X Boyfriend anataka kumuoa wifi yangu

X Boyfriend anataka kumuoa wifi yangu

hayo sasa matusi, mie nimeolewa na naheshimu ndoa yangu sana, ningekuwa wa kugegedwa nao ndani ya hiyo miaka 6 tungeshatafutana, asante kwa ushauri

USHAURI MKUU
fanya yafuatayo,
1.mwombe Mungu akusaidie kulishinda jaribu lililombele yako.
2.Si mweleze mume wako ukweli wote wala usiogope kuachwa na Mumeo wakati unapo ueleza ukweli,
3. Jitahidi kutokuwa nakumbukumbu yoyote juu yake na msahau kiakili, muone kama ndugu yako nasi x wako.
4. Usimpe nafasi nyingine hasa ya kukaanaye karibu muda wowote mtakapo kutana mkiwa wawili tu.
5. Jitahidi kutokuwa na hisia zozote juu yake.
6. Mwamini mumeo sana na zidisha mapenzi kwa mumeo.
7. Ipende sana familia yako kuliko kitu kingine.
8. Zungumza na wifi yako kwa karibu zaidi na mfanye kuwa dada yako wa damu nasi wifi yako kimtazamo. Ili x wako awe shemeji yako kwa dada yako wa damu kimtazamo.
9. Zingatia ratiba yako na usiache kutekeleza hata moja ndani ya ratiba yako.
10. Mwamini mungu. Na epuka ushauri mbaya wa marafiki.
 
tatizo si kusema ukweli ila umeshafikiria ni nini kitafuata baada ya wewe kuongea uo ukweli....ninacho ona apa ukweli wako utakua kwa lengo la kubomoa na si kujenga ata kidogo.

Hahahahahahahaha
 
Wazima wapendwa, jamani X boyfriend wangu anataka kumuoa wifi yangu, walikkutana vp sifaham, wana uhusiano mda gani sifaham lakini juzi ndio tumetabulishwa rasmi nikiangalia mgeni ni Xboyfriend bado kidogo nizimie maana nilijikaza tu jamani mume wangu akijua yule alikuwa x wangu itakuwaje? vp nimwambie wifi yangu kama jamaa alikuwa x? ama kweli bongo kijiji sikulitegemea hili kabisa. Naombeni mawazo yenu naona huu mtihani utakuja kunikorofisha na familia mbeleni japo sina wazo wala siwezi kudate tena na huyo X na wala hatukuwa na mawasiliano kwa almost 6 yrs.

we c umeshaolewa,wataka nn tena mpenz?au bado unampenda
 
Pole sana inaonesha upo obsessed na huyo jamaa na yeye alilitambua hilo akaamua kukukomoa kabisa!
 
Huo ni utata mkubwa....

Ukiweza mwambie huyo x asije kumwambia wifi yako kwamba uliwahi kungonoka naye....

Inahitaji busara sana kwa pande zote (mumeo na wifi yako) kuelewa kwamba hamko tena na uhusiano maana mumeo anaweza kufikiria kwamba wewe umekuwa na mawasiliano naye na ukaona umuunganishie na wifi yako kabisa....,
naima79 labda kama ulishawahi kumweleza mumeo na kumtajia jina la mtu wako huyo wa zamani, basi si vibaya ukashauriana naye namna ya kulishughulikia suala hilo maana na wifi yako akijua kwamba alikuwa wa kwako kutatokea ufa (mpasuko) mkubwa katika hiyo familia.

Ila chunga tu maneno yasemwayo kwamba mahawara hawaachani..., kuna hatari kubwa naiona kwamba mtajikuta mnakumbushia..................
 
Last edited by a moderator:
The past is the past...., waambie wote kwamba yule alikuwa rafiki yako wa karibu.., hatua watakayochukua ni wao wenyewe...

Hata kama ingekuwa ni kosa (kumbuka ku-date mtu sio kosa) huwezi kuhukumiwa kwa kitendo kilichotendeka huko nyuma, ukizingatia kitendo chenyewe sio kosa.., ila kuficha ficha inaweza kuleta picha kwamba unaficha maovu / au ulifanya maovu
 
Back
Top Bottom