Wizi wa Fastjet, TCAA mpo kweli?

Wizi wa Fastjet, TCAA mpo kweli?

Leo asubuhi nikielekea Mwanza, nimekutana na kisa cha ajabu sana na Fastjet.

Kuna mtoto mdogo wa kiume miaka kama 14 aliyekuwa wa mwisho kwenye foleni kwenye check in kuelekea Mwanza. Ilipofika zamu yake, akafungiwa kwamba muda umepita. Huyu mtoto hakuelewa cha kufanya na kukosa ndege.

Matokeo yake kaambiwa aende kwenye desk iliyopo nyuma ya check in desks. Mbaya zaidi pale pia akaambiwa atoke nje ya Geti akabadilishe ticket. Kwa vile nilikuwa na muda, nililazimika kutoka naye nje. Huko nje pia kaambiwa alipie Tsh. 300,000. Kwa kipi, nilishindwa kuelewa kusema kweli.

Hii nchi inaendeshwa kana kwamba hakuna sheria. Mtu unanunua ticket kwa Shillingi 130,000 lakini hawajali, wana kuambia ulipie karibia mara tatu? TCAA na Ndugu Suleiman nadhani wamelala au kama wako macho, wameyafumbia macho haya.

Watanzania hii ya Fastjet tulipiganie. Huu ni wizi wa mchana kweupe!

Seleman hausiki na TCAA.....Malalamiko yako yana msingi sana sana
 
Kwa watu kama ninyi, bora murudishiwe mikia.

Mtu anaandika kitu alichoshuhudia, ninyi munajifanya wenye kampuni.
Tatizo kubwa kabisa ni check-in desk. Hao watu wamekuwa ni corrupt. Wamekuwa wakilaimisha mtu achelewe hata kama amewahi, wakitegemea utoe chochote ili wajidai kukupa nafasi. Hata hivyo nani asiyejua kwamba hii ni kampuni ya kiswahili tu!
mkuu mi sisafiri na hizo ndege daladala,mfano mdogo tu ni kwamba last month on way from Italy to Denmark nilikaa kwenye foleni sio.mpaka nafika check inn wananambia umekosea ikawa too late boarding.by the way ni wao walichange check inn door no,ndege iliondoka ikaniacha.nikawa refunded na first class ticket na huduma zoote nilizotumia pale Belgium kwa masaa manne ilikua juu yao.
Fastjet inawezekana wana system nzuri tu,tatizo utakuta kuna kina mwajuma na sefu wafanyakazi hapo wanalazimisha kupata chochote na ndio wanaowaumiza.
 
Unalolisema ni jipya sidhani kama unaweza kuondoka na ndege hiyhiyo maana ungekuwa hujachelewa bac kama inawezekana, kama vp ckunyngine mfly na prcision ss ambao hata ukichelewa kidogo wanaweza wakakufanyia mpango coz wanahudumia ndege zao wenyewe unlike fastjet
i mean unabadilishiwa ndege inayokwenda mda huo kwenye destination yako.ila hapa ni international zaidi,huko kipawa sidhani
 
Kama mnaweza kujustify hiyo scenario, wasiliana na TCAA-CCC. Ofisi zao ziko PPF tower, hawa ndo wanahusika moja kwa moja na kumlinda mlaji wa huduma za anga. Otherwise poleni sana wakuu.

Duh, unaambiwa umechelewa kuchek in, halafu ili uweze kupata msaada inakulazimu kufunga safari hadi PPF Tower, aina hii ya msaada inapatikana Tanzania tu.
 
Nyuma ya huyo dogo wa 14 yrs kulikuwa na watu? Au yeye ndo alikuwa wa mwisho?
Kama hao watu waliokuwa nyuma yake walifanya nin baada ya hapo?

we nawe mgum wa kuelewa umeambiwa dogo alikiwawa mwisho we bado unauliza badala ya kupiga mstari
 
Duh, unaambiwa umechelewa kuchek in, halafu ili uweze kupata msaada inakulazimu kufunga safari hadi PPF Tower, aina hii ya msaada inapatikana Tanzania tu.

Muwe mnasoma mnaelewa sio kukurupuka kujibu post. Mtoa mada amesema huyo kijana wamemfanyia hila mpaka wamemtoa nje, maana yake kusafiri kwa wakati huo itakuwa ni ngumu. Ushauri niliompa hapa ni namna gani anaweza kupata haki yake. WEWE PIA MSHAURI HUO MSAADA AMBAO SIO WA TANZANIA.
 
Nyuma ya huyo dogo wa 14 yrs kulikuwa na watu? Au yeye ndo alikuwa wa mwisho?
Kama hao watu waliokuwa nyuma yake walifanya nin baada ya hapo?

we nawe mgum wa kuelewa umeambiwa dogo alikiwawa mwisho we bado unauliza badala ya kupiga mstari
 
nafikiri mleta uzi hataki kusema ukweli kuhusu huyo mdogo wake kuwa alichelewa. jamani usafiri wa ndege sio kama dala dala au mabasi ya mikoani una taratibu zake. siku nyingine muwahishe huyo mdogo wako masaa 2 kabla ya safari halafu uone kama ataachwa. watanzania walio wengi wagumu sana kwenda na muda.
Wengi humu hayajawakuta....utatamani ardhi ipasuke tena zaidi kama uko na wageni wa nje..hi kitu fastjet sitaki hata kusikia,nakula basi kama kawa na story nyingi mpaka nafika nakokwenda..wafanyakazi wake ndiyo kero zaidi ya hiyo Fastjet
 
Nao bei zao si rafiki,
unajua kama tukitumia hivi vidogo vi cessna 208 kwa wingi
bei yaweza shuka mpaka sh 40,000 incL. VAT...lakini FITNA<FITNA<FITNAAAAA inalimeza taifa.....

Kweli kabisa mkuu. Are you piloting these ndege aina ya Cessna?
 
Fastjet dala dala. Hata usafi hawafanyi vizuri.
 
Fast Jet wapo strict sana kwenye checkin deadline ukizubaa wanakuzingua, ila mi nadhani wapo serious na kazi ndo maana wabongo wengi tunaachwa , FJ wanastandard za kimataifa checkin inabidi uwepo atleast 2 hours kabla ya ndege yako kusepa ili kuepuka kukimbia kimbia
 
Mhhh hawa jamaa ni wahuni sana last week, mwanza to dar reporting time saa 6:05 am tumefika 6:10 am tukakuta check in tayari ndege badala ya kuondoka 8:05 am tukandoka 7:05 am nahisi kuna watu waliachwa wasio enda na muda

Kuondoka kabla ya muda wake si hoja, huwa wanacheck kama abiria wote wameishaingia, sasa wakae wanasubiri nini wakati abiria wao wote wameishaingia mkuu?
 
Kuondoka kabla ya muda wake si hoja, huwa wanacheck kama abiria wote wameishaingia, sasa wakae wanasubiri nini wakati abiria wao wote wameishaingia mkuu?

Mhhhh...mbona kuna siku JKNIA waliacha abiria kama 8 au 9 upuuuzi wao wa kuwahi kuondoka...
Inshort kampuni ya kisengery sana
 
Kifupi jamaa wamejipanga vizuri sana nawafurahia kinoma
 
Naomba kuuliza mfano ukichelewa ku check in ikawa ndege imekuacha kuna kukubadlishia Siku yakuondoka kwel?
 
Back
Top Bottom