye. Kuna kesi moja iliwahi kutokea inafanana na hii, na iliishia kuwa na ugomvi wa mara kwa mara kwenye familia ya yule dada baada ya kutoa hiyo siri. Ila for now, bado naunga mkono haya mawazo yako Roulette.
 
Last edited by a moderator:
Wazima wapendwa, jamani X boyfriend wangu anataka kumuoa wifi yangu, walikkutana vp sifaham, wana uhusiano mda gani sifaham lakini juzi ndio tumetabulishwa rasmi nikiangalia mgeni ni Xboyfriend bado kidogo nizimie maana nilijikaza tu jamani mume wangu akijua yule alikuwa x wangu itakuwaje? vp nimwambie wifi yangu kama jamaa alikuwa x? ama kweli bongo kijiji sikulitegemea hili kabisa. Naombeni mawazo yenu naona huu mtihani utakuja kunikorofisha na familia mbeleni japo sina wazo wala siwezi kudate tena na huyo X na wala hatukuwa na mawasiliano kwa almost 6 yrs.


We ka ulijipaka Hertz Tomato Ketchup, ukamdanganya bado uko sealed, unalo.
 
Wazima wapendwa, jamani X boyfriend wangu anataka kumuoa wifi yangu, walikkutana vp sifaham, wana uhusiano mda gani sifaham lakini juzi ndio tumetabulishwa rasmi nikiangalia mgeni ni Xboyfriend bado kidogo nizimie maana nilijikaza tu jamani mume wangu akijua yule alikuwa x wangu itakuwaje? vp nimwambie wifi yangu kama jamaa alikuwa x? ama kweli bongo kijiji sikulitegemea hili kabisa. Naombeni mawazo yenu naona huu mtihani utakuja kunikorofisha na familia mbeleni japo sina wazo wala siwezi kudate tena na huyo X na wala hatukuwa na mawasiliano kwa almost 6 yrs.
Kama huna wazo la Kudate nae tena wasiwasi wako ni nini?
 
Tatizo lako nini? Si umesema ni X au ulimdanganya husband wako kuwa hukuwahi kukutana na mwanaume, lakini pia kama bikira hakuiondoa yeye basi usiwe na wasiwasi.
 
ahsante mamaaaa muzuriiiiii...........kuwa muwazi ndio turufu pekee iliyobaki katika hizi vurugu za kimapenzi, i concluded!!!!

Wanaume wengine wanasababisha wapenzi wao wasiwe wawazi katika mahusiano yaliyopita au majanga wanayokutana nayo. Kuna rafiki yangu mmoja baada ya kumpata mpenzi wake ambaye ni mme sasa alijitahidi kuweka mambo yake wazi ili yasije leta shida siku za mbeleni. Historia ile aliyoweka wazi imekuwa fimbo kwa mme kila wanapishana kiswahili katika maisha yao ya ndoa. Mara ndiyo maana x bf wako alikuacha mara tabia yako siyo nzuri ndiyo maana fulani alikutenda hivi.

Kwa hali hii watu uwazi kwa wenzi wao unaleta shida siku za mbeleni kama utakutana na mtu hasiyeelewa.
 
Wanaume wengine wanasababisha wapenzi wao wasiwe wawazi katika mahusiano yaliyopita au majanga wanayokutana nayo. Kuna rafiki yangu mmoja baada ya kumpata mpenzi wake ambaye ni mme sasa alijitahidi kuweka mambo yake wazi ili yasije leta shida siku za mbeleni. Historia ile aliyoweka wazi imekuwa fimbo kwa mme kila wanapishana kiswahili katika maisha yao ya ndoa. Mara ndiyo maana x bf wako alikuacha mara tabia yako siyo nzuri ndiyo maana fulani alikutenda hivi.

Kwa hali hii watu uwazi kwa wenzi wao unaleta shida siku za mbeleni kama utakutana na mtu hasiyeelewa.

Asante kaka mkubwa well said
 
Wazima wapendwa, jamani X boyfriend wangu anataka kumuoa wifi yangu, walikkutana vp sifaham, wana uhusiano mda gani sifaham lakini juzi ndio tumetabulishwa rasmi nikiangalia mgeni ni Xboyfriend bado kidogo nizimie maana nilijikaza tu jamani mume wangu akijua yule alikuwa x wangu itakuwaje? vp nimwambie wifi yangu kama jamaa alikuwa x? ama kweli bongo kijiji sikulitegemea hili kabisa. Naombeni mawazo yenu naona huu mtihani utakuja kunikorofisha na familia mbeleni japo sina wazo wala siwezi kudate tena na huyo X na wala hatukuwa na mawasiliano kwa almost 6 yrs.

Ukome nani alikuambia ugawe mbunye yako kabla ya kuolewa.K yako ilikuwa ni kwa ajili ya mumewe tu na si mtu mwingine.Ngoja mumewe akijua utaipata fresh na lazima ajue maana siku wifi yako akimpa jamaa dozi safi huenda akaweka mambo hadharani.Ndio ukome na iwe fundisho kwa vicheche wengine wanaogawa mbunye zao kama pipi.
 
.....wewe ndo unamjua mume wako kuliko mtu yoyote hapa. Inawezekana kumwambia kukaharibu ndoa yako kabisa ( wengine wana wivu mbaya sana), maana jamaa anaweza kuwaza mengi na anaweza asikuamini tena (saikolojia zetu na ulewa umetofautiana sana).
.....Inawezekana ukimwambia mumeo, then atamwambia dada yake na familia ikalijua hilo, ndio ni past ila hisia na uelewa wetu unatofautiana., kumbuka ni X ila leo yuko na mdogo wa mumeo.
.....Kosa hapo ni kutoambiana mambo yenu yaliyopita, sasa akija jua patachimbika, that's for sure.
 
Pole sana dada yangu, Kwa mawazo yangu mimi, ingekuwa ni bora ukamwambia tu mmeo na wala sio wifi yako, ila inategemea na upeo na uelewa wake kuhusu mambo ya mapenzi na historia yake kwa ujumla kuhusu mapenzi kabla ya kuingia katika ndoa.
Kwa ufupi ni vijana wachache sana wake kwa waume ambao huingia ktk ndoa wakiwa hawajaguswa(mabikira either wa kiume au wakike). Kwani wengi wao huanza haya mambo ya kuwa na ma-boy friends na ma-friends mapema na pengine unakuta mtu anaweza kuwa na x-boys hata 10 au ma x-girls kwa idadi hiyo hiyo.

Na siku zote na sio sheria kwamba kila mtu unayekuwa nae wakati huo anaweza kuwa mke au mmeo, kwani mnaweza kuwa ni katika ile hali ya kufurahishana tu na kupeana-company kwa muda husika. Hivyo dada yangu nikirudi kwako , kilichotokea hapo ni bahati mbaya tu ,kwa huyo x-boy wako kuja kutaka kumchumbia wifi yako.

Lakini pia kwa mtazamo wangu sio vizuri wifi yako kumjulisha , ila kaa kitako na mume mweleze kwa kina kuhusu huyo jamaa, na mwambie kwamba huna mpango nae kabisa kwani ni miaka 6 imepita toka uachane nae.Na kama kweli mume anakupenda kwa dhati sidhani kama kutakuwa na tatizo , kwani hata kama ulikuwa na boy friends wengi wakati huo (kwani siku zote hata kufikia katika kuoana lazima watu wapitie mchakato wa b&f friend kwanza na wewe ulikuwa unatafuta Mr Right katika hao lkn haikuwa ridhiki mpaka ukampta yeye) cha muhimu sasa ni kwamba uko na yeye na yeye ndio wako wakufa na kuzikana wala nyuma hugeuki tena.


Pia inabidii huyo x-wako usiwe na ukaribu nae kabisa zaidi ya salamu tu hakuna biashara nyingine,
 
Nafikiri hakuna haja ya kumwambia maana itakuwa ni sawa na kuamsha maiti, ila hapo kwenye red ndio muhimu.
Bora amwambie mume wake. Asipo mwambia na baadae mume akaja kugundua anaweza kusema maybe she hid it from him sababu waliendelea. bora amwambie tu.
 
Me nataka kujua baada ya huyo EX kumuoa wifi yako (dada wa mume wako) mtakuwa mnaishi karibu au mbalimbali? Japo jambo hili hujalizungumzia lkn ni la muhimu sana. Kama baada ya ndoa yao wanaenda kuishi mbali mf. mkoa mwingine na unaoishi wewe na mumeo hapo sioni kama kutakuwa na tatizo ukimwambia mumeo kuhusu uhusiano wako na huyo X. Ila kama mtaishi karibu baada ya hiyo ndoa hapo ukimpa tu taarifa mumeo ugomvi lazima uibuke. Mumeo hatakuwa na imani na wewe wala huyo X wako maana cku nyingine X wako anaweza kukutembelea ghafla na wewe hutaweza kumfukuza, hapo mume wako atahisi bado mnaendelea na uhusiano wa kimapenzi hata kama sio kweli. Kingine wewe ndio unayejua tabia ya huyo X wako, pengine mliachana wakati bado mnapendana au (samahani lkn) pengine huyo X ni fundi kitandani kuliko mumeo we unafikiri utaweza kumkwepa? Hapa siri unayo mwenyewe moyoni. Huo ni mtazamo wangu lkn, kila m2 ana namna ya kulipokea jambo ila KAMA MIMI NDIO NINGEKUWA MUMEO HALAFU UNANIPA HIZO HABARI WALA NISINGEKUBALI HUYO MWANAUME AMUOE DADA YANGU. NINGEONA DHARAU YAANI JAMAA ANAKUFAHAMU UNDANI WA MWILI WAKO HLF NA DADA YANGU PIA IWE HIVYO HIVYO. Ningehakikisha ndoa haifungwi hapo.
 
Because he was your ex and he is now part of the family .

Dah!!...
I can only imagine how crappy this can feel [lol...I dont speak for all men]
Ila nita-mind sana kila nikimuangalia jamaa na kukumbuka kuwa amekula mke wangu na dadangu pia...sad😡
 
kuwa muwazi mapema. dont wait when it comes to too late...
 
Wanaume wengine wanasababisha wapenzi wao wasiwe wawazi katika mahusiano yaliyopita au majanga wanayokutana nayo. Kuna rafiki yangu mmoja baada ya kumpata mpenzi wake ambaye ni mme sasa alijitahidi kuweka mambo yake wazi ili yasije leta shida siku za mbeleni. Historia ile aliyoweka wazi imekuwa fimbo kwa mme kila wanapishana kiswahili katika maisha yao ya ndoa. Mara ndiyo maana x bf wako alikuacha mara tabia yako siyo nzuri ndiyo maana fulani alikutenda hivi.

Kwa hali hii watu uwazi kwa wenzi wao unaleta shida siku za mbeleni kama utakutana na mtu hasiyeelewa.

kweli kabisa, nimekuelewa sana.....ila uwazi bado ni nguzo kuu ya mahusiano, jukumu la kila mpenzi kuangalia aina ya mpenzi awake maana kweli kuna wengine ukiwaambia ukweli ndio umeharibu kabisa
 
Back
Top Bottom