Wizi wa Fastjet, TCAA mpo kweli?

Wizi wa Fastjet, TCAA mpo kweli?

Kuna uwezekano kuwa imetokea na si makosa ya FJ, labda kutokujua, kuna siku binti alikuwa anakwenda Mbeya alfajiri, nilimsindikiza hadi JNIA nikamwelekeza vizuri kuwa apange foleni ya kwenda Mbeya na akisha-check in anipigie simu ili nami niondoke kuelekea kazini

Basi nimesubiri hakuna kitu, kuchungulia nikakuta binti yupo kwenye foleni ya kwenda Mwanza wakati huo Mbeya karibu wanafunga gate, ikabidi nimwombe jamaa akamwambie ndo ikawa salama yake vinginevyo angeishia kulalamika kaonewa.

Una bahati sana! siyo hawa FAstjet! wakati wanaanza walikuwa wanabembeleza wateja sana ila siku hizi sheria kali na nyingi ni kuongeza kipato zaidi! Unafika pale check in 40mns kabla ya ndege kuondoka unaambiwa umechelewa!

Angalia wamebadili hata muda wa kubuku tiketi na kulipia! Kwa sasa ni ndani ya dkk 20 tu !
 
Mhhh hawa jamaa ni wahuni sana last week, mwanza to dar reporting time saa 6:05 am tumefika 6:10 am tukakuta check in tayari ndege badala ya kuondoka 8:05 am tukandoka 7:05 am nahisi kuna watu waliachwa wasio enda na muda

Taratibu tutanzaa kuelewa maana ya ontime ukiambiwa reporting time ni saa tisa usiku usibishe ukiona kwako mbali nenda saa nne ulale uwanjani Watanzania nafikiri bado atujazoea KUTUNZA MUDA tulikuwa tunatoka nchi fulani kuja Tanzania reporting time ilikuwa ni saa tisa usiku sisi tuliondoka hotelini saa nane au saa saba usiku na tukafikaa nakukaa mpaka mda wa check in ulipofika tukaingia kwende ndege hvy nikajifunza kwenye ndege hakuna samahani hata kidogo na tuliomba tupewe flight ya mchana tukambiwa tuengeze dola 100 zaidi na nikusibiri mpaka wa confirm ndege yakufika nairobi then connection ya Tanzania hivyo ndugu jifunze kutunza muda hakuna huruma kwenye masuala ya angani.
 
tueleweshane mkuu apo kwenye 95,500 ni bei ya kukodi au mnakuwa na abiria wengine?
mwanangu hii ni zaidi ya daladala
tunataka haya mambo yawe ya kawaida sana...lakini tcaa wanatumaindi.
We kama unakwenda mwanza au iringa au kigoma sema tupange muda.
 
Haya matatizo ya hii kampuni sijui yataisha lini kwamaana kuna haya pia........

Fastjet-798x350.jpg


MAMLAKA ya Usafiri wa Anga nchini (TCAA), imeitaka Menejimenti ya Shirika la Ndege la Fastjet kuorodhesha na kuwasilisha katika mamlaka hiyo majina ya mawakala wake, wanaoruhusiwa kuuza tiketi za shirika hilo kwa wateja wake tofauti na ilivyo sasa ambapo kila mtu ana uwezo wa kuuza tiketi hizo kwa wateja wao kwa bei isiyoeleweka, FikraPevu imejulishwa.

Agizo hilo la TCAA kwa kampuni hiyo ya Fastjet, limetolewa na Mkuu wa Ukaguzi wa Usafiri wa Anga katika mamlaka hiyo, Daniel Malanga kutokana na madai ya kuwepo kwa malalamiko ya muda mrefu kutoka kwa wateja wa sekta hiyo ya usafiri wa anga juu ya mawakala wa teketi wa kampuni hiyo kutoeleweka vyema kwa wateja wao.

Kwa mujibu wa TCAA, bei za tiketi za usafiri wa ndege za kampuni hiyo zimekuwa hazieleweki kwa wateja wake hata kwa mamlaka hiyo, jambo ambalo ni kinyume cha sheria za usafiri wa anga, lakini pia hali inayowachanganya wateja wa kampuni hiyo.

Soma zaidi FikraPevu kwa muda mrefu sasa imekuwa ikipokea malalamiko..



 
Una bahati sana! siyo hawa FAstjet! wakati wanaanza walikuwa wanabembeleza wateja sana ila siku hizi sheria kali na nyingi ni kuongeza kipato zaidi! Unafika pale check in 40mns kabla ya ndege kuondoka unaambiwa umechelewa!

Angalia wamebadili hata muda wa kubuku tiketi na kulipia! Kwa sasa ni ndani ya dkk 20 tu !

Alikuwa bado ndani ya muda kama dk tano hivi. Kwa upande wangu wananichosha kupora watu Perfume zao hata kama umeweka kwenye begi inayolipiwa na kupakiwa na wao. Mchezo huu upo sana mwanza jamaa wanakomaa kichizi eti hairuhusiwi, naamini ndani ya muda mfupi watafungua duka maana wanaiba kweli.
 
Kama mnaweza kujustify hiyo scenario, wasiliana na TCAA-CCC. Ofisi zao ziko PPF tower, hawa ndo wanahusika moja kwa moja na kumlinda mlaji wa huduma za anga. Otherwise poleni sana wakuu.

Ebu lindeni lugha jamani! Kuna MLAJI WA HUDUMA ZA ANGA? Nani anaweza kula huduma za anga? Kwanini usiseme mtuamiaji wa huduma za anga?
 
Wewe ni mwongo.Haiwezekani mtu akiwa kwenye foleni akaambiwa muda umeisha.
What if check in Clerk alikuwa too slow katika kazi yake?

Hilo unalolisema halipo.As long as upo kwenye mstari, au umeikuta foleni ni lazima ucheck in.

Usitake kutufanya wote humu wajinga.


Ndio na mimi nashangaa kwenye hili. Ukishakaa kwenye check in hamnaga mda kuisha.
Mpaka zoezi likamilike lazima uwe checked in.
Huo utakuwa ni usoro na kitendo cha wao kukubali kauli ya mda umeisha na wao ni masoro.
Wameliwa tayari.
Oteeee
 
Alikuwa bado ndani ya muda kama dk tano hivi. Kwa upande wangu wananichosha kupora watu Perfume zao hata kama umeweka kwenye begi inayolipiwa na kupakiwa na wao. Mchezo huu upo sana mwanza jamaa wanakomaa kichizi eti hairuhusiwi, naamini ndani ya muda mfupi watafungua duka maana wanaiba kweli.

Dawa yao ndogo sana.
Onyesheni uzalendo kwenye ndege yenu ya Precision Air. Mbona imesharudi hewani na inafanya kazi vizuri tu
 
Dawa yao ndogo sana.
Onyesheni uzalendo kwenye ndege yenu ya Precision Air. Mbona imesharudi hewani na inafanya kazi vizuri tu
Nao bei zao si rafiki,
unajua kama tukitumia hivi vidogo vi cessna 208 kwa wingi
bei yaweza shuka mpaka sh 40,000 incL. VAT...lakini FITNA<FITNA<FITNAAAAA inalimeza taifa.....
 
Haya matatizo ya hii kampuni sijui yataisha lini kwamaana kuna haya pia........




MIkampuni kama hii iko radhi kuhonga mamilioni kwa wenye dhamana ili tu,Air Tanzania isifufuke.
Hivi kweli,kweli,kweeeeli Tanzania tunashindwa kuwa na ndege?
Uwezo wa kila namna kwenye fani hii mbona tunao?
 
Presha za nn,tumia usafiri wa basi hata likikuacha utalifukuzia utakutana nalo linapima uzito pale chalinze
 
Tatizo ni serikali yetu kutokua na ndege ndio maana tunafanyiwa wanachotaka wao.wewe uliona wapi 20kg lazima ulipie ? Ndege inaonekana ni starehe hapa kwetu wakati ni kitu cha kawaida tuu.hakuna lugha nzuri kati ya abiria na wahusika.naomba tupate wawekezaji wengine waje ktk ushindani huu yoote yataisha haya.
 
Back
Top Bottom