Wizi wa magari Dodoma

Wizi wa magari Dodoma

Dawa yao ni hii
IMG-20200324-WA0001.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 

Muda huo washakupulizia dawa za usingizi au wamekufungia
Jaribuni kuwa wabunifu. Ukiachana na njia official kama za kuweka alarm, tracking devices etc fanya ujanja wa kuzaliwa. Sehemu unapolaza gari isiwe mbali na dirisha la chumba unacholala, halafu tafuta nguzo ya chuma ndefu eg taruma la reli. Ichimbie chini kama unavyosimika nguzo za umeme , lakini iingie ardhini karibu yote na uache ichomoze kwa juu kama futi moja tu. Imarisha na sementi ikiwezekana. Kwa juu ya nguzo chomelea sehemu ya kuweka mnyororo. Wakati wa kuilaza gari isogeze gari mpaka isimame juu ya nguzo (nguzo iwe imechomoza kwenye uvungu wa gari). Kisha tumia mnyororo wa chuma imara, ingia uvunguni wa gari na kufunga eg diff ya gari kwenye nguzo kwa kofuli kubwa na imara. Wezi watakapokuja hawatajua kuwa kuna kikwazo cha aina hiyo. Wakiwasha gari na kujaribu kuliondoa halitasogea. Fanya ubunifu zaidi kwa kuunganisha huo mnyororo na taa na spika zilizofichwa sehemu. Spika unganisha na kinasa sauti utakachorekodi sauti. Wezi watakaposogeza gari likivuta ule mnyororo taa ziwake ziwamulike huku spika ikipiga kelele ''ua, washenzi hawa'' ua wezi hawa''

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mnaozungumzia relay sijui kma mnaijua inavyofanya kazi au la, relay ni switch ambayo inategemea, zipo zibazokua On zikipokea umeme na zipo zinazokua Off zikipokea umeme, ni rahisi sana mtu ku-improvise akiwa anafahau. Kuhusu fuse ndo msijisumbue kabisa. Mana ni kujua tu fuse ya power ni ipi kisha unachomeka waya mdogo unaounganisha kitu kimejipa. Hii tumeifanya sana garage, umeachiwa gari utengeneze jamaa kaondoka na key, unafanya mafekeche inawaka.
 
Uko sahihi, magari ya sasa hayana point hayana madistibyuta wala makabuleta mbadala wake imekuwa koili za kila silinda kompyuta ndio inazipatia mwako tofauti na distribyuta ambayo ilikuwa inapeleka myoto kwenye maplagi...hivi ule uzi wa magari Prondo upo maswali ya hivi yajibiwage kule
Gari za zamani ndio zilikuwa na distributor. Gari za kisasa hazina distributor. Electronic fuel injection imeondoa distributor.

Mfano GX100 kavu ina distributor ila GX100 VVTi haina distributor. Maybe I'm wrong.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ndo maana raia wakikamata mwizi wanammaliza.yani watu wanaumiza vichwa kuwadhibiti kwa kila mbinu lkn bado wataiba tu hata utumie mbinu za kisasa ama za kizamani,Ila ipo siku za mwizi ni fote(40)

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Unapolala toa battery ya gari weka ndani.
Ukilala toa upepo tairi zote.

Hakikisha unakicompressor kidogo cha kujazia upepo kinachotumia 12VDC.
Namimi nasema ukialala fungua tairi zote za gari kalale nazo chumbani...
 
zinayo mkuu bila hiyo gari haiwezi kuwaka kamwe
Gari za sasa nyingi hazina distributer.

Ni either distributerless Ignition system au coil on plug ignition system.

Hizo system gari inakuwa na camshaft position sensor na crankshaft position sensor.

Hizo sensor zinapeleka taarifa kwenye ECU/PCM na hivyo PCM ndio inaamua cylinder gani ifanye ignition kutokana na taarifa ilizopokea....
 
Hizi majuzi nimesikia watu watatu ninao wafahamu wameibiwa magari Dodoma. Na jhuu wizi unafanyika kibabe sana, wanakuja nyumbani wanafunga grill zenu kwa kufuli hata mkiamka wakato wanawasha gari msiweze kutoka.

Tena naskia kama una geti la ku slide wanaruka ukuta wanaingia ndani kisha wanavunja kufuli na kifungua gari...

hawa jamaa inaelekea ni wajuzi sana kiasi kwamba wanaweza washa gari lolote na hata kama lina alarm zinakuwa disabled.

Magari wanayopenda mpaka sasa ni Run X, Toyota Allex, Kluger, IST, n.k

Ushauri
Tufunge car tracking, japo sijui kama wanaweza.kuzi.disable au kujua kama ipo

Funga kamera nyumbani au motion detector

Kama kuna mwenye ujuzi zaid tujuzane maana hii hali ni hatar kw mkoa wa DODOMA kwa sasa... Polisi naona ni kama wameanza mishe za kuyasaka.. Mungu atusaidie.

Sent using Jamii Forums mobile app
Ukitaka usiibiwe Gari lako chomoa fuel injection relay(Au imeandika EFI).

hapo mwizi labda aje kutow hilo gari. Maana halitowaka.
 
Hizi majuzi nimesikia watu watatu ninao wafahamu wameibiwa magari Dodoma. Na jhuu wizi unafanyika kibabe sana, wanakuja nyumbani wanafunga grill zenu kwa kufuli hata mkiamka wakato wanawasha gari msiweze kutoka.

Tena naskia kama una geti la ku slide wanaruka ukuta wanaingia ndani kisha wanavunja kufuli na kifungua gari...

hawa jamaa inaelekea ni wajuzi sana kiasi kwamba wanaweza washa gari lolote na hata kama lina alarm zinakuwa disabled.

Magari wanayopenda mpaka sasa ni Run X, Toyota Allex, Kluger, IST, n.k

Ushauri
Tufunge car tracking, japo sijui kama wanaweza.kuzi.disable au kujua kama ipo

Funga kamera nyumbani au motion detector

Kama kuna mwenye ujuzi zaid tujuzane maana hii hali ni hatar kw mkoa wa DODOMA kwa sasa... Polisi naona ni kama wameanza mishe za kuyasaka.. Mungu atusaidie.

Sent using Jamii Forums mobile app
Fuga mbwa,german sherphard,miriki bastola,funga cctv/motion camera,
Mpaka wanawasha gari,lazima utasikia,fungua dirisha twanga mtu risasi ya kiuno,

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom